Wazolee
Tujikite kuamini Quran.
Quran ndio imeelezea vizur Kuhusu Yesu. Nabii Issa .
Jinsi alivyozaliwa.
Alivyotwaliwa na Allah kwa kupaa.
Na kuwa ndio Nabii pekee atarud siku ya Kiama.
Quran 3:45
"Na pale Malaika walipo sema: Ewe Maryamu! Hakika Mwenyezi Mungu anakubashiria (mwana) kwa neno litokalo kwake. Jina lake ni Masihi Isa mwana wa Maryamu, mwenye hishima katika dunia na Akhera, na miongoni mwa walio karibishwa (kwa Mwenyezi Mungu).”
Quran 3:47
"Maryamu akasema: Mola wangu Mlezi! Vipi nitampata mwana na hali hajanigusa mwanaadamu? Mwenyezi Mungu akasema: Ndivyo vivyo hivyo, Mwenyezi Mungu huumba apendacho. Anapo hukumu jambo, huliambia: Kuwa! Likawa.”
Quran 66:12
"na tukampulizia humo aliye linda ubikira wake, kutoka roho yetu, na akayasadiki maneno ya Mola wake Mlezi...”
Quran 4: 157-158
"Na kwa kusema kwao: "Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, Mtume wa Mwenyezi Mungu." Lakini hawakumuuwa wala hawakumsulubu, bali walifananishiwa tu. Na hakika waliokhitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi wowote nayo, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini.”
Quran 3:55
"Pale Mwenyezi Mungu alipo sema: Ewe Isa! Mimi nitakufisha, na nitakunyanyua kwangu, na nitakutakasa na wale walio kufuru, na nitawaweka wale walio kufuata juu ya wale walio kufuru, mpaka Siku ya Kiyama. Kisha marejeo yenu yatakuwa kwangu, nikuhukumuni katika yale mliyo kuwa mkikhitalifiana"