DPP wa Tanzania: Ni Kihiyo wa Sheria, Msanii au Mbabaishaji?

kapelwa

New Member
Sep 4, 2008
4
1


Nimeshitushwa na kauli za mara kwa mara za DPP wetu kuhusu ugumu wa kuishitaki kampuni ya KAGODA. Nimeshitushwa zaidi na matamshi yake yaliyonukuliwa na gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Aprili 12, 2009 kuwa: wamiliki wa KAGODA watafunguliwa mashitaka ikiwa itathibitika kuwa kampuni hiyo haikupewa kazi ya kukusanya madeni na kampuni za nje! Hivyo basi, DPP wetu sasa hivi anahangaika kuzitafuta kampuni hizo huko nje!

Kwa msimamo huo wa kichekesho, mimi najiuliza: DPP WETU NI KIHIYO WA SHERIA, MSANII AU MBABAISHAJI TU? Nashindwa kupata jibu sahihi, maana ushahidi wote wa kumfungulia mashtaka Rostam Aziz na washirika wake upo!!! Kazi aliyojipa DPP wetu si yake ni ya mawakili wa utetezi kuleta ushahidi kuwa KAGODA ilikuwa imetumwa na kampuni fulani ya nje ambayo itaitwa kutoa ushahidi! Anayoyafanya DPP wetu ni upuuzi na mchezo wa kitoto unaotia kichefuchefu, unaowageuza Watanzania wapumbavu wa mwisho duniani. Hivi, nauliza, wamiliki wa makampuni mengine wako mahakamani kutokana na kwamba DPP ana uthibitisho wa makampuni yote kutoka nje? Aliyemwambia DPP wetu kuwa ONUS OF PROOF katika kesi za jinai inamwangukia yeye, ni nani? Huyu kasoma kweli shule, mbabaishaji au msanii ambaye amewekwa hapo kuwahadaa Watanzania?

Katika kesi ya Herniman dhidi ya Smith ya mwaka 1938 ambayo iliamuliwa na Mahakama ya Juu ya Uingereza (House of Lords) na uamuzi wake ukapokewa baadaye na Mahakama Kuu ya Tanganyika kama mwongozo katika kesi ya Ali Mohamed Osman dhidi ya DC Hill, msimamo wa kisheria ni kwamba si wajibu wa upande wa mashtaka kuhakiki kila kipengele cha ushahidi kabla ya kuchukua hatua za kushitaki. Nanukuu:
"... It is not required of any prosecutor that he must have tested every possible relevant fact before he takers action. His duty is not to ascertain whether there is reasonable and probable cause for prosecution. ... there is no obligation to call on the cheat and ask for an explanation in as much as to ask for this may only have the effect of causing material evidence to disappear or to be manufactured ..."

Na kweli kabisa, anachofanya DPP ni kumruhusu Rostam kutengeneza ushahidi na makampuni ya nje! Kwa sisi wazee tuliokaa ndani ya taaluma ya sheria kwa zaidi ya miaka 50 sasa, tunachokiona ni KIOJA! Ili kumfikisha mtu mahakamani, DPP hahitaji kujiridhisha na ushahidi wote, anachohitaji ni ushahidi kiasi unaojenga "reasonable and probable cause to prosecute". Ushahidi wa aina hiyo, tayari DPP Elieza Feleshi anao!

Tanganyika Law Society mko wapi? Wanasheria wa Tanzania mko wapi kuiokoa taaluma yenu ambayo sasa inabakwa? Tofauti yenu na laymen iko wapi?
 
Hili la kuchanganya taaluma na siasa tabu sana! Nilishawahi kusema hapo nyuma kwamba baadhi ya hizi office zinaitaji kufanyiwa 'vetting' na Bunge kabla ya kushika hizi nyadhifa. Na tena ziwe kwa mikataba let say miaka 5 then unarudi kupimwa through vetting ...mbona waganda wameweza sisi tunashindwa nini?
 
Duh, mimi ndio maana sipendi jukwaa la siasa na ninalichukia. Nimesoma hii post najikuta nikianza kupandwa na Moli. Wao wafanye wanavyotaka na kama sisi watu wakawaida ni wajinga hatujui kitu ni kwanini watu wamataifa mengine unakuta wana akili sana, mfano hawa Jewish kwanini? Nakama viongozi wataenda kinyume na sheria na sisi raia wema hatujui sheria tutafanya nini zaidi ya kuangalia?
 
Lakini Mzee Kapelwa, naelewa unaandika kwa abstraction ya juu mno. Naomba suala moja liwe wazi kwa wana JF. Kisheria, onus of proof katika criminal matters iko kwa DPP, lakini si katika stage ambayo Mzee Kapelwa unaielezea na kunukuu authorities, yaani stage ya kuamua whether to prosecute or not. Hapo DPP hana wajibu kabisa wa kuthibitisha, kinachohitajika ni "reasonable and probable cause to prosecute", yaani msingi au sababu za kuridhisha tu kumshitaki mtu, ambazo na mimi nakubali kuwa DPP wetu anazo siku nyingi!
Vilevile hii ni changamoto kwa wanasdheria wote. Msiangalie tu mambo yanaharibika. Hivi hamwezi kuingilia kati kufanya private prosecution? Huyu ROSTAM mpaka aje kuomba kugombea Urais ndo mshituke?
 
Lakini Mzee Kapelwa, naelewa unaandika kwa abstraction ya juu mno. Naomba suala moja liwe wazi kwa wana JF. Kisheria, onus of proof katika criminal matters iko kwa DPP, lakini si katika stage ambayo Mzee Kapelwa unaielezea na kunukuu authorities, yaani stage ya kuamua whether to prosecute or not. Hapo DPP hana wajibu kabisa wa kuthibitisha, kinachohitajika ni "reasonable and probable cause to prosecute", yaani msingi au sababu za kuridhisha tu kumshitaki mtu, ambazo na mimi nakubali kuwa DPP wetu anazo siku nyingi!
Vilevile hii ni changamoto kwa wanasdheria wote. Msiangalie tu mambo yanaharibika. Hivi hamwezi kuingilia kati kufanya private prosecution? Huyu ROSTAM mpaka aje kuomba kugombea Urais ndo mshituke?



Jamani Nchi hii inawataalamu wengi mno wa sheria kwanini msitie maguu kwenye hiyo issue kama haiendi sawa?
 
Naweza kusema Tanzania hatuna wanasheria wenye kuzijua sheria na kama wapo basi nao ni mafisadi tu!!!
 
Sheria inapindishwa makusudi kwa baadhi ya watuhumiwa kwa maslahi ya kisiasa ila siku ipo tutaulizana kilichokuwa kinatokea.
 
DPP wa Tanzania si kihiyo wa sheria, bali ni msanii, mbabaishaji, fisadi, mvivu wa kufikiri, hana professional ethics na hana hofu ya Mungu ndani yake
 
Hebu tusome hizi doc, kama kweli hakuna ushahidi katika Kagoda. Haya yote yalianikwa humu JF...

i350_Kagoda2.jpg

i351_Kagoda3.jpg

i352_Kagoda4.jpg

i353_Kagoda5.jpg
 
............. anachofanya DPP ni kumruhusu Rostam kutengeneza ushahidi na makampuni ya nje! .......

Wenzako walishakamilisha hilo (quoted in red) ndio maana wanasema sasa hivi......otherwise wangekuambia......."No Comment"
 

Aliyemwambia DPP wetu kuwa ONUS OF PROOF katika kesi za jinai inamwangukia yeye, ni nani?

Katika kesi ya Herniman dhidi ya Smith ya mwaka 1938 ambayo iliamuliwa na Mahakama ya Juu ya Uingereza (House of Lords) na uamuzi wake ukapokewa baadaye na Mahakama Kuu ya Tanganyika kama mwongozo katika kesi ya Ali Mohamed Osman dhidi ya DC Hill, msimamo wa kisheria ni kwamba si wajibu wa upande wa mashtaka kuhakiki kila kipengele cha ushahidi kabla ya kuchukua hatua za kushitaki. Nanukuu:

"... It is not required of any prosecutor that he must have tested every possible relevant fact before he takers action. His duty is not to ascertain whether there is reasonable and probable cause for prosecution. ... there is no obligation to call on the cheat and ask for an explanation in as much as to ask for this may only have the effect of causing material evidence to disappear or to be manufactured ..."

Naomba mamlaka (kesi au sheria ya Bunge) inayosema mshitakiwa jinai ana hatia mpaka atakapojisafisha mahakamani, na yeye ndio ana mzigo kudhihirisha hana makosa, na kazi ya prosecutor ni kutuhumu lolote lile.
 
Mara nyingi suala la Kagoda siku hizi watu hupata kigugumizi kujadili, mbona iko kazi mwaka huu!!!!???
 
Hebu tusome hizi doc, kama kweli hakuna ushahidi katika Kagoda. Haya yote yalianikwa humu JF...

i350_Kagoda2.jpg

i351_Kagoda3.jpg

i352_Kagoda4.jpg

i353_Kagoda5.jpg

Humu kuna maswali mengi ambayo Bwana Feleshi anatakiwa kuyajibu si kutafuta watu wa nje wamsaidie kujibu. Atoe hoja kama zile alizotumia kuwashitaki kina Rajabu Maranda na Jeetu Patel. Tunajua mahusiano yake na Andrew Chenge na kundi lake na hivyo kuwa vigumu kwake kushughulikia Kagoda na rada, lakini kazi ndio muhimu udugu baadaye bwana Feleshi
 


Nimeshitushwa na kauli za mara kwa mara za DPP wetu kuhusu ugumu wa kuishitaki kampuni ya KAGODA. Nimeshitushwa zaidi na matamshi yake yaliyonukuliwa na gazeti la Tanzania Daima la Jumapili, Aprili 12, 2009 kuwa: wamiliki wa KAGODA watafunguliwa mashitaka ikiwa itathibitika kuwa kampuni hiyo haikupewa kazi ya kukusanya madeni na kampuni za nje! Hivyo basi, DPP wetu sasa hivi anahangaika kuzitafuta kampuni hizo huko nje!

Kwa msimamo huo wa kichekesho, mimi najiuliza: DPP WETU NI KIHIYO WA SHERIA, MSANII AU MBABAISHAJI TU? Nashindwa kupata jibu sahihi, maana ushahidi wote wa kumfungulia mashtaka Rostam Aziz na washirika wake upo!!! Kazi aliyojipa DPP wetu si yake ni ya mawakili wa utetezi kuleta ushahidi kuwa KAGODA ilikuwa imetumwa na kampuni fulani ya nje ambayo itaitwa kutoa ushahidi! Anayoyafanya DPP wetu ni upuuzi na mchezo wa kitoto unaotia kichefuchefu, unaowageuza Watanzania wapumbavu wa mwisho duniani. Hivi, nauliza, wamiliki wa makampuni mengine wako mahakamani kutokana na kwamba DPP ana uthibitisho wa makampuni yote kutoka nje? Aliyemwambia DPP wetu kuwa ONUS OF PROOF katika kesi za jinai inamwangukia yeye, ni nani? Huyu kasoma kweli shule, mbabaishaji au msanii ambaye amewekwa hapo kuwahadaa Watanzania?

Katika kesi ya Herniman dhidi ya Smith ya mwaka 1938 ambayo iliamuliwa na Mahakama ya Juu ya Uingereza (House of Lords) na uamuzi wake ukapokewa baadaye na Mahakama Kuu ya Tanganyika kama mwongozo katika kesi ya Ali Mohamed Osman dhidi ya DC Hill, msimamo wa kisheria ni kwamba si wajibu wa upande wa mashtaka kuhakiki kila kipengele cha ushahidi kabla ya kuchukua hatua za kushitaki. Nanukuu:
"... It is not required of any prosecutor that he must have tested every possible relevant fact before he takers action. His duty is not to ascertain whether there is reasonable and probable cause for prosecution. ... there is no obligation to call on the cheat and ask for an explanation in as much as to ask for this may only have the effect of causing material evidence to disappear or to be manufactured ..."

Na kweli kabisa, anachofanya DPP ni kumruhusu Rostam kutengeneza ushahidi na makampuni ya nje! Kwa sisi wazee tuliokaa ndani ya taaluma ya sheria kwa zaidi ya miaka 50 sasa, tunachokiona ni KIOJA! Ili kumfikisha mtu mahakamani, DPP hahitaji kujiridhisha na ushahidi wote, anachohitaji ni ushahidi kiasi unaojenga "reasonable and probable cause to prosecute". Ushahidi wa aina hiyo, tayari DPP Elieza Feleshi anao!

Tanganyika Law Society mko wapi? Wanasheria wa Tanzania mko wapi kuiokoa taaluma yenu ambayo sasa inabakwa? Tofauti yenu na laymen iko wapi?

Kagoda siyo Rostam, yeye ni chambo tafuteni kwa undani muijue Kagoda
wakpo watu nyeti wakitajwa tutashangaa na kuona kuwa nchi hii imeisha yumba siku nyingi ndo kwa maana DPP anapata kigugumizi.Advocate Sanze na Benjamin Mwangonda mbona hawatusaidii maana hao ni mashahidi ukiangalia
hati za usajili wameanguka sahihi zao hapo,ndugu zangu Kagoda ni sirikali.
 
Naomba mamlaka (kesi au sheria ya Bunge) inayosema mshitakiwa jinai ana hatia mpaka atakapojisafisha mahakamani, na yeye ndio ana mzigo kudhihirisha hana makosa, na kazi ya prosecutor ni kutuhumu lolote lile.

Huku sasa ni kuchanganya madawa kwa makusudi,... Ni nani aliyesema kuwa mtuhumiwa ana hatia mpaka atakapojisafisha mahakamani?... Nani aliyesema kazi ya prosecutor ni kutuhumu lolote lile.

Kilichosemwa ni "DPP hahitaji kujiridhisha na ushahidi wote, anachohitaji ni ushahidi kiasi unaojenga "reasonable and probable cause to prosecute".

Tusiharibu mijadala kwa spinning zisizojenga.
 
Kutokana na hasira za watu dhidi ya ufisadi, wasiopenda utawala wa sheria, wanaona hata kesi za ufisadi ni kupoteza muda. Wangetaka hukumu moja kwa moja.
Kwa upande wangu, naungana na DPP, anayatumia kikamilifu mamlaka yake aliyopewa na katiba!. Jee mnayajua mamlaka ya DPP?.

Niliwahi kuandika mahali, kati ya watendaji wote wa serikali, ukimuondoa rais wa JMT kwa madaraka kwa mujibu wa katiba, DPP ndiye mtu wa pili mwenye mamlaka ya ajabu ambayo hata
Rais hana uwezo wa kuyabeza.

Ni DPP ndiye mwenye mamlaka ya kukubali kuwa hapa kuna kesi ama la. Na akiamua hakuna kesi, hakuna mamlaka yoyote ya kumuuliza kama rais akiamua kumteua yoyote kushika nafasi yoyote akiona anafaa, hakuna mamlaka ya kuuliza, ni utekelezaji tuu.

Mamlaka ya DPP, hayaishii kwenye kuendesha mashitaka, bali ana mamlaka nyingine kubwa na ya ajabu inayoitwa 'Nolle Proseque'
Hii ni mamlaka ya kusema hakuna kesi ya kujibu wawakati wowote kesi ikiwa hatua yoyote kabla ya hukumu, hata kama ushahidi wa hatia ni asilimia 100%. Mamlaka hiyo inatamka DPP akiamua 'nolle prosequi', hakuna mamlaka yoyote ya kumuuliza why, hata rais hawezi!.
Mtu pekee mwenye mamlaka ya kuruhusu Private 'prosecuition ni huyo huyo DPP, na uamuzi wake ni wa mwisho.

Angalau Prof.Shivji ameuthibitishia umma kuwa baadhi ya maamuzi ya serikali yanayoelezwa kuwa ni ya mwisho, yanaweza kuwa challenged before the court of law kesi ya Bawata, mbona ya DPP hayaguswi?!.

Kagoda inajulikana ni nani, pesa zilikokwenda kunajulikana, kazi nzuri ya fedha hiyo inajulikana, na matokeo yapo wazi na yanajulikana. Anachofanya DPP ni kutimiza wajibu wake,anatumia mamlaka yake halali kusema 'No Case to Answer', kwa mujibu wa katiba, mnashangaa nini?. Amevunja sheria gani?.

Mimi sio mwanasheria, ila tongotongo nimetoa, hawa wanasheria wetu waliobobea wanayajua mamlaka hayo na hawajawahi kuyachallenge, leo ndio wanashangaa?,
Mbona haya ni ya Musa tuu, subirini ya Farao kwenye kesi ya Yona, Mramba na Mgonja!.
 
Kutokana na hasira za watu dhidi ya ufisadi, wasiopenda utawala wa sheria, wanaona hata kesi za ufisadi ni kupoteza muda. Wangetaka hukumu moja kwa moja.
Kwa upande wangu, naungana na DPP, anayatumia kikamilifu mamlaka yake aliyopewa na katiba!. Jee mnayajua mamlaka ya DPP?.

Niliwahi kuandika mahali, kati ya watendaji wote wa serikali, ukimuondoa rais wa JMT kwa madaraka kwa mujibu wa katiba, DPP ndiye mtu wa pili mwenye mamlaka ya ajabu ambayo hata
Rais hana uwezo wa kuyabeza.

Ni DPP ndiye mwenye mamlaka ya kukubali kuwa hapa kuna kesi ama la. Na akiamua hakuna kesi, hakuna mamlaka yoyote ya kumuuliza kama rais akiamua kumteua yoyote kushika nafasi yoyote akiona anafaa, hakuna mamlaka ya kuuliza, ni utekelezaji tuu.

Mamlaka ya DPP, hayaishii kwenye kuendesha mashitaka, bali ana mamlaka nyingine kubwa na ya ajabu inayoitwa 'Nolle Proseque'
Hii ni mamlaka ya kusema hakuna kesi ya kujibu wawakati wowote kesi ikiwa hatua yoyote kabla ya hukumu, hata kama ushahidi wa hatia ni asilimia 100%. Mamlaka hiyo inatamka DPP akiamua 'nolle prosequi', hakuna mamlaka yoyote ya kumuuliza why, hata rais hawezi!.
Mtu pekee mwenye mamlaka ya kuruhusu Private 'prosecuition ni huyo huyo DPP, na uamuzi wake ni wa mwisho.

Angalau Prof.Shivji ameuthibitishia umma kuwa baadhi ya maamuzi ya serikali yanayoelezwa kuwa ni ya mwisho, yanaweza kuwa challenged before the court of law kesi ya Bawata, mbona ya DPP hayaguswi?!.

Kagoda inajulikana ni nani, pesa zilikokwenda kunajulikana, kazi nzuri ya fedha hiyo inajulikana, na matokeo yapo wazi na yanajulikana. Anachofanya DPP ni kutimiza wajibu wake,anatumia mamlaka yake halali kusema 'No Case to Answer', kwa mujibu wa katiba, mnashangaa nini?. Amevunja sheria gani?.

Mimi sio mwanasheria, ila tongotongo nimetoa, hawa wanasheria wetu waliobobea wanayajua mamlaka hayo na hawajawahi kuyachallenge, leo ndio wanashangaa?,
Mbona haya ni ya Musa tuu, subirini ya Farao kwenye kesi ya Yona, Mramba na Mgonja!.

Nimekuelewa Pasco. Kunamambo mengi yanahitajika ili kuikomboa Tanzania. Kama hatutaki mapinduzi
 
Hakuna cha Feleshi wala nini. Hiki kigugumizi ni kutoka juu! Unafikiri JK angetaka Rostam apelekwe mahakamani angekuwa uraiana hadi leo? Hapa sasa ndio JK atakapoiona nchi chungu. Yaani kawapeleka kundi la Mkapa - kina Mramba - mahakamani lakini hakuna hata mwanamtandao mmoja aliyeguswa! Anawapa watu ndani ya CCM cha kusema
 
Kutokana na hasira za watu dhidi ya ufisadi, wasiopenda utawala wa sheria, wanaona hata kesi za ufisadi ni kupoteza muda. Wangetaka hukumu moja kwa moja.
Kwa upande wangu, naungana na DPP, anayatumia kikamilifu mamlaka yake aliyopewa na katiba!. Jee mnayajua mamlaka ya DPP?.

Niliwahi kuandika mahali, kati ya watendaji wote wa serikali, ukimuondoa rais wa JMT kwa madaraka kwa mujibu wa katiba, DPP ndiye mtu wa pili mwenye mamlaka ya ajabu ambayo hata
Rais hana uwezo wa kuyabeza.

Ni DPP ndiye mwenye mamlaka ya kukubali kuwa hapa kuna kesi ama la. Na akiamua hakuna kesi, hakuna mamlaka yoyote ya kumuuliza kama rais akiamua kumteua yoyote kushika nafasi yoyote akiona anafaa, hakuna mamlaka ya kuuliza, ni utekelezaji tuu.

Mamlaka ya DPP, hayaishii kwenye kuendesha mashitaka, bali ana mamlaka nyingine kubwa na ya ajabu inayoitwa 'Nolle Proseque'
Hii ni mamlaka ya kusema hakuna kesi ya kujibu wawakati wowote kesi ikiwa hatua yoyote kabla ya hukumu, hata kama ushahidi wa hatia ni asilimia 100%. Mamlaka hiyo inatamka DPP akiamua 'nolle prosequi', hakuna mamlaka yoyote ya kumuuliza why, hata rais hawezi!.
Mtu pekee mwenye mamlaka ya kuruhusu Private 'prosecuition ni huyo huyo DPP, na uamuzi wake ni wa mwisho.

Angalau Prof.Shivji ameuthibitishia umma kuwa baadhi ya maamuzi ya serikali yanayoelezwa kuwa ni ya mwisho, yanaweza kuwa challenged before the court of law kesi ya Bawata, mbona ya DPP hayaguswi?!.

Kagoda inajulikana ni nani, pesa zilikokwenda kunajulikana, kazi nzuri ya fedha hiyo inajulikana, na matokeo yapo wazi na yanajulikana. Anachofanya DPP ni kutimiza wajibu wake,anatumia mamlaka yake halali kusema 'No Case to Answer', kwa mujibu wa katiba, mnashangaa nini?. Amevunja sheria gani?.

Mimi sio mwanasheria, ila tongotongo nimetoa, hawa wanasheria wetu waliobobea wanayajua mamlaka hayo na hawajawahi kuyachallenge, leo ndio wanashangaa?,
Mbona haya ni ya Musa tuu, subirini ya Farao kwenye kesi ya Yona, Mramba na Mgonja!.
Aisee kumbe DPP Ana mamlaka makubwa mno
 
Back
Top Bottom