Uchaguzi 2020 Dodoma yazizima kwa Maandalizi ya Lissu kuchukua fomu 8.8.2020

Usilinganishe raisi wa nchi na raia wa kawaida. Raisi atazunguka popote kutimiza majukumu yake. Hatuna maraisi wawili nchi hii. Hiyo ndiyo incumbency advantage.
Umenena vema mkuu, kuna watu watu wanafananisha mkuu wa nchi na vitu vya ajabu.
 
Sisi sio chama bali ni washabiki wa Cdm tunaotoa maoni yetu kupitia mitandao ya kijamii. Maoni yetu ni kwa ajili ya kuboresha, iwapo chama kitaona maoni yetu yanafaa watayachukua, na kama tayari wanayo watayaboresha zaidi. Kupewa nchi hatupewi kwa utashi wa ccm, bali kwa maamuzi ya wananchi.
Maoni yenu hayawezi zingatiwa kwakuwa nyinyi hamuusiki kwenye chama cha familia ya Mbowe.
 
Wajaribu waone
Ila kama hamjachukua Rendez-vous. Nahisi mtakuta office zimefungwa. Kama mliwajulisha before basi hapo hakuna tatizo. Nachelea kusema nyie ndo mnaojua zaidi. Inawezekana labda NEC hufanya kazi 7days/7 no matter what.
 
Ila kama hamjachukua Rendez-vous. Nahisi mtakuta office zimefungwa. Kama mliwajulisha before basi hapo hakuna tatizo. Nachelea kusema nyie ndo mnaojua zaidi. Inawezekana labda NEC hufanya kazi 7days/7 no matter what.
Ndiyo maana yake
 
Kesho ni siku ya sikukuu ya nanenane ni mapumziko hakuna kazi, ofisi hazitafunguliwa.
Usiishi kwa kukariri.

Kukuelimisha - mara mchakato wa uchaguzi ukianza, ofisi zote za Tume ya Uchaguzi hufanya kazi siku zote bila ya kujali ni sikukuu au Jumapili au Jumamosi.

Kaa nalo hilo kichwani ili usiendelee kupotosha. Kama hujui, uliza. Unapoongea kama vile una uhakika, unautumia ujinga wako kuwapotosha watu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tunashukuru Molemo kwa kuleta hii habari. Kuna uzito fulani kwenye kitengo cha habari cha cdm, kiasi kwamba kuna uzi humu jukwaani unaohimiza kitengo cha habari kuamka. Kuna ushauri pia kuhusu Tundu Lisu jinsi ya kufanya siasa zake bila kupoteza credibility yake. Ni vyema kama chama mkakaa na Lisu na kumfunda. Kuna baadhi ya maneno anaongea yanampotezea haiba yake.
Kwa kuongezea suala la yy kushambuliwa isiwe ajenda kabisa tena ikibidi asiliongelee Hilo suala kbs
 
Tunashukuru Molemo kwa kuleta hii habari. Kuna uzito fulani kwenye kitengo cha habari cha cdm, kiasi kwamba kuna uzi humu jukwaani unaohimiza kitengo cha habari kuamka. Kuna ushauri pia kuhusu Tundu Lisu jinsi ya kufanya siasa zake bila kupoteza credibility yake. Ni vyema kama chama mkakaa na Lisu na kumfunda. Kuna baadhi ya maneno anaongea yanampotezea haiba yake.

Be specific...

Kwani una maana gani kusema awe makini na mwisho;

"....bila kupoteza credibility yake..."??

Ni nini umekiona kwa Tundu Lissu ambacho kinaweza kumpotezea what you call " credibility ?"

Kwa sababu, mimi binafsi ninachokiona kwa watu ni HOFU waliyonayo dhidi ya mtu huyu. Hakuna kitu kingine....

Kama kuna mtu ambaye hana "credibility" ya uongozi si mwingine bali ni mgombea wa CCM, ndg Magufuli....

Anafanya makosa mengi ya wazi kuanzia kuongea kwake, kutenda kwake na hata kupumua.....
 
Tume ya Taifa ya Uchaguzi imeishatoa utaratibu wa wagombea kuchukua fomu sasa kama mnajitia vichwa maji jaribu muende kwa maandamano, muone mtakavyofumuliwa.
 
Back
Top Bottom