kuna mada niliiweka miaka kadhaa iliyopita humu Jf kuhusu namna ya kutunza magurumu ya gari. Itafuteni, bado ni nzuri. Thread Inaitwa 'Je matairi yako ni salama?
Weka link boss sio kila mtu anaweza kuitafuta
1.Epuka sana safari fupifupi kwani kawasha gari na kuizima kabla ya nusu saa hivi,engine inakuwa haijapata joto la kutosha hivyo inasababisha uchakavu wa haraka zaidi kwa engine.
2.Kupandisha au kushusha power windows gari ikiwa imezima ni kosa la jinai! Hii inapelekea betri kufa mapema zaidi!
du kali kweli ishi na watu upate vitu
aisee nimepata shule zaidi hapa aisee.....
Nashukuru mkuu
Heri muwasaidie kwani wengi ni wale waliojifunzia kwenye kupiga raundi mtaani, mafunzoni waliona km wamewekewa makanika na madereva wa malori/ofisi so hawakuona umuhimu wa kwenda na matokeo yake hata matunzo ya vimeo vyao hawajui
Usiendeshe gari ukiwa umenuna! Hii huchangia ajali za barabarani!
kama gar gan mkuu!Gari yako ya mwaka gani? yani kabla ya kuzima kila saa uzime radio na ac kwanza!!!! nunua gari za kisasa zinazojua ni muda gani radio izimwe bila ya wewe kuzima hasa unapoiwasha.
Ikiwezekana jaza mafuta kwenye kituo kimoja na kutosha kumalizia mizunguuko ya siku hiyo ili kama kuna tatizo la mafuta ni rahisi kufuatilia historia ya ujazaji wa mafuta (sio unajaza lita 2 kituo hiki ukipiga misele kidogo inazuka safari nyingine unajaza kituo kingine na wakati wa kurudi tena unajaza wese kituo kingine)
kama gar gan mkuu!
Nyongeza
15. Hakikisha "site mirror" zako zote hazina hitilafu kuona na kupata taswira ya maderreva wenzango wa kila upande.
16. Usishindane na wenzio barabarani wapishe wababe, wasaidie wenye matatizo ya uendeshaji maana utawaona tu wanavyojikanganya.
17. Traffic ni rafiki si adui msemeshe kwa upole na hoja.
18. Epuka misafara maana haizingatii sheria za barabarani.
19. Ukitaka kuwahi kwenye foleni unga nyuma ya ambulance ikibahatika kupita na si msafara
20. Uwe na fundi mmoja tu wa kutengeneza gari hata kama ni wa chini ya mti.
21. Jitahidi uijue gari yako kama unavyomjua mwenza