Dr. Kafumu (CCM) avuliwa ubunge Igunga!

Dr. Kafumu (CCM) avuliwa ubunge Igunga!

Pole sana Bwana Kafumu kwa kushindwa!
Hivi wewe ulitegemea nini kwa maamuzi ya kesi hii? Hebu ngoja nikukumbushe baadhi ya madudu kwenye kampeni za Igunga. Yaliyotokea ni haya hapa:

  1. Jinsi jamaa zako wa CCM walivyoiba kura,walivyoua watu.
  2. Jinsi walivyotumia mali ya serikali zikiwemo Fedha na Magari kwenye kampeni.
  3. Jinsi kina Magufuli walivyotoa ahadi zenye harufu ya rushwa kwa kuahidi kujenga daraja na barabara iwapo Wanaigunga wataichagua CCM.
  4. Jinsi Mkuu wa wilaya alivyokamatwa na Wanachadema akiifanyia CCM kampeni.
  5. Jinsi Mbunge wa Tabora mjini bwana Rage alivyokwenda kwenye kampeni na Bastola.
  6. Jinsi Wabunge wa CCM kina Mchemba na wenzake walivyotumia bastola kutaka kuwateka baadhi ya Viongozi na wanachama wa Chadema?
  7. Jinsi Nchemba alivyokamatwa akifanya zinaa na mke wa kada mwenzake kwenye nyumba za wageni akidai ni kampeni ya kitanda kwa kitanda!

Yako mengine mengi ambayo sina muda ya kuyaorodhesha. Kwa hiyo briefly hii hukumu ya kupigwa chini kwa Dr. Kafumu ilitarajiwa kwa hali yoyote ile. Hata hivyo bado CCM mnaweza kukata rufaa ili haki itendeke kama mnaona mmeonewa.

Wasaalamu.

Jinsi Bakwata walivyotoka povu na tamko lao!
 
Dr Kafumu kasema Siasa tena baaas, hii inamaanisha hatakata rufaa.Ila kama atakata rufaa itabidi kusubiri si chini ya miezi 6 kujua kama kutafanyika uchaguzi mwingine ama la! Jambo ambalo kiu ya wanaigunga kupata Mbunge halali itakua imechelewa sana
 
Mbele ya ofisi ya CDM wilaya ya igunga wananchi wamefurika kufurahia matokeo ya hukumu. muziki unaandaliwa tayari kunogesha furaha hii,.....full shangwe.
 
naona mahakama imetoa hukumu ya aina yake, wengi hawakutegemea ila binafsi sishangai kwani naamini tanzn kuna demokrasia na uhuru japokuwa bado tuna safari ndefu.
Pongezi kwa mahakama.

waliokuwa hawakutegemea ni wale wlaiokuwa hawafuatilii hii kesi....hoja 8 zilikuwa zimesimama sawia na ndizo zilizopelekea kuvuliwa ubunge kafumu kati ya 13
 
Ohooooo, Kumbe Mahakama wanasoma historiaaaaa! Wangefanya kihuni kama alivyofanya wa Arusha, kamuulize zawadi aliyozawadiwa na Mungu anayesikia maombi ya wanaodhurumiwa mchana kweupe.
 
Pro-Chadema JF vipi mahakama imetenda haki Ikulu hawakuingilia uhuru wa mahakama.
 
images

hahahahahahahahahhahahhaha, mbona machozi hayamtoki.
 
first eleven aliomfumua Kamfum na kumponza Kamfumu ni-:
1. Mwigulu
2.Lusinde
3. Nape
4. Magufuli
5. Mkapa
6.DC Hawa
7. Bakwata Igunga
8.Wassira
9. Ester Bulaya
10. aliekuwa mbunge wa Sumbawanga...
11......
11.Alhaj Ismail Aden Maharage
12. John Pombe Magufuli
13. Philip Mangula
14. B.W Mkapa
 
Ngoja tusubili kama kakata rufaa tuingoje au tusubiri uchaguzi mdogo pamoja na wana igunga kulimda kura zao

ila kufumuliwa wakati ulikuwa dalali ina uma sana!

jamani tayari kafumu si mbunge wa igunga tena!kashinje fanya mambo japo kwa muda mfupi!haki ya mtu haiibiwi inacheleweshwa tu!
 
first eleven aliomfumua Kamfum na kumponza Kamfumu ni-:
1. Mwigulu
2.Lusinde
3. Nape
4. Magufuli
5. Mkapa
6.DC Hawa
7. Bakwata Igunga
8.Wassira
9. Ester Bulaya
10. aliekuwa mbunge wa Sumbawanga...
11......

11. Rage a. k.a Mr Bastola, mwenyekiti
 
sasa ile mishahara na posho alizochukua kipindi chote alichokuwa mbunge batili inakuwaje? hebu tujuzane kwa wale wataalamu wa sheria
 
Funzo la leo: 1.Tusibeze mahakama zetu. Yaani penye ushindi ndio tunasema haki imetendeka 2. CCM na vyama vyote vya siasa lazima muwe strategic kusimamisha watu wanaokubalika katika jamii na pia tupige marufuku kampeni zozote (za maji taka) zinazoweza kukidhalilisha chama. Ni mwiko kutumia fedha kujaribu kuwashawishi watu maana vitendo kama hivi huwa vina backfire
 
Muda wa mwajiri Ndo ushaisha.Wacha nikanywe Bia Zangu sasa Raha tele IDD tatu hii!
 
Back
Top Bottom