Acha kabisa LIBIDOZY kwani tofauti kati ya Buberwa na Dr. Ndondi ni sawa na tofauti kati ya Farao na Musa.
Buberwa ni member wa group ya anti-Christ na nina sema hivi kutokana na hotuba zake ambazo hazina hadhi ya kuitwa mahubiri bali KEJELI zinazosababishwa na UPOFU WA KIROHO.
Dr. Ndondi anakusaidia si lazima ukanunue dawa lakini vipindi vyake ni dawa tosha. ni kweli ni mtu muhimu mno katika jamii ya watanzania ingawaje hawa madaktari wetu wa kuchonga wamemkataza kujitangaza kwa kigezo eti SI RUKSA KIMAADILI YA UTABIBU DAKTARI KUJINADI KWA WAGONJWA. Huyu dokta hata kma hana doctorate ya Darasani lakini ni zaidi sana kuliko hawa wanaozeeka au kufa na utaalam wao bila kmnufaisha mtu zaidi ya familia zao.
Wadanganyika kuweni makini sana ...Convicing power anayo na si kila mwenye convicing power anaongea ukweli..kwa tulio somea taaluma huwa tunaona anavyoibia watu kwa kuchanganya changanya maneno...He is a good at marketing tho what he markets is totally a lie...amkeni wadanganyika si kila unachoambiwa ni kweli....ni kama ilivyo internate si kila habari unayoiona kwenye net ni kweli kazi kwako kuchuja,,,,watoto wa mjini wanasema akili kumkichwe.
Ndondi ni kweli ni public speaker mzuri mwenye mvuto na asiyechosha anapokalia kipindi chake sawasawa.
Mwanaume anaongea kama mwanamke!! Tapeli mkubwa mshenzi huyo.
jamani mbavu zanguBinafsi nimekuwa mfuatiliaje wa Vipindi vya Dr Isaack Ndondi kuanzia vile Channel 10 mpaka StarTv. Ukweli ni kwamba kuna baadhi ya mambo ya msingi katika jamii ambayo uwepo wake kwenye screen kumewasaidia wengi. Vipindi vyote hivyo anavifanya kwa gharama zake mwenyewe, kwa hiyo hata gharama zake kimatibabu lazima ziwe juu. Laiti kama watanzania wasingeendelea kuifanya mioyo kuwa migumu na kumsaidia huyu bwana kama basi angekuwa msaada mkubwa jamii
Binafsi huwa napata burudani saaaaafi napokuwa naangalia kipindi chake. Ni zaidi ya comedy . Pamoja na kujaliwa kipaji cha kuongea haraka haraka, pia huwa anajaribu kutumia lugha ambayo inaweza kueleweke kwa kila mtu.[/QUOTE]
umesema pwent. alienda mabibo hostel kutoa mada zake za ujana na uchumba kuelekea ndoa siku ya ijumaa fulani then nadhani jumamosi yake yakatokea yale mauaji ya kinyama. watu hawamsikilizi. kuhusu kutumia lugha. angekuwa muwazi kiivyo ingekuwa balaa hasa kwa watoto. mwenyewe huwa anasema hutumia tafsida hasa yanapokuja mambo ya kiutu uzima. "unamlamba chenga golikipa hadi anakuwa hoi kisha unafunga bao lako saaafi!"
Dah! Old good days dada yetu!Jambo mkuu me nakuogopa sana hayo majicho.
wadau nahitaji contacts za huyu ndugu maana naona meno yanataka kunisumbua. Kuna dawa moja aliitangaza kwenye tv kuhusu kutibu meno permanently
Ukimkosa nenda Loliondo kwani ni yaleyale...utapeli kila kona Tz
Raia fulani, huwa anasema ofisi zake ziko magomeni, jaribu kumtembelae kweny ofisi zake
Huyu Dokta/Mchungaji tena kijana ni mfano wa kuigwa.Napenda vipindi vyake vya redio na TV kwa maana anazungumzia mambo ya maisha ya kawaida kabisa.Kipindi chake cha juzi Jumatano kuhusu namna ya kuchagua mchumba kwa vijana wa kike na kiume kilinivutia sana.Laiti angejiunga hapa akaweza kuchangia hizi mada kwenye jukwaa la mahusiano na JF Dr.
Watanzania bwana, siku moja niliwahi kumsikiliza huyo Dk. Ndondi akizungumzia kuhusu digestive system ya binadamu, nilicho sikia humo sikuamini masikio yangu - nakajiuliza hivi huyu mtu anajuwa anacho zungumza humu lakini! Je anajuwa kwamba kuna watanzania wengi wanao juwa vizuri maswala hayo vizuri tu na siyo kuleta mambo ya "SANGOMA"
Mwishowe nika-conclude kwamba huyu mtu kitu anachofanya ni kusoma vitabu tu kuhusu vyakula na athali zake lakini uelewa wake kuhusu jinsi ya internal organs za binadamu zinavyo fanya kazi ni mdogo sana, sema Mungu amemjalia kuwa a good orator (mzungumzaji/muhigizaji).
Kama wenzangu walivyo zungumza kwenye forum hii tatizo letu watanzania ni wavivu wa kusoma, matatizo yote kuhusu vyakula, magonjwa, madawa na ushauri wa bure wa kisayansi kutoka kwa watu walio elimika kweli kwenye fani hizo vyote hivyo vinapatikana humu kwenye internet huitaji watu wenye questionable qualification kukupa ushauri.
Chunga sana watu wanao sema dawa ya kutibu ubongo tunayo, yakutibu ini tunayo, yakurudisha uterus hata kama hilitolewa na mdaktari tunayo, kongosho tunayo, enzymes zote tunazo, red/white cells tunayo, serum tunayo; in short take heed of master of all trade it may cost you an arm and leg at the end of the DAY.
Sikatai wasifanye kazi zao lakini wa ache ku-exaggerate huwezo wao wakumbuke watanzania wa sasa hivi siyo wa miaka ya arobaini na SABA, alafu anapo zungumza kwenye radio au television anapashwa kuwa mwangalifu anayo yaongea, nampa ushari huo wa bure, kama yeye ni Mtu wa Mungu anapashwa kuwa mkweli anayo yajuawa/yaweza aseme anayajuwa hasiyo yajuwa vizuri hakili kwamba kusema kweli hayajuhi kiundani, hakuna atakaye mcheka.