DPP Biswalo Mganga unalazimika kuwajibika kujiuzulu baada ya kumtoa "mahabusu" Nusrat Hanje gerezani akawe ghafla Mbunge

Ivi kweli tunakubali katiba na.sheria zetu zikanyagwe na kundi la watu wachache tuliowapa dhamana ya kuilinda? Utawala wa sheria umekoma kabisa Tanzania, Viongozi wetu, oneni aibu.
 
Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni.

Ndivyo ninavyolazimika kuianza "thread" yangu kutokana na sakata hili la kumwachia mahabusu Nusrat Hanje kinyume cha sheria na taratibu za nchi hii.

Kama kweli nchi yetu inaendeshwa kwa utawala bora, DPP Biswalo Mganga analazimika kujiuzulu kutokana na sakata linaloendelea kumtoa mahabusu, Nusrat Hanje, kinyume cha sheria, usiku wa tarehe 23/11/2020, kwa lengo moja tu la "kumuwahisha" ili aende kuapishwa Bungeni Dodoma kesho yake ya tarehe 24/11/2020.

Wewe uliwahi kuona wapi, Mahabusu yeyote hapa nchini anatolewa gerezani usiku, bila kwanza kupitia kwenye Mahakama iliyomuhukumu aende rumande kwenye gereza hilo na kuifunga dhamana yake kwa siku 133 mfululizo?

Ndivyo ilivyotokea kwa Mahabusu Nusrat Hanje, Kiongozi wa Bavicha Taifa, baada ya kutuhumiwa na Jeshi la Polisi nchini, kufanya mkusanyiko usio halali, hapo mwezi June mwaka huu.

Tunamuomba Biswalo Mganga aueleze Umma wa watanzania, kulikuwa na udharula gani, hadi "azitengue" sheria za nchi hii na kulazimisha kumtoa Mahabusu, Nusrat Hanje, kisiri siri, tena usiku wa tarehe 23/11/2020?

Huyo Nasrat Hanje aliamka akiwa rumande tarehe 23/11/2020 akiwa hajui hili wala lile, baada ya juhudi kubwa zilizofanywa na Ndugu, Jamaa, Viongozi wa Chama chake cha CHADEMA pamoja na wanasheria wao kufanya juhudi kubwa ya kumtoa rumande kwa siku 133 bila mafanikio yoyote.

Ghafla jioni hiyo ya tarehe 23/11/2020 ndipo ilipokuja amri kutoka kwa DPP, Biswalo Mganga, kwa Mkuu wa gereza alilokuwemo kuwa atolewe gerezani humo na yeye ni mtu huru kuanzia dakika ile!

DPP anaelewa fika "procedure" za kufuata kabla ya mahabusu yeyote kuachiwa Huru na utaratibu huo ni pamoja na huyo mahabusu kuachiwa majira ya asubuhi hadi mchana pekee na ipelekwe taarifa kwenye mahakama aliyotuhumiwa na ipate kibali kwa "kusainiwa" na Hakimu mwenye kusikiliza kesi hiyo.

Utaratibu huo haukufuatwa kabisa, kwa kuwa "mahabusu" huyo aliachiwa majira ya saa 1.30 jioni ya tarehe hiyo ya 23/11/2020 na taarifa yake haikupelekwa kwa Hakimu anayesikiliza kesi yake ili "aisaini" kuidhinisha kutoka kwake huko Mahabusu.

Lakini kilichobainika baadaye ni kuwa amri hiyo ya kumwachia "mahabusu" huyo Nusrat Hanje na DPP, Biswalo Mganga, kuamua kwa makusudi kuvunja utaratibu mzima wa kuachiwa kwa Mahabusu huyo ni kwa sababu tu ili awahi kwenda apishwa Ubunge wa viti maalum vya Chadema, kesho yake ya tarehe 24/11/2020 mjini Dodoma!

Kwa "blunder" hii kubwa iliyofanywa na DPP Biswalo Mganga, wananchi tunaomba ajiuzulu wadhifa wake wa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini kwa kutofuata taratibu za kumwachia huru huyo "mahabusu" Nusrat Hanje, kwa kuwa nchi hii inaendeshwa kwa taratibu na sheria, ambazo kwa makusudi, DPP Biswalo Mganga hakutaka kuzifuata, katika sakata hilo la kumwachia mahabusu huyo, Nusrat Hanje.

Kwa mtu ambaye Taifa hili lilimwamini sana kuwa atatekeleza wadhifa wake huo kwa uaminifu mkubwa na kwa kufuata sheria za nchi kwa hii "blunder" kubwa aliyoifanya, analazimika kuwajibika kujiuzulu ili alinde heshima yake na alinde heshima ya Rais ambaye alimwamini kwa kumpa wadhifa huo mkubwa sana wa utumishi wa Umma, akiwa ni Mwendesha Mashitaka Mkuu wa nchi hii

Kama atagoma kujiuzulu tunamwomba Rais Magufuli ambaye ndiye aliyemteua kwenye nafasi hiyo amfukuze kazi mara moja, kwa kuwa kwa kitendo chake hicho amelisababishia Taifa hili aibu na fedheha kubwa ndani ya nchi na hata kwenye Jumuia ya Kimataifa.
Watanzania tunachezewa Sana,...yaaani tunapelekwa Kama gari bovu... daaah..
 
Kwani kaweka na nani pale? Naye ana maboss wake, hivyo tulia usitafute makubwa mkuu
 
Yaani huyu Jiwe anaona kama aliyetutawala ni maiti!

Hivi inawezekanaje mtu aliyefanya "blunder" ya dhahiri kama hii, aendelee kumkumbatia?

Atamfukuzaje wakati hiyo kazi amemtuma yeye mwenyewe, na anaifanya kwa ufanisi anaoutaka mwenyewe Jiwe..?
 
Toka lini na nyie CHADEMA mmwite Nusrat Hanje? Simmewabatiza wao ni Covid 19? Kwani Biswalo ndo amewatimua kwa mbwembwe na fedhuri kwenye kikundi chenu??Mbona CHADEMA mnazidi kuchanganyikiwa juuu ya hawa wamama wa watuu? Waacheni wapumuzike sio kushinda mnawasengenya mitandaoni tena Mliwatimua haraka sana, sasa mnawataka nini tena?
Wewe kichaa kwa umoja wao ni covid 19, kwa mmoja anatambulika kwa Jina lake. Kiungo gani unachotumia ?
 
Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya Firauni.

Ndivyo ninavyolazimika kuianza "thread" yangu kutokana na sakata hili la kumwachia mahabusu Nusrat Hanje kinyume cha sheria na taratibu za nchi hii.

Kama kweli nchi yetu inaendeshwa kwa utawala bora, DPP Biswalo Mganga analazimika kujiuzulu kutokana na sakata linaloendelea kumtoa mahabusu, Nusrat Hanje, kinyume cha sheria, usiku wa tarehe 23/11/2020, kwa lengo moja tu la "kumuwahisha" ili aende kuapishwa Bungeni Dodoma kesho yake ya tarehe 24/11/2020.

Wewe uliwahi kuona wapi, Mahabusu yeyote hapa nchini anatolewa gerezani usiku, bila kwanza kupitia kwenye Mahakama iliyomuhukumu aende rumande kwenye gereza hilo na kuifunga dhamana yake kwa siku 133 mfululizo?

Ndivyo ilivyotokea kwa Mahabusu Nusrat Hanje, Kiongozi wa Bavicha Taifa, baada ya kutuhumiwa na Jeshi la Polisi nchini, kufanya mkusanyiko usio halali, hapo mwezi June mwaka huu.

Tunamuomba Biswalo Mganga aueleze Umma wa watanzania, kulikuwa na udharula gani, hadi "azitengue" sheria za nchi hii na kulazimisha kumtoa Mahabusu, Nusrat Hanje, kisiri siri, tena usiku wa tarehe 23/11/2020?

Huyo Nasrat Hanje aliamka akiwa rumande tarehe 23/11/2020 akiwa hajui hili wala lile, baada ya juhudi kubwa zilizofanywa na Ndugu, Jamaa, Viongozi wa Chama chake cha CHADEMA pamoja na wanasheria wao kufanya juhudi kubwa ya kumtoa rumande kwa siku 133 bila mafanikio yoyote.

Ghafla jioni hiyo ya tarehe 23/11/2020 ndipo ilipokuja amri kutoka kwa DPP, Biswalo Mganga, kwa Mkuu wa gereza alilokuwemo kuwa atolewe gerezani humo na yeye ni mtu huru kuanzia dakika ile!

DPP anaelewa fika "procedure" za kufuata kabla ya mahabusu yeyote kuachiwa Huru na utaratibu huo ni pamoja na huyo mahabusu kuachiwa majira ya asubuhi hadi mchana pekee na ipelekwe taarifa kwenye mahakama aliyotuhumiwa na ipate kibali kwa "kusainiwa" na Hakimu mwenye kusikiliza kesi hiyo.

Utaratibu huo haukufuatwa kabisa, kwa kuwa "mahabusu" huyo aliachiwa majira ya saa 1.30 jioni ya tarehe hiyo ya 23/11/2020 na taarifa yake haikupelekwa kwa Hakimu anayesikiliza kesi yake ili "aisaini" kuidhinisha kutoka kwake huko Mahabusu.

Lakini kilichobainika baadaye ni kuwa amri hiyo ya kumwachia "mahabusu" huyo Nusrat Hanje na DPP, Biswalo Mganga, kuamua kwa makusudi kuvunja utaratibu mzima wa kuachiwa kwa Mahabusu huyo ni kwa sababu tu ili awahi kwenda apishwa Ubunge wa viti maalum vya Chadema, kesho yake ya tarehe 24/11/2020 mjini Dodoma!

Kwa "blunder" hii kubwa iliyofanywa na DPP Biswalo Mganga, wananchi tunaomba ajiuzulu wadhifa wake wa Mkurugenzi wa Mashitaka nchini kwa kutofuata taratibu za kumwachia huru huyo "mahabusu" Nusrat Hanje, kwa kuwa nchi hii inaendeshwa kwa taratibu na sheria, ambazo kwa makusudi, DPP Biswalo Mganga hakutaka kuzifuata, katika sakata hilo la kumwachia mahabusu huyo, Nusrat Hanje.

Kwa mtu ambaye Taifa hili lilimwamini sana kuwa atatekeleza wadhifa wake huo kwa uaminifu mkubwa na kwa kufuata sheria za nchi kwa hii "blunder" kubwa aliyoifanya, analazimika kuwajibika kujiuzulu ili alinde heshima yake na alinde heshima ya Rais ambaye alimwamini kwa kumpa wadhifa huo mkubwa sana wa utumishi wa Umma, akiwa ni Mwendesha Mashitaka Mkuu wa nchi hii

Kama atagoma kujiuzulu tunamwomba Rais Magufuli ambaye ndiye aliyemteua kwenye nafasi hiyo amfukuze kazi mara moja, kwa kuwa kwa kitendo chake hicho amelisababishia Taifa hili aibu na fedheha kubwa ndani ya nchi na hata kwenye Jumuia ya Kimataifa.
Aya yako ya mwisho,unapomuomba Maghu,amfute kazi,unashangaa,madudu yote haya Yana baraka za Maghufuri,Kama Kuna mtu anaamini ujambazi wote huu unaofanyika kuanzia jeshi la polisi,mahakamani,mpaka bungeni,Maghufuri hajuhi,inabidi akapimwe akili
 
Back
Top Bottom