Dogo aliyeandika bongo fleva mtihani wa kidato cha nne 2011

Kufanya jambo lolote bila ya kuwa na msingi wa Elimu hautafanikiwa au ukifanikiwa itakuwa ni asilimia ndogo kulinganisha kama ungekuwa na elimu. Ni vizuri huyu kijana akajua kuwa alitakiwa kuwa na msingi mzuri wa elimu walau afaulu form four, ili imjengee msingi wa kipaji chake. Kuimba hakuhitaji elimu lakini inategemea unataka kuimba nini na kwa ajili ya nani na nini. Hiyo elimu anaikataa kwa sasa lakini atahitaji hapo mbele kidogo, ndugu niwaambie Mungu akimsaidia akipata kibali kwa wakubwa na mataifa mengine atafanyaje??? Ni kweli kusoma sio kuelimika lakini kuna mambo ya msingi kwamba destiny yako ni mpaka uiandae. Watoto wangu tayari najua vipaji vyao au talanta zao siwezi kuwaruhusu saa hizi eti waanze (masaa yote) kucheza mpira wa miguu, muziki, kareti, ngumi, nk wakati hata elimu ya kufuta ujinga yaani Form four hawajafika. Napalilia vipawa vyao na wakati ukifika wakijua mwelekeo sahihi I will release them and one day i will say that is my product. Kawaida watoto hufanya kabla hawajafikiria lakini sisi wakubwa tunafikiria kwanza ndio tunafanya na mtoto anahitaji kusaidiwa to seize their dream.
God Bless You.
 
Absolutely true mr. Julius, umediriki ku-shake system!Being educated never guarantee success, education & achvment r zero r/ship!We as LDCs we 'll continue starvng wc poverty coz of poor cstm we ev 2 addres t!We must change our mindset on edcation 4 dvt!
 
Mi nimemuelewa sana dogo!atleast kuna wachache kama yeye wanaweza kusema mbele za watu kuwa mfumo wa elimu ni mbovu kwasababu ili mtu afanikiwe kimaisha inabidi aende na mfumo unavyotaka!kungekuwa na means za kuendeleza vipaji vya watoto tungejenga taifa lenye watu wanaoeleweka.
 
Baadhi ya mistari-
Wanaofanya madudu nawatosa kwenye baraza,
wananitia aibu kwa wananchi wananikwaza,
Nilikuwa kipenzi chao hadi mkasema mi chaguo la Mungu,
Kwenye uchaguzi nikapiga bao ila leo mnaniona mchungu,
Mara mnaiba wanyama mara mnakula cha juu,
Af bado mnataka muongezewe posho huko East Zuu,
Ndo maana maana napenda kusafiri ili nipunguze stress

Ni hii kweli au hii ni yako mkuu?
 
Mimi ni mmoja wapo niliyeumizwa na kitendo chake cha kuandika bongo fleva kwenye mtihani but leo nimemuelewa alikuwa ana maanisha nini

Kiukweli kijana ametuchallenge watu wengi, ni shujaa aliyeamua kupambana na system. Anapaswa kupewa fursa kubwa kueleza umma mawazo yake.
 
Clouds FM inafanya mahojiano na yule dogo aliyeandika bongo fleva kwenye mitihani ya kidato cha nne mwaka 2011. Dogo anadai alifanya hivyo ili kufikisha ujumbe kwa wahusika kuwa mfumo wa sasa wa elimu hautambui vipaji vya watu. Dogo anasema yeye hakuwa mtu wa kusoma ingawa alijitahidi sana. Anasema maumbile yake aliyoumbwa na Mungu si ya kusoma. Dogo anadai mfumo wa elimu Tanzania hautambui vipaji vingine zaidi ya formal education, yaani uende shule, usome kisha utafute kazi.
Anasema kuwa mfumo huu wa elimu, mtu anayeshindwa kuufuata basi mfumo unamtupa nje.....
Mashairi aliyoyaandika katika mtihani wake ni ya maelezo haya ambayo watu hawakuelewa anamaanisha nini. Dogo huyo kwa jina anaitwa JULIUS, anasema ana umri wa miaka 23, akaulizwa kwa nini alimaliza form four akiwa na umri mkubwa akajibu alikuwa akirudiarudia form two mara nyingi sana.
Anamalizia kwa kusema wazazi waangalie vipaji vya watoto wao ili wasipoteze pesa zao kwa kusomesha mtu asiye na uwezo wa kusoma. Anaomba msamaha kwa watanzania wote kwa aliyoyafanya, hakuwa na jinsi ya kufikisha ujumbe kwa jamii. Ametoa alblum yake inaitwa Mr. PRESIDENT.
Nawasilisha.

Hapo amechemka hajui kuwa ili ufanikiwe msingi wake ni elimu
 
nampongeza huyu kijana kwa kuweka bayana ukweli wa mfumo wa elimu tanzania. ni vizur kukawa na mfumo wa elimu ya vipaji maalum kama muziki, michezo na hiyo ya elimu aka vipaji maalum.

Mimi binafsi simpi- support huyu kijana pamoja na kujitetea kwake.

Hivi itawezekana kweli yeye awe na kipaji ambacho hakihitaji Elimu, Hivyo Bongo Fleva lazima awe na elimu ndipo atunge wimbo na kuandika mistari.

Ajitafakari kisha achukue hatua ya kubadilisha mwenendo wake. Hapa ameongea Pumba huyu Dogo atakuja jutia maisha baadaye, wenzake tunatamani ingeliwezekana nilirudie Darasa la Kwanza Primary jinsi maisha ninavyoyaona magumu pasipo elimu.

Shame upon him!!!!!!!!!



MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Baadhi ya mistari-
Wanaofanya madudu nawatosa kwenye baraza,
wananitia aibu kwa wananchi wananikwaza,
Nilikuwa kipenzi chao hadi mkasema mi chaguo la Mungu,
Kwenye uchaguzi nikapiga bao ila leo mnaniona mchungu,
Mara mnaiba wanyama mara mnakula cha juu,
Af bado mnataka muongezewe posho huko East Zuu,
Ndo maana maana napenda kusafiri ili nipunguze stress

ahahaha...nimependa sana hiyo mistari yake aise
 
Kufanya jambo lolote bila ya kuwa na msingi wa Elimu hautafanikiwa au ukifanikiwa itakuwa ni asilimia ndogo kulinganisha kama ungekuwa na elimu. Ni vizuri huyu kijana akajua kuwa alitakiwa kuwa na msingi mzuri wa elimu walau afaulu form four, ili imjengee msingi wa kipaji chake. Kuimba hakuhitaji elimu lakini inategemea unataka kuimba nini na kwa ajili ya nani na nini. Hiyo elimu anaikataa kwa sasa lakini atahitaji hapo mbele kidogo, ndugu niwaambie Mungu akimsaidia akipata kibali kwa wakubwa na mataifa mengine atafanyaje??? Ni kweli kusoma sio kuelimika lakini kuna mambo ya msingi kwamba destiny yako ni mpaka uiandae. Watoto wangu tayari najua vipaji vyao au talanta zao siwezi kuwaruhusu saa hizi eti waanze (masaa yote) kucheza mpira wa miguu, muziki, kareti, ngumi, nk wakati hata elimu ya kufuta ujinga yaani Form four hawajafika. Napalilia vipawa vyao na wakati ukifika wakijua mwelekeo sahihi I will release them and one day i will say that is my product. Kawaida watoto hufanya kabla hawajafikiria lakini sisi wakubwa tunafikiria kwanza ndio tunafanya na mtoto anahitaji kusaidiwa to seize their dream.
God Bless You.
Rev Kenda nadhani hujaelewa kiwango cha elimu cha huyu kijana... Amefika form four tena kwa kurudiarudia mara nyingi sana!!! Kwa hiyo elimu ama kukaa darasani amekaa muda mrefu kuliko inavyotakiwa kuwa, ila cheti ndo hana!!!! Ni form four leaver without a certificate!!!!
 
Hata akina Thomas Edison elimu rasmi iliwapa taabu; na Bill Gates ni drop out. Nakubaliana na "Dogo" kuwa formal education (elimu rasmi) si kigezo pekee cha mafanikio, lkn bado elimu ni kigezo cha mafanikio. Sijakijua kipaji chake, lkn kwa Bongo fleva amepotea.
 
Back
Top Bottom