Dogo Edu wa Tamthilia ya Pazia ndiye muigizaji Bora kijana atakayekuja kushika Bongomovie

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,904
Habari Wakuu!

Leo Kwa habari za Burudani na Sanaa, nimekuwa nikifuatilia Tamthilia za hapa na pale za bongo kama sehemu ya kusapoti na kuona kile wakifanyacho wenzetu katika Tasnia hiyo.
Nikakutana na Dogo mmoja hivi ambaye ameigiza kwenye Tamthilia ya Pazia, namfahamu Kwa jina moja "EDU" Wataalamu mtakuja kunisaidia jina lake halisi.

Taikon kama BINGWA, tupa wa mambo ya Fasihi. Kwa jicho la kisanaa nimemuona huyu Dogo kama hataletewa zengwe, husda na kijicho basi hakuna kijana wa kumzidi wala kumfikia, nazungumzia kijana wa umri wake.
Ni muigizaji mzuri, anayejua kuigiza. Nafikiri waigizaji wakongwe na wakubwa ambao wameshaona akiigiza watajua nazungumzia Jambo Gani.

Mambo ambayo Edu anatakiwa kuyaongeza ili azidishe kipaji chake na kuifanya kazi yake iwe Bora.

1. Aongeze usomaji wa vitabu
2. Ajifunze kuzungumza Lugha ya kingereza imkolee.
3. Ajifunze kuandika Tamthilia na drama zake, kama maandalizi ya kuachiwa mikoba ya Bongomovie hapa Tanzania. Kisha atafute Waandishi na watunzi wa Riwaya na Tamthilia wavipitie na kukushauri.
4. Ajifunze Sanaa zingine kama za martials art's. Zitamsaidia katika uhusika wa filamu za mapigano na ujasusi katika miaka 10 ijayo.
5. Asome mambo magumu gumu yanayohusu Siasa, Rushwa, ujasusi, Teknolojia na ambayo yanaendana na dunia ya SASA na ijayo. Ili abaki kwenye Fomu Kwa muda mrefu. Asiwe kama Kaka zake ambao wameishia kwenye mapenzi.

6. Akae Kwa ukaribu na wasanii wakubwa wenye utulivu kama Jacob Steven, Johari(huyu dada pia ni muigizaji mzuri na anajitahidi kwenye uandaaji wa filamu, kama anamapungufu basi ni mapungufu ya kiwakati).

7. Ajifunze kuwa muongoza filamu iwe Kwa kusoma au kukaa na waongoza filamu mahiri. Au atafute waongoza filamu Wazuri kama maandalizi ya kuchukua mikoba.

Mwisho, akishaanza kuandaa filamu zake basi ajiepushe na urafiki au undugu kwenye ishu za kazi, atafute Wahusika kulingana na Scripts zinavyotaka.

Hayo ni machache Kati ya mengi.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Habari Wakuu!

Leo Kwa habari za Burudani na Sanaa, nimekuwa nikifuatilia Tamthilia za hapa na pale za bongo kama sehemu ya kusapoti na kuona kile wakifanyacho wenzetu katika Tasnia hiyo.
Nikakutana na Dogo mmoja hivi ambaye ameigiza kwenye Tamthilia ya Pazia, namfahamu Kwa jina moja "EDU" Wataalamu mtakuja kunisaidia jina lake halisi.

Taikon kama BINGWA, tupa wa mambo ya Fasihi. Kwa jicho la kisanaa nimemuona huyu Dogo kama hataletewa zengwe, husda na kijicho basi hakuna kijana wa kumzidi wala kumfikia, nazungumzia kijana wa umri wake.
Ni muigizaji mzuri, anayejua kuigiza. Nafikiri waigizaji wakongwe na wakubwa ambao wameshaona akiigiza watajua nazungumzia Jambo Gani.

Mambo ambayo Edu anatakiwa kuyaongeza ili azidishe kipaji chake na kuifanya kazi yake iwe Bora.

1. Aongeze usomaji wa vitabu
2. Ajifunze kuzungumza Lugha ya kingereza imkolee.
3. Ajifunze kuandika Tamthilia na drama zake, kama maandalizi ya kuachiwa mikoba ya Bongomovie hapa Tanzania. Kisha atafute Waandishi na watunzi wa Riwaya na Tamthilia wavipitie na kukushauri.
4. Ajifunze Sanaa zingine kama za martials art's. Zitamsaidia katika uhusika wa filamu za mapigano na ujasusi katika miaka 10 ijayo.
5. Asome mambo magumu gumu yanayohusu Siasa, Rushwa, ujasusi, Teknolojia na ambayo yanaendana na dunia ya SASA na ijayo. Ili abaki kwenye Fomu Kwa muda mrefu. Asiwe kama Kaka zake ambao wameishia kwenye mapenzi.

6. Akae Kwa ukaribu na wasanii wakubwa wenye utulivu kama Jacob Steven, Johari(huyu dada pia ni muigizaji mzuri na anajitahidi kwenye uandaaji wa filamu, kama anamapungufu basi ni mapungufu ya kiwakati).

7. Ajifunze kuwa muongoza filamu iwe Kwa kusoma au kukaa na waongoza filamu mahiri. Au atafute waongoza filamu Wazuri kama maandalizi ya kuchukua mikoba.

Mwisho, akishaanza kuandaa filamu zake basi ajiepushe na urafiki au undugu kwenye ishu za kazi, atafute Wahusika kulingana na Scripts zinavyotaka.

Hayo ni machache Kati ya mengi.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Umekosa hata kapicha kake kweli (mtibeli)!!!!?
 
Dogo Edu
images (20).jpeg
 
Itabidi watumie nguvu ya ziada kuwashawishi watu kwakweli

Waache kuigiza vitu vilevile au waongeze ubunifu.
Mfano, tamthilia ya Huba, ni tamthilia nzuri lakini inamkwamo wa visa, yaani imedorora, haiendi Mbele. Mpaka inachosha.

Angalia thamthilia kama Siri ya mtungi, Siri za Familia, Selina, Mpali, Kovu, Kina. Utaona tofauti.
 
Waache kuigiza vitu vilevile au waongeze ubunifu.
Mfano, tamthilia ya Huba, ni tamthilia nzuri lakini inamkwamo wa visa, yaani imedorora, haiendi Mbele. Mpaka inachosha.

Angalia thamthilia kama Siri ya mtungi, Siri za Familia, Selina, Mpali, Kovu, Kina. Utaona tofauti.
Selina, Pete, Kina, Njoro wa uba na saivi Pepeta nazifatilia sana na wako vizuri mno. Uhalisia unaonekana yaani mnajikuta familia nzima mnatulia na mnaangalia kwa amani na furaha.

Ila njoo kwa wabongo hayo mavazi wadada wanavaa nguo za ajabu hazina staha + uhalisia zero. Ni kama wanafanya show off na ubunifu zero.

Wangetulia wakajifunza kwa majirani zetu wakenya, watapata kitu cha maana
 
Selina, Pete, Kina, Njoro wa uba na saivi Pepeta nazifatilia sana na wako vizuri mno. Uhalisia unaonekana yaani mnajikuta familia nzima mnatulia na mnaangalia kwa amani na furaha.

Ila njoo kwa wabongo hayo mavazi wadada wanavaa nguo za ajabu hazina staha + uhalisia zero. Ni kama wanafanya show off na ubunifu zero.

Wangetulia wakajifunza kwa majirani zetu wakenya, watapata kitu cha maana
Kingine kinachoniuzi ni Drama zinazungushwa sana Esp: Jua kali
ifike mahala kitu kiishe kianze kingine
 
Selina, Pete, Kina, Njoro wa uba na saivi Pepeta nazifatilia sana na wako vizuri mno. Uhalisia unaonekana yaani mnajikuta familia nzima mnatulia na mnaangalia kwa amani na furaha.

Ila njoo kwa wabongo hayo mavazi wadada wanavaa nguo za ajabu hazina staha + uhalisia zero. Ni kama wanafanya show off na ubunifu zero.

Wangetulia wakajifunza kwa majirani zetu wakenya, watapata kitu cha maana

Kwenye ishu ya maigizo Wakenya wametupiga, hapo tunakasafari.
Walau Muziki Vijana WA muziki wanasongesha gurudumu vizuri
 
Back
Top Bottom