Leo katika kipindi cha tuongee
asubuhi,nimemsikia makam mkuu wa
chuo wa sauti akiwalaumu na
kuwakashifu waislaam kuwa ndio
waliofanya ugaidi wa Arusha.kaongea
kwa hisia kubwa mithili ya mtu mwenye
kuwafahamu waliohusika na tukio
hilo.kimsingi mwalimu wangu
kakurupuka,na kaonyesha udhaifu
mkubwa ktk hoja yake kiasi kwamba
kaweka pembeni usomi wake na
kutawaliwa na ushabiki wa kidini na
kisiasa.hapo ndipo tunapata tofauti ya
msomi na usomi.nampinga kwa hija
zifuatazo 1.Migogoro na chuki ipo pia
miongoni mwa wakristo kwani hata wao
ni binaadamu .mfano hivi karibuni
kulitokea mgogoro wakati wa
kumsimika Askofu wa Anglican kanda
ya magharibi(Rukwa) kwa waumini
kupinga uteuzi wa askofu huyi.matokeo
yake watu walifanya fujo na
wakaamuliwa kwa mabomu ya machozi
yaliyopigwa na FFU. 2.Pia hivi karibuni
tulishuhudia kashfa iliyomkumba Padri
wa kanisa katoliki akiwa kafumaniwa na
mke wa muumini wake nyumbani
kwake.je huyu mume wa huyo mama
aliridhika kwa kitendo kilichofanywa na
Padri wake?je kama angemkuta peke
yake bila mashahidi na akaamuwa
kumchoma kisu au risasi nani ambae
angeamini kuwa hakuuawa na
waislaam?je mwalumu wangu
angekubari kuwa Padri kauawa na
muumini wake? 3.Hivi karibuni Dunia
imeshuhudia PAPA Benedicto
akijiudhuru na wachambuzi wa duru za
kimataifa wamekiri kuwa kanisa
lilikumbwa na mgogoro mkubwa
uliopelejea Papa kujiudhuru,lkn kabla ya
papa huyo kujiudhuru yupo papa aliwahi
kupigwa risasi akiwa ndani ya
vatican.je haya nayo yamesababishwa
na waislaam. 4.Tukio la juzi bristo
lilihusishwa na uislaam lkn baada ya
uchunguzi kufanyika FBI wamejiridhisha
kuwa hakuna mwislaam alie husika.
5.Mauaji ya kimbali ya rwanda na
Burundi,engeneers walikuwa maaskofu
na mapadri na wala si mashekh ingawa
wapo huko Burundi na Rwanda.na
ushahidi kuwa maaskofu walisababisha
machafuko ya Rwanda na Burundi,ni
kuwa wao ndio mpaka leo wanajibu
mashtaka mahakama ya kimataifa ya
ICC. Nahitimisha kwa kuwaasa
watanzaniwa wenzangu kuwa swala la
kufanya mauaji linaweza kufanywa na
mtu yeyote bila kujali dini yake.ndio
maana wapo majambazi
wakristo,waislaam na wapagani.hivyo
kuwamilikisha dini fulani na matendo ya
mauaji ni kuwaficha na kuwalinda
wahalifu toka dini nyingine.Victor
Ambrose ndio mtu wa kwanza
kukamatwa tena waumini waliokuwepo
kwenye tukio ndio waliomkamata na
kutaka kumuua.polisi ndio
waliomuokoa.huenda alihusika au
hakuhusika lkn tusubiri vyombo vya
dola vifanye kazi yakena huo ndio
utawala wa sheria. Baada ya ugunduzi
wa rasilimali kadhaa kama vile
Gesi,mafuta,uraniam na madini
mengine.dunia inatamani kuona
Tanzania inakiwa na machafuko kama
ilivyo DRC,Angola .lengo lamabepari ni
kutugombanisha ili wafanye uporaji
kama wanavyopora huko DRC ambapo
wamepageuza shamba la
bibi.tuwakatae wNasiasa wenye nia
mbaya na taifa letu bila kujàli
wanatokea.pia tuwakatae viongozi wa
dini wanaotumiwa na mabeberu kwa
lengo la kutumia ushawishi wao ili
kuivuruga amani yetu.mungu ibariki
Africa,mungu ibariki Tanzania yetu