Domestic violence

Domestic violence

Asante sana kwa kupanua definition ya domestic violence. Nadhani masuali yangu ya mwanzo yanahusika pia hapa ingawa hatuwezi kupata jibu la uhakika hapa, but we can still share thoughts: Kwanini victims hawajitokezi? Kwanini pepetrators wanafanya hivo na ni kitu gani sisi kama jamii tunaweza kufanya ili kupunguza domestic violence around us?
Ni muhimu sana victim asiwe ndio responsible kwa yalio mtokea. Kuna familia ambapo binti anabakwa na wanaishia kumtuma hyo huyo binti aende boarding school au kijijini kwa kufunika ile aibu. Inakua as if she is punished for what people did to her. Hili linawafanya watoto wengine ndani ya faamilia wakae kimya pale wanapokutana na tatizo lile lile.
yani wala si uongo!
linapotokea hilki kwenye familia kila mtu anabaki kujali image ya familia ile kwa walio wazunguka!
muathirika anabaki na kidonda kikubwa maishani!
tusibaki kushangaa tu kuwa kwanini siku hizi hakuna mapenzi
watoto wanakua kwenye mazingira gani?
binti aliyebakwa na babake/kaka/mabinamu na shemeji au kijana aliyenyanya sika kijinsia na mama mwenye nyumba/mjomba /kaka/babu huyu anawezaje kupenda ukubwani!
nani anakua akishuhudia mamake anaburuzwa mtaani akiwa uchi kwa kipigo kutoka kwa baba anaweza kuipa thamani halisi ndoa!
so ni swla pana sana kwa kweli!
hakuna aliye tayari kuwajibika pengine wala hatujali kuwa ni tatizo mtambuka!tunabaki ah shauri yao!
 
Mkuu mtu hadundwi mwanzoni mwanzoni, anaviziwa akishaanza kulewa mapenzi ndio visa vinaanza.

Mi naona kumpiga mwanamke (au kupigana na mwanaume mwenzako) ni lazima mtu utakuwa na uduni wa kufikiri sana na utu pia. Sasa tutajitofautishaje na viumbe visivyofikiri??? Totally immoral and should be condemmed by all men.


Kupigana na kupendana mbona haviendani kabisa.

Utampendaje mtu anayekudunda?
 
tatizo hilo chanzo chake ni mila na desturi zetu maana ktk jamii nyingi binti anafunzwa kuwa mvumilivu kwa mumewe na kutotoa siri nje hata kama anafanyiwa ndivyo sivyo, hiyo humfanya ahisi ni aibu kulalamika au kumshtaki mumewe.

suala la kutoa mahari (mathalani mahari kubwa) nalo huwafanya baadhi ya wanaume wahisi wake zao ni sehemu ya mali zake hivyo kumfanyia lolote bila kujali utu wake.

mfume dume nao ni tatizo linalosababisha wanaume wengi kutopenda kuwapa nafasi ya kuzungumza na wake zao.

elimu nayo ni tatizo kwa baadhi ya wanaume na wanawake.

kuutibu hili tatizo inahitaji kuanza kushughulika na hivyo vyanzo ingawa kwa sasa labda tuelekeze nguvu zaidi ktk kutoa elimu inaweza kuwa njia rahisi na nyepesi kabla hatujaenda kwenye vyanzo vingine
 
Nimewahi kushuhudia visa vingi sana na ukatili mwingi sana juu ya wanawake.
Wanawake wamekuwa wakifungwa sana na heshima yao katika jamii, kujaribu hutunza heshima ya familia, na pia wanafungwa na commitment yao katka kulea watoto wake.

Nimeshuhudia wengine wakishinikizwa na wazazi na ndugu zao watengane na waume zao baada ya kukaa kesi nyingi za masuluhisho, lakini mwanamke anaamua kurudi kwa mumewe kwa ajili ya kulea watoto wake. (Huruma) wengine hata wakafunguliwa biashara na ndugu zao lakini bado wamerudi kuungana na watoto wao. (MAMA aheshimiwe milele)


Vitu kadhaa niligundua ni kwamba
  1. mwanaume kumpiga mwanamke doesn't necessarily mean hampendi, but it certainly means ni hatari kwa mke wake.
  2. Mwanamke anae mvumilia mume wake ambae ni abusive doesn't necessarily do it because she is weak and intimidated, it could also mean she had alternatives but decided to do this.
  3. Jamii ina role kubwa sana ya ku-play katika kusaidia couples ku-recover from such a climate (mfano wanawake walio pata support ya familia in rural area walirecover in 2-4 month, wale walio ikosa but walipitia a psychiatrist to deal with it, in urban area walipona baada ya miaka 2)

* All studies zinapatikana on demand via PM (please note that most of them are in french)
 
tatizo hilo chanzo chake ni mila na desturi zetu maana ktk jamii nyingi binti anafunzwa kuwa mvumilivu kwa mumewe na kutotoa siri nje hata kama anafanyiwa ndivyo sivyo, hiyo humfanya ahisi ni aibu kulalamika au kumshtaki mumewe.

suala la kutoa mahari (mathalani mahari kubwa) nalo huwafanya baadhi ya wanaume wahisi wake zao ni sehemu ya mali zake hivyo kumfanyia lolote bila kujali utu wake.

mfume dume nao ni tatizo linalosababisha wanaume wengi kutopenda kuwapa nafasi ya kuzungumza na wake zao.

elimu nayo ni tatizo kwa baadhi ya wanaume na wanawake.

kuutibu hili tatizo inahitaji kuanza kushughulika na hivyo vyanzo ingawa kwa sasa labda tuelekeze nguvu zaidi ktk kutoa elimu inaweza kuwa njia rahisi na nyepesi kabla hatujaenda kwenye vyanzo vingine

Kweli kuna mengi yanachangia ila kumbuka hata huko ambako hawatoi mahari na wanako encourage wansichana kufunguka bado kuna domestic violence. Probably sababu mbili au tatu huchangia in a single case.
 
Kweli kuna mengi yanachangia ila kumbuka hata huko ambako hawatoi mahari na wanako encourage wansichana kufunguka bado kuna domestic violence. Probably sababu mbili au tatu huchangia in a single case.

Binafsi labda nihitimishe kwa kusema labda asili ya uumbaji ina mchango kwenye hili kwani mwanaume ameumbwa kabla ya mwanamke na mwanamke kutokana na mwanaume.

vitabu vya dini vimempa mwanaume nguvu ya kumtawala mwanamke na mwanamke kunyimwa hata haki ya kuswalisha au kusalisha kwa baadhi ya dini. mwanaume amepewa upendeleo wa kuona zaidi ya mke mmoja kwa baadhi ya dini lakini siyo kwa mwanamke.

yawezekana nguvu hiyo ya uumbaji inawatawala wanawake wengi kuwa inferior kwa waume zao na wanaume kuwa superior kwa wake zao.
 
Roulette, the simple thought of a man laying his hands on me makes me SICK. Kama tumeshindwana basi kila mtu na hamsini zake. Siwezi kukubali kupigwa, kunyanyaswa na jitu tulokutana ukubwani. Mpaka hapa nimefika, najua zuri na baya so hamna kosa ambalo hatuwezi kuelekezana kama watu wazima. What gives a man the audacity to think he can hit me? I refuse to be a victim of domestic Violence.
 
Last edited by a moderator:
Asante sana. Hapo nilipo pigilia mstari nadhani it is worth mentioning kua wanaume wengi walitoa hilo kama sababu la kuwapiga wake zao. But this comes back to one thing: Kuzidiwa hoja. Wakati mwanamke anapandisha sauti na kuchomekea maneno mabaya tayari ameshaanzisha diagram ya violence, probably sababu yeye mwenyewe ameishiwa hoja. Mwanaume anatakiwa either kuhairisha mazungumzo au kumuomba arudie maneno yake na kuyaeleza kwa kutumia maneno mengine. Mfano mwanamke anaweza kumwambia mwanaume kua "hivi na wewe unajiita mwanaume"? (a common one) na mwanaume akahisi kudharauliwa kupita kiasi. Instead of kurusha kofi anatakiwa amuulize: what is your definition of mwanaume? Unaweza kunipa vigezo? This simple question breaks the diagram and forces the interlocutor to be rational in his/her argument

Nimefurahi ku share machache juu ya thead hii yenye kichwa Domestic violence, hakika mimi lazima nikiri ya kwamba binafsi natoka kwenye jamii ambayo hayo mambo yamekuwepo sana na pia nimeyashuhudia sana, nimeyaishi sana japo pia kwa sasa yanapungua kwa kiasi kikubwa japo sio sana.

Hapo penye red ndio pagumu kwa walio wengi na ambao kwao malezi ya mfumo dume ndiko walikokulia kama jamii ninayotoka mimi binafsi. Inahitaji busara sana ikibidi hata kuahirisha mjadala kwa siku hiyo na kutafuta siku nyingine katika mazingira tofauti ili kujadili mada husika. Hili hakika husaidia sana hasa mnapokuwa katika mambo mengine basi unapata upenyo wa kuingiza ama kukumbushia mada ambayo uliiahirisha siku za nyuma na hapo utaona mwenzako anavyojutia alichokifanya (Hii nina ushahidi nayo binafsi)

Jamani elimu ya Kimungu inahitajika sana kusaidia kuondoa hizi domestic violence katika jamii zetu, hii itasaidia sana kujenga familia zetu ili ziwe kwenye malezi mazuri na mwisho wa siku hizi tamaduni za kuumizana kwenye familia na jamii kwa ujumla zitapungua kama sio kuisha kabisa.

Ahsante.
 
Roulette, the simple thought of a man laying his hands on me makes me SICK. Kama tumeshindwana basi kila mtu na hamsini zake. Siwezi kukubali kupigwa, kunyanyaswa na jitu tulokutana ukubwani. Mpaka hapa nimefika, najua zuri na baya so hamna kosa ambalo hatuwezi kuelekezana kama watu wazima. What gives a man the audacity to think he can hit me? I refuse to be a victim of domestic Violence.

Tena ww unavoongea tu unaonyesha makofi ndo njia pekee ya kukupa maelekezo
 
Last edited by a moderator:
Yaan unambie mimi "nawewe unajiita mwanaume?" Afu nikuache ivi ivi, kwanza kabisa I will neva forget those words...na lazima nikupe kichapo, otherwise uwe unachunga domo lako, Kama unajijua una hasira na uwezi mabishano niache niongee mwenyewe kama chizi, Dharau tena kutoka kwa mke wangu ni kitu ambacho siwezi vumilia hata dk 0
 
Yaan unambie mimi "nawewe unajiita mwanaume?" Afu nikuache ivi ivi, kwanza kabisa I will neva forget those words...na lazima nikupe kichapo, otherwise uwe unachunga domo lako, Kama unajijua una hasira na uwezi mabishano niache niongee mwenyewe kama chizi, Dharau tena kutoka kwa mke wangu ni kitu ambacho siwezi vumilia hata dk 0
hapa tayari unaonyesha wewe si mwanamme maana wanaume huwa hawana hasira za kijinga na kuwapiga wake zao! mwanamme mwenye akili ni yule anayetumia busara na akhli yake kusuluhisha mambo ukiona mwenye kutumia nguvu ujue ni mpumbavu na kichwani hamnazo na nguvu ndio silaha yakd
 
Mie naomba niwe msomaji tu...


Ingawa kiukweli si mshabiki wa mambo ya kunyanyasana na kuchapana makondo (kudundana), mazingira yetu yananifanya niamini kwamba hili tatizo tutaendelea kuwa nalo kwa muda.

Babu DC!!
 
Hivi wewe naye Mwanaume
Hivi wakiitwa Wanaume na wewe utaenda
Wewe Mwanaume suruali tu
Wewe Baba Juma ulikuwa zamani sasa hivi umeshajiishia hata senti huna
Wanaume wapo kibao usinibabaishe tumekutana wote tukiwa na meno 32
Una hakika hawa watoto ni wako, usinitibue...achana na mimi

............................
CC: Asprin
Mwanamtoka pabaya
 
Last edited by a moderator:
Roulette, the simple thought of a man laying his hands on me makes me SICK. Kama tumeshindwana basi kila mtu na hamsini zake. Siwezi kukubali kupigwa, kunyanyaswa na jitu tulokutana ukubwani. Mpaka hapa nimefika, najua zuri na baya so hamna kosa ambalo hatuwezi kuelekezana kama watu wazima. What gives a man the audacity to think he can hit me? I refuse to be a victim of domestic Violence.
Hongera dear kwa kujiamini na kustand tall. Hata mimi siwezi kubali. Binafsi it goes as far as siwezi KABISA kumvumilia mtu anae nipandishia sauti. Na bahati nzuri I make it clear toka mwanzo na katika mahusiano yangu iliwahi kutokea nikiwa 19 years tu (Mwanaume kunipandishia sauti), ndio ilikua mwanzo na mwisho (we broke up there and then). Attitude yangu wakati wa discussion is such as hata huwezi jua pakuanzia kuleta violence. Na ikitokea bahati mbaya nikakutana na hao violent men ndio deal breaker tayari.
I have met some in my professional life na nikawachukulia hatua moja kwa moja. Pamoja na kuonekana "not tolerant" au kupangwa majina ya ajabu I have never tolerated a violent behavior kazini, iwe toward me au toward watu wengine (wa kiume au wa kike)
 
Mie naomba niwe msomaji tu...


Ingawa kiukweli si mshabiki wa mambo ya kunyanyasana na kuchapana makondo (kudundana), mazingira yetu yananifanya niamini kwamba hili tatizo tutaendelea kuwa nalo kwa muda.

Babu DC!!

Kama tutaendelea kua nalo kwa muda basi naomba useme tu how we can minimize it, tunawezaje kuwasaidia hawa majeruhi? Na ni mazingira yapi hayo?
 
hii thread muhimu hv bado ipo 2nd page!
mweee bandughuuuuuuuuuu!
ingekuwa ''mke wangu kazaa na mdogo wangu'' sasa?
jamani haya mambo yanafanyika sana under our very noses!
hv unaweza kuimagine binti yako au mtoto wako wa kiume anadhalilishwa na kijana wako wa kazi au mdada wako wa kazi?
unaweza kuimagine mwanao anafinywa na kisu cha moto kila siku baada tu ya kumuacha na kismall house chako?
unaweza kuimagine watoto wako wanaonyeshwa picha za ngono kila uchao we ukiwa kazini?
na mkeo/mumeo anayekupiga kila usiku ?
na mke anayekutukana matusi ya kudhalilisha uanamume wako?
mume anayekuleta wanawake ndani na kipigo juu,kusah unanyamaza tu kisa unale watoto,?
aaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaargh!
 

Mtoto wa kike mwenye umri wa miaka tisa (jina linahifadhiwa), amefanyiwa unyama wa kutisha na baba yake wa kambo kwa kunajisiwa, kulawitiwa na kulazimishwa kulamba mbegu zake za kiume.

nimeitoa kwa MziziMkavu!
yapo mengi sana yanafanyika kwenye kuta za nyumba zetu !
aidha tunayajua au hatujui!
ila uuuwih!MUNGU WANUSURU TU WATOTO !
 
.. Vitu kadhaa niligundua ni kwamba
  1. mwanaume kumpiga mwanamke doesn't necessarily mean hampendi, but it certainly means ni hatari kwa mke wake.
  2. Mwanamke anae mvumilia mume wake ambae ni abusive doesn't necessarily do it because she is weak and intimidated, it could also mean she had alternatives but decided to do this.
Roulette, loo imekaaje hii!!?

Unaonaje nikisema hizo conditions mbili ni ugonjwa a clinical case of "battered women syndrome" nafikiri umekutana na hii syndrome in your study? Au?!!!

Yaani ... Ukweli ni kwa chuki, hasira, kinyongo and all negative emotions zinakuwa kama sumaku ya "kuunganisha" hapa hizo emotions zinawaauganisha wife and husband huku wakiendelea kutesana, bila kuweza kutengana au kupata utatuzi kirahisi ... finally in some cases wanaweza kuumizana kabisa. Ni clinical syndrome ... inatibiwa kama ugonjwa!! ..Pinga, jitetee, chukua hatua zote unazotaka lakini bila chuki, hasira, kinyongo and all kind of resentment!!

Bottom line? You cant solve/separate from any abuse/violence by using of negative emotions!!!!

Im sure you are familiar with the concept of Love Hate Relationship .. Ni ka syndrome ... wanawake wanatakiwa kupinga abuse kwa kila namna bila kuzalisha hizo negative emotions kwani wakifanya hivyo, zitawa bind na hakika hawataweza kuachana/kurekebisha hayo mahusiano .. huku wakitoa visingizo kibao!!

Kwa mfano hiyo namba 2 naona kama ni kujitetea tu, while hiyo ni syndrome !
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom