Dr. Magufuli: Genius anayepambania urais

Dr. Magufuli: Genius anayepambania urais

Naona leo mmeambiwa mje huku mumtangaze.....mzee wa sitawaangusha.....wala rushwa.......
 
Genius Wa kukariri takwimu za uongo eti Bahari ya Hindi INA Samaki milioni mia saba Na sitini Na tatu hata Wizara husika hawajui

kama zake za uongo ungeenda wewe kuhesabu hao samaki utuletee takwimu za kweli!
 
Episode 1

Dr John Pombe Maghufuli, mgombea urais kupitia CCM ni mgombea mwenye haiba ya kipekee kati ya wagombea wote katika uchaguzi mkuu Wa 2015, uwezo wake Wa kiuongozi umeanza muda mrefu kwa kujipambanua kila wizara anayopewa kuiongoza tangu aingie kwenye siasa 1995
Ni mwanasayansi nguli aliyeleta mapinduzi ya kujenga barabara toka tupate uhuru

Ni mwanasiasa alieingia kwenye rekodi ya CCM kwa kushinda kura nyingi kwenye Mkutano Mkuu,

Ni mwanasiasa mwenye Akili nyingi za kuzaliwa (genius) , hii limethibitishwa pia na kipindi maalum cha historia yake kilichorushwa na ITV siku ya jumatano saa 3:15 Usiku

Ni mzalendo Wa kweli asiyetiliwa shaka na uadilifu wake ni grade A

Ni kiongozi mwenye kuthubutu na kusimamia anachokiamini, na ni kiongozi mwenye muono Wa mbali

Ni kiongozi atakaeingia kwenye historia ya kuitoa Tanzania kutoka nchi ya kundi maskini kwenda uchumi Wa kati na kuingia katika nchi tajiri Afrika


Ni kiongoz anaependwa kukumbukwa kwa mazuri aliyofanya na atafanya hivyo

Ni kipenzi cha Watanzania wengi na kawekeza kwenye mioyo ya watanzania kumkubali sana katika uchapakazi wake


WAPINZANI WAKE KWA UJUMLA

Ni watu wababaishaji na wasio na ueledi na uelewa Wa mambo
Ni watu wenye fani za sanaa na maonyesho kiufupi mazingaombwe

Ni watu wasio na dira wala dhamira Bali tamaa na ufisadi uliotukuka

Ni watu wasiojua Tanzania inataka nini ila wanaangalia wao wanataka nini

Ni vilaza kimawazo na kimtazamo kwani hawawez kusimamia jambo kwa muda mrefu Bali tamaa ya pesa

Ni watu wasiokuwa na uwezo Wa kusoma alama za nyakati Bali alama za kununuliwa


Asanteni ,,,,,itaendelea episode 2
. Utakuwa una wazimu wewe Magufuli awe genius? Hata waliosoma naye katoke seminary hawajawahi kumutaja kama genius. Labda demu wake Sundi ndo kaandika haya. Halafu unaandika kwa mihemko juu ya wapinzani wake. Wanasayansi na magenius wako busy kufanya ugunduzi huko wala hutowasikia kwenye siasa na mbwbwe za Aliselema. Inatia shaka Uwezo wako. Mwanasayansi amuvumbua mini?
 
Hao jamaa wako EXPLOSIVE sana, alafu wanataka kwenda Ikulu.Magu ni level nyingne.Tunahtaji akili yake baada ya mafisadi kumzunguka Dr.

Khaa!! Ngoja aingie ikulu kisha ayapige kufuli mifisadi yote tusonge mbele. Sijui eddo atarudishaje mabilion yake
 
Mmh ushabiki umezidi sasa,namkubali Magu lakini sidhani kama ni genius ....Lakini kwani tunahitaji genius ndio aongoze au ? Jk alikuwa genius au ? ...Usisimfie sana ukamharibia sasa ,,,yeye ni PhD holder wa science na kweli atakuwa Raisi wa kwanza wa Tanzania kuwa nayo.....Magufuli au Lowasa ni wanasiasa punguzeni sukari...#nisiasatu ....
 
Hivi wengine mlisomea wapi kama hata kuandika lugha yenu hamuwezi??!
Huu ndiyo ukweri =Huu ndio ukweli

Kiswahili ni lugha tu. ndio na ndiyo su chanzo cha kumdhalilisha mtu. Sisi wasomaji twataka hoja. Mwinzio ana muamini Magufuli kama kingozi bora. Kama we we wapinga basi toa hoja yako na siyo kutaka tofauti ya ndiyo na ndio. Kumbuka asiye kubali kushindwa siyo mshindani.
By the way, ni sio au siyo?
 
Mtu kuwa genius haimanishi anauwezo wakutatua matatizo ya nchi. Hata Isac Newtown the genius of physics alipo ingizwa kwenye bunge la wingereza aliongea sentensi moja tu na muongo mwingine uliyofuata hakuludishwa. Hiyo sentensi ilikuwa(fungua dirisha nasikia joto) Kuwa genius haimanishi unaweza ongoza nchi. Huo niuongo.
 
  • Thanks
Reactions: KVM
Wakiitwa PhD na yeye ataenda
Ivi kuna mtu anasoma PhD teana ya Science alafu ni waziri
embu tuache ushabiki
Nakumbuka nilipokuwa nachukua PhD yangu hata kitanda nakisahau alafu leo hii mtu anakuja
eti kasoma rusting technology tena akiwa waziri it is not that easy!!!

Watu wanaleta mchezo na shule-wanavyoona Wasomi wanalipwa kimagumashi wanachukulia shule poooa
 
Episode 1

Dr John Pombe Maghufuli, mgombea urais kupitia CCM ni mgombea mwenye haiba ya kipekee kati ya wagombea wote katika uchaguzi mkuu Wa 2015, uwezo wake Wa kiuongozi umeanza muda mrefu kwa kujipambanua kila wizara anayopewa kuiongoza tangu aingie kwenye siasa 1995
Ni mwanasayansi nguli aliyeleta mapinduzi ya kujenga barabara toka tupate uhuru

Ni mwanasiasa alieingia kwenye rekodi ya CCM kwa kushinda kura nyingi kwenye Mkutano Mkuu,

Ni mwanasiasa mwenye Akili nyingi za kuzaliwa (genius) , hii limethibitishwa pia na kipindi maalum cha historia yake kilichorushwa na ITV siku ya jumatano saa 3:15 Usiku

Ni mzalendo Wa kweli asiyetiliwa shaka na uadilifu wake ni grade A

Ni kiongozi mwenye kuthubutu na kusimamia anachokiamini, na ni kiongozi mwenye muono Wa mbali

Ni kiongozi atakaeingia kwenye historia ya kuitoa Tanzania kutoka nchi ya kundi maskini kwenda uchumi Wa kati na kuingia katika nchi tajiri Afrika


Ni kiongoz anaependwa kukumbukwa kwa mazuri aliyofanya na atafanya hivyo

Ni kipenzi cha Watanzania wengi na kawekeza kwenye mioyo ya watanzania kumkubali sana katika uchapakazi wake


WAPINZANI WAKE KWA UJUMLA

Ni watu wababaishaji na wasio na ueledi na uelewa Wa mambo
Ni watu wenye fani za sanaa na maonyesho kiufupi mazingaombwe

Ni watu wasio na dira wala dhamira Bali tamaa na ufisadi uliotukuka

Ni watu wasiojua Tanzania inataka nini ila wanaangalia wao wanataka nini

Ni vilaza kimawazo na kimtazamo kwani hawawez kusimamia jambo kwa muda mrefu Bali tamaa ya pesa

Ni watu wasiokuwa na uwezo Wa kusoma alama za nyakati Bali alama za kununuliwa


Asanteni ,,,,,itaendelea episode 2

Magufuli siyo Genius angekuwa hivyo asingesoma diploma ya Mwalimu angeenda uni direct. Magufuli alikuwa anajituma shuleni lakini siyo genious!
 
Fanya utafiti mfupi tuu juu ya wale wanaomuunga mkono lowasa kwa kulinganisha na wale wanaomuunga mkono magufuli. Utagundua kuwa lowasa anaungwa mkono na madereva Bodaboda na walevi na vijana wamachinga wa kariakoo na watu walioshindwa siasa ndani ya ccm. Kwa kifupi anaungwa mkono na watu wasio na elimu na waliokosa taaluma. Watu kwenye elimu woye kama Prof. Lipumba nikiwemo na Mimi hawawezi kumuunga mkono Lowasa. Kumbuka birds of the same feathers flock together.... Show me your friends and I will tell who you are.
 
Fanya utafiti mfupi tuu juu ya wale wanaomuunga mkono lowasa kwa kulinganisha na wale wanaomuunga mkono magufuli. Utagundua kuwa lowasa anaungwa mkono na madereva Bodaboda na walevi na vijana wamachinga wa kariakoo na watu walioshindwa siasa ndani ya ccm. Kwa kifupi anaungwa mkono na watu wasio na elimu na waliokosa taaluma. Watu kwenye elimu woye kama Prof. Lipumba nikiwemo na Mimi hawawezi kumuunga mkono Lowasa. Kumbuka birds of the same feathers flock together.... Show me your friends and I will tell who you are.

Sisi madereva wa bodaboda na walevi wa viroba ndio baba zako kwa kuwa tunashinda na mama yako kilabuni huku kijijini na ndio maana hakusumbui na hivo vihela vyako kwa ajilimya kununua mafuta ya vibatari
 
Wakiitwa PhD na yeye ataenda
Ivi kuna mtu anasoma PhD teana ya Science alafu ni waziri
embu tuache ushabiki
Nakumbuka nilipokuwa nachukua PhD yangu hata kitanda nakisahau alafu leo hii mtu anakuja
eti kasoma rusting technology tena akiwa waziri it is not that easy!!!

Kuna ugumu gani. Si inategemeana tu na uwezo wako kiakili na nidhamu ya kufanya hiyo PhD?
 
Hivi wewe unajua Genius kweli?. Genius anatumiaga njia ya mkato?. Ukitaka kujua siyo genious, check historia yake, ilibidi asome kwanza Diploma ya Ualimu alafu ndio aende Chuo kikuu, 'Mature Age Entry'. Wenzake walioenda huo direct utawaitaje!?. miungu au?. Shame on you. Hii peke yake inaonyesha kuwa ni mtu ambaye anastruggle sana kuelewa mambo.

Pia ukimcheki kelele nyingi na ubabe kuliko hoja, hii inamaanisha kukosa uwezo na hivyo kupiga kelele ili usikike kuwa na wewe umeo...wazungu wanasema'the loudest in the room is the weakest one'. Hebu tafuta hotuba zake umsikilize. Mweupeeeeeee. Peeee.

Geniuses wengi duniani walishindwa kuendelea au kufeli shule kwenye hatua za mwanzo lakini baadaye walioendelea na shule walionyesha jinsi waliyokuwa na akili. Jibu hili halimuungi mkono mtoa hoja kuwa Magufuri ni Genius bali linapinga usemi wako kuwa geniuses wanendelea na shule moja kwa moja
 
Hahaha

Halafu nashangaaga sana unakuta mtu ana familia kabisa na watoto...kabisa imeshaonekana wazi kua TZ under "sisi m" hamna future....Narudia tena...chini ya hiki chama..hii nchi mbele ni giza ... ila unakuta anaipigia debe "sisi m".

kwa miaka hii...walio salama angalau..ni

1) watanzania waishio nje ya nchi na ambao hawana mpango wa kurudi

2) watanzania (kama mimi) ambao hatuna familia wala watoto , sina wasiwasi wa kizazi changu kuangamia wala kupata shida...cause, its simple...sina mtoto.

Sasa wewe mwenzangu ambae una watoto..tena wengine wako nursery /primary...afu unaipigia debe "sisi m" unahitaji kupimwa akili.

kwa hali ya saivi ni kua hatuna tena rasilimali...zimeibwaaaa...zoteee...mfano..juzi mmeskia meno ya tembo yamekatwa uwanja wa taifa kwa wenzetu huko ...walioko serious, ila yalipita uwanja wetu bila kushikwa.

Tanzania ipo kwenye list ya nchi zinazoongoza kwa madeni..,, ni nchi ya 90 duniani kwa madeni https://en.wikipedia.org/wiki/List_of_countries_by_external_debt )

na ipo kwenye Heavily indebted poor countries ( https://en.wikipedia.org/wiki/Heavily_indebted_poor_countries )


TAFAKARI....CHUKUA HATUA.

USHAURI: kwa wewe mwenzangu ambae huna mtoto, nakushauri kabisa ...nimefatilia mustakabali wa hii
nchi...Madeni,wizi wa mali za umma etc...nakushauri bila kupepesa macho. "sisi m" ikishinda oct. usizae , kama utapenda kutomuona mwanao akiteseka

kwa wale ambao wana watoto wadogo...anza kumwandalia mwanao ajira...mfungulie biashara...mapema..kwasababu...takwimu zinaonesha Unemployment rate inaongezeka TZ, miaka 3 ijayo... hakuta kua na sjui mtoto wa mwenye hela au mtoto wa maskini.
kwa anaetaka ushauri zaidi .....anicheki PM, kwa wale wataobisha...nawashauri kitu kimoja.... SOMENI , SIKU HIZI KILA KITU KIPO ,VITABU ..MITANDAO.. TAKWIMU ZOTE ZINAEKWA ONLINE.
 
Back
Top Bottom