Dowans lazima walipwe

AMARIDONG

JF-Expert Member
Jun 24, 2010
2,502
180
Baada ya kuupitia vizuri mkataba wa TANESCO na Richmond wa June 2006, na baadaye nikaupitia mkataba wa Dowans na TANESCO wa December 2006, pamoja na madudu yote ambayo Richmond waliyafanya dhidi ya TANESCO, bado kulikuwa na concert ya Waziri na serikali, hata kama tunasema Richmond walihamisha mkataba kwenda Dowans bila kuwaeleza TANESCO. Si kweli kwani Waziri Karamagi alikubaliana na Richmond.

Jambo la pili na muhimu ni kwamba nimepitia hukumu ya ICC kwa mapana yake na kipengele kimoja ambacho waamuzi wa ICC wanakishikilia bango ni kuwa Dowans waliperfom na TANESCO walipokea umeme wa Dowans.

Hili ni la muhimu na Watanzania wanatakiwa kujua hata kama mkataba wa TANESCO na Dowans ulikuwa sio halali, bado unawishwa kuwa halali kwa sababu ya TANESCO kupokea umeme wa Dowans. Kama TANESCO wasinglipokea umeme wa Dowans basi mkataba ungekuwa batili, lakini as long as the Dowans performed and TANESCO received those whether one or hundred megawatts, maana yake ni kuwa kulikuwa na mkataba halali na TANESCO kuuvunja ilikuwa ni batili.

Kwa ushauri wangu, serikali iwalipe Dowans hizo bilioni lakini sasa irudi kwa Kina Karamagi na wengine wote waliohusika kuirubuni TANESCO wakamatwe, wafilisiwe na wawekwe ndani. Huu uwe mfano.

Angalizo: Kama TANESCO na serikali yetu ikikataa kuwalipa Dowans, balozi zetu nje ya nchi zitakuwa attached na mwisho wa siku tutawalipa kwa riba kubwa sana.

Watanzania, msioogope kuwalipa Dowans bilioni 94, hao Dowans wameshalipwa zaidi ya bilioni 172 mpaka sasa kwa ajili ya mitambo waliyoinunua kwa shilingi bilioni 60. Nchi hii ina hela nyingi sana, kazi yetu tunatakiwa kuwadhibiti wale wanaotumia fedha zetu vibaya.
 
Ni kweli hapa hatuna ujanja hawa jamaa wametushika pabaya na mimi niwaambie watz wenzangu tuache mzuka usio na msingi hawa jamaa tusipowalipa tutalipa mabilioni mengi zaidi baadae ni bora walipwe sasa

Serikali walipeni DOWANS mtuondolee hii kero
 
Mbona moyo unanienda mbio jama?

Pole sana ila tukichelewa hawa ICC wana haki ya kuatach mali zetu kokote ulimwenguni na hii itakuwa mbaya zaidi kwani;

Kwanza tutalipa bila kupenda
Pili tutalipa na riba kubwa
Tatu-tutalipa na gharama zote za usumbufu na utaratibu
Nne-Tutakuwa tumechafua jina la nchi yetu kote ulimwenguni
Mwisho-Tutaweka rekodi mbaya ICC na hatutashinda kesi yoyote pale kwani THIS WILL BE TAKEN AS THE COURT PRECEDENT

SERIKALI WALIPENI DOWANS HARAKA ILA CHUKUENI HATUA ZA KINIDHAMU JUU YA WOTE WALIOIPOTOSHA TANESCO
 
Kulipa ni muhimu kama tunafuata utawala wa sheria, lakini nahisi malipo yataambatana na mabadiliko ya serikali kutoka ile iliyotuingiza kwenye mkataba na kuingiza serikali ya watu ambao hawakuhusika na mkataba huu. Katiba ya CCM haifanani na ile ya ANC?
 
Watanzania,

MSIOGOPE KUWALIPA DOWANS BILION 94,HAO DOWANS WAMESHALIPWA ZAIDI YA BILIONI 172 MPAKA SASA KWA AJILI YA MITAMBO WALIYOINUNUA KWA SHILINGI BILIONI 60,NCHI HII INA HELA NYINGI SANA KAZI YETU TUNATAKIWA KUWADHIBITI WALE WANAOTUMIA FEDHA ZETU VIBAYA.



nimeshagundua wewe sio mtanzania.....reasoning yako ina fanana na mtu kutoka Costa Rica
 
Tusiende kukimbilia kuwalipa. Tayari hukumu imeshasajiliwa mahakama kuu ya Tanzania ili watu wapate wasaa wa kuipitia na kujua nini kipi ndani. Na kwa sababu upo uwezekano wa pingamizi ndio maana kuna kesi imefunguliwa mahakamani na kituo cha haki za binadamu. So haya yote inabidi tuyape wasaa kwanza kabla ya kufanya upumbavu.
 
Hatutawalipa na tuone mwisho wetu.

Mbona CUBA hadi leo bado wanaishi?

Tusiwalipe na mwisho wa siku, tuvunje MUUNGANO na wao wabaki wakiidai TANZANIA ambayo haitakuwepo.

Kama wao wanaujua huu, sisi tunaujuwa huu.
 
Mh wale wale.Nna wasiwasi na hii thread ilivokuwa organized na pia ilivochangiwa kwa haraka na watu wa aina ileile.Wametumwa au ndo mkakati wa RA kutumia watu kutupumbaza.Kweli mkono mtupu haulambwi.
 
baada ya kuupitia vizuri mkataba wa tanesco na richmond wa june 2006,na baadae nikaupitia mkataba wa dowans na tanesco wa december 2006,pamoja na madudu yote ambayo richmond waliyafanya dhidi ya tanesco bado kulikuwa na concert ya waziri na serikali hata kama tunasema richmond walihamisha mkataba kwenda dowans bila kuwaeleza tanesco si kweli kwani waziri karamagi alikubaliana na richmond.

jambo la pili na muhimu ni kwamba nimepitia hukumu ya icc kwa mapana yaek na kipengle kimoja ambacho waamuzi wa icc wanakishikia bango ni kuwa dowans waliperfom na tanesco walipokea umeme wa dowans

hili ni la muhimu na watanzania wanatakiwa kujua hata kama mkataba wa tanesco na dowans ulikuwa sio halali bado unawishwa kuwa halali kwa sababu ya tanesco kupokea umeme wa dowans kama tanesco wasinglipokea umeme wa dowans basi mkataba ungekuwa batili ,lakini as long as the dowans perfomed and tanesco received those whether one or hundred megawats ,maana yake ni kuwa kulikuwa na mkataba halali na tanesco kuuvunja ilikuwa ni batili

cha kufanya

kwa ushauri wangu,serikali iwalipe dowans hizo billion lakini sasa irudi kwa kina karamagi na wengine wote waliohusika kuirubuni tanesco wakamatwe,wafilisiwe na wawekwe ndani huu uwe mfano.

angalizo

kama tanesco na serikali yetu ikikataa kuwalipa dowans,balozi zetu nje ya nchi zitakuwa atached na mwisho wa siku tutawalipa kwa riba kubwa sana,


watanzania,

msiogope kuwalipa dowans bilion 94,hao dowans wameshalipwa zaidi ya bilioni 172 mpaka sasa kwa ajili ya mitambo waliyoinunua kwa shilingi bilioni 60,nchi hii ina hela nyingi sana kazi yetu tunatakiwa kuwadhibiti wale wanaotumia fedha zetu vibaya.

tunaanzia hapa dowans kuwadhibiti hawa mabwege mafisadi. Kwa sababu wamewahi kulipwa mahela mengi zai di bilioni 172, kama wanataka wachukue mali zilizoko ubalozi ethiopia.
 
Son of Soil, kuwalipa Dowans, lazima tuwalipe, ila sababu halisi za kuwalipa, sio hizi wewe ulizoziorodhesha, bali tutawalipa Dowans smply because ni wakubwa wanajilipa.

Tusipowalipa Dowans, hakuna mali ya Tanzania itakayoshikiliwa kama attachment, kwa sababu mdaiwa ni Tanesco as an entitiy na sio serikali, afterall, serikali yatu haina movable assets mahali popote duniani, hatuna meli, wala ndege ya kusema wataishikilia. Nyumba zote za serikali tunazozimiliki nje ya Tanzania, ni ofisi za Ubalozi, zina kinga ya Rome/Geneve Convention on Diplomatic immuninity, kuwa kila aridhi ya ubalozi, ni sehemu ya nchi husika, yaani ofisi yetu London, ni aridhi ya Tanzania, ardhi ya nchi, haishikiki as attachment.
 
Pasco you're right, on a diplomatic point of view we have nothing to lose as a country if we refuse to pay Dowans! I'm speakin as a school of diplomatic mediation and negotiation regarding the international relations & trading.
 
Son of Soil, kuwalipa Dowans, lazima tuwalipe, ila sababu halisi za kuwalipa, sio hizi wewe ulizoziorodhesha, bali tutawalipa Dowans smply because ni wakubwa wanajilipa.

Tusipowalipa Dowans, hakuna mali ya Tanzania itakayoshikiliwa kama attachment, kwa sababu mdaiwa ni Tanesco as an entitiy na sio serikali, afterall, serikali yatu haina movable assets mahali popote duniani, hatuna meli, wala ndege ya kusema wataishikilia. Nyumba zote za serikali tunazozimiliki nje ya Tanzania, ni ofisi za Ubalozi, zina kinga ya Rome/Geneve Convention on Diplomatic immuninity, kuwa kila aridhi ya ubalozi, ni sehemu ya nchi husika, yaani ofisi yetu London, ni aridhi ya Tanzania, ardhi ya nchi, haishikiki as attachment.

Umezungumza vizuri ila kuna kitu umesahau Tanesco ni mali ya URT,Diplomat immunity vested by Geneva Convention inahusika kwa arthi mlizonunua na kumiliki sio Arthi za balzo nyingi za Tanzania ambazo tumepewa na Nchi husika na nyingi kati ya hizo hatuna hati ya umiliki hii ni hatari kwani balozi nyingi zitakuwa hatihati

Usisahau Tanzania ina meli zinazunguka duniani kama MV Tanzania na Mapinduzi ,hata kama ATC imekufa ila ilikuwa na ofisi zake nje ya nchi na assets
 
Mkuu hapo nakubaliana na wewe kitu kimoja.... For me hata wakilipwa au wasilipwe lazima waliotuingiza kwenye hili janga wawajibike..., kwangu ni bora tupoteze hizo bilioni lakini watu wawajibike..... sababu ninachoogopa ni kwamba kutokuwalipa huenda watanzania tukaona ni adhabu tosha...., kumbe hawa jamaa watabuni mbinu nyingine za kutuibia.
 
Mkuu Son of Soil nimekusoma na nimeona Logic yako, lakini hatuwezi kuuacha ukweli eti kwa sababu Dowans walizalisha na kuuza umemem kwa TAnesco
Mkuu hoja inarudi nyuma kabisa na wala sheria haianzi juu kuja chini bali inaanza chini kuja Juu
Richmond walishakiuka masharti ya mkataba, Wao waliingia Ubia na Dowans Bila kuwashirikisha Tanesco ikiwa na maana kuwa huo Mkataba kati ya Dowans na Richmond ni batili, kwa hiyo Dowans Amekuja Tanesco kama mtoto HAramu amepewa nguvu na Richmond bila kumshirikisha Upande wa Pili, hicho kifungu kinainyima Dowans Haki ya kulipwa chochote hata kama walizalisha na kuuza umemem kwaTanesco
 
Mambo rahisi ni magumu. Tuwaachie wenye akili na nguvu. Wanyonge tukichoka tunajua la kufanya mifano ya kuigwa ipo, muhimu tusionee na tusionewe.
 
Pole sana ila tukichelewa hawa ICC wana haki ya kuatach mali zetu kokote ulimwenguni na hii itakuwa mbaya zaidi kwani;

Kwanza tutalipa bila kupenda
Pili tutalipa na riba kubwa
Tatu-tutalipa na gharama zote za usumbufu na utaratibu
Nne-Tutakuwa tumechafua jina la nchi yetu kote ulimwenguni
Mwisho-Tutaweka rekodi mbaya ICC na hatutashinda kesi yoyote pale kwani THIS WILL BE TAKEN AS THE COURT PRECEDENT

SERIKALI WALIPENI DOWANS HARAKA ILA CHUKUENI HATUA ZA KINIDHAMU JUU YA WOTE WALIOIPOTOSHA TANESCO

Hayo yote yakifanyika Rostam ataendelea kuwa Raia wa Tanzania na Mbunge wa Igunga?
 
Haya ndio wanayosema wanaharakati wetu wamesahau hata mambo ya msingi katika mkataba

1. Proposal and acceptance
2. Consideration – lawful consideration with a lawful object
3. Capacity of parties to contract – competent parties
4. Free consent
5. An agreement must not be expressly declared to be void.
6. Writing and Registration if so required by law
7. Legal relationship
8. Certainty
9. Possibility of performance
10. Enforceable by law.

Wao wanasema yafuatayo ndiyo wanayasimamia jamani mbona naona haya sound na hayana mshiko

1: Kwamba Bodi ya Zabuni ya Tanesco (TTB) ilikuwa na watalaam weledi katika kufanya kazi ya kuchambua zabuni, na kwa hakika huko nyuma ilikwisha kufanya kazi nyingine nyingi. Kwa maana hiyo kama kulikuwa na wasiwasi juu ya uwezo wa TTB katika suala zima la mkataba wa Richmond, basi ingebidi kupitia zabuni zote za huko nyuma na si wa Richmond pekee;

2: Kwamba kamati iliyoundwa na Wizara ya Nishati na Madini kupitia mchakato wa kufungwa kwa mkataba wa Tanesco na Richmond iliundwa nje ya utaratibu wa Sheria ya Ununuzi wa Umma (PPA);

3: Kwamba Tanesco ilishughulikia vilivyo zabuni ya Richmond kitaalam na kufikia hitimisho kuwa kampuni hiyo, haikuwa na uwezo wa kitaalam wala wa kifedha kufanya kazi hiyo. Richmond haikuwa na historia (rekodi) ya kufanya kazi kama hiyo walioyokuwa wameomba kama moja ya sharti mojawapo la msingi la kupata zabuni hiyo ambalo liliwekwa kwenye tangazo la kuomba kazi kama hiyo (kuzalisha umeme) na angalau kuwa na mtaji wa Dola za Marekani milioni tano (wakati huo Sh. bilioni tano).

4: Kwamba hata pale kazi ya kutafuta mzabuni wa kufanya kazi ya kuzalisha umeme megawati 100 ilipochukuliwa na Wizara ya Nishati na Madini, haikufanywa na Bodi ya Zabuni ya wizara hiyo, kitu ambacho ni kinyume kabisa na sheria ya PPA.

5: Kitu pekee kilichorejesha mchakato wa zabuni hiyo kwa Tanesco ni kutafutwa kwa saini ya kiongozi wa Tanesco ambaye hata hivyo alilazimishwa kusaini baada ya kuambiwa kwamba kama akikataa kitu chochote kingeweza kumpata;

6: Kwa maana hii basi, mchakato wote ambao uliishia kuipa Richmond kazi ya kufua umeme wa megawati 100, ulifanyika bila kuitishwa kwa zabuni kwa mujibu wa sheria ya PPA, lakini pia bila kushirikisha mamlaka zozote ambazo kisheria zinawajibu wa kushughulikia zabuni hizo, yaani Bodi ya Zabuni ya Wizara au Bodi ya Zabuni ya Tanesco (TTB);

7: Kwamba uchunguzi wa Kamati teule ya Bunge na ule wa Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA), uligundua kuwa Richmond haikuwa ni kampuni iliyosajilia kama jina lake lilivyokuwa linasema na hata jina la RDEVCO LLC ambalo pia Richmond ilikuwa inajitambulisha kwalo, ilikuwa ni kampuni nyingine tofauti kabisa na Richmond iliyoomba kazi ya kufua umeme nchini;

8: Kwamba Richmond ilitoa anwani sawa na ile ya RDEVCO, lakini ofisi zao zilipotembelea na Kamati ya Bunge, iligundulika kwamba (RDEVCO) haikuwahi kufanya shughuli yoyote ya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia na kwa maana hiyo haikuwa na ujuzi wala fedha za kuweza kutekeleza kazi hiyo iliyoomba;

9: Kwamba TTB yaani Bodi ya Zabuni ya Tanesco ilikuwa sahihi kabisa kwa kutupilia mbali maombi ya Richmond katika kutekeleza kazi hiyo, kwa kuwa haikuwa na uwezo na haikukidhi masharti ya tangazo la zabuni la kazi ya kuzalisha umeme wa dharura wa megawati 100;

10: Kwamba Wizara ya Niashati na Madini iliishinikiza TTB na Bodi ya Tanesco kuvunja sheria kwa kupunguza siku za kutangaza zabuni kutoka 45 hadi 20; lakini utarartibu unaokubalika na PPA wa ama kutafuta kampuni ya kimataifa (International Shopping au Single sourcing) ukiwekwa kando, kwa kuwa katika utaratibu huu Tanesco ingewajibika kutafuta kampuni yenye historia ya kufanya kazi ya kuzalisha umeme wa dharura ambayo Richmond moja kwa moja isingefikiriwa kwa kuwa ilikwisha kujuliakana haina uwezo;

11: Wizara ya Nishati na Madini ililazimisha Tanesco na Bodi ya Tanesco ibadili zabuni iliyokataliwa yaani Richmond kuwa iliyokubaliwa licha ya kuwepo kwa vigezo vya dhahiri kabisa, kitaalam na uwezo wa fedha, ambavyo vilikuwa vimekwisha kumweka kando Richmond; kwa kufanya hivyo sheria ya PPA ilivunjwa;

12: Kwamba kamati iliyoundwa na Wizara ya Nishati na Madini kushughulikia zabuni ya Richmond, haikuwa na mamlaka ya kufanya kazi hiyo, ilivunja sheria ya PPA hata kama ilikuwa imechukua wataalam kutoka Tanesco na Wizarani.

13: Kwamba kamati hiyo, yaani ya wizara, ilifanya mchakato wa zabuni wa kufufua umeme wa megawati 100 ambao ushindi alipewa Richmond, kwa kutumia nyaraka ambazo Bodi ya Zabuni ya Tanesco ilikwisha kuzifuta kwa kuwa Richmond ilishindwa kutumiza matakwa ya tangazo la zabuni;

14: Kwamba Richmond aliruhusiwa kuwasilisha nyaraka nyingine za ziada kwenye kamati ya Wizara, ambazo hazikuwa kwenye zabuni iliyotangazwa Februari 27, 2006 na kisha Richmond ikashindwa; kwa kifupi kulikuwa na utaratibu wa makusudi wa kuhakikisha Richmond inashinda;

15: Kwamba wakati Richmond ilisajili jina la RDEVCO LLC Machi 2008 hii ilikuwa ni baada ya matukio mawili, kwanza baada ya kuwa imekwisha kuingia mkataba na Tanesco Juni 23, 2006 kwa bosi wa Tanesco kutishwa ili asaini, lakini pia baada ya Dowans kuwa amekwisha kuchukua mkataba huo; Lakini pia jina hilo halikusajiliwa kwenye mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura uliofikiwa Juni 23, 2006.

16: Kwamba Mamlaka ya Manunuzi ya Umma (PPRA) ilithibitisha pasi na shaka yoyote kwamba mchakato wa ufungaji wa mkataba wa Richmond na Tanesco ulikiuka sheria ya manunuzi ya umma;
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom