Dotto Biteko: Tumsaidie Rais Samia kujenga Nchi

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,532
Reaction score
3,192
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko amewashukuru marafiki na wanafunzi aliosoma nao katika Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustine Mwanza (SAUT) na kuwataka kufanya kazi kwa bidii ili kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan kutimiza azma ya kujenga uchumi wa nchi na Watanzania.

Ujumbe wa Marafiki waliosoma na kiongozi huyo ukiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Hai, Saashisha Mafuwe umetoa pongezi kwa Dk. Biteko kwa kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.
 
Ngoja nimalizie kujenga kwangu kwanza nitakuja kumsaidia kama muda utapatikana
 
..Biteko anaonekana amepwaya ndio maana kaletwa Makonda kusaidia kutafuta kura za kanda ya ziwa.
Mbona mapema hivi? Kubadili watu wanachokiamini uhitaji muda.....
 
Huyu nae Kila siku ni kuongea ongea misemo mipya harafu hakuna anacho deliver
 
Cement ipi tutumie kujengea nchi

Ova
 
Ujumbe wa Marafiki waliosoma na kiongozi huyo ukiongozwa na Mbunge wa Jimbo la Hai, Saashisha Mafuwe umetoa pongezi kwa Dk. Biteko kwa kuteuliwa na Rais Samia Suluhu Hassan kuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati.
Hawajamwambia awakumbuke katika ufalme wake?
 
Jamaa kapewa kazi, badala ya kufanya kazi ANAFANYA UCHAWA.

Pumbavuuu
 
Hiki cheo cha naibu waziri mkuu ni kipya kabisa au huwa kipo kikatiba?
 
Unamsaidia mtu anayetaka kusaidiwa ,mtu anaiba na rais yupo tu anaishia kusema stupidi basi hachukui hatua unategemea nini
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…