Huyu mwandishi inaonekana ana maslahi na Mshinda. Ameacha historia ya shule za nyuma akarukia Masters. Alibebwa maana zamani ilikuwa huruhusiwi kusoma PhD bila Bachelor degree. Na unasomaje masters bila kuwa Bachelor? Ndiyo hayo hayo ya Executive Masters degree zitolewazo na Mzumbe. Hopeless. Mtu hana basic degree anarukia Masters!! Sawa na gap ya form six, utamuona mtu anbaye hajasoma A level hata kama ana PhD!!! Najua mtatukana,
Inategemea alisoma nchi gani hiyo Masters, kwa kuwa miaka ya nyuma kwenye nchi nyingi za Ulaya mashariki na magharibi hawakuwa na Bsc wala MA, bali ulikuwa na unasoma unagraduate na Masters (Miaka mitano ya kusoma). Nchi kama ujerumani, Bulgaria, Polanda Scheck,). Hata leo ujerumani kuna vyo bado vina mfumo huo wa Masters unasoma miaka mitano kwa kuwa inajumuisha masomo yote ya awali na yale ya ngazi ya juu.
Nadhani alistahili kuwa DG wa NIMR kuliko kupelekwa COSTECH. Simfahamu Mshinda kama mdini ama la,lakini lazima niseme wanasayansi wetu wengi walioko katika Taasisi za utafiti wamejisahau sana. Mfano ni TPRI Arusha ambayo huwezi jua wanafanya nini siku hizi. Nakumbuka kuna kipindi aliteuliwa mkurugenzi mmoja(mtanzania)aliyekua amejipatia sifa kubwa huko Japan,alipofika TPRI akapigwa vita na wakurungezi na senior staffs waliokua wamezoea ubangaizaji wa kitanzania. Kwa hiyo naelewa kama Mshinda alitimua hao wakurungezi maana watakua walikua kikwazo katika Taasisi.
Sasa wewe Mchungaji Masa kama ungelikuwa Muislaam, sasa hivi ungelikuwa boss wa Costech 🙂 Wewe ukaenda kuwa Mchungaji.
Hili shirika lilikuwa kubwa na linatisha enzi za Prof. Kayumbo.
Sasa hivi bora liende.... RIP COSTECH.
Hizi thread imejaa wivu na choyo tu Mimi ni mkristu halafu niko katika sekta ya afya hapa nchini lakini namkubali Dr Mshinda kuwa ni mtendaji ambaye amebobea katika tafiti za Malaria na dunia inatambua hata kama baadhi ya wana JF walio COSTECH hawamkubali. Kuhusu kutoka Diploma kwenda Msc hakuna cha ajabu bali inategemea chuo kimachotoa Msc kinavyokitambua chuo alichosomea hiyo Diploma yake. Naomba niwahakikishie vijana wanaofikiri eti ukiwa BA au Bsc ya chuo cha Tanzania basi unaweza kwenda kusoma chuo popote hapa duniani kama Oxford au Bradford au Cambridge! Si kweli bali lazima uwepo uhusiano wa kiacademia kati ya vyuo hivyo ambapo mitaala ya vyuo vyote viwili huwa shared mutually. Ninawafahamu waalimu wangu wenye Bachelors degree 2 yaani moja toka UDSM enzi hizo na moja toka chuo cha Birmingham ndiyo wakaruhusiwa kufanya MBA. Kwa hiyo hakuna automation ya kwamba sijui nina Bsc au BA ya chuo fulani Tanzania basi nitakubaliwa kwenye chuo chenye reputation UK au US, No labda uende vyuo vya mitaani.
Nikirudi kwenye hoja Dr Hussein Mshinda alisoma Diploma ya Lab hapo Muhimbili ikiwa chini ya UDSM na chuo alichokwenda kufanya Msc kilikuwa kina itambua UDSM kwa hiyo wakapitia mtaala wa hiyo Diploma wakamuona anafaa kufanya MSC. Katika uteuzi wake swala la dini halipo kabisa bali ni excellency yake kwenye performance. Tena nakumbuka COSTECH inabidi ifurahie ujio wake kwani kuna tafiti moja ya Malaria toka kwa wafadhili aliyoiandikia akiwa IHI ilipoletwa ilikuja kwa jina lake na akaiingiza hapo COSTECH kwa vile walikubali kui finance kwa kutegemea usimamizi wake. Huyu atawafaa COSTECH kwa kuwa mutakuwa busy na tafiti kuliko mulivyokuwa wakati wa Pr Kohi ambapo paligeuka kuwa kijiwe cha mission town.
Sikonge,
Sikutegemea kauli kama hii kutoka kwako.
Btw maoni yako ni yepi katika uteuzi na utendaji wa Daktari Mshinda? Hasa hili la elimu una lolote la kusema?
Mimi sina shaka na uwezo na qualification za Dr. Mshinda japo aliruka from Ad Dipl na kufanya MSc kwa kukingiwa kifua na Waswiss hasa Prof. Marcel Tanner wa Basel University.
Hayo machapisho yote kwenye peer review journals mengi amekuwa co-author sio kwamba kwasababu ame-contribute scientifically kwenye hizo papers lakini tu kwasababu alikuwa head wa IHI. It is WRONG lakini ndivyo Taasisi za Utafiti Tanzania zinavyoendeshwa. Wazungu wanatufahamu na wanafanya hivyo.
Mtu ambaye pamoja na sasa hivi kuwa head wa IHI lakini anafanya sayansi (utafiti) bila kubebwa na cheo chake ni Dr. Abdullah Salim. Huyu Mzanzibari ni kichwa, hata Mshinda anamfahamu na anamuheshimu sana kwasabbu ya uwezo wake. Ni Wanasayansi wacahache sana Tanzania wanaoweza kuchapisha tafiti zao kwenye majarida kama NATURE, LANCET etc as first author lakini Dr. Salim amefanya hivyo hata kabla hajawa head wa IHI.
Let a SPADE CALL A SPADE Weakness kubwa ya Dr. Mshinda ni UDINI. Mshinda ni MDINI wa kutupwa, uliza jamaa wote waliofanya kazi naye IHI. Hutakiwi kuwa a rocket scientist kujua kwamba huo UDINI ndiyo pia utakaotokea hapo COSTECH. Sio kwamba haya ni majungu because alishaambiwa in BLACK and WHITE mbele ya Prof Marcel Tanner, Mzungu in a soft laguage akamwambia afanyie kazi hizo tuhuma.
Ugonjwa wa UDINI wa Dr. Mshinda ni miaka nenda miaka rudi, ameshindwa kujirekebisha.
Kwa mara nyingine umeshindwa kuthibitisha tuhuma hizo, pia rudi ukaangalie ni vigezo gani mtu anakuwa co-author katika published article, sio kweli kwamba kwa kuwa director mtu automatically anakuwa co-author, kila journal inaainisha contribution y mtu katika chapisho lolote. niambie ni journal gani ambayo mtu anakuwa automatically co-aothored kwa kuwa director, sio kweli hata kidogo watu wengine wanakuwa acknowledged to incase hawakucontribute effectively.
Acha ubabaishaji na chuki binafsi katika hili.
Nasubiri majibu yako, na ukitaka nitakupa giidelines za hayo majournal yote kuwa co-aothored.
Kama hujui sema sijui sio kudanganya watu
Nilivyosikia ni kuwa kulikuwa na RUSHWA katika kupitia scientific proposal za research zinazowasilishwa COSTECH kwa ajili ya kupatiwa fedha. Nadhani mnakumbuka kuwa kuna fedha 1% ya GDP iliyokuwa imeahidiwa na serikali, japo haikutoka yote COSTECH walipatiwa kiasi fulani. Sasa ninavyosikia hiyo fedha ndiyo imewaondoa.
Tatizo lao ilikuwa ili proposal ya mtu ipite ilikubidi utoe % fulani kwa hao wadau.
Ila kimsingi Dr. Mshinda ni KICHWA!! Tafuta CV yake utaona.
Huyu DG amewafanyia fitna wakurugenzi wote waliopo chini yake mpaka wamehamishwa COSTECH. Yaani wakurugenzi wote waliopo chini yake na baadhi ya senior employees ambao aliona wanamwekea kiwingu amewafanyia zengwe mpaka wizara ikawaondoa COSTECH.
Ninazungumzia wafanyakazi wa COSTECH 15 wameondolewa pale kwa wakati mmoja. Hawa ni watu ambao walimkaribisha Dr. Mshinda pale COSTECH na kumfundisha kazi miaka 3 iliyopita. Leo hii ameota mapembe na kuwafanyia fitna. Na sasa wakurugenzi hawa wameenda kupewa "desk" tupu katika wizara nyinginezo.
Sasa sijui amefanya hivyo kwa kusudio gani?....Kwa sababu, kuwafukuza wakurugenzi 15 kwa mpigo kuna walakini!! Isitoshe huyu jamaa aliingia COSTECH akiwa ha-qualify kabisa na hiyo post a U-DG. Alipachikwa kwa kupitia memo tu...
By the way, Dr Mshinda ni cousin (au nephew) wa IGP Said Mwema, ambaye ni Shemeji wa Kikwete go figure !!
This is what I got from everywhere you google the name. Take care of the initial education. Kila unapoangalia ananzia Masters... hutaona Bachelor wala shule ya nyuma ya bachelor. Uliza halafu utafunika uso kwa aibu.Acha uongo na chuki binafsi...namjua Dr. Hassan Mshinda personally kama rafiki na pia likuwa boss wangu!
Google profile ya Dr Hassan Mshinda halafu niambie kama katika 'top ten' ya scientist wa Tanzania hatakuwepo! He is a PhD holder, Malariologist, research guru, with hundreds of research publications in 'internationally accredited' journals. Ana awards nyingi tu katika uwanja wa research kutokana na kazi zake katika malaria.
.........................................
Ndg Mlaki si ameshastaafu halafu huyu ni mtaalamu wa records management tu au librarian iweje ajiongeze abuni miradi yote ya jengo la costech kweli wachaga wanatisha.Aliyeandika huu UPUUZI atakuwa si Mtanzania na tena hata ART hakusoma achilia mbali SCIENCE. Huwezi kuwa Mtanzania wa kweli ukaukimbia ukweli na kutaka uungwe mkono katika upuuzi wako eti kisa DINI. Hizi ni shield-guards mufilisi za wasio na hoja bali vioja. Na ukitaka kuwa domo la Wanasayansi ni vema utambue vizuri kanuni, taratibu na lugha za Ki-sayansi. Wanasayansi wa kweli hawaongei wala kuongelewa kwa hoja lojolojo kama za huyu Quemu.
Bahati nzuri naifahamu COSTECH kitambo na kiundani kiasi. Kabla ya Dr. Mshinda kuletwa hapa, COSTECH kilikuwa kijiwe kwa maana ya kijiwe cha uswazi; mahala pa watu kupata ghahawa na kashata. Ilikuwa kama anwani tu ya Wapi Utampata a, b, au c. Waliokuwa wajanja kama T. Mlaki wakatumia kijiwe ilivyo kujinufaisha kimaslahi. Vitu vingi ikawa ni shaghala-baghala. Kohi pamoja na elimu zake zote (U-Dokta, U-Profesa, n.k) na vyeo (Jenerali, DG, n.k) akafunikwa na Mlaki. T. Mlaki akawa kama ndiye DG wa COSTECH. Miradi mingi sana imeanzishwa na Mlaki huku DG akiwa hajui kitu. Na nchi wafadhili nyingi zilidhani Mlaki ndiye DG. Na Mchaga hakufanya kosa. Palipo na upenyo anafanya kweli.
Can you imagine:
Wengi mmeandika kuhusu uwezo mkubwa wa Dr. Mshinda kwa kurejea mafanikio yake pale Ifajara. Nami ninaafiki na siongezi wala kupunguza; salute kwa Dr. Mshinda.
- COSTECH litoe huduma kama ISP na hakuna mtu ndani ya shirika anajua nani analipwa?
- Jengo zima la serikali, hazina ya Tafiti za Kisayansi lipigwe rangi za matangazo ya Vodacom na bado waliomo wajione wana hadhi?!
Hawa wanaojiita wanasayansi 15 mie napenda tuwaite wanafunzi 15. Wanasayansi gani toka wamehitimu hizo PhD, MSc hawajawahi kushiriki au kuandika wenyewe Tafiti hata moja? Wakiandika basi wameshirikishwa! Ni Aibu Wanataka waitwe wanasayansi, wapewe na vyeo vya mseleleko na heshima wasiyostahili. Sasa hakuna mseleleko wala heshima bila ku-publish. Baadhi ya hawa wanaojiita wanasayansi 15 walishindikana hata huko kwenye vyuo vya elimu ya juu wakafukuzwa. Wana matatizo kweli kweli.
Huyu Quemu na wote wanaokimbilia hoja mfu za UDINI wanatia hasira kweli. Wanawanyima moyo hawa watu wema, Wazalendo na washapakazi. Hatupaswi kuwaendekeza. Lazima JF Admn nayo ione haja ya kuwaongeza watu wa namna hii kwenye vifungo (BAN). Wanaitia sana hasara nchi kwa kuikwamisha kuiletea maendeleo kwa kuwagawa watu.
Nashukuru Quem amepata majibu yanayomstahili. Arudi akawaambie wanafunzi wenziwe kuwa vioja vyetu vimebainika. Badala ya kumpaka tope Dr. Mshinda tumesababisha watu wamtambue zaidi kwa mshango wake mwema kuiendeleza nchi.