DODOMA: Bashe, Musukuma na Malima waachiwa

DODOMA: Bashe, Musukuma na Malima waachiwa

Kuna taarifa zinatembea mitandaoni kuwa bashe, Malima na musukuma wamefukuzwa/ wamevuliwa uananchama wa ccm. Kama ni kweli ccm haitakiwi kufika huku. Demikrasia IPI mnayoihubiri Kwa wananchi wenu km watu ambao mnapingana nao mnawavua uanachama.

Bashe kwa nafasi yake ya ubunge bungeni huwa anaibrand ccm sana bungeni.!! Kuwafukuza wakina bashe ni kuonekana chama hakina misingi imara. Chama kikubwa lazma kiwe mfano wa mambo mazuri.

Kama ni kweli hawa wamefukuzwa mjiangalie upya !! Uchaguzi umepita tokea 2015 lakini mpaka leo bado mnatibu majeraha ya uchaguzi..
Kiongozi mzuri ni yule anayewaungasha watu wote wasiompenda na wanaompenda.
Haiwezekani eti waliomuunga mkono lowasa mpaka Leo bado ni maadui wa chama. Mnakosea sana. Na hapa ndiyo mnadhihirisha uafrika wenu. Afrika tunafanya maamuzi yetu Kwa kuangalia hisia zaidi badala ya ueledi, ujuzi na busara. Fukuza fukuza haisaidii chama wala haiongozi kura za 2020 kwenye uchaguzi.

Uongozi wa chama ni tofauti na serikali, uongozi wa chama lazma uwe very diplomatic na mwenye busara sana..kwenye chama lengo kubwa ni kuongeza wanachama na supporter wengi..!! Kwahiyo kiongozi ni yule anayewauunganisha watu wote. Sophia simba amesema hatogombea tena, sasa kwann mmemfukuza uanachama.

Kinana wewe ni katibu mkuu, ebu yaepushe haya na mshauri vyema bosi wako.

Huwez ongeza wanachama Kwa kufukuza fukuza.
Chagueni leo hii ni nani mtamtumikia!huku unataka kule unataka!wasaliti tupa kule!chama hubomolewa na wasaliti ndani ya chama!
 
Wale madiwani wanne walivyofukuzwa na chadema Mbona sisi hatakuwaingilia, mngefata demokrasia chadema wale msingewafuta uanachama au msingewahi kufukuza wanachama Leo hii tungekuwa tunajadili kwa upana wake hiyo demokrasia
 
Ni mpumbavu tu ndiye angedhania kuwa ule uhuni uliofanywa wakati wa kumtafuta mgombea wa urais wa ccm 2015 ungeachwa kwa ule utaratibu wa funika kombe mwamahara apite, na eti wahusika wasichukuliwe hatua za kinidhamu. Yeyote mwenye mawazo kama haya atakuwa mpumbavu na mpuzi.

Na washawasha!
 
Wanachama kufukuzwa siyo vyema kabsa - mkuu watu wanafutwa ushirika makanisani unashangaa kwenye siasa.
kama hawawezi kutimiza ndoto zao huko wanauwanja mpana nje ya ccm. Kikubwa haki na utaratibu ufanye na adhabu ziwe proportion na kosa kwa kuangalia taratibu za chama zinasemaje kwa kosa husika.
Vigogo wanafurushwa wewe[emoji83] [emoji196] [emoji216] unajipendekeza. Subiri wakubashite[emoji778] [emoji196]
 
Wale madiwani wanne walivyofukuzwa na chadema Mbona sisi hatakuwaingilia, mngefata demokrasia chadema wale msingewafuta uanachama au msingewahi kufukuza wanachama Leo hii tungekuwa tunajadili kwa upana wake hiyo demokrasia
Mbona mleta mada hajaandika kuhusu chadema,au Usipo wataja hao waume zako huridhiki.
 
Nawashangaa wote mnaolalama kwani chama kikiamua kujisafisha chenyewe kuna shida.kwako unapotoa utandu wa buibui kwenya madirisha na milango au kupiga deki nyumba unakuwa unaharibu au unaboresha?
 
Polisi imechukua nafasi ya Green Brigade kuzuia watu wasiongee......

Kamata kamata kama vile tuko kwa Jammeh
Bora hata kwa jameh, maana kule inajulikana kwamba kimeshanuka, sasa kwetu kimenuka kisiri siri!
 
Huko kote naona kama ulikua unazunguka m-buyu tu.
Hapo hoja ya msingi ni Kinana kuokoa jahazi kwa kumshairi Pombe.
Kwa hili nina mashaka hata Kinana anahofia kiti chake
 
Umeandika kwa haraka haraka Mno, Tulia, halafu weka hoja, watu tumeshakushanya popcorn za kutosha, tupo kusoma mawazo yako,
Sijaona wazo la msingi kadiri ya Uzi ulivyotambulishwa. Sababu za kufukuzwa kwao ni zipi?
 
Akili za Bashe,si za kiccm ccm ni za ki UKAWA UKAWA.
Wacha wamtimue,tulambe kichwa imara hicho.

Kumbukeni kuwa,Bashe haitaji tena kujinadi,hivo mukimtema tuu jimbo la ukawa.

Badala mumtumie kwa maslahi ya chama,mnafanya figisu na fitna afukuzwe mleteni sasa.
 
Wameachiwa muda si mrefu usiku huu.

Nini wamehojiwa?

Kwanini wameachiwa?

Nini hatma yao?

Tutajua baadae. Ila wako huru sasa!
========

Kulingana na taarifa ya kamanda wa polisi mkoa wa Dododma, wahusika walikamatwa kwa kufanya vurugu katika vikao vya chama cha mapinduzi vinavyoendelea mjini Dodoma.
Kweli rais JPM ambaye ni Mkiti wa CCM namkubali. Nilidhani upinzani tu ndiyo wanawekwa lock up, kumbe hata wabunge wa ccm wanaisoma namba?!! Mimi sina chama lkn nawaomba wapiga kura wenzangu huyu bwana tumpe awamu nne nchi itakuwa imefikia uchumi wa kati.
 
Huko kote naona kama ulikua unazunguka m-buyu tu.
Hapo hoja ya msingi ni Kinana kuokoa jahazi kwa kumshairi Pombe.
Kwa hili nina mashaka hata Kinana anahofia kiti chake


Mkubwa anashauriwa kimafumbo mzee...unataka nikanyee ndoo kwani miye mke wangu simpendi
 
Back
Top Bottom