Malungu acha kutumiwa au kutoa hoja kwa kutumia thread za jf. Hakuna kata, wala kijij,wala kitongoji, wala mtaa wala familia nzimanzima niliwahi kupata upinzani. Nimetoka ziara hivi majuzi watu wananing'ang'ania mpaka hawataki niondoke. Kisharita nilifanya mkutano watu zaidi ya 500 mpaka saa mbili usiku na nimeondoka watu wamebeba majani mabichi. Nilikuwa kisiriri wakasema wewe ni malaika sio mbunge. Juzi ndago nimeongea watu wakalua machozi nikapewa zawadi mbuzi 8 vitambaa kumi nishone suruari.sijawahi kwenda eneo nikafyonzwa au kuulizwa swali la kejeli. Nitajie acha kijiji familia nzima inayonikataa. Kama mimi mwongo mwacheni mtu wenu aje majibu yatatoka kwa wenye mamlaka. Hujui hata uwezo niliowajengea wanyiramba mpaka sasa. Nimepeleka mradi wa over 600milion mingela, over 600 milion ndago, over 100 milion kyengege. Barabara ya mlimani kidaru imepanda daraja. Mtoa shelui iliyokuwa hapitiki hata kwa miguu bila kuvua viatu tangu uhuru nenda leo. Bado ya ntuike tyulia kidaru mwaka huu inapanda na kuwekewa fedha. Sina mashaka hata chembe. Hii habari ya kutokuwapa watu pesa subiri uwe mbunge usiwape ili mimi kwa dini yangu najua KUSOMESHA YATIMA NI IBAADA NA WALE WALIOFAULU MAALUM WAZAZI HAWANA KITU NITWAENDELEA KUWASOMESHA. ANAECHUKIA HILI ATAPAMBANA NA MUNGU. MBONA NDUGU YENU ALIJENGA KIRABU CHA POMBE NA KUWANUNULIA WATU POMBE? IPI HERI POMBE AU KUWAGAWIA YATIMA?