Dr. Kitila Mkumbo tunakutaka Iramba Magharibi!

Dr. Kitila Mkumbo tunakutaka Iramba Magharibi!

Mimi nawafahamu hao watani zangu wa Kinyaramba na Wanyaturu. Kawaida yao wanachagua mwenye hela na cheo. Kwa mazingira ya sasa ni kazi ngumu sana Kitila Kumshinda Mwigulu maana Dr kitla hana hela na cheo kama cha Mwigulu. Kumbuka kuwa Mwigulu sasa hivi atajipanga kushinda jimbo atatumia hela za chama kujenga mazingira kiasi kwamba Kitila ataonekana hana maana. Mkumbuke kuna kitu kinaitwa vikoba vya kina mama, Mwigulu anavitembelea na kuwapa mtaji wa kukopeshana kina mama. Sijui kama Dr Kitla ana hizo hela. Kazi yake itakuwa ngumu kutokana nature ya watu. THIS IS MY OBSERVATION, time will tell us.
 
attachment.php

harakati zimeshaanza tayari, jimbo ni lako 2015
 

Attachments

  • 603205_543477845665400_702402410_n.jpg
    603205_543477845665400_702402410_n.jpg
    30.3 KB · Views: 273
Mimi ni kwetu ni Shellui nimeongea na wananchi wa hapa wamechoka na Mwigulu Nchemba wanasema kwamba Dr. Mkumbo uvute soksi kwani 2015 jimbo ni lako.

Kumwondoa mzinzi siyo kazi rahisi, Kitila Mkumbo kama kweli amedhamiria kwenda Iramba awe amejiandaa kweli kweli
 
Last edited by a moderator:
Ndugu wanajamvi leo nimeamua kuwaletea mpambano wa wanyiramba hawa wawili ambao wanatarajia kumenyana kwenye kinyang'anyiro cha ubunge mwaka 2015 kwenye jimbo la iramba,wasomi hawa wamekuwa na mvuto wa tofauti katika jimbo la iramba.

Kwa upande wa Mwigulu Nchemba amekuwa kivutio pale anapofika jimboni na kugawa pesa kwa vijana wa stendi, sokoni na mitaa yote anayopita hivyo amefanikiwa kuwa na wafuasia wanaopenda pesa zaidi kuliko yeye mwenyewe hii ni kutokana na pale anapofika jimboni akiwa hana pesa huwa anaambulia matusi na kejeli kutoka kwa vijana wa iramba.

Kwa upande Dr. Kitila Mkumbo huwa akifika jimboni watu wengi hupenda kupiga nae picha, vijana hupenda kusikiliza nasaha zake ambazo huwa zinalenga ktk masuala ya elimu na ujasiriamali, anapenda sana kuwasaidia wazee wanaopendelea kunywa pombe za kienyeji kwa mfano ktk kijiji cha mugela aliwasaidia wazee kwa kuwaezekea kilabu chao cha pombe yao ya kienyeji maarufu kama mtukuru.

Kitila akifika jimboni hupendelea kupita kwenye shule za mkoa mzima kwa mfano aliwahi kupita kwenye shule za A-level za mwenge na tumaini kuwapa ushauri na hamasa ya umuhimu wa kusoma kwa bidii.

Kwa upande wa elimu zao Mwigulu anafanya PhD na kitila anafanya ya uprofesa hivyo kila mtu hapo anaitumia elimu yake kwa jinsi tofauti coz Mwigulu anaamini katika sera za Prof. Lipumba za kugawa pesa na Kitila anaamini katika kuwapa elimu bora wanyiramba ili waweze kufanya biashara zao vyema.

NAOMBA KUWASILISHA.
 
I See, Mkumbo ana kampeni ya raha sana. Natamani ningekuwa mimi niligaragaze hili chemba vibaya.
 
Mwigulu hana vision coz elimu yake ina utata,kujenga hoja enyewe humu hawezi zaidi ya kuleta siasa za ccm za kizamani za kina Mangula.nashindwa kuamini kuwa hata BOT alishafanya kazi.
 
Mkumbo ni kichuguu nchemba hivyo kumlinganisha kisiasa iramba unamvunjia heshima mwigulu nchemba
 
Hahahaa unajua Iramba kwa wajomba zangu na unanifurahisha ulivyosema pombe za kienyeji "mtukuru" ha ha ha a
 
Hao wote ni ndege katika kiota kimoja na wanajuana kwa kilemba.

Dr. Kitila Mkumbo ni " masalia" kulingana na madai ya Ben saa8 (double agent) and his clone (mgogoro wa madiwani Arusha)

Mwiguru Nchemba ni sponsor wa "masalia" kulingana na madai ya baadhi ya wana jf

'Ndugu' huwa hawapambani wenyewe kwa wenyewe ili kupata mlo bali wanapeana.

Ndiyo maana hata akili zao ni zile zile. Mwingine anagawa pesa na mwingine anagawa pombe. Stupid idea.
 
Unamzungumzia Mwigulu original au Lameck? Ebu check kushabihiana kwa majina yao! Mwigulu na Mulugo!!
 
Mkumbo ni kichuguu nchemba hivyo kumlinganisha kisiasa iramba unamvunjia heshima mwigulu nchemba

mwigulu nchemba havunjiwi heshima make yupo analima na kuchunga ng'ombe uko kijiji, huyu anaitwa lameck madelu a.k.a 1st class holder a.k.a naibu katibu mkuu wa ccm
 
Nimegundua sasa hasira za Mwigulu Nchemba zinatokana na nini. Kumbe jimbo karibia linamponyoka? Kazi anayo
 
Last edited by a moderator:
Hao wote ni ndege katika kiota kimoja na wanajuana kwa kilemba.

Dr. Kitila Mkumbo ni " masalia" kulingana na madai ya Ben saa8 (double agent) and his clone (mgogoro wa madiwani Arusha)

Mwiguru Nchemba ni sponsor wa "masalia" kulingana na madai ya baadhi ya wana jf

'Ndugu' huwa hawapambani wenyewe kwa wenyewe ili kupata mlo bali wanapeana.

Ndiyo maana hata akili zao ni zile zile. Mwingine anagawa pesa na mwingine anagawa pombe. Stupid idea.

Kitila Mkumbo alimtaka Ben kuhakikisha analiangamiza kundi haramu la Pindua Mbowe-PM7
 
Kitila Mkumbo alimtaka Ben kuhakikisha analiangamiza kundi haramu la Pindua Mbowe-PM7

Mkuu naona ndugu yetu hakusoma vizuri hile taarifa ya Mkuu Ben saanane.....Dk Kitila Mkumbo anafaa kabisa kusimama pale Iramba na kupeperusha Bendera ya chama makini CHADEMA ambacho ndio tumaini kubwa la Watanzania wapenda mabadiliko,
 
Pia mimi kwetu ni Mwanza! Wiki mbili nilikuwa Singida maeneo ya IGUGUNWA,
Katika tafiti zangu za kikazi watu wengi wamedai Ndugu Mwigulu Nchemba hafai hata kidogo, Dr kitila Mkumbo naamini kabisa utashinda jimbo hillo la huyo jamaa ambae aitwaye Chemba kwani tafiti zinaonyesha nae ni wa EPA ndo maana anatetea sana CCM.
Naahidi kuja kuongeza nguvu wakati wa kampeni hadi Nchemba aondoke.
 
Back
Top Bottom