Dodoma: Watu 5 wa Familia moja wauawa

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,492
54,895
20220123_081142.jpg
Watu watano wa familia moja wameuawa na watu wasiojulikana katika eneo la Zanka wilayani Bahi mkoani Dodoma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Onesmo Lyanga amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amebainisha kuwa Jeshi hilo linaendelea na uchunguzi juu ya tukio hilo.

Chanzo: Radio One

=======

Watu watano wa familia moja wakazi wa kijiji cha Zanka wilayani Bahi Mkoa wa Dodoma wameuawa na watu wasiojulikana.

Waliouawa ni mume, mke, watoto wawili na mjukuu mmoja wote wa familia moja.

Mdogo wa baba wa familia hiyo, Noah Kapande amesema miili hiyo iligunduliwa na watoto waliokwenda kufungua ng'ombe jirani na nyumba hiyo jana Jumamosi saa 10 jioni baada ya kusikia harufu.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka akiongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa huo amewataka wakazi wa kijiji hicho na ndugu kutoa ushirikiano ili waliofanya kitendo hicho wajulikane.

“Hili jambo litakuwa limefanywa kwa ushirikiano na watu wa hapa hawezi kuja mtu kutoka huko kwenye nyumba ya mtu akaua watu watano asiwe na mwenyeji hapa,”amesema.

Ameagiza vyombo vyote vya ulinzi na usalama na uchunguzi vya mkoa kuhamia katika kijiji hicho kufanya uchunguzi wa tukio hilo na waone namna ya kushirikiana na wenzao kama italazimika kufanya hivyo.

“Ni lazima hawa watu wapatikane ni lazima.labda wananzaka muwe wanafiki naomba wananchi watoe ushirikiano…, hii ni damu ya watu watajisema tu,” amesema.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Onesmo Lyanga amesema madaktari wanafanya uchunguzi miili hiyo na baada ya uchunguzi watakuwa na nafasi ya kusema watu hao waliuawa kwa namna gani.

“Polisi tunaendelea kufanya uchunguzi tunatarajia tutawapata waliohusika na hili tukio lakini kwa sasa bado mapena kusema nani kahusika moja kwa moja,” amesema.

Mwananchi
 
Mauaji yanazidi kwa kasi sana...ndugu zangu tumrudieni Mwenyezi Mungu ili tuwe na upendo. Kwa sasa upendo umekwisha baina yetu, bila Mungu hatuwezi kutatua hili swala!. Eeeh Mwenyezi Mungu tuokoe waja wako..
Watu waelimishwe tu, hamna cha maombi hapo, kitafutwe chanzo cha mauaji, tatizo mnachagua aina ya ukatili na watu wanaofanyiwa, mf. Ukatili unasemwa dhidi ya wanasiasa hamkemei wala hamna maombi, kumbe ndio mnapanda mbegu ya chuki na ukatili!
 
Watu waelimishwe tu, hamna cha maombi hapo, kitafutwe chanzo cha mauaji, tatizo mnachagua aina ya ukatili na watu wanaofanyiwa, mf. Ukatili unasemwa dhidi ya wanasiasa hamkemei wala hamna maombi, kumbe ndio mnapanda mbegu ya chuki na ukatili!
Ndugu, Amini usiamini bila Mungu kuwepo moyoni mwetu hatuwezi kuwa na upendo. Upendo ndio kila kitu, bila kuwa na moyo wa upendo watu wataelimishwa lakini chuki zitaendelea kubaki tu na mauaji yataendelea.
 
Back
Top Bottom