Domestic violence

Domestic violence

Roulette

JF-Expert Member
Joined
Dec 15, 2010
Posts
5,568
Reaction score
5,387
Domestic violence (Kwa maana ya language, physical or sexua abuse/assault) ni jmabo linanikera sana na linanitia udhuni. Kwa muda mrefu niliwaza kuweka thread yenye kuhusu domestic violence ila sikujua from which angle to tackle the matter. I am not sure this is the best way to share what I had to say. If you have more on domestic violence please changia, kwa mifano maoni au critics.

Nimefanya kazi na majeruhi wa domestic violence na wote nimekutana nao hadi sasa ni wanawake (ingawa majeruhi wa kiume wapo pia). Kwenye thread hii tutazungumzia majeruhi wa kike zaidi. Suali langu la mwanzo lilikua hili: kwanini majeruhi wa domestic violence hawajitokezi ili hatua za kijamii na za kisheria zichukuliwe dhidi ya wenzao? Suali lingine lilikua kwanini wanaume wanaamua kuwapiga au kuwa-assault wake zao regularly and still pretend to love them? Mwisho kabisa nilijiuliza ni namna gani tunaweza kusaidia couples zenye matatizo haya (maana kuna ambao wanayamaliza kabisa na kuendelea vizuri, wengine wanaumia physically or emotionaly kwa muda mrefu sana)

Katika maongezi yangu na majeruhi nilipata majibu mbali mbali ila jibu lililo rudi zaidi ni kwamba wanaogopa kua indexed as wasaliti wa ndoa zao. Jamii zetu hazina huruma kwa wanawake kama ilivo kwa wanaume hivo mwnaamke anae mshtaki mwanaume kuhusu domestic violence anaonekana hafai kua mke mwema sababu anashindwa kutunza siri za ndani ya ndoa na sometimes the blame goes as far as "kama alipigwa kuna sababu aulizwe vizuri" or "kama alibakwa maana yake hakumpa mume haki yake".
Jibu lingine ambalo sikutegemea ni kwamba wanaogopa mahusiano kuisha. Sio tu kwa financial and social comfort (ingawa kuna ambao walikiri hili lipo), but because they are genuinely in love with the guy na wanahisi kushtaki kutavunja mahusiano yao and she will miss him because even after what he did she still loves him.

Kwa kujibu swali la pili nilielekea wataalam wa kisaikolojia ambao walinambia mara nyingi wanaume wanao abuse wake zao wanafanya hivo sababu hawana uwezo wa kupata suluhisho kwa matatizo yanayo wakabili. They have developed a diagram whereby any problem is solved through violence that divet the attention from real existing problems as the defeated opponent is left to deal with trauma. Baada ya kupigwa ubishi ukiendelea unakua "kwanini ulinipiga" which is an easy question to deal with: you didn't listen.
Tatizo hili linaisha mwanaume anapo funnzwa njia zingine za kumaliza matatizo kwa kupitia maongezi ya moja kwa moja au kwa kupitia mediator. Ni jambo linaweza kushangaza sana kua mwanaume mzima hajui kwamba matatizo yanaisha kwa kuongea. wanaume kadhaa walisema kumaliza matatizo kwa kuongea ni alama ya udhaifu sababu wanalazimika kukaa kimya na kummsikiliza mwenzao, au wanalazimika kufanya concession.

Tafiti zimeonesha kua couples zenye uhakika kua ndoa haito vunjika baada ya kuzungumzia masuala haya na watu wa nje zipo more willing to share, na pia couples zinazo jifungua kwa third parties (Baraza za familia, wachungaji wa dini, support and sharing groups, matrone au best men etc) kuhusu matatizo haya zina uwezo mkubwa zaidi ya kumaliza matatizo yao na kuendelea maisha ya kawaida, mnamo muda mfupi zaidi kuliko couples zinazo jifungia na matatizo yao.
Bahati mbaya washahuri wengi wa kwanza (just as the violence occurs, and the victim talks to a friend or a sibling) wanashahuri kuvunja mahusiano hivo kuwafanya majeruhi kuto rudi tena kulalamika ikiwa violence inatokea tena. Hapa pia ilionekana kua majeruhi wengi wanajifungua zaidi kwa ndugu zao wenyewe au kwa rafiki zao, ila wale walio jifungua kwa ndugu wa mume au kwa rafiki wa mume/wa couple, walishahuriwa kumaliza matatizo bila kukata mahusiano (not always but often)

Vitu kadhaa niligundua ni kwamba
  1. mwanaume kumpiga mwanamke doesn't necessarily mean hampendi, but it certainly means ni hatari kwa mke wake.
  2. Mwanamke anae mvumilia mume wake ambae ni abusive doesn't necessarily do it because she is weak and intimidated, it could also mean she had alternatives but decided to do this.
  3. Jamii ina role kubwa sana ya ku-play katika kusaidia couples ku-recover from such a climate (mfano wanawake walio pata support ya familia in rural area walirecover in 2-4 month, wale walio ikosa but walipitia a psychiatrist to deal with it, in urban area walipona baada ya miaka 2)

* All studies zinapatikana on demand via PM (please note that most of them are in french)
 
Naskia Wanawake wa Kikuria kule Mara asipopigwa na mumuwe anaona kama vile mume hampendi!

Hadi lini Western civilization will stop lecturing to we Africans how we should love our women? Do we as Africans need to read a book how to love each other? Remember we have been living and loving each other for centuries!!
 
Naskia Wanawake wa Kikuria kule Mara asipopigwa na mumuwe anaona kama vile mume hampendi!

Hadi lini Western civilization will stop lecturing to we Africans how we should love our women? Do we as Africans need to read a book how to love each other? Remember we have been living and loving each other for centuries!!
Hizi tafiti ni za africa, na walio jibu ni waafrika. Kwa hiyo sioni hayo ya kuwahusisha wazungu yametoka wapi.
Hayo ya mwanamke kusema akipigwa ndio anapendwa nimekutana nayo pia, ila nilipotaka kuelewa nilihisi they meant display of jealousy, not the beating. Mfano walisema katika kuonesha mapenzi yao wanaume wanaruhusiwa kupandisha sauti na sometime kofi linaruhusiwa pia. Ila sio kupigana hadi mnatoana meno au kuvunjana miguu
 
Whaaat?!
Hiyo conxlusion namba moja siikubali. Huwezi kumpenda mtu na kisha ukampiga na kuendelea kumpenda. Lakini above all ukishampiga mtu sidhani kama atakupenda ever again ( anaweza kubaki for security, status ama mali lakini sio upendo.)

Watu wanaopigwa na wanakataa kuchukua hatua ni kwa sababu mostly wameaminishwa kuwa walistahili kipigo. Kwa kweli kama kuna kitu ambacho sidhani naweza kutolerate ni physical and sexual assault. I feel hysterical even thinking of it! Kuna mtu anapigwa na mqenza wake na ukimuambia kuwa wewe hujawahi guswa haamini na anaona unasema uongo. Jamii imetubrainwash haswaa. Ni kama ilivyo ngumu kwa mwanaume kusema napigwa na mke wangu. Hatapata support hata kutoka polisi unless he is bleeding enough!
 
Mie sijakutana nazo kwenye ndoa lkn nime experience hizo katika mazingira ya kazi..Mara nyingi wanaume wana abuse wanawake hasa wakihisi kuwa ni threat kwao kwa namna yoyote au kama wanawataka kimapenzi..Hii inaathiri kwa kias kikubwa carrier ya mwanamke na wanawake mara nyingi wanakaa nayo moyoni kwa sababu hata wakisema msaada haupo zaidi ya kujidharirisha
 
Whaaat?!
Hiyo conxlusion namba moja siikubali. Huwezi kumpenda mtu na kisha ukampiga na kuendelea kumpenda. Lakini above all ukishampiga mtu sidhani kama atakupenda ever again
Ushapiga cha Arusha mchana? Mama yangu alininyuka sana enzi hizo na mpaka leo nampenda upeo. Na kama si kichapo chake mida hii labda ningekuwa Segerea nanyea ndoo. Kichapo saa nyingine kinasaidia mtu kurekebisha tabia.

Yani nikufumanie unalabuliwa kitandani kwangu afu nisikupe za uso? Ntakuchapa sana tu. Afu naweza kukusamehe vilevile na maisha yakasonga mbele.
 
Ushapiga cha Arusha mchana? Mama yangu alininyuka sana enzi hizo na mpaka leo nampenda upeo. Na kama si kichapo chake mida hii labda ningekuwa Segerea nanyea ndoo. Kichapo saa nyingine kinasaidia mtu kurekebisha tabia.

Yani nikufumanie unalabuliwa kitandani kwangu afu nisikupe za uso? Ntakuchapa sana tu. Afu naweza kukusamehe vilevile na maisha yakasonga mbele.

Job true
 
Whaaat?!
Hiyo conxlusion namba moja siikubali. Huwezi kumpenda mtu na kisha ukampiga na kuendelea kumpenda. Lakini above all ukishampiga mtu sidhani kama atakupenda ever again ( anaweza kubaki for security, status ama mali lakini sio upendo.)

Watu wanaopigwa na wanakataa kuchukua hatua ni kwa sababu mostly wameaminishwa kuwa walistahili kipigo. Kwa kweli kama kuna kitu ambacho sidhani naweza kutolerate ni physical and sexual assault. I feel hysterical even thinking of it! Kuna mtu anapigwa na mqenza wake na ukimuambia kuwa wewe hujawahi guswa haamini na anaona unasema uongo. Jamii imetubrainwash haswaa. Ni kama ilivyo ngumu kwa mwanaume kusema napigwa na mke wangu. Hatapata support hata kutoka polisi unless he is bleeding enough!

Hun, huu naandika ni ukweli kabisa. Hata mimi niliamini kua mwanaume akimpiga mwanamke maana yake hampendi but unajikuta unaongea na mwanaume na unaona kua anampenda mwenzie na anajuta sana kufika alikofika na all he wants ni kurudisha mambo kama kawaida. He even tells you a series of resolutions he has taken to make sure it doesn't happen again. Ila sasa next time wanapata matatizo na anahisi mke wake is about to be right and him being wrong, ana ona ataweza kuyamaliza kwa intimidation na hatimae he becomes violent. Later ukiongea na wanaume walio saidiwa na wakajifunza how to deal with their vilent habits you realise that they were suffering too, somehow.
 
Mie sijakutana nazo kwenye ndoa lkn nime experience hizo katika mazingira ya kazi..Mara nyingi wanaume wana abuse wanawake hasa wakihisi kuwa ni threat kwao kwa namna yoyote au kama wanawataka kimapenzi..Hii inaathiri kwa kias kikubwa carrier ya mwanamke na wanawake mara nyingi wanakaa nayo moyoni kwa sababu hata wakisema msaada haupo zaidi ya kujidharirisha
I have delt with abusive men in the work place. Mwanaume anatoka na mentality zake za kichauvinist and macho huko anadhani wanawake wote ni sawa. Ofisini hakuna cha mwanamke na mwanaume, kuna professionals na kila mtu afanye kazi yake. If you can't do the job somebody else will do it, full stop.
 
Haya mambo yapo sana katika jamii nyingi za kiafrika na hata nje ya Afrika yaani Ulaya na Amerika japo kwa wenzentu ni kwa viwango vya chini tofauti na huku kwetu.

Binafsi nahisi hili ni swala gumu sana kuliondoa kwenye jamii zetu tunamoishi. Imagine watu kabla ya kuoana (sio wote) japo majority wanakuwa wanapendana sana, ukiwatazama unaweza kudhani haipo siku hata watakuja kukwaruzana, lakini hali ni tofauti sana pindi wanapokuwa pamoja as a family. Sisemi kwa vile kukwaruzana kupo, then solution ni mmoja kumpinga mwenzake la hasha, lakini ikumbukwe pia sisi tumelelewa katika culture tofauti, ambapo kwa namna moja ama nyingine unaweza kukuta mmoja wetu especially mwanaume anatoka kwenye jamii ambayo kwayo mke kupigwa once amekosa ni normal, hakika hili litatokea.

Wengine wanafikia hatua ya kuwapiga wake zao baada ya swala la majadiliano ama maonyo kwa njia ya mdomo kushindikana na hivyo kuishia kupandwa na hasira kupita kiasi na kujikuta wamewapiga. Hawa baada ya kitendo huwa na aina fulani ya majuto moyoni mwao maana huwa sio kusudio lao.

Wanawake wengi wamejaliwa sana uwezo mkubwa wa kuongea maneno mengi kwa muda mfupi, so mnapokuwa kwenye mgogoro na katika harakati za kutatua mgogoro hili jambo huchangia wanaume wengi aidha kupandwa na hasira na kujikuta wakitoa adhabu ya kichapo.

Wapo wanandoa wengi pia ambao wamejikuta kwenye ndoa pasipo upendo wa dhati kwa pande zote, mfano mwanamke anampenda mwanaume na kushinikiza ndoa kwa njia yoyote ile mfano njia za giza (ushirikina) nk, vile na kwa wanaume ama mtu anachelewa sana kuolewa, umri unakwenda siku akijitokeza mtu hata kama hampendi anasema acha tu niolewe nami nipate jina na heshima Mrs somebody, so watu wa namna hii aina yoyote ya tofauti wengi wao (sio wote) huishia kwenye mapigano nk.

Na kuhusu hayo mambo mengine mara mume kabaka mke, dah inakuwa ngumu kulitolea maelezo kwamba sababu ni nini, lakini kwa nini hili litokee kama mtu uko mzima na afya yako, hii inaweza changia ama kuchangiwa na mambo ya cheating ndani ya ndoa. Imeandikwa tusinyimane kwenye ndoa (Mume ampe haki yake mke na vice versa is also true)

Mwisho kabisa watu wanatakiwa kuishi kwa upendo kama tunavyoelekezwa na Mwenyezi Mungu. Tumeaswa tupendane hii ndio amri kuu kuliko zote tuliyopewa na kwa kufanya hivyo hayo mambo mengine tutapata kwa ziada, kumbe basi ili kulifanikisha hili tumrudie Mwenyezi Mungu, imeandikwa mume ampende mwanamke kama anavyojipenda yeye mwenyewe na mwanamke amheshimu mwanaume.
 
Hapo kwenye abusive language mie napaona pagumu

Manake kuna mwengine ukimwambia "huna adabu" anaona ushamu-abuse kupita maelezo

Akakushtaki kwa hilo?
 
ahsante Roulette kwa kusikia ombi na kilio changu!(u knw wat i mean,ryt!)
well.
domestic violences zipo sana na kwa kweli zinaumiza sana mahusiano katika jamii
na wala sio katika ndoa na mapenzi tu!
kuna maisha ya wanaotutegemea au walio chini ya paa la nyumba zetu!
mabinti wa kazi ni wahanga sana katika hili!
watoto tunaowalea wanaathirika sana na hili
wakati mwingine hata watoto wetu wa kuwazaa ni wahanga!

fikiria mfano wa binti anayebakwa na kila member wa kiume wa familia fulani!
fikiria kuhusu mtoto anayelazimishwa kushuhudia mzazi wake akidhalilisha iwe ni kwa matusi,kipigo au kingono!
fikiria kuhusu watoto wanaoishi na mzazi asiyejua adhabu na aina tofauti ya kukanya zaidi ya kuchoma moto viungo vya mtoto
fikiria kuhusu mwenza anayeshuhudia mwenza wake wa ndoa akileta na kufanya uchafu wa kuumiza hisia mbele yake
fikiria kuhusu mwenza asiye na tafsiri nyingine ya hasira zaidi ya matusi na kutesa
fikira kuhusu mtoto anayezaliwa kwenye mazingira ya kukataliwa(binti kazaa na babake,dada kazaa na kakake,na nyingine za aina hiyo!

hizi zote jamii hazioni kama ni tatizo
pengone kwa kutokujua upana na uhalisia wake
pengine kwa kutokukubali kuwa lipo
pengine kwa wahusika kutokubali uwepo wake
laini pengne kwa jamii kuona kuwa ,suluhisho ni kukaa kimya kwa kuhofia athari zaiid ya hizi!
maumivu yanabaki kwa wahusika au kwa mhusika !na bahati mbya huwa hakuna anayejua siri ya ndoo au mtunzi zaidi ya kata!
 
Last edited by a moderator:
Hapo kwenye abusive language mie napaona pagumu

Manake kuna mwengine ukimwambia "huna adabu" anaona ushamu-abuse kupita maelezo

Akakushtaki kwa hilo?
Ikiwa mtu hana adabu kweli na unaweza kumpa mifano ya vitu amefanya kwanini usimwambie? But I have to admit kua, as it is kwa mambo yote ya mahusiano, hili nalo linahitaji watu kufahamiana na somehow kukubaliana hata tacitely.
Abusive langunguage (inayo husiana na vilence) ninayo ongea hapa ni pale mwanaume anampandishia mwanamke sauti na kumwambia maneno machafu/mabaya hadi mwanamke anakua traumatized na anaogopa hata kusema kua she is living those things.
 
ahsante Roulette kwa kusikia ombi na kilio changu!(u knw wat i mean,ryt!)
well.
domestic violences zipo sana na kwa kweli zinaumiza sana mahusiano katika jamii
na wala sio katika ndoa na mapenzi tu!
kuna maisha ya wanaotutegemea au walio chini ya paa la nyumba zetu!
mabinti wa kazi ni wahanga sana katika hili!
watoto tunaowalea wanaathirika sana na hili
wakati mwingine hata watoto wetu wa kuwazaa ni wahanga!

fikiria mfano wa binti anayebakwa na kila member wa kiume wa familia fulani!
fikiria kuhusu mtoto anayelazimishwa kushuhudia mzazi wake akidhalilisha iwe ni kwa matusi,kipigo au kingono!
fikiria kuhusu watoto wanaoishi na mzazi asiyejua adhabu na aina tofauti ya kukanya zaidi ya kuchoma moto viungo vya mtoto
fikiria kuhusu mwenza anayeshuhudia mwenza wake wa ndoa akileta na kufanya uchafu wa kuumiza hisia mbele yake
fikiria kuhusu mwenza asiye na tafsiri nyingine ya hasira zaidi ya matusi na kutesa
fikira kuhusu mtoto anayezaliwa kwenye mazingira ya kukataliwa(binti kazaa na babake,dada kazaa na kakake,na nyingine za aina hiyo!

hizi zote jamii hazioni kama ni tatizo
pengone kwa kutokujua upana na uhalisia wake
pengine kwa kutokukubali kuwa lipo
pengine kwa wahusika kutokubali uwepo wake
laini pengne kwa jamii kuona kuwa ,suluhisho ni kukaa kimya kwa kuhofia athari zaiid ya hizi!
maumivu yanabaki kwa wahusika au kwa mhusika !na bahati mbya huwa hakuna anayejua siri ya ndoo au mtunzi zaidi ya kata!

Asante sana kwa kupanua definition ya domestic violence. Nadhani masuali yangu ya mwanzo yanahusika pia hapa ingawa hatuwezi kupata jibu la uhakika hapa, but we can still share thoughts: Kwanini victims hawajitokezi? Kwanini pepetrators wanafanya hivo na ni kitu gani sisi kama jamii tunaweza kufanya ili kupunguza domestic violence around us?
Ni muhimu sana victim asiwe ndio responsible kwa yalio mtokea. Kuna familia ambapo binti anabakwa na wanaishia kumtuma hyo huyo binti aende boarding school au kijijini kwa kufunika ile aibu. Inakua as if she is punished for what people did to her. Hili linawafanya watoto wengine ndani ya faamilia wakae kimya pale wanapokutana na tatizo lile lile.
 
Haya mambo yapo sana katika jamii nyingi za kiafrika na hata nje ya Afrika yaani Ulaya na Amerika japo kwa wenzentu ni kwa viwango vya chini tofauti na huku kwetu.

Binafsi nahisi hili ni swala gumu sana kuliondoa kwenye jamii zetu tunamoishi. Imagine watu kabla ya kuoana (sio wote) japo majority wanakuwa wanapendana sana, ukiwatazama unaweza kudhani haipo siku hata watakuja kukwaruzana, lakini hali ni tofauti sana pindi wanapokuwa pamoja as a family. Sisemi kwa vile kukwaruzana kupo, then solution ni mmoja kumpinga mwenzake la hasha, lakini ikumbukwe pia sisi tumelelewa katika culture tofauti, ambapo kwa namna moja ama nyingine unaweza kukuta mmoja wetu especially mwanaume anatoka kwenye jamii ambayo kwayo mke kupigwa once amekosa ni normal, hakika hili litatokea.

Wengine wanafikia hatua ya kuwapiga wake zao baada ya swala la majadiliano ama maonyo kwa njia ya mdomo kushindikana na hivyo kuishia kupandwa na hasira kupita kiasi na kujikuta wamewapiga. Hawa baada ya kitendo huwa na aina fulani ya majuto moyoni mwao maana huwa sio kusudio lao.

Wanawake wengi wamejaliwa sana uwezo mkubwa wa kuongea maneno mengi kwa muda mfupi, so mnapokuwa kwenye mgogoro na katika harakati za kutatua mgogoro hili jambo huchangia wanaume wengi aidha kupandwa na hasira na kujikuta wakitoa adhabu ya kichapo.


Wapo wanandoa wengi pia ambao wamejikuta kwenye ndoa pasipo upendo wa dhati kwa pande zote, mfano mwanamke anampenda mwanaume na kushinikiza ndoa kwa njia yoyote ile mfano njia za giza (ushirikina) nk, vile na kwa wanaume ama mtu anachelewa sana kuolewa, umri unakwenda siku akijitokeza mtu hata kama hampendi anasema acha tu niolewe nami nipate jina na heshima Mrs somebody, so watu wa namna hii aina yoyote ya tofauti wengi wao (sio wote) huishia kwenye mapigano nk.

Na kuhusu hayo mambo mengine mara mume kabaka mke, dah inakuwa ngumu kulitolea maelezo kwamba sababu ni nini, lakini kwa nini hili litokee kama mtu uko mzima na afya yako, hii inaweza changia ama kuchangiwa na mambo ya cheating ndani ya ndoa. Imeandikwa tusinyimane kwenye ndoa (Mume ampe haki yake mke na vice versa is also true)

Mwisho kabisa watu wanatakiwa kuishi kwa upendo kama tunavyoelekezwa na Mwenyezi Mungu. Tumeaswa tupendane hii ndio amri kuu kuliko zote tuliyopewa na kwa kufanya hivyo hayo mambo mengine tutapata kwa ziada, kumbe basi ili kulifanikisha hili tumrudie Mwenyezi Mungu, imeandikwa mume ampende mwanamke kama anavyojipenda yeye mwenyewe na mwanamke amheshimu mwanaume.

Asante sana. Hapo nilipo pigilia mstari nadhani it is worth mentioning kua wanaume wengi walitoa hilo kama sababu la kuwapiga wake zao. But this comes back to one thing: Kuzidiwa hoja. Wakati mwanamke anapandisha sauti na kuchomekea maneno mabaya tayari ameshaanzisha diagram ya violence, probably sababu yeye mwenyewe ameishiwa hoja. Mwanaume anatakiwa either kuhairisha mazungumzo au kumuomba arudie maneno yake na kuyaeleza kwa kutumia maneno mengine. Mfano mwanamke anaweza kumwambia mwanaume kua "hivi na wewe unajiita mwanaume"? (a common one) na mwanaume akahisi kudharauliwa kupita kiasi. Instead of kurusha kofi anatakiwa amuulize: what is your definition of mwanaume? Unaweza kunipa vigezo? This simple question breaks the diagram and forces the interlocutor to be rational in his/her argument
 
Ushapiga cha Arusha mchana? Mama yangu alininyuka sana enzi hizo na mpaka leo nampenda upeo. Na kama si kichapo chake mida hii labda ningekuwa Segerea nanyea ndoo. Kichapo saa nyingine kinasaidia mtu kurekebisha tabia.

Yani nikufumanie unalabuliwa kitandani kwangu afu nisikupe za uso? Ntakuchapa sana tu. Afu naweza kukusamehe vilevile na maisha yakasonga mbele.
Kesi ya kuwachapa watoto wanapo kosea ni nyingine kabisa. Binafsi sisupport ila wanao support wanasema ni mkataba kati ya mzazi na mtoto ambapo makubaliano yanakua wazi KABLA ya tukio: Ukishindwa shule unachapwa. Ukienda kucheza kombolela na ukakaa sana huko na kayayi, ikigundulika utachapwa. So this teaches the kid some sense of responsibility.
Domestic violence ni tofauti sababu the violent reaction comes AFTER the trigger and often in a relation where violence has never been considered a solution. Kwamba mwanaume na mwanamke hawajawahi kubaliana kua kuna vya kupigana, but in the heat of the argument jamaa anatumia nguvu zake kum-silence mwenzie.
 
Back
Top Bottom