Do's and Dnt's kama unalipenda Gari lako

Do's and Dnt's kama unalipenda Gari lako

Mkuu kama una garage ya uhakika nikuletee VW yangu nipi mbeya huku kumwaga oil tu mafundi wanaharibu waneshaniharibia sana hii gari next month mwishoni nakuja nayo mjini kuitengeneza kama upi fit nikutafute matatizo mengi ni umeme lakini
Samahani nimeajiriwa na kampuni ya utalii hapa Arusha yenye magari kama 500 hivi. airuhusiwi kufanyia kazi gari isiyo ya kampuni hata la kwangu nafanyia nje. Ila kwa ushauri uwe na uhakika nitautoa bure.
 
  1. Zima gari lako unapopaki hata kama unaingia na kutoka. Utaokoa mafuta yako
  2. Warmup unapowasha gari asubuhi ni upotevu wa mafuta, anza kuendesha tu taratibu (unless upo Makete 🙂)
  3. Ukiwa kwenye foleni ndefu zima gari pamoja na taa uache parking lights tu
  4. Epuka breki za ghafula, unamaliza mafuta, na breki zenyewe
  5. Kama hakuna joto wala vumbi, kiyoyozi cha nini? :shock:

Najua kuna gari za kisasa zinajizima, au ku "sleep" unaposimama hasa kwenye folini ya zaidi ya sekunde kadhaa, na kujiwasha tena ukitoa handbrake au kuanza tena safari.

Ila kwa magari yetu haya ya kizamani, sina uhakika sana na hizi pointi, zinahitaji wajuzi kuchangia.

Ku warm-up gari asubuhi ni muhimu, na sio kwa maresi mengi au kwa muda mrefu. kuzima zima gari na kuyawasha tena kwenye mafolini yetu naona kama ndio unatumia mafuta zaidi, maana kila unapozima mafuta yanarudi kwenye tangi na ule mlolongo wa mafuta kwenda kwenye engine unakatika, ukiwasha tena mafuta mengi zaidi yatatumika kuiwasha gari, nahisi kama mafuta yanatumika zaidi kuliko kuliacha gari silenti.

Ebu wataalam watujuze....
 
1. Hata kama uko makete hakikisha walau mara moja kila wiki unawasha AC kwa muda usiopungua nusu saa kusudi AC ya gari yako idumu.
2. Kila baada ya kupita kwenye mazingira yenye vumbi vumbi kagua cabin filter, ibadilishe ikibidi ili AC yako iendelee kukupa hewa safi
3. Epuka safari za mwendo mdogo (mf below 60km/hr) kwa muda mrefu. Kama kuna ulazima wa kusafiri kwa spidi ndogo kila mara (kwa sababu ya foleni au ubovu wa barabara) hakikisha unapata safari ya mwendo kasi (angalau 80km/hr) kila wiki au baada ya wiki mbili kuiweka gari katika hali nzuri
4. Usisahau betri za maji zinahitaji ku-refill mara kwa mara ili betri yako idumu
5.Taa ya oil ikiwaka wakati wowote gari ikiwa inatembea hakikisha unapunguza mwendo haraka na kusimama ( haijalishi kama uko katikati ya serengeti). Ni kwa faida yako na gari yako.
6. Taa yoyote (hasa usiyoielewa) ikiendelea kuwaka kwenye dashboard (hata kama gari inaweza kutembea) waone wataalamu mara moja.
7. ....mengine itabidi tuweke tozo kidogo...ha ha ha...watu wanaweza kugraduate humuhumu bure..lol
 
  • Thanks
Reactions: ram
Wanasiasa wanafiki sana.
Huwa hawaoni kabisa positove side ya JF.
Imagine watu wangapi wamefaidika na hii thread!
Big up Chemwali

Umeona eeh?
Wao wanaangalia jukwaa la siasa tu, kujua wameandikwaje. Hawawazi kuwa hapa tuna majukwaa ya kila namna, kuanzia sheria, elimu, michezo na teknohama.
 
1. Hata kama uko makete hakikisha walau mara moja kila wiki unawasha AC kwa muda usiopungua nusu saa kusudi AC ya gari yako idumu.
2. Kila baada ya kupita kwenye mazingira yenye vumbi vumbi kagua cabin filter, ibadilishe ikibidi ili AC yako iendelee kukupa hewa safi
3. Epuka safari za mwendo mdogo (mf below 60km/hr) kwa muda mrefu. Kama kuna ulazima wa kusafiri kwa spidi ndogo kila mara (kwa sababu ya foleni au ubovu wa barabara) hakikisha unapata safari ya mwendo kasi (angalau 80km/hr) kila wiki au baada ya wiki mbili kuiweka gari katika hali nzuri
4. Usisahau betri za maji zinahitaji ku-refill mara kwa mara ili betri yako idumu
5.Taa ya oil ikiwaka wakati wowote gari ikiwa inatembea hakikisha unapunguza mwendo haraka na kusimama ( haijalishi kama uko katikati ya serengeti). Ni kwa faida yako na gari yako.
6. Taa yoyote (hasa usiyoielewa) ikiendelea kuwaka kwenye dashboard (hata kama gari inaweza kutembea) waone wataalamu mara moja.
7. ....mengine itabidi tuweke tozo kidogo...ha ha ha...watu wanaweza kugraduate humuhumu bure..lol

hebu tufafanulie kwanini niepuke kuendesha 60km/hr....kwa sabubu nijuavyo mimi 60km/h ni nzuri kwa ulaji wa mafuta na usalama wako na watumiaji wengine wa barabara(speed limit sehemu nyingi urban ni btn 40-60km/hr

 
hebu tufafanulie kwanini niepuke kuendesha 60km/hr....kwa sabubu nijuavyo mimi 60km/h ni nzuri kwa ulaji wa mafuta na usalama wako na watumiaji wengine wa barabara(speed limit sehemu nyingi urban ni btn 40-60km/hr

Ni masuala ya lubrication kwenye moving parts, ni darasa refu kidogo lkn yatosha tu kusema kwamba hayo uliyoeleza ni sahihi (ukiacha la ulaji wa mafuta) lakini pia kuna pros and cons kwa kila jambo. Mengine not that much obvious. Pokea tu huo ushauri kama unataka engine, wheel-bearings etc zidumu
 
Samahani nimeajiriwa na kampuni ya utalii hapa Arusha yenye magari kama 500 hivi. airuhusiwi kufanyia kazi gari isiyo ya kampuni hata la kwangu nafanyia nje. Ila kwa ushauri uwe na uhakika nitautoa bure.

Okay Thanks Mkuu hata kwa ushauri bado utakuwa na msaada sana kwangu
 
Nejifunza mengi. Kweli gari ukikaa nalo kwa kipindi flani linakuwa kama mtu that unaongea nalo kama mwanao u can't miss it even a day.
 
da jamani pamoja na yooooooooooooooote hakikisha una kidumu kwenye buti jamani maana du....unaweza kuumbuka aisee.....
 
Kagua maji, engine oil, brakes, na tairi zote kabla ya kuondoka. Pia usione raha kufukia mashimo gari linapo kuwa jipya kwani utaua bush na shockups zote ndani ya mudamfupi.
 
Asante wakuu kwa shule. JF is everything, kuna Great Thinkers katika kila angle. Kila ninachokijua katika gari naona kimedondoshwa hapa kwa usahihi kabisa. Keep it up the spirit people. Halafu kina Juma Ngamia (bingwa wa matusi ya nguoni) anataka JF ifungwe!!! Sijui ni liandishi gani la habari hili ambalo halijui faida za social forums, hasa JF ambayo ina kila jukwaa hadi la afya, mapishi. Tupilia mbali hili Lingamia 2015.
 
-Na kwa Wale mnaopenda harufu nzuri ndani ya gari kuweni makini na airfresher ambazo mnaziweka kwenye dashboard hapo kwenye kioo cha mbele au kioo cha nyuma ziko ambazo zikipata joto sana (kama umepaki juani kwa muda mrefu) hulipuka kwa kishindo kikubwa kama bomu na kupasua kioo chot
-Pia watumiaji wa Simu za Android mnaweza kudownload application inayoitwa Logbook katika Playstore na kutumia Simu yako kuweka record mbalimbali za gari yako.
 
6. Akina dada, epuka kuendesha gari huku mmevaa skuna mchongoko (kama si mzoefu) Beba flati za kukanyagia.

7. Epuka kunywa soda zenye gesi au vinywaji baridi vyenye gesi wakati unaendesha kwani hufanya mapigo ya moyo kuongezeka.
 
Back
Top Bottom