Leo katika kipindi cha tuongee asubuhi,nimemsikia makam mkuu wa chuo wa sauti akiwalaumu na kuwakashifu waislaam kuwa ndio
waliofanya ugaidi wa Arusha.Kaongea kwa hisia kubwa mithili ya mtu mwenye kuwafahamu waliohusika na tukiohilo. Kimsingi mwalimu wangu kakurupuka,na kaonyesha udhaifu mkubwa katika hoja yake kiasi kwambakaweka pembeni usomi wake na kutawaliwa na ushabiki wa kidini na kisiasa. Hapo ndipo tunapata tofauti ya msomi na usomi, nampinga kwa hoja zifuatazo
1.Migogoro na chuki ipo pia miongoni mwa wakristo kwani hata wao ni binaadamu. Mfano hivi karibuni kulitokea mgogoro wakati wa kumsimika Askofu wa Anglican kanda ya magharibi(Rukwa) kwa waumini kupinga uteuzi wa askofu huyo, matokeo yake watu walifanya fujo na wakaamuliwa kwa mabomu ya machozi yaliyopigwa na FFU.
2.Pia hivi karibuni tulishuhudia kashfa iliyomkumba Padri wa kanisa katoliki akiwa kafumaniwa na mke wa muumini wake nyumbani
kwake.je huyu mume wa huyo mama aliridhika kwa kitendo kilichofanywa na Padri wake? Je kama angemkuta peke yake bila mashahidi na akaamuwa kumchoma kisu au risasi nani ambae angeamini kuwa hakuuawa na waislaam? Je mwalumu wangu angekubari kuwa Padri kauawa na muumini wake?
3.Hivi karibuni Dunia imeshuhudia PAPA Benedicto akijiudhuru na wachambuzi wa duru za kimataifa wamekiri kuwa kanisa lilikumbwa na mgogoro mkubwa uliopelejea Papa kujiudhuru, lakini kabla ya Papa huyo kujiudhuru yupo Papa aliwahi kupigwa risasi akiwa ndani ya Vatican. Je haya nayo yamesababishwa na waislaam.
4.Tukio la juzi bristo lilihusishwa na uislaam lkn baada ya uchunguzi kufanyika FBI wamejiridhisha kuwa hakuna mwislaam alie husika.
5.Mauaji ya kimbali ya rwanda na Burundi, engeneers walikuwa maaskofu na mapadri na wala si mashekh ingawa
wapo huko Burundi na Rwanda, na ushahidi kuwa maaskofu walisababisha machafuko ya Rwanda na Burundi, ni kuwa wao ndio mpaka leo wanajibu mashtaka mahakama ya kimataifa ya ICC. Nahitimisha kwa kuwaasawatanzaniwa wenzangu kuwa swala la kufanya mauaji linaweza kufanywa na mtu yeyote bila kujali dini yake, ndio maana wapo majambazi wakristo, waislaam na wapagani, Hivyo kuwamilikisha dini fulani na matendo ya mauaji ni kuwaficha na kuwalinda wahalifu toka dini nyingine. Victor Ambrose ndio mtu wa kwanza kukamatwa tena waumini waliokuwepo kwenye tukio ndio waliomkamata na kutaka kumuua polisi ndio waliomuokoa, huenda alihusika au hakuhusika lakini tusubiri vyombo vyadola vifanye kazi yakena huo ndio utawala wa sheria. Baada ya ugunduzi wa rasilimali kadhaa kama vile Gesi, mafuta,uraniam na madini mengine, dunia inatamani kuona Tanzania inakiwa na machafuko kama ilivyo DRC, Angola lengo lamabepari ni kutugombanisha ili wafanye uporaji kama wanavyopora huko DRC ambapo wamepageuza shamba la bibi, tuwakatae wNasiasa wenye nia mbaya na taifa letu bila kujàli wanatokea, pia tuwakatae viongozi wa
dini wanaotumiwa na mabeberu kwa lengo la kutumia ushawishi wao ili kuivuruga amani yetu, mungu ibariki Africa ,mungu ibariki Tanzania yetu.