TANZIA Dkt. Mwele Ntuli Malecela afariki Dunia, aligombea Urais wa JMT 2015

Kwahiyo kurud salama ndio akawa jasus mbobezi?? Wabongo wakikupenda aisee vyeo vyote watakupa
sikutaka kueleza kiundani,kwa nn alitumwa kule ,nn kilimkuta akiwa live na idd Amin,alikaa siku 5 akiwa bado huko Uganda .ni stor ndefu ,nimefupisha tu mkuu.kwenda kwa hasimu wako ambae mmekamiana kivita ,na ukamfanya adui akufurahie na kukupokea na kukuzungusha mjini mkiwa wawil tu na walinzi wachache ,halafu akushushe hadharani na kukukubali mbele ya raia wake,sio kitu kidogo. unaambiwa Amin alipokuwa na malecela ikulu kwake ,alimuimba watoke yy na malecela tu,John alijua jamaa anakwenda kumaliza kazi,Amin aliwasha gari ikagoma kuwaka,akachukua ya pil ikagoma pia ,hapo John alishukuru izmegoma,lkn ghafra mlinzi akasogeza nyingine ikakubali kuwaka wakaondoka .
 
Pole mzee Malecela. Ila huyu mzee alimmaindigi Lowasa akiwa kijana baada ya kumuibia kwenye deal walifanya kadhia iyo akaiweka moyoni hadi kijana wake naye lemutuz alikuwa nayo chuki kwa Lowasa.

Lowasa alipokuwa anataka kuwa rais kwa udi na mzee John aliiapa atapigana Don asichukue nchi.

July 2015 alikatisha kabisa matibabu yake nje faster nakurudi Bongo alipofika JNIA akaonganisha faster Dodoma eti alichodai kwenda kuongeza nguvu Lowasa kukatwa na kuchinjiwa baharini. Hakuna mtu Tanzania aliyfurahi Lowasa kukatwa jina lake july 2015 kama mzee

Simulizi kutoka vijiwe vya umbea vya wanavitengo waliostaaf

R.IP Mwele
mm mwenyewe adui yangu ,akifeli najiskiaga burudani!!
 
Tumempoteza mwana sayansi mwenye viwango vya kimataifa..
Na ni wachache mno kutoka nchi ya utopoloni...
Na alibezwa na yule mwenye phd feki ya utopolo ....
R.I.P Clinical Scientist...
 
Dr mwele ametangulia kwa Mungu ila amemuacha baba ake hapa duniani .Wanasema usiombe mzazi azike mtoto .Mzee malecela alikuwa na Mtoto wake Dr mwele mpaka alipofariki .Mungu akiamua ameamua .Amen
Mhh...Malechela yupo Dar anasuniri mwili,na alisema,mwenyewe kuwa waliopo hiko ni wanawe ....na akaeleza,kuwa wanapigiana simu na WHO ,Geneva ,kuhusu taratibu ...au Sea View siku hizi ipo Geneva!?
 
pole zimuendee huyu mkongwe na gwiji la siasa hapa nchini,ni jasusi mbobezi haswa ,membe hatii mguu. kabla ya Vita kuanza ,vuguvugu lilikuwa ndo limewaka Moto,idd Amin alimpaga Salam mwal.kuwa atamchapa risasi live , kiongozi yeyote wa tz atakayejipendekeza kupeleka pua yake Uganda,Sasa bana mwal. akamtumaga mzee malecela aende Uganda kwa Amin ,ajaribu kuongea na Amin aache chokochoko,mzee John alienda ,na kurudi salama.
Kweli awamu ya kwanza na ya nne zilijua kubinya fikra za watanzania na kujiona wao ni miungu.
 
Hata yeye ni Mzee mwenye akili sana, ukimuondoa Nyerere Malecela ni mtu ninayemkubali sana,
Ni yeye na SAS Ndio walifaa sana kuwa Marais wa Tanzania baada ya Nyerere.
Kwanini unasema hivi? Huyu si alikataliwa na Nyereere
 
Pole mzee Malecela. Ila huyu mzee alimmaindigi Lowasa akiwa kijana baada ya kumuibia kwenye deal walifanya kadhia iyo akaiweka moyoni hadi kijana wake naye lemutuz alikuwa nayo chuki kwa Lowasa...
Ngoja Pascal Mayalla atupe ufafanuzi. Ninachokumbuka ni kwamba le mutuz alikuwa upande wa lowasa. Alipokatwa akalaum saana kisha baadae akaanza kumsapot the late magu
 
Back
Top Bottom