Dr. Hassan Mshinda, DG wa COSTECH...


Sitaki ku koment maeneo mengine ya tuhuma hizi kwa kuwa siyajui. Ila Saidi Mwema asili yake ni Mngazija wa Comoro na mama yake ni mchaga ila Saidi mwenyewe alikulia ujombani kwake Moshi.... hivyo kwa kukiri kama Dr. Mshinda naye ni Mngazija inawezekana kweli kuna uhusiano wa kidugu kati ya Saidi na Hassan.

Kikwebo.
 
chonde chonde msituharibie jamvi ligeuke sehemu ya majungu, Dr Hassan Mshinda ni mmoja kati ya wana sayansi wachache ambao tunajifunia. namfahamu kidogo Dr mshinda, naomba niwaambie kitu ambacho labda hamkijui. mimi binafsi ofisi yangu ipo hapa jengo la costec
Dr hassani ameingoza ifakara health center kwa mafanikio makubwa sana na wakati huo huo costech ilikuwa chini ya mwanajeshi jeneral cohi , hakukuwa na lolote la maana, watu wengi sana walijaa maofisini nafasi moja watu wawili mpaka watatu, jaribu kufikiri bosi mmoja alikuwa na sekretari wawili, jaribu kufikiri
upande wa account kulikuwa na watu kumi na mbili jaribu kufikiri
vijana wanaofanya usafi zaidi ya kumi na tano na wakimaliza usafi asubuhi basi wanakuwa wapo wapo tuuuuuu mpaka tena kesho
kwa ufupi ofisi ilikuwa inaboa sana watu wanaacha makoti asubuhi then wako kwenye mishe mishe, sasa alipokuja Dr mshinda kapunguza nafasi zisizo na ulazima, mfano akapunguza watu wote ambao walikuwa na elimu ya darasa la saba zaidi ya watu 30 walipungua unaweza pata picha kulikuwa na kusanyiko la aina gani.
then akapunguza nafasi zote ambazo zilikuwa zinashikiliwa na watu zaidi ya wawili. na kwa muda wa miaka mitatu aliyokaa ameweza kurekebisha mahali hapa hata nidhamu ya kazi imerejea sana tu.
na juzi hapa mfuko wa bill and gate wameahidi kutoa 100biln kwa ajiri ya miladi ya utafikti hivyo dr mashinda anahitaji wataalam ili wakamilishe hii miladi , kwa sasa kuna vijana wadogo wengi zaidi ya 40 wengi ni fresh frm college wapo hapa wanapiga kazi, hawa wakurugenzi unaowasema hawaendani na kasi ya Mshinda ndio maana wamepelekwa huko wakaendelee kufika ofisini saa 4 na kusoma magazeti . mshinda anastahili pongezi sio lawama
 
Dr Mshinda ndio ni mwanasayansi mzuri lakini huyo jamaa anafitina sana,nakumbuka hata Dr Andrew Kitua alipokuwa mkurugenzin wa Ifakara alikuwa anamfanyia fitina sana,pia alikuwa anapigana kufa na kupona awe mkurugenzi wa NIMR,akaukosa fitina anajua
 
Kumbe ni daktari wa binadamu. Nadhani the best place for him would be NIMR or his former place, IHI. Pale COSTECH angewekwa mtu wa fani tofauti na hizi za kutoa fenegani
 


umesomeka mkuu
 
Mh, nimeshangaa sana kukutana na mtu anaye challenge utendaji wa Mshinda. Namjua vizuri sana Hassan Mshinda, sio mdini kiasi hicho maana aliajiri watu wengi tu IHI ambao sio Waislam. Mshinda anataka mtu mchapa kazi sio kuzuga ofisini. Tuache majungu jamani.
 
kusema ukweli na mimi nasikia Mshinda ni kichwa. na nimeshahudhuria mikutano ambayo yeye ni mshiriki au facilitator. He is good technically.
problem ambaye watu wanamuongelea ni UDINI, hilo nimelisikia hasa alipokuwa Ifakara Health institute.
 
mtu akiwa na lake analibwaga hapa ili watu wamalizane, acheni hizo ndugu, MUNGU anayajua hayo.
 
Kwa wafahamu IHI - Ni yapi MAFANIKIO yake dhidi ya Malaria? Maana mpaka sasa Malaria ni ugonjwa unaoua sana especially under 5!
 
Mshinda kweli ni kichwa, lakini tufike mahali tutofautishe kazi za research na mambo ya utawala!!!!!!!!, mdau hebu tupe majina ya waliohamishwa , inawezekana ni watu ambao cv zao tunazijua.
 
Tupe orodha ya waliohamishwa ili nao tu google profile zao,ila hii habari ya kusema kwa vile ana PHD ndo kuwa kichwa haina uhusiano na zengwe kama kweli lipo kuna maprof kibao tu lakini maamuzi yao ukiyasikia utatamani usiku ufike haraka ukalale.
Kuna mmoja sipendi kumtaja alifanya utafikti kule morogoro kuhusu dawa ya kuua wadudu waharibifu wa mazao badala ya dawa ile kuua wadudu iliwavutia zaidi kula mazao,badae nasikia ni mtu mzito kwenye system,tz bana.
Nadhani wangine wanashabikia kwa vile kasomea liverpool hata kama angesomea ARSENAL perfomance na efficincy ndo kipimo.
 
sisi tuliowahi kufanya kazi na costech tunaweza kusema kuwa pale walikuwa wanafanya kazi kwa mazowea, labda mabadiliko makubwa kama hayo yanaweza yakawasitua na kufanya kazi kwa misingi ya haki na ukweli, just imagine unaandika barua ya kuomba kibali kufanya utafiti ukiwa nje ya nchi, haujibiwi, unakuja mwenyewe in personal unaletewa longolongo kibao, watu wamekaa kwenye viyoyozi tu hawafanyi kazi, hebu tuone na hao wapya kama wataendana na standard za Dr. Mshinda km waliofanya naye kazi wanavosema, natusubiri!!!
 
Huyu mzee kwa .... na Udini ndiye mweneywe, Uliza pale Ifakara health Institute

Ukitaka kujua upeo na uwezo wa mtu kujibu na kuchangia hoja, angalia anapojengea hoja zake.Huyo Dk Hassan Mshinda una hakika kama ni Muislamu? Unaswali naye Msikiti gani? Wenzako kuna wakati waligundua majina si kitu, wakasema kuanzia sasa hawataangalia majina.
Kuna Wakristo nawafahamu wana majina ya "kiislamu" na hawajawahi kuwa Waislamu .
Wako Mafisadi waendao kanisani na hawatetewi hapa?
 
kusema ukweli na mimi nasikia Mshinda ni kichwa. na nimeshahudhuria mikutano ambayo yeye ni mshiriki au facilitator. He is good technically. problem ambaye watu wanamuongelea ni UDINI, hilo nimelisikia hasa alipokuwa Ifakara Health institute.

Mshinda has to go. Tatizo lake sio Udini. ni jina lake. Ni Uislam.

Baada ya Dr Idrisa Rashid kuondoka Tanesco nadhani huyu anafaa kuwa next target. Kuna Dr Dau pia ila naona kawa mgumu licha ya makelele!
Unajua problem ya wagalatia wengi wa nchi hii hawataki kuamini kwamba wapo waislam waliosoma. Na ilivyo Muislam akipewa post ya juu anafanya kuweli. Maana hadi anafika hapo ujue kaingia kwa sifa. Hakuna kubewa huko. Tafakari kidogo.

Kibaya zaidi wagalitia hamuwahamasishi hao jamaa zenu kufanya kazi. Hebu angali huo mzigo uliowekwa pale Tanesco baada ya Dr Idrissa kuondoka. Tazama uharo aliofanya Balali pale BoT baada ya kuondoka Dr Idrissa. Tengeneza list ya mafisadi wa nchi uone imejaa kina nani!

Acheni kilialia wagala, fanyeni kazi!

Shame on you wavivu wa kufanyakazi na kufikiri. Mmeiua nchi kwa ubinafsi na sasa mnajenga chuki na wachapakazi kwasababu ya majina yao tu!!
 
Mwaga source and names plse..by the way hivi ni kweli kuwa our first lady ni mmachame!! kwani kinachofahamika ni kuwa IGP ni mchaga wa Machame.
 


Aliyeandika huu UPUUZI atakuwa si Mtanzania na tena hata ART hakusoma achilia mbali SCIENCE. Huwezi kuwa Mtanzania wa kweli ukaukimbia ukweli na kutaka uungwe mkono katika upuuzi wako eti kisa DINI. Hizi ni shield-guards mufilisi za wasio na hoja bali vioja. Na ukitaka kuwa domo la Wanasayansi ni vema utambue vizuri kanuni, taratibu na lugha za Ki-sayansi. Wanasayansi wa kweli hawaongei wala kuongelewa kwa hoja lojolojo kama za huyu Quemu.

Bahati nzuri naifahamu COSTECH kitambo na kiundani kiasi. Kabla ya Dr. Mshinda kuletwa hapa, COSTECH kilikuwa kijiwe kwa maana ya kijiwe cha uswazi; mahala pa watu kupata ghahawa na kashata. Ilikuwa kama anwani tu ya Wapi Utampata a, b, au c. Waliokuwa wajanja kama T. Mlaki wakatumia kijiwe ilivyo kujinufaisha kimaslahi. Vitu vingi ikawa ni shaghala-baghala. Kohi pamoja na elimu zake zote (U-Dokta, U-Profesa, n.k) na vyeo (Jenerali, DG, n.k) akafunikwa na Mlaki. T. Mlaki akawa kama ndiye DG wa COSTECH. Miradi mingi sana imeanzishwa na Mlaki huku DG akiwa hajui kitu. Na nchi wafadhili nyingi zilidhani Mlaki ndiye DG. Na Mchaga hakufanya kosa. Palipo na upenyo anafanya kweli.

Can you imagine:
  • COSTECH litoe huduma kama ISP na hakuna mtu ndani ya shirika anajua nani analipwa?
  • Jengo zima la serikali, hazina ya Tafiti za Kisayansi lipigwe rangi za matangazo ya Vodacom na bado waliomo wajione wana hadhi?!
Wengi mmeandika kuhusu uwezo mkubwa wa Dr. Mshinda kwa kurejea mafanikio yake pale Ifajara. Nami ninaafiki na siongezi wala kupunguza; salute kwa Dr. Mshinda.

Hawa wanaojiita wanasayansi 15 mie napenda tuwaite wanafunzi 15. Wanasayansi gani toka wamehitimu hizo PhD, MSc hawajawahi kushiriki au kuandika wenyewe Tafiti hata moja? Wakiandika basi wameshirikishwa! Ni Aibu Wanataka waitwe wanasayansi, wapewe na vyeo vya mseleleko na heshima wasiyostahili. Sasa hakuna mseleleko wala heshima bila ku-publish. Baadhi ya hawa wanaojiita wanasayansi 15 walishindikana hata huko kwenye vyuo vya elimu ya juu wakafukuzwa. Wana matatizo kweli kweli.

Huyu Quemu na wote wanaokimbilia hoja mfu za UDINI wanatia hasira kweli. Wanawanyima moyo hawa watu wema, Wazalendo na washapakazi. Hatupaswi kuwaendekeza. Lazima JF Admn nayo ione haja ya kuwaongeza watu wa namna hii kwenye vifungo (BAN). Wanaitia sana hasara nchi kwa kuikwamisha kuiletea maendeleo kwa kuwagawa watu.

Nashukuru Quem amepata majibu yanayomstahili. Arudi akawaambie wanafunzi wenziwe kuwa vioja vyetu vimebainika. Badala ya kumpaka tope Dr. Mshinda tumesababisha watu wamtambue zaidi kwa mshango wake mwema kuiendeleza nchi.
 
Kwa wafahamu IHI - Ni yapi MAFANIKIO yake dhidi ya Malaria? Maana mpaka sasa Malaria ni ugonjwa unaoua sana especially under 5!

Hii thread haitoshi kuongelea mafanikio ya Dr Mshinda..google na utaona hundreds of pages!

Wewe huifahamu IHI...kama unaifahamu IHI hutakosa kujua kuwa 'IHI is Dr Mshinda'! Thats the best way I can put it! Tangu inaanza kama Swiss Tropical Institute Field Laboratory (STILF, nenda Ifakara mpaka leo waNdamba wabaita hivyo ofisi za IHI)...ikaja kuwa IHRDC na finally IHI. Ukisema Dr Mshinda ni mdini sijui una maana gani? Yes ni muIslam swala tano, lakini udini (kwa ninavyoelewa mimi) sio kumcha mungu wako..bali ni kuwabagua wenzako kwa dini zao ukipendelea wale wenye kama yako! IHI ilipanuka haraka akiwa mkurugenzi toka wafanyakazi less than 100 to 600, na ilifanyika survey ya profiles za wafanyakazi ili kujua human resource capacity kutegemeana na kazi/miradi inayokuja kwa wingi IHI...Christians waliku almost two-thirds (karibu 66%) ya staffs wote, sasa udini upomwapi hapo? Na kulikuwa hakuna mNgazija mwingine zaidi yake!


Dr Mshinda alipanua IHI toka kuwa na field offices 2 (STILF Ifakara na Rufiji) mpaka kuwa 5 accredited centre (Ifakara, Rufiji, Bagamoyo, Mtwara na Dar es salaam), kufungua demographic surveilance sites 3 Africa (Kilombero, Ulanga, Rufiji) na kaondoka akifungua ya 4 Kigoma (hii ndio iliyompa uwenyekiti wa INDEPTH Africa)...Bagamoyo centre ilifunguliwa chini ya uongozi wake is one of the centres of excellence for clinical research in Africa...IHI has an accredited entomological lab (Ifakara) in Africa, and a very strong entomology team...etc! Ingia hapa uone mafanikio ya IHI Mshinda akiwa DG, na mafanikio ya Mshinda binafsi kama mwanasayansi: www.ihi.or.tz
 

Tatizo ni jina au dini? Hili jina ni la dini gani JAKAYA KIKWETE ?
 
Aliyetuma hii thread inaonekana amekutana na panga hilo au nduguye. Aseme ukweli inawezekana hao wakurugenzi walikuwa mzigo, wapinzani wa DG huyo au walikuwa na makundi na hivyo kufifisha maendeleo ya taasisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…