kama watanzania wote tungekuwa tunafikiri kwa mtazamo huu au mpana zaidi ya huu nchi hii ingekuwa mbali sana.makosa au mapungufu ya viongozi wa cdm yakisemwa hadharani basi utasikia mlinganisho na mtu wa ccm,sasa unajiuliza ya nini kuwaondoa ccm madarakani kama hao hao ndio role modo wenu?
angalia maccm yalivyo paronchial. halafu si ajabu hawa kina chicco ni wasomi hata wa masters level au hata zaidi. kwani wewe chicco unashindwa kuelewa ni kwa nini huo mlinganisho unatolewa? angalia nyuma ya huo mlinganisho utakuta kuna kitu watu wanakihoji japo hawakitaji straight. najua hata wewe unakijua lakini kwa sababu ndicho kinachowalinda mafisadi wa nchi hii, ndicho kinachowalinda majangili ya nchi hii, unajifanya hukijui na unabakia tu kusema kuwa cdm inahalalisha makosa just because ccm nayo inatenda makosa. embu toka nje ya box la simply ulinganisho then tulonge. Chicco kwa nini wewe ukiiba uitwe shujaa lakini moshdar akiiba katika nchi ileile apigwe mawe hadi kufa? kwa nini?
Jibu ni rahisi......M.F.U.M.O
ni Mfumo dhaifu wa kifedhuli umejengwa makusudi na ma-ccm ili kuwalinda makahaba wa uchumi wa waTanganyika, wazinzi wa maliasili za tanganyika, majangili ya meno ya tembo, wauza sembe wanaoua wenetu kwa sembe zao, wezi wa mali ya umma, wadini, wakabila nk nk na hapo hapo mfumo huo ukimkandamiza mnyonge na asiye na sauti....kwamba akinya kuku kanya lakini akinya bata kaharisha huyo. ndiyo, ni mfumo.....huo ndo tunaotaka ufumuliwe ujengwe upya. na siku si nyingi....utafumuliwa tu, pendeni msipende! wakati ni ukuta na embe limeshaivia mtini, kwamba litaanguka ama la si mjadala tena, mjadala ni kuwa embe litaanguka lini?
As usual hamuwezi kutoa hoja bila matusi. Shida sana nyie watu!
Inahitaji Weledi wa hali ya juu kumuelewa Nguli Kitila Mkumbo, Pale tutakapoacha kushabikia Viongozi na badala yake kupenda CHAMA, tutaweza kuchambua hoja za msingi na kasoro zilizopo katika uongozi.
Sijui kama kumbukumbu zangu ziko fresh ila Dr. Mkumbo, Kitilla alikuwa mmoja wa watu ambao wako katika vetting selection pale CHADEMA mfano Ubunge Viti Maalum na mambo mengine. Hili suala ni sawa sawa na mtu kuokota tope na kumrushia mwingine lazima mrushaji na anayerushiwa wachafuke. Kwa hiyo Uongozi CHADEMA, kundi la akina Z.Z.K mjitazame wote na mjipime makosa yenu. Naamini CHADEMA wamechemka katika kulikurupukia suala hili pengine timing na technicalities za 2015. Lakini hili suala sio jepesi kama lilivyochukuliwa na uongozi. Lakini hata hao waliotolewa wasijione kama ni super human beings wajishushe kwani CHADEMA kama taasisi itaendelea kuwapo na ilikuwapo hata kabla ya wao kuwa wanachama.
Hapa ni vigumu kwa mambulala na washabiki bandia wa CDM kumuelewa Kitila. Hawa wamekaririshwa kupinga chochote kinachokosoa uongozi wa CDM na kuunga chochote kinachotoka kwa akina Mbowe. Ni ushabiki uliotupofusha na sasa tunajidai hakuna mgogoro. Leo Mbatia katupigia vizuri kiaina!
Nakubaliana na mawazo ya mwamdishi hapo juu bila mashaka kabisa.Dr Mkumbo hakujua mkakati wa ZZK pamoja na kwamba ni msomi aliyebobea na hata kuaminiwa kuongoza DUCE pamoja na kuwa mshauri mkuu wa CHADEMA katika kuandaa mpango mkakati wa kuwapata wabunge wa viti maalumu ndani ya CHADEMA.Kitendo cha yeye kuaminiwa na chama ni dhahiri kuwa weledi wake haukuwa na mashaka kipindi kile anapewa majukumu hayo mazito.Inawezekana ni kweli Dr. Mkumbo naye pamoja na kuwa msomi lakini hajamuelewa ZZK vizuri juu mpango wake pale cdm.
Sasa kama wanatafuta chama mbdadala wa cdm na ccm ni kwa nini anaenda Mahakamani kulazimisha kubakia kwenye chama 'kisichostahili'!?
Kama kweli CC ambayo ipo kikatiba maamuzi yake yanaitwa ya kidikteta basi nami pamoja na kutosoma, natilia mashaka usomi wa hawa waandaaji wa waraka.
uko sahihi mkuu.me sio kwamba napingana na wewe au vipi but huwa sipendi sana hii tabia.mbowe katumia pesa ya umma kwenda kustarehe na mtu wake ughaibuni lijitu linakuja linakujibu mbona mwigulu naye kafanye hivyo!!!!so what?kwamba coz mwigulu kafanya(actually ni kosa) ndio ihalalishe kufanya mbowe?(point of correction:natambua kuwa katibu wa bunge ameweka sawa hii issue so sio kwamba namtuhumu mbowe itz just an example).kwa nini cdm wasiwe tofauti?kwa nini wahalalishe maovu yao coz tu wa ccm nao wamefanya?angalia maccm yalivyo paronchial. halafu si ajabu hawa kina chicco ni wasomi hata wa masters level au hata zaidi. kwani wewe chicco unashindwa kuelewa ni kwa nini huo mlinganisho unatolewa? angalia nyuma ya huo mlinganisho utakuta kuna kitu watu wanakihoji japo hawakitaji straight. najua hata wewe unakijua lakini kwa sababu ndicho kinachowalinda mafisadi wa nchi hii, ndicho kinachowalinda majangili ya nchi hii, unajifanya hukijui na unabakia tu kusema kuwa cdm inahalalisha makosa just because ccm nayo inatenda makosa. embu toka nje ya box la simply ulinganisho then tulonge. Chicco kwa nini wewe ukiiba uitwe shujaa lakini moshdar akiiba katika nchi ileile apigwe mawe hadi kufa? kwa nini?
Jibu ni rahisi......M.F.U.M.O
ni Mfumo dhaifu wa kifedhuli umejengwa makusudi na ma-ccm ili kuwalinda makahaba wa uchumi wa waTanganyika, wazinzi wa maliasili za tanganyika, majangili ya meno ya tembo, wauza sembe wanaoua wenetu kwa sembe zao, wezi wa mali ya umma, wadini, wakabila nk nk na hapo hapo mfumo huo ukimkandamiza mnyonge na asiye na sauti....kwamba akinya kuku kanya lakini akinya bata kaharisha huyo. ndiyo, ni mfumo.....huo ndo tunaotaka ufumuliwe ujengwe upya. na siku si nyingi....utafumuliwa tu, pendeni msipende! wakati ni ukuta na embe limeshaivia mtini, kwamba litaanguka ama la si mjadala tena, mjadala ni kuwa embe litaanguka lini?
Nakubaliana na mawazo ya mwamdishi hapo juu bila mashaka kabisa.Dr Mkumbo hakujua mkakati wa ZZK pamoja na kwamba ni msomi aliyebobea na hata kuaminiwa kuongoza DUCE pamoja na kuwa mshauri mkuu wa CHADEMA katika kuandaa mpango mkakati wa kuwapata wabunge wa viti maalumu ndani ya CHADEMA.Kitendo cha yeye kuaminiwa na chama ni dhahiri kuwa weledi wake haukuwa na mashaka kipindi kile anapewa majukumu hayo mazito.
Katika waraka wake hapa JF,yeye binafsi ameonyesha madhaifu maengi amabyo hakuyapa majibu na wala hakuona sababu ya kuyajadili.Moja kubwa zaidi ni,kwanza CHADEMA ni chama cha siasa mabacho uanachama wake ni wa hiari (siyo wa lazima),na kwamba ili uwe mwanachama wa vyama vya hiari ni lazima ukubaliane na KATIBA ya chama husika.Dr Mkumbo alilijua hili.Hoja hapa ni kwamba endapo utaona kuna mapungufu ya KIKATIBA ndani ya chama hicho,zipo njia sahihi za kufuata ili kurekebisha/kuondoa mapungufu hayo kupitia marekebisho ya KATIBA.Ni kwa nini Dr MKUMBO hakufuata taratibu sahihi ili kukidhi haja zake pamoja wafuasi wake?
Pili,sina mashaka kwamba Dr MKUMBO alisoma na kuielewa ipasavyo KATIBA ya CHADEMA,na ndiyo maana aliweza kuaminiwa na uongozi hadi kuandaa mpango mkakati wa namna ya kupata wabunge wa viti maalumu.Mpango huo ulikubaliwa na chama na umefuatwa hadi leo.Je ni kwa nini viongozi waliaomwamini sasa hivi wanaonekana ni madikiteta.Hakuwana kipindi kile anaaminiwa na kupewa kazi nzito ndani ya chama? Jibu rahisi ni kwamba Dr MKUMBO ni kweli alifuata MKUMBO wa ZZK bila kujua nini anafanya? Kama ni kweli kwamba Dr MKUMBO haakujua alichokuwa anafanya,hii inanifanya niamini yafuatayo "An educated person learns more and more about less and less until he/she learns everything about nothing".
Natumia maneno hayo kwa maana ya kwamba,Dr Mkumbo alikumbwa na upofu (turn of vision) wa kuona nini kitatokea (adhabu dhiki yake na wenzake) baada ya kukiuka KATIBA kupitia WARAKA wake wa Mabadiliko ndani ya chama.Lakini pili, Dr Mkumbo ameonyesha wazi kwamba hawezi kuwa na hoja za nguvu kukidhi kiu za wananachi wanaopenda kujua ni kwa nini alifanya hivyo sababu amekiri mwenyewe kuwa ni mjinga na ana maslahi katika mgogoro huu ndani ya CHADEMA na hapa ninanakiri maneno yake "Sitarajii katika makala haya kukidhi kiu ya watu wengi wanaotamani kujua ukweli wa mgogoro ndani ya CHADEMA na pengine mimi siye mtu sahihi kueleza jambo hili kwa kuwa nina maslahi ya moja kwa moja. Ninatoa changamoto kwa watafiti wa sayansi ya siasa kulifanyia utafiti jambo hili na kuliweka bayana, ili watu wapate kujifunza na kulijua vizuri"
Dr Mkumbo katika aya moja kabla ya aya niliyomkariri amesema yafuatayo "Kwa sababu hii nazipokea lawama zote kwa unyenyekevu pia na ninakubali kwamba nimeshiriki, bila kutarajia, kusababisha usumbufu na kutatiza tamanio na tumaini la mamilioni ya Watanzania katika kuitoa CCM madarakani. Hata hivyo, taswira ya mgogoro huu ni pana kuliko inavyoonekana na pengine tutapata nafasi nzuri zaidi mbele kueleza vizuri kilichotokea katika maandishi ili watu waelewe na waielewe CHADEMA na viongozi wake vizuri, na kuweka kumbukumbu kwa vizazi vijavyo"
Kwa ufupi kabisa katika aya hiyo ni yeye na kundi lake wamesabisha usumbufu kwa wananchi wengi (mamilioni) wenye matumaini na CHADEMA na hivyo napengine atapata nafasi zaidi ya kuueleza umma kwa maandishi.Hii ni katika kutafuta sympathy ya umma,sababu amekiri kwamba hatakidhi kiu ya watu na kuwa yeye ana maslahi katika mgogoro huo. Hoja hapa ni kwa mtu mwenye maslahi atawezaje kuyakinisha mtatizo yaliyotokea? Lakini pia amependekeza kufanyika utafiti ili kubaini kilichotea ndani ya CHADEMA,aidha amesahahu kuwa watafiti wengi ni biased kulingana na maslahi yao binafsi au ya mtu/kikundi kilicho nyuma yake.Kama ni hoja yake ni bora independent committee iundwe kuchunguza mgogoro huo ili tupate majibu sahihi.
Napingana na Dr Mkumbo kuwa ushabiki uliojitokeza kati ya ZZK (kundi lake) na CHADEMA ulikuwa na maslahi ya chama tawala ili kuuamisha umma kwamba vyama vingine si lolote ila CCM pekee.Siyo sahihi kuwa wote waliokuwa/wanamuunga mkono ZZK ni wanachama wa CHADEMA,miongoni mwao ni CCM na vyama vingine pinzani,lakni pia wapo wasio na chama ambao aidha walitaka kuonyesha uungaji mkono walitumika baada ya kushawishiwa na wenzao ama kwa ujira mdogo au kufuata mkumbo.Hii inanipa tafsiri ya kwamba,mgogoro huo si mkubwa kiasi hicho ila umekuzwa tu.Chama kilibaki na ulinzi mkubwa sana,kwani kundi kubwa lilikuwa/lipo kwa CHADEMA,siyo Dr Slaa au Mh Mbowe kama ambavyo Dr Mkumbo anataka umma uamini.
Mwisho,nakubaliana na Dr Mkumbo kuwa njia mbadala zifanyike kusuluhisha suala hili hili nje ya mahakama.Naamini viongozi wa chama watakuwa wanafikiria au wameanza kulifanyia kazi jambo hili kwani wapo watu makini ndani ya chadema.Uzoefu unaonyesha kuwa mediators kupitia mazungumzo humaliza migogoro kwa njia za amani bila kuathiri pande zote.
Inatosha tunahitaji chama mbadala cha ccm na cdm, sasa sijui kitakuja chama gani, nashauri ccm ijisahihishe sana na kujirekebisha iondoe yale malalamiko ya wananchi labda tutapata ccm-original