Dowans: Another Richmond in making?


Kuandikwa na RAI = kazama kisiasa na kimaadili vile vile

Hii conclusion kali sana na labda ndio zinahitajika kuwaongoza watanzania wa aina yako ndugu yangu.

Nadhani umesahau kuwa RAI kumekuwa na uasi wa aina fulani lakini pia kuna uwezekano kuwa walioandika taarifa/makala hiyo wanalenga hukohuko ulikofikia na pia ni sehemu ya vita ya wenyewe kwa wenyewe ya CCM. Ni kweli kuwa msimamo wa Zitto unamweka katika hali ngumu KISIASA na hata kuwapa nafasi MAFISADI wa makundi yote ndani ya CCM kumtumia kuendeleza mapambano yao lakini kamwe hatuwezi kufikia cheap conclusion just because "ametetewa" na RAI.

omarilyas
 

Ni kweli kuna a lot of well wishers katika mjadala huu lakini KGM na moelex23 sio miongini mwao. Wao kwao hii ni nafasi ya "kummaliza Zitto" wanasahau kuwa tofauti na vijiwe vingine Jamboforum kuna watu makini wasiokubali kubabaishwa na cheap spinning kama zao. Mchango kama wako ndio tunaweza kusema kuwa una nia njema na Zitto pamoja na Tanzania yetu kwa ujumla. Keep it up


omarilyas
 

Nisaidie ndugu yangu mita ya Luku. Na huko kuunganishiwa chap ni muda gani, maana wengine twasubiri na vibanda vyetu vya madongo kuinama.
 
Wabunge wa ulaya wananguvu sana huyo rais angekua ulaya angekua ameshafanya press conf. Kama kumi kuhusiana na dowans
 

Wewe acha maneno mingi bwana, unataka kuniambia ZITO hajui anachokifanya?. Hivi unajua humu janvini Zito alifikia hatua ya kutukana watu? Hakujua alichokuwa anafanya?. Tulishaamua kupambana na MAFISADI basi hatua haja kumwangalia mtu usoni.

Zito ni Fisadi kama MAFISADI wengine hivyo hatuna urafiki naye maadamu tumeshaamua kupambana na mafisadi. Ukweli nikuwa tunasikitika lakini hatuna Jinsi. Mimi nimeshaandika huko nyuma kwamba Wapenda mageuzi tumepata pigo sana. Mimi sina umaarufu wowote lakini napenda mageuzi sana. Tuliyemweka mbele tukamwamini ametusaliti sasa unataka tucheke naye.

Fisadi ni Fisadi 2.
 

Mitambo haijatengenezwa na DOWANS ila DOWANS walinunua kutoka katika kampuni inayotengeneza mitambo hiyo. Katika hili naamini ni muhimu kufuatilia zaidi na kujua jinsi gani Tanzania itaathirika ama kufaidika itakapotokea matatizo yanayohitaji uhusika wa waliotengeneza mitambo hiyo na kujua mikataba kati ya DOWANS na hiyo kampuni inasemaje na kampuni yenyewe ina hali gani kwa sasa tukichukulia hali ya kiuchimu duniani.

Vilevile ni vizuri kujua kama KAMATI MASHIRIKA YA UMMA ambayo ndio iliyoamua kuishauri serikali kuangalia uwezekano wa TANESCO kununua mitambo hiyo ilishauri inunuliwe mitambo yote ikihusisha na ile iliyoletwa na RICHMOND ama ile tu iliyoletwa na DOWANS.

Vilevile ni muhimu kujua endapo Tanesco watanunua mitambo hiyo nini itakuwa mustkalbali wa madai ya Tanesco dhidi ya DOWANS na kama fedha ambazo Tanesco inadai DOWANS zitakuwa sehemu ya manunuzi hayo kama yekiwezekana.

Mimi kama mtanzania wa kawaida msimamo wangu ni Serikali kutaifisha mitambo hiyo lakini pia nahofia zoezi hilo lisije likatufikisha katika halia kama ya VALAMBHIA na manunuzi ya silaha ambayo mwisho wake ni hasara kubwa kwa taifa na ulaji usiokwisha wa wanasheria ukiacha athari kubwa kwa nadharia nzima ya utawala wa sheria ambayo serikali inapswa kuwa mfano wa kuigwa hata katika kulinda maslahi ya Taifa.

Again kaka ingawa una tone kali katika huu mjadala lakini wazi kuwa upo genuine katika nia na mawazo yako.

omarilyas
 


Mitambo tayari ipo ni $39million for 100MW mipya pamoja na warranty ya miaka 7 from the world biggest company of manufacturing Turbine and Jet engine ni kwenda kuchukua na kuwasha, hakuna kununua second hand kwa $60million.
 


Moelex23;
Usimpe mtu yeyote a blank check iwe Dr. Mwakyembe, Seleli, Mama Malecela, Zitto, Slaa etc.
  1. Zitto inaelekea (a) Ana-kaulevi ka madaraka aliyopewa kwenye kamati, (b) Ana-ukosefu wa uzoefu wa mambo ya uongozi na biashara (c) Ameonyesha kuwa ni mgumu kukubali hard criticism. Lakini at least he has a record behind him ya kupigania wananchi. Tusimuweke pembeni bali tuendelee kumdadisi na kumsaidia ikibidi.
  2. Lakini mtu kama Mama Malecela sio wa kuamini kabisa, she is a populist na sijaona matendo yake yakafanana na anayopigiaga kelele. Ameifanyia nini nchi hadi hivi sasa badala ya kujipandishia tu chati kwa kelele bungeni?
  3. Dr. Mwakyembe na Seleli wana maneno mazuri tunayotaka sikia, lakini hawajawahi kusimamia kidedea issues ambazo wanazijua kwa undani kuliko watu wengine na zina utata hadi leo (Richmond-Dowans). Baada ya kuandika ripoti, Dr. Mwakyembe akiwa ni mwanasheria, je wamefanya nini zaidi kuhakikisha kuwa Richmond-Dowans inakuwa dealt with once and for all?
Dont give anyone a blank check, they all need to qualify for one.
 

Kwa hiyo unadhani kuwa ni wewe tu mwenye haki ya kutukana watu. Sasa kwa kuwa Zitto ni mheshimiwa basi asikwambie kama ni mpuuzi hata kama madai yako ni ya kipuuzi?

Tatizo umezoea viongozi wanaowadanganya na kuwapamba kila wakati kwa minajili ya kura hata kama unakosea. Msimamo wa Zitto na ujasiri wake wa kutokunyenyekea wakati ukimtuhumu kipuuzi ndio uongozi tunaautaka ili tuendelee na sio siasa za matumbo ambazo wewe umezizoea....

omarilyas
 

Kaka Dr Mwakyembe hakuandika ile ripoti kama mwanasheria bali MAMLUKI WA KISIASA. Na hapa ndio tatizo langu na MWAKYEMBE hata kama alisaidia kuangusha KINARA WA UFISADI WA ENZI MPYA.....

Ripoti ilikuwa na mikogo ya kisiasa mno kiasi ya kwamba ikashindwa hata kujumuisha/kukusanya taarifa kuhimu ambazo kama zingekuwepo zingelisaidia sana kumaliza huu utata wa RICHMOND?DOWANS.

Kingine ni lazima tutambue kuwa kuna ushindani mkubwa kati ya kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma(POC) na kamati zingine kamati ya nishati na madini. Hizi kamati zingine zimekuwa zikijaribu kuinyang'anya kamati ya mahesabu ya mashirika ya umma baadhi ya majukumu yake ama kwa nia njema lakini pia kutaka kujipatia ulaji. No wonder Mwakyembe alispin suala la posho wakati akijua wazi msimamo wa Zitto kupinga suala la posho kutoka katika asasi za umma katika suala hilo tangia alipopewa madaraka ya uenyekiti wa hiyo. Kitu ambcho kilipeleka hata kuanza kwa uhasama na baadhi wanakamati wake ambao wanaamini posho hizo ni haki yao.


omarilyas
 
Last edited:
Kaka, huku kwetu ukituma maombi ya Luku unapewa 21 days baada ya kukamilisha malipo watakuwa wameshafunga ila sanasana wanachukua 14 days tayari stima imeshapatikana, na mgao haupo tena, labda kama kunamatengenezo kama kuondoa matawi ya miti kwenye nyaya.

Juzi niliumwa sikio na mtu wa tanesco kuwa mita zimejaa tele stoo. Lugha chafu pale reception sasa hakuna nasikia wanafundishwa customer care.
 

Kwani Hawa DOWANS haswa ni nani? Na wali-urithi makataba wa Serikali na Richmond katika mazingira gani. Je kulikuwa na Tenda ya wazi?

Huyu Idris Rashid, alikuwa wapi wakati Richmond inapewa mkataba. Hivi wakuu ni lini aliingia Tanesco?
 

===============
Breaking News: 100% verified.

Tayari keshapata taarifa kwamba mitambo mipya ipo tayari kutoka kwa biggest manufacture of Gas turbine na bei yake ni $39million for 100MW ndo maana hakupenda kusema uongo mbele ya waandishi wa habari maana angejimaliza moja kwa moja. Mitambo hipo tayari ni kwenda kuchukua tu na kuwasha. Warranty ni 7 years with commissioning for 30 years. hiyo mitambo Serikali watakaa nayo kwa miaka 40-50. hiyo mipya toka kwa huyo manufacture . Mtambo mpya kwa hali ya kawaida ni $35-46million na siyo $90million labda kama inatengenezwa mbinguni.
 

KGM,
Una ushahidi gani wa hiyo accusation yako? I disagree with Zitto kwa jinsi alivyolishughulikia hili suala la TANESCO-DOWANS, lakini ku-conclude kuwa yeye ni fisadi kwa vile tu amesema ambacho Rostam anataka kusikia, ni kuonyesha kuwa ulikuwa una nia ya kumpa hiyo branding no matter what na ulikuwa unatafuta tu nafasi ya kufanya hivyo kwani hakuna ushahidi wowote wa ufisadi wa Zittto.
 
Omari kaka, sio "spin" sasa makampuni makubwa yanaajiri Strategic Managers/Directors, kwa ajiri ya kuandaa Long term objectives na strategic missions. Kuna pia "Strategic Business" ambayo inatakiwa iwe directed na huyu Strategic Manager.
 
Omari kaka, sio "spin" sasa makampuni makubwa yanaajiri Strategic Managers/Directors, kwa ajiri ya kuandaa Long term objectives na strategic missions. Kuna pia "Strategic Business" ambayo inatakiwa iwe directed na huyu Strategic Manager.

Kuhusu ajira sina uhakika lakini naamini wanayo master plan tatizo inakingana na sera na maamuzi ya kisiasa hivyo huwa inabidi kuwekwa viraka kila wakati kutimiza matakwa ya wakati uliopo na kukingana na matakwa ya muda mrefu...

omarilyas
 
Kwa majibu hayo machache tu inaonyesha kuwa kwa msimamo wa Serikali, Dr. Mwakyembe na kundi lake wameanguka na Mh. Zitto na kundi lake wameibuka kidedea.

Lakini tusubiri filimbi ya mwisho..

Mkuu, sidhani hapa ni suala la kuanguka kwa Mwakyembe and his so-called "kundi lake", ni kuanguka kwa Watanzania wote mikononi mwa mafisadi! Ngeleja na Idris Rashid ni kundi moja na Rostam Aziz lenye historia kutokea VODACOM ambalo Rostam analitumia kama atakavyo, mithili ya toilet paper. Wenye nchi tutahakikisha Ngeleja anafuata mkumbo wa akina Karamagi. Akina Zitto na utumwa wao wa fedha wataishia kudhalilika tu.
 
==========

Well said. Binafsi niko tayari kumpa another chance and benefit of doubt ikiwa atarudi jamvini na kushughulikia hii hard ball.
Ni kweli kauzoefu kanapungua kwa kijana huyu. Lakini tufanyeje, in the absence of ... hata mwenye jicho moja tunamshangilia.
 
Hakuna anayezuia kununua mitambo bali ni sheria.Pia wabunge wanaingizwa "choo cha kike" kwani Tanesco yenyewe inaogopa kununua mitambo hiyo ndio maana wanataka kuwauzia wabunge ili lolote litakapo jitokeza lilaumiwe bunge.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…