Habari wana JF!
Ninafurahishwa sana na wapiga kura wa mkoa wa Dodoma kwa kuipa CCM ushindi kila chaguzi.
Natamani watu wa Mwanza, Mbeya na Moshi waige mfano huu ili kuharakisha maendeleo katika mikoa yetu hiyo.
CCM bado ndio chama IMARA Tanzania.
Kwa kuwa haujui hali ya umaskini, miundombinu mibaya na hali mbaya ya huduma za jamii katika maeneo mengi ya mkoa wa Dodoma, sishangii kuona kauli kama hii. Nimeishi na kufanya kazi Dodoma kwa miaka zaidi ya 10 sasa. Nafahamu maeneo mengi ya vijijini katika mkoa huu. Kwa kifupi ni kuwa ni mkoa ambao uko nyuma sana kimaendeleo katika nyanja karibu zote ukilinganisha na mikoa uliyoitaja. Ni mkoa ambao hauna wawakilishi makini wa wananchi kwenye majimbo karibu yote bali una watu wanaojiita wabunge lakini kimsingi ni watetezi wa sisiemu na serikali yake.
Kwa kukumbusha tu ni kwamba, kwa sasa mkoa wa Dodoma una majimbo na wabunge wafuatao: Lusinde aka kibajaji au kamusi ya matusi (Mtera), Teu ambaye pia ni naibu waziri wa viwanda (Mpwapwa), Simbachawene, naibu waziri wa nishati na madini (Kibakwe), Chibulunje (Chilomwa), Badwel (Bahi), Nkamia (Kondoa Kusini), Zubein Mhita (Kondoa Kasikazini) na Malole (Dodoma Mjini).
Tuweke ushabiki wa chama pembeni, nani kati ya wabunge hawa ni watetezi wa wananchi na maslahi ya Taifa? Je, uliwasikia kwa mara ya mwisho lini wakichangia mijadala bungeni au hata tu kuuliza swali la nyongeza (ukiaacha hao manaibu waziri)? Kwa mara ya mwisho walionekana majimboni kwao lini kuzungumza na wananchi au kuhamasisha shughuli za maendeleo?
Hii ni picha ya jumla tu, lakini ninaweza kueleza hali ya jimbo moja baada ya jingine, kijiji baada ya kijiji... kutoka Nondwa, Chali Makulu, Mpangalanga (Bahi); Potea, Mulua, Mondo (Kondoa Kaskazini); Bilise, Chase, Humekwa, Lalta (Kondoa Kusini), Chamae, Sagara (Kongwa) hadi Mpwayungu (Mtera) na Zuzu, Mbabala (Dodoma Mjini).
Kwa kifupi umaskini na ujinga wa wananchi katika maeneo haya ndio umeendelea kuwa mtaji wa CCM kwa miaka mingi. Taratibu sasa wananchi wanaanza kuona mwanga na kugundua kuwa wamedanganywa vya kutosha, wamedhulumiwa vya kutosha, wamedhalilishwa vya kutosha...na sasa karibu watasema sasa yatosha!