Dkt. Mpango: Kodi si tatizo Bandarini

Dkt. Mpango: Kodi si tatizo Bandarini

Hiyo ndio hali halisi na ndio ukweli wa bandari yetu mizigo mingi ilikuwa hailipiwi kodi hivyo ni bora wasije kabisa....!

Kwa nini tunaconclude haraka kwamba huu upungufu ni kwa sababu watu walikuwa wanakwepa kodi? Vipi kuhusu ile VAT iliyoanzishwa sasa kwa magari yote yalikokuwa yanatransit (additional cost kwa importation tax)?
 
Hata Mugabe alipokuwa akiiteketeza Zimbabwe vibaraka wake walikuwa wakiimba Mzalendo na Miadilifu huku wakimpamba kwa kila hali! Baada ya muda watu wakawa wananunua mkate na kapu la hela, hakika tuliuona huo uzalendo wa Mugabe na tunauona huo uzalendo wa Magufuli!!
 
Kuna msemaji mmoja kaongea kwa hasira kweli... Nafkiri alitukana kabisa.
 
Naipongeza serikali kwa hatua hii ya kudhibiti kwa sasa tunajua kabisa tunapata mizigo ya aina gani na kiasi gani.. Nina hakika kwa sasa mtu akiagiza gari lake hato ibiwa...!
kwa experience ya wengi upande wa magari ICD's binafsi kuna usalama zaidi,na gari unaikuta intact
 
Hali hii imepelekea uongozi wa mamlaka ya bandari kufuta bandari kavu hii ni baada ya wafanya biashara kuikimbia.
Chanzo itv
Sio kufuta! Ni kusisitisha kutokana na makubaliano yao kwamba ikiwa bandarini kuna mizigo basi babdari kavu watapata kazi vinginevyo ni kinyume chake! ITV
 
Kama meli hazitakuja tutawezaje kuuza mbaazi...?na msimu ndio huu umekwisha anza wanunuzi ni wa huko India sisi hapa nchini hatutumii Mbaazi ila kidogo hivi , ukizingatia mbaazi hazivumilii wadudu ni rahisi sana kushambuliwa na wadudu kama meli haziingii nchini Zitasafirishwaje....?
Utasafirisha kwa ndege
 
Msijali watanzania, Magufuli atawaletea Tanzania ya asali, maziwa na viwanda! Hiyo ndiyo Tanzania ya Magufuli.. CCM hoyeee
 
Sababu Ni udikteta uchwara

Mutaita majina yote, mnayemwita dikteta uchwara ni mukombozi wa wengi, sasa majipu yanawiva, Kama muliziwea kuvuna kwenye shamba la bibi poleni sasa limewekwa kufuli sasa ni kazi tenda za kuiuzia selikali nyanya moja millions moja wakati nyanya zimetoka kwenye shamba la bibi umepita sasa ni kazi. Accept it and move on.
 
Hivi ni kodi tu kupanda ama kulipwa ndio ikimbize wateja wote ?? Aisee kuna kitu hakipo sawa hapa
UncleBen, naamini unajua kabisa kuwa ukishaona nchi inatetea na kutegemea Kodi pekee kama source of income ni tatizo kubwa sanaaa.

Nchi zote zilizoendelea ziliwekeza kwenye Agriculture na viwanda, viwanda hivi vyetu vitaendeshwa kwa source gani of energy? Umeme huu wa kusuasua hata bila viwanda?

Hili la kodi litaumiza watanzania wengi.
 
ccm mbele kwa mbeleee!

mtukufu mwenyenzi mungu wa tanzania yupo busy na kutafuta wanafunzi "hewa" bhana, hiyo bandari kama vipi ifieeee mbeleee!

NO VISION NO MISSION!
WE ARE HEADING TO HELL!
 
Tatizo ni Makauli ya Raic. Kulipa kodi sio tatizo. Kumbuka kodi haimuumizi mfanyabihshara. Inamuumiza mtumiaji wa mwisho.

Jamaa si alisema anataka waish kma mashetani. Sasa very soon yeye ndye ataish kama ibilisi Lucifa.
 
Hilo ndiyo tatizo la nchi kuendeshwa kwa staili ya ONE MAN SHOW.....

Hashauliki wala haambiliki.......................

Kila kitu anataka kutoa maagizo yeye tu na hataki mtu yoyote atoe sababu zozote za kutotekelezwa kwa maagizo yake......

Tulimsikia JPM akitamba kuwa wacha hizo meli ziende kwenye hizo bandari za nchi ambazo wanazokubali bandari zao kupitisha mizigo bila kulipa kodi!

Lakini Mkuu wa nchi angetakiwa kuwa msikivu zaidi ili kujua sababu halisi za kupungua mizigo bandarini badala ya kufanya conclusion kuwa mizigo hiyo imepungua kutokana na wale waliokuwa hawalipi kodi kuhamishia mizigo yao kupeleka kwenye bandari za nchi nyingine zinazoruhusu bandari zao kupitisha mizigo bila kulipa kodi!

Kauli nyingine ya kibabe ya Mkulu ni ile ambayo alitoa kuwa watalii wasiotaka kulipa VAT waliyoianzisha ni bora wasije nchini, kwa kuwa yeye anataka watalii matajiri wenye uwezo wa kulipa kodi!

Kwa ubabe huo wa Presidaa wetu tayari sekta ya utalii nayo ishapata athari kutokana na kupungua kwa kiasi kikubwa kwa watalii wanaoingia nchini.....

Naamini kwa mwendo huu nchi yetu inaelekea kuwa Zimbabwe nyingine, kwa kuwa hulka ya Rais wetu inashabiana sana na yule Mzee asiyetaka kung'atuka kule Zimbabwe.........

Nchi hii haiwezi kuwa Kama Zimbabwe chini ya Magufuli, lakini Kikwete angeendele kuwa Rais kwa meizi Sita mingine nchi ingekuwa kama Zimbabwe. Economy ya Tanzania ilikuwa ya uwongo, mteja wa Kila biashara ilikuwa serikali, matajiri waliyotajirika bila ya kufanya kazi Bali wizi jasho linawatoka. Fanyeni kazi siyo kutajirika kwa dhuruma ya wengi.
 
Mliambiwa Mafisadi wakishikwa Nchi Itayumba hamkumuelewa Pinda... Hapa Kazi tu ya kurejea Nyumbani Bandarini hakuna kazi... Na Bandari kavu zishafungwa zote... ati tunaaminishwa zitahamishiwa Dodoma.... Sophia sophia
 
Back
Top Bottom