Dogo aliyeandika bongo fleva mtihani wa kidato cha nne 2011

Malyenge

JF-Expert Member
Jan 16, 2012
6,658
3,646
Clouds FM inafanya mahojiano na yule dogo aliyeandika bongo fleva kwenye mitihani ya kidato cha nne mwaka 2011. Dogo anadai alifanya hivyo ili kufikisha ujumbe kwa wahusika kuwa mfumo wa sasa wa elimu hautambui vipaji vya watu. Dogo anasema yeye hakuwa mtu wa kusoma ingawa alijitahidi sana. Anasema maumbile yake aliyoumbwa na Mungu si ya kusoma. Dogo anadai mfumo wa elimu Tanzania hautambui vipaji vingine zaidi ya formal education, yaani uende shule, usome kisha utafute kazi.
Anasema kuwa mfumo huu wa elimu, mtu anayeshindwa kuufuata basi mfumo unamtupa nje.....
Mashairi aliyoyaandika katika mtihani wake ni ya maelezo haya ambayo watu hawakuelewa anamaanisha nini. Dogo huyo kwa jina anaitwa JULIUS, anasema ana umri wa miaka 23, akaulizwa kwa nini alimaliza form four akiwa na umri mkubwa akajibu alikuwa akirudiarudia form two mara nyingi sana.
Anamalizia kwa kusema wazazi waangalie vipaji vya watoto wao ili wasipoteze pesa zao kwa kusomesha mtu asiye na uwezo wa kusoma. Anaomba msamaha kwa watanzania wote kwa aliyoyafanya, hakuwa na jinsi ya kufikisha ujumbe kwa jamii. Ametoa alblum yake inaitwa Mr. PRESIDENT.
Nawasilisha.
 
kwa mbali naona pana point anataka kuisema. ila wenye mamlaka wanatakiwa kuufumua au kurekebisha mfumo wa elimu yetu
 
Kajieleza kweli anaijua mistari,
hebu tuwekeeni hiyo korusi ya 'mr president'
pengine itafanana na wakwetu.
 
nampongeza huyu kijana kwa kuweka bayana ukweli wa mfumo wa elimu tanzania. ni vizur kukawa na mfumo wa elimu ya vipaji maalum kama muziki, michezo na hiyo ya elimu aka vipaji maalum.
 
Clouds FM inafanya mahojiano na yule dogo aliyeandika bongo fleva kwenye mitihani ya kidato cha nne mwaka 2011. Dogo anadai alifanya hivyo ili kufikisha ujumbe kwa wahusika kuwa mfumo wa sasa wa elimu hautambui vipaji vya watu. Dogo anasema yeye hakuwa mtu wa kusoma ingawa alijitahidi sana. Anasema maumbile yake aliyoumbwa na Mungu si ya kusoma. Dogo anadai mfumo wa elimu Tanzania hautambui vipaji vingine zaidi ya formal education, yaani uende shule, usome kisha utafute kazi.
Anasema kuwa mfumo huu wa elimu, mtu anayeshindwa kuufuata basi mfumo unamtupa nje.....
Mashairi aliyoyaandika katika mtihani wake ni ya maelezo haya ambayo watu hawakuelewa anamaanisha nini. Dogo huyo kwa jina anaitwa JULIUS, anasema ana umri wa miaka 23, akaulizwa kwa nini alimaliza form four akiwa na umri mkubwa akajibu alikuwa akirudiarudia form two mara nyingi sana.
Anamalizia kwa kusema wazazi waangalie vipaji vya watoto wao ili wasipoteze pesa zao kwa kusomesha mtu asiye na uwezo wa kusoma. Anaomba msamaha kwa watanzania wote kwa aliyoyafanya, hakuwa na jinsi ya kufikisha ujumbe kwa jamii. Ametoa alblum yake inaitwa Mr. PRESIDENT.
Nawasilisha.
frankly,kijana julius ameongea vizuri sana na wimbo wake mzuri
 
Kajieleza kweli anaijua mistari,
hebu tuwekeeni hiyo korusi ya 'mr president'
pengine itafanana na wakwetu.

Baadhi ya mistari-
Wanaofanya madudu nawatosa kwenye baraza,
wananitia aibu kwa wananchi wananikwaza,
Nilikuwa kipenzi chao hadi mkasema mi chaguo la Mungu,
Kwenye uchaguzi nikapiga bao ila leo mnaniona mchungu,
Mara mnaiba wanyama mara mnakula cha juu,
Af bado mnataka muongezewe posho huko East Zuu,
Ndo maana maana napenda kusafiri ili nipunguze stress
 
Nina ndugu yangu mmoja kama huyu,yeye alimwambia mama yake wazi wazi kwamba elimu sio kipaji chake,alimshauri mamake ampeleke VETA akasomee ufundi seremala lakini mama yake akakataa.Kilichotokea ni kurudia form 2 mara mbili na alipofika form 4 kigurunyembe moro yaani kama ingekuwepo score ndogo kuliko zero basi angepata hiyo,kiufupi alipiga nyuzi 360.
 
Ni mwenyewe aliyeandika bongo fleva kwenye mtihani au kalishwa maneno mtu mwingine? maana hao clouds kwa kutaka sifa ndo wenyewe.
 
Back
Top Bottom