Dkt. Mwigulu: Deni la Taifa limeongezeka hadi Tsh. Trilioni 79.19, bado ni himilivu

HIMARS

JF-Expert Member
Jan 23, 2012
69,373
94,566

Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba leo Bungeni Dododma amewasilisha Bungeni taarifa ya Hali ya Uchumi wa Kitaifa kwa Mwaka 2022 na Mpango wa Maendeleo ya Taifa wa Mwaka 2023/2024 ambapo moja ya mambo aliyoyasema ni kwamba hadi kufikia mwezi Aprili 2023, deni la Serikali lilikuwa shilingi bilioni 79,100.19 sawa na ongezeko la 13.9% ikilinganishwa na Shilingi bilioni 69,440.01 kwa kipindi kama hicho mwaka 2022.

“Kati ya kiasi hicho, deni la nje ni shilingi bilioni 51,162.60 na deni la ndani ni Shilingi bilioni 27,937.59, ongezeko la deni limetokana na kupokewa kwa fedha za mikopo kwa ajili ya kugharamia miradi mbalimbali ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa miundombinu ya barabara, reli, viwanja vya ndege, umeme, elimu na afya, aidha tathmini ya uhimilivu wa deni la Serikali iliyofanyika Desemba, 2022 imeonesha kuwa deni ni himilivu na viashiria vya deni viko ndani ya wigo unaokubalika kimataifa katika kipindi cha muda mfupi, wa kati na mrefu”

“Machi 2023, kampuni za Fitch Ratings na Moody’s Investors Service zilianza zoezi la kuifanyia Nchi tathmini ya kukopesheka katika masoko ya fedha ya kimataifa, zoezi hilo lilikamilika ambapo kampuni ya Moody’s Investors Service ilichapisha matokeo ya tathmini hiyo Mei 2023 na kampuni ya Fitch Ratings mwezi Juni 2023, kwa mujibu wa matokeo hayo, Tanzania imewekwa katika daraja la B2 POSITIVE na Kampuni ya Moody’s Investors Service na daraja la B POSITIVE na Kampuni ya Fitch Ratings ambayo yanaashiria taswira chanya kwa Nchi kimataifa”

“Pamoja na mambo mengine, matokeo hayo yamechangiwa na mwenendo mzuri wa ukuaji wa uchumi, usimamizi makini wa deni la Taifa, kuweka mazingira wezeshi ya uwekezaji kwa sekta binafsi, kuimarisha ushirikiano wa kimataifa pamoja na kuleta maridhiano ya kisiasa ndani ya Nchi, kukamilika kwa zoezi hilo, kutaiwezesha Nchi kutambulika katika masoko ya fedha ya kimataifa na hivyo, kuongeza wigo wa upatikanaji wa mikopo kwa Serikali na sekta binafsi”
 
Waziri wa Fedha, Dkt. Mwigulu Nchemba, amesema hadi kufikia Aprili, 2023, Deni la Nje ni Tsh. Trilioni 51.60 wakati Deni la Ndani ni Tsh. Trilioni 27.59 ambapo ongezeko hilo limechangiwa na kupokelewa kwa Fedha za Mikopo.

Kuhusu akiba ya Fedha za Kigeni, amesema hadi kufikia Aprili 2023, kulikuwa na Dola za #Marekani Bilioni 4.88 ambayo inatosheleza uagizaji wa huduma kutoka nje ya Nchi kwa kipindi cha miezi 4.

Juni 6, 2023, Benki Kuu ya #Tanzania (BoT) ilisema Nchi ina upungufu wa Dola za Marekani ingawa hali hiyo bado ni himilivu kwasababu Serikali kila siku BoT inauza Dola Milioni 2 kila siku, kulinganisha na Nchi nyingine.

BUNGE TV


 
Back
Top Bottom