WanaJF
Dodoma Inazizima.Ndivyo tunavyoweza kusema kwa Sasa.
Mapokezi kabambe yanamsubiri mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia Chadema Tundu Antipass Lissu ambaye atachukua rasmi fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kesho siku ya Nane Nane.
Inatarajiwa mgombea huyo kusindikizwa na umati mkubwa wa wakazi wa jiji la Dodoma katika kile kinachoonyesha Imani kubwa waliyo nayo kwa kiongozi huyo.
Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu ametoa wito rasmi kwa wakazi wa jiji la Dodoma na mikoa jirani kumsindikiza mgombea huyo Safari itakayoanzia makao makuu ya Chadema Kanda ya Kati Area C Mtaa wa Makongoro.
Katika mahojiano na wakaazi kadhaa wa jiji Hilo wameonyesha shauku kubwa ya kutaka kumuona Tundu Lissu ikiwa ni miaka mitatu alipoondolewa katika jiji Hilo akiwa nusu mfu baada ya kupigwa risasi kumi na sita na watu wasiojulikana na Sasa anarejea jiji Hilo Hilo akiwa mzima wa afya na akitembea kwa miguu yake miwili huku wabaya wake waliotaka kumuua wakifichama kusikojulikana.
Hapo Jana wanafunzi wa vyuo vikuu vya UDOM, CBE na Mipango walikuwa katika vikao vya namna ya kumsindikiza Lissu ambaye walimwita shujaa wao.
Tundu Lissu amejizolea uungwaji mkono na umaarufu mkubwa kutokana na sera yake ya kuwapa watu Uhuru wa kusema na kutoa maoni yao bila kuingiliwa na vyombo vya Dola endapo atachaguliwa kuwa Rais.Na pia kuruhusu vyama vya siasa. NGO's na vyombo vya Habari kufanya kazi zake kwa Uhuru Kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Chadema leo inatarajiwa kutoa ratiba njia atakazopita mtetezi huyo wa wanyonge na Msemaji wa wasio na sauti ili walau watu kujipanga manjiani kumsalimia na kumsindikiza.
#NiYeye2020
Updates leo tarehe 8/8 Jumamosi
Tayari mgombea wa Urais Tundu Lissu amewasili katika ofisi ya Chama Kanda ya Kati na amesaini kitabu Cha wageni na kupata ukaribisho na maelezo mafupi kutoka viongozi wa Kanda.
Kwa Sasa msafara wa kuelekea Tume ya uchaguzi umeanza ukiongozwa na pikipiki nyingi, magari makubwa ya mabasi na madogo huku wananchi wengi wakiwa kandokando ya Barabara waliounga mikono
Live Millard Ayo na UTV ya Azam
Saa 5 kamili Jumamosi
Mgombea wa Urais Tundu Lissu ndiyo anaingia hapa Time ya Taifa ya Uchaguzi akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa chama wafuasi na wananchi.
Chadema imetii masharti ya Tume ya Uchaguzi kwamba wafuasi na mashabiki wabaki nje na ndani wameingia viongozi wachache kumsindikiza Lissu.Viongozi waliomsindikiza Lissu ndani kwenye ukumbi ni Godbless Lema,Peter Msigwa,John Heche,Suzane Kiwanga na Baraka Mwago wote wakiwa Wajumbe wa Kamati Kuu.
Hamasa ni kubwa Sana na hapa ukumbini Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi yupo na meza yake Kuu wakisubiri kuingia mgombea Urais na Mwenza wake
Saa 5.20
Lissu akiwa na mgombea Mwenza wake wameingia kwenye ukumbi na Mkurugenzi wa uchaguzi ndiyo anatoa maelekezo kwa wagombea
Mheshimiwa Lissu anasikiliza kwa umakini mkubwa na kwa utulivu maelekezo ya Mkurugenzi wa Tume.
Sasa Mkurugenzi amemaliza kuongea na amemkaribisha Mwenyekiti Jaji Kaijage kukabidhi fomu kwa wagombea.Mwenyekiti anatoa maelezo mafupi ya nyongeza
Saa 5.27
Rasmi Sasa Tundu Lissu anakabidhiwa fomu za kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano baada ya kukamilisha mambo yote muhimu.Mgombea Urais na Mgombea Mwenza wanapokea kwa Pamoja huku makofi yakipigwa.
Saa 5.32
Shughuli zimekamilika rasmi hapa ndani ya ofisi ya Tume na kuagana rasmi Kati ya viongozi wa Tume na Chadema.
Umati mkubwa Sana wa wafuasi wa Chadema unasubiri nje ya ofisi ya Tume huku watu wengi wakiwa wanafuraha kubwa isiyoelezeka
Kinachoendelea baada ya Kutoka Ofisi za Tume:
Kwa Sasa ni maandamano makubwa yakiongozwa na pikipiki nyingi, magari yasiyo na idadi huku mgombea wa Urais Tundu Lissu akiwa katika gari ya wazi akipungia watu waliojipanga kando kando ya Barabara.
Gari ya Mgombea Tundu Lissu imezingirwa na maafisa wa Usalama wa Chama maarufu Kama Red Brigade ambapo idadi ya walinzi wa gari lake waliozunguka hawapungui 12 kwa Idadi
Dodoma Inazizima.Ndivyo tunavyoweza kusema kwa Sasa.
Mapokezi kabambe yanamsubiri mgombea wa Urais wa Tanzania kupitia Chadema Tundu Antipass Lissu ambaye atachukua rasmi fomu Tume ya Taifa ya Uchaguzi kesho siku ya Nane Nane.
Inatarajiwa mgombea huyo kusindikizwa na umati mkubwa wa wakazi wa jiji la Dodoma katika kile kinachoonyesha Imani kubwa waliyo nayo kwa kiongozi huyo.
Mwenyekiti wa Kanda ya Kati Lazaro Nyalandu ametoa wito rasmi kwa wakazi wa jiji la Dodoma na mikoa jirani kumsindikiza mgombea huyo Safari itakayoanzia makao makuu ya Chadema Kanda ya Kati Area C Mtaa wa Makongoro.
Katika mahojiano na wakaazi kadhaa wa jiji Hilo wameonyesha shauku kubwa ya kutaka kumuona Tundu Lissu ikiwa ni miaka mitatu alipoondolewa katika jiji Hilo akiwa nusu mfu baada ya kupigwa risasi kumi na sita na watu wasiojulikana na Sasa anarejea jiji Hilo Hilo akiwa mzima wa afya na akitembea kwa miguu yake miwili huku wabaya wake waliotaka kumuua wakifichama kusikojulikana.
Hapo Jana wanafunzi wa vyuo vikuu vya UDOM, CBE na Mipango walikuwa katika vikao vya namna ya kumsindikiza Lissu ambaye walimwita shujaa wao.
Tundu Lissu amejizolea uungwaji mkono na umaarufu mkubwa kutokana na sera yake ya kuwapa watu Uhuru wa kusema na kutoa maoni yao bila kuingiliwa na vyombo vya Dola endapo atachaguliwa kuwa Rais.Na pia kuruhusu vyama vya siasa. NGO's na vyombo vya Habari kufanya kazi zake kwa Uhuru Kama ilivyokuwa miaka ya nyuma.
Chadema leo inatarajiwa kutoa ratiba njia atakazopita mtetezi huyo wa wanyonge na Msemaji wa wasio na sauti ili walau watu kujipanga manjiani kumsalimia na kumsindikiza.
#NiYeye2020
Updates leo tarehe 8/8 Jumamosi
Tayari mgombea wa Urais Tundu Lissu amewasili katika ofisi ya Chama Kanda ya Kati na amesaini kitabu Cha wageni na kupata ukaribisho na maelezo mafupi kutoka viongozi wa Kanda.
Kwa Sasa msafara wa kuelekea Tume ya uchaguzi umeanza ukiongozwa na pikipiki nyingi, magari makubwa ya mabasi na madogo huku wananchi wengi wakiwa kandokando ya Barabara waliounga mikono
Live Millard Ayo na UTV ya Azam
Saa 5 kamili Jumamosi
Mgombea wa Urais Tundu Lissu ndiyo anaingia hapa Time ya Taifa ya Uchaguzi akisindikizwa na viongozi mbalimbali wa chama wafuasi na wananchi.
Chadema imetii masharti ya Tume ya Uchaguzi kwamba wafuasi na mashabiki wabaki nje na ndani wameingia viongozi wachache kumsindikiza Lissu.Viongozi waliomsindikiza Lissu ndani kwenye ukumbi ni Godbless Lema,Peter Msigwa,John Heche,Suzane Kiwanga na Baraka Mwago wote wakiwa Wajumbe wa Kamati Kuu.
Hamasa ni kubwa Sana na hapa ukumbini Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi yupo na meza yake Kuu wakisubiri kuingia mgombea Urais na Mwenza wake
Saa 5.20
Lissu akiwa na mgombea Mwenza wake wameingia kwenye ukumbi na Mkurugenzi wa uchaguzi ndiyo anatoa maelekezo kwa wagombea
Mheshimiwa Lissu anasikiliza kwa umakini mkubwa na kwa utulivu maelekezo ya Mkurugenzi wa Tume.
Sasa Mkurugenzi amemaliza kuongea na amemkaribisha Mwenyekiti Jaji Kaijage kukabidhi fomu kwa wagombea.Mwenyekiti anatoa maelezo mafupi ya nyongeza
Saa 5.27
Rasmi Sasa Tundu Lissu anakabidhiwa fomu za kugombea Urais wa Jamhuri ya Muungano baada ya kukamilisha mambo yote muhimu.Mgombea Urais na Mgombea Mwenza wanapokea kwa Pamoja huku makofi yakipigwa.
Saa 5.32
Shughuli zimekamilika rasmi hapa ndani ya ofisi ya Tume na kuagana rasmi Kati ya viongozi wa Tume na Chadema.
Umati mkubwa Sana wa wafuasi wa Chadema unasubiri nje ya ofisi ya Tume huku watu wengi wakiwa wanafuraha kubwa isiyoelezeka
Kinachoendelea baada ya Kutoka Ofisi za Tume:
Kwa Sasa ni maandamano makubwa yakiongozwa na pikipiki nyingi, magari yasiyo na idadi huku mgombea wa Urais Tundu Lissu akiwa katika gari ya wazi akipungia watu waliojipanga kando kando ya Barabara.
Gari ya Mgombea Tundu Lissu imezingirwa na maafisa wa Usalama wa Chama maarufu Kama Red Brigade ambapo idadi ya walinzi wa gari lake waliozunguka hawapungui 12 kwa Idadi