DOWANS: Slaa ulituongopea!

Ngeleja anasema wamiliki wa dowans Tanzania Ltd "niDowans Holding S.A ya Costa Rica (81) na Portek Systems and Equipment (PTE) LTd (54)."
Total ya hizi shares ni 135 lakini kuna mahali alitaja asilimia, hii inamaanisha ni 84% na 54% which adds up to 135%!!!!???..
Nakubaliana na wachangiaji humu kuwa hizo kampuni zinamiliki dowans na hao aliowataja ni wakurugenzi wa hizo kampuni si lazima wawe wamiliki. Sheria ya makampuni inaturuhusu kulift vail of incorporation na kutaja wamiliki hasa. Kama hao wakurugenzi ndio wamiliki pia basi angetutajia shares wanazohold kwenye kampuni hizo.
Katika utetezi tanesco inatueleza nani alikuwa anapokea fedha za Dowans. Soma ile siri ya dowans iliyo kwenye pdf file page 31 clause 17.11 uone namna Rostam Aziz, a Tanzanian politician alivyoitrick Tanesco na kuidhinishwa kuchukua fedha toka CRDB kwa niaba ya Dowans.
Kama mnakumbuka vizuri katika ripoti ya Mwakyembe "Mashahidi wawili, Ndugu Daniel Yona na Mhe. Rostam Aziz, (Mb) walipelekewa hati za kuitwa mbele ya Kamati Teule lakini hawakufika kwa maelezo kwamba walikuwa nje ya nchi."
This is home of great thinkers; ebu tutafakari yote yanayowekwa humu na utaona wazi kuwa mmiliki ni nani






 

Ningekuwa Ngeleja ningejiuzuru....
 
Enyi wana JF,msimlaumu,hapo ndipo uwezo wake wa kufikiri umeishia! Asipokula kuku na mayai ya kichina anaweza kufikiri zaidi ya hapo. Kama JK anaamini hahusiki na DOWANS hebu aend mahakamani,mbona alitajwa kwenye orodha ya MAFISADI na haendi mahakamani. Tetea hizo Hela ili uhongwe 2015
 



Kinachoshangaza Watanzania wengi nikiwa mmojawapo, ni kwa nini Hakuna Juhudi zozote zinazo onekana kufanywa na viongozi wa serikali kupinga uamuzi wa ICC badala yake kila kauli na nguvu ni katika kuilipa DOWANS!! Kuna nini hapa????????
 
hivi kwa akili ya kawaida tu isiyohitaji kutumia msuri ulitegemea kuna mtu yoyote serikalini ambae angekuja na kusema kua wamiliki wa dowans ni rosta,mkwere,na lowassa?kama ulifuatlia suala ili toka awali na yote yaliyojili bungeni,longolongo za brela,blah blah...mpaka ikapita miaka mitatu ndio tunakuja kutajiwa wamiliki fake basi usingeweza kuweka thread hii
 

MAJAMBO haihitaji uwe genius ili kubaini kuwa watanzania tunapigwa mchanga wa macho kuhusu wamiliki wa DOWANS, kumbuka msajili wa makampuni wa COSTA RICA anasema huko kwao hakuna kampuni iliyosajiliwa kwa jina la DOWANS, lakini katika kutaja wamiliki wa DOWANS bado wanadai kampuni hiyo imesajiliwa COSTA RICA na bado MAJAMBO unawahamini kauli zao kuliko kauli ya msajili makampuni wa costa rica eti unataka ushaidi! Walivyotajwa kwa majina kuwa wameiba BOT fedha ya EPA walisema kama wewe kuwa wanataka utolewe ushahidi leo kila kitu kipo hadharani kuhusu EPA. DEEP GREEN na MEREMETA zilipotajwa wakasema ni uzushi wakadai utolewe ushahidi, lakini BUNGENI baada ya kubanwa sana PINDA akasema yupo radhi kusulubiwa kuliko kuzungumzia hizo kampuni eti itaathiri usalama wa taifa . Hadi leo watu ambao kauli zao MAJAMBO anaziamini wanashindwa kumtaja mmiliki wa KAGODA.

RICHMOND haikusajiliwa Marekani kama walivyokuwa wanadai wapambe wake, lakini ilishinda zabuni ya kuzalisha umeme Tanzania. MAJAMBO na wenzake wakaaminishwa kuwa ni kampuni safi mambo yalivyo haribika ukweli ukawa hadharani kampuni hiyo ni kimeo. MAJAMBO funguka macho nchi hii haina mwenyewe, mwenyewe nchi NYERERE alishakwenda....................... Waliobaki ni wawekezaji wa NDANI (wakoloni weusi)
 

bora kua mjinga kuliko kuitwa mpumbavu, we mweupeee upstairs!
 

Ngereja asinge weza kufanya zaidi ya hapo, ndivyo walivyowalivyo isajili hiyo Dowans, kulikuwa na thread huko nyuma zilizungumzia headnquarter ya Dowans sa..
.... Yana mwisho!
 

Kama unavyotoa maoni yako hapa, ni yaki ya Majambo pia kutoa maoni yake. Hajavunja sheria za JF.

Na pia kama unavyotaka Majambo afunguke macho, kwa aliyoandika pale anadhani umefumba macho.
 

wewe tafuta mahali pa kwenye kuropokea maneno yako..

Hivi wewe board members ndiyo owners wa kampuni?

Slaa hakusema jk ndiye mmiliki wa dowans bali alisema anafaidika na dowans...

Dowans ni ya rostam aziz hilo haliepukiki.. Na ukweli uko siku utajulikana tu..
 
Mungu ni Mwema: Kila aliyemsingizia mwenzako uongo, ukweli utafahamika hapa hapa duniani!

  • Rostam anamililiki DOWANS
  • Mabox ya kura Mbeya
  • Kura za Urais zimeibwa
  • JK ni mmiliki wa DOWANS
Bado... Mungu ni mwema.
 
Hakuna namna hao wamiliki waliotajwa wanaweza kuhojiwa.
Nafikiri tunahitaji kusikia kauli zao.
Waandishi wa habari tunawategemea kwa hilo.
 
Ngeleja anatakiwa ahojiwe ,ngeleja amewekwa na mafisadi nani hajui anawatetea hao wakina RA.na EL Kwanza atuombe radhi ,fedha hizo zingine zimelipwa kinyemela na hao watu wawili waliokuwa wakisimamaia aankra za malipowalizopenyezewa na mafisadi deni la ngeleja sio kweli wana jf ametamka hivyo kupunguza makali watanzania wone ni mzigo mdogo wanancheza na akili zetu ukweli ni kwamba dowans wanadai billion 185 sio vinginevyo
 
Sasa mbona hajatoa ushahidi mpaka sasa?

Kumbe Dr Slaa alituongopea watanzania?????:A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down:
 

Hoja yako ni ipi, kuwa wazi!
 
Majambo-Your at risk to became mentally blockage.Stupit threads like this,just post to your cousin.Wewe ni mvivu wa kufikiri, muombe king'asti wako japo akusaidie.
 
Sasa mbona hajatoa ushahidi mpaka sasa?

Kumbe Dr Slaa alituongopea watanzania?????:A S thumbs_down::A S thumbs_down::A S thumbs_down:


unahitaji ushahidi gani zaidi ya kile anachokisema au akili zako mdando.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…