Dkt. Mpango: Kodi si tatizo Bandarini

Dkt. Mpango: Kodi si tatizo Bandarini

Waziri Mpango usipate shida ya kuona kwamba unawajibika kuwajibu hao wazushi wasioitakia mema nchi yao. Baadhi yetu tulipoona picha zinazosemekana ni za bandari kavu zikiwa tupu tuliiponge u ubicadas za serikali tukijua kwamba hayo ni matokeo ya kibano cha serikali kwa wale waliokuwa wakiingiza makontena bure kwa kukwepa ushuru. Na ndio hao wanaosambaza taarifa za kizushi. Nchi zilizoendelea hutoza kodi iweje kwa Tanzania iwe nongwa eti mizigo haiji kutokana na kodi!

Mhe. Waziri Mpango wakosoaji wasikunyime usingizi wala kukutia pressure. Usijali maneno ya wapinga maendeleo. Watasema mchana ucku watalala! Piga kazi tu, maana hakuna asiyejua hizi ni zama za Hapa Kazi Tu!
Acha umbulula wewe kama jpm anaamini na kutoa matamko tena kwenye matangazo ya TRA kuwa nchi haiwezi kupata maendeleo bila kukusanya kodi sasa leo kodi imepungua karibu 50% ya makusanyo hayo maendeleo yatatoka wapi. Tuache unafiki. Kwanza umewahi kwenda bandarini siku za karibuni au unaleta pumba zako humu?
 
"Sukari imepanda Tanzania kwa sababu wachina wameongeza matumizi ya sukari hivyo bei ya sukari imeongezeka nchini china, kwa sababu wachina ni marafiki zetu, bei ya sukari haina budi kupanda nchini Tanzania............Mchumi"
ha ha ha mara ohh tutagawa bure sukari iliyofichwa ipo wapi mie sijawahi kupata ya bure hata kijiko kimoja
 
Ama kwa hakika huyu waziri hajielewi kabisa. Picha haoni. Eti kupungua kwa mizigo bandarini kwa takribani asilimia 70 kunatokana na uchumi wa China kuyumba? kwamba china ndo ina form that 70% ya mizigo bandarini? kwamba kodi haina uhusiano na importation kupungua? how about transit cargo to rwanda, burundi, DRC, Zambia, Malawi??

Haya ni Maajabu!
Nenda tunduma kaangalie kama utakuta ile misururu ya malori ya makontena na magari yaliyoagizwa"IT". hawa wanafikiria watanzania ni walewale wa zamani kila jambo wanaliamini
 
Nilishasema hapa kwamba sisi kazi yetu ni moja tu,kuimba mtukufu, mtukufu,mtukufu.........
 
Wafanya biashara wakubwa wanaokwepa kodi si ni marafiki zenu jamani ? Si ndio wanaowafadhili? Sass inakuwaje mnawananga?
 
Mkuu hapo kwa mombasa kachemka vibaya mombasa sasa hivi ipo busy ile mbaya
Tatizo lake anajaribu kumridhisha Rais kwa kila hali kuhusu makusanyo ya pesa. Imagine mpaka pesa za wafadhiri anataka chengi iingie serikalini. Kwa jinsi inavyokwenda lazima atachemka au atakwama somewhere .... na huo ndiyo utakuwa ni mwisho wake!!
 
Tatizo lake anajaribu kumridhisha Rais kwa kila hali kuhusu makusanyo ya pesa. Imagine mpaka pesa za wafadhiri anataka chengi iingie serikalini. Kwa jinsi inavyokwenda lazima atachemka au atakwama somewhere .... na huo ndiyo utakuwa ni mwisho wake!!
Nakubaliana na wewe mkuu
 
Magari nayo yanatoka China?
Kama
“Walipe kodi tu ili serikali iweze kuwahudumia, haiwezekani bandari itoe huduma kwa wafanyabiashara pasi na wao kulipa kodi, hapana.”
Hivi kwa nini gari unanunua nje kwa bei nafuu lakini hapa wapigwa KODI ya kikatili na kiuwaji?
USHAURI
Kama gari litatumika kwenye miji mikubwa pigeni kodi kubwa...kama gari litatumika huko NKASI kuweni wazalendo kwa kuweka kodi ndogo.
....SENT.....
 
Leo hakuna wakuhoji sukari kwanini imepanda bei na tulihakikishiwa malighafi hiyo itashuka bei hadi 1800! Ngoja tusubiri maana wao wamekuwa wazee wa kubadili gia hewani.
Mimi nadhani hii ni sabotage tu ya wafanya biashara waliozoea kula bila kulipa kodi. Lkn nadhani kuwa na bandari kwa faida ya wachache haina maana kabisa lazima tuendelee kubanana kuliko kuachia watu wafanye wanavyotaka kwa masilahi yao huku nchi ikiendelea kuwa kwenye lindi la umaskini. Singapole imeendelea kwa sababu ya bandari tu na bila kulipa kodi wafanya biashara sidhani ingefika hapo ilipo tunatakiwa kukaza tu hadi kitaeleweka
 
Kenya Yaichezea rafu Tanzania,,,, Soma yote Katika gazeti la RAIA MWEMA

Kodi ya VAT kwenye utalii, ni kuwa East Africa Finance Ministers walijadili, ila Kenya Kapiga chenga

Tanzania mumewin Bomba la Mafuta Uganda to Tanga, Kenya wana win Tourism.....

Tanzania bado sana kuwaweza wakenya, japo sio koloni..

Labda tujaribu Rwanda --Koloni letu
 
Acha umbulula wewe kama jpm anaamini na kutoa matamko tena kwenye matangazo ya TRA kuwa nchi haiwezi kupata maendeleo bila kukusanya kodi sasa leo kodi imepungua karibu 50% ya makusanyo hayo maendeleo yatatoka wapi. Tuache unafiki. Kwanza umewahi kwenda bandarini siku za karibuni au unaleta pumba zako humu?
Mapovu yanakutoka ya nini ndugu yangu. Humu kila mtu anatoa mawazo yake. Kama hukubaliani nayo jibu kistaarabu. Kwani nchi lazima itegemee mapato toka bandarini tu ndio maendeleo yapatikane? Ina maana nchi ambazo hazina bandari kamwe hazitakuwa na maendeleo?

Na wewe acha umbulula! Hahahaaaaa!
 
anajaribu kutufanya sisi mambulula kama alivyojaribu kamishna mkuu wa TRA aliyesema VAT ni kodi inapolipwa na mfanyabiashara badala ya mlaji matokeo yake wakakimbia kipima joto ITV
Ha ha ha ha ha
 
Bravo Dk.Mpango, mimi nilikuwa nashangaa hawa watu kwa nini wana andaa vipindi vya malumbano kwenye TV wanaeleza uzushi mwingi wenye lengo la kutisha Serikali wanadai bidhaa/mizigo inapitishwa Durban kwa kuogopa ushuru - msikilizaji ambaye yuko makini unaona wazi wazi kwamba kuna usanii fulani unaendelea katika utayarishaji na urushwaji wa vipindi hivi vinavyo husu utozaji kodi ya mizigo bandarini.
 
Ukweli wafanyabiashara hawapendi kulipa kodi, kama wameshindwa kufanya biashara hapa tanzania wapo huru kuondoka na kwenda kufunya nchi nyingine ambako watafanya ufisadi wao wa kutokulipa kodi.

Hakuna Taifa linalo weza kuvumilia wakwepa kodi - hayo yalikuwa yanafanyika hapa Tanzania tu. Baada ya JPJM kuwabana wanaishia kulalama tu na kutoa visingizio chungu nzima.
 


Hali hii imepelekea uongozi wa mamlaka ya bandari kufuta bandari kavu hii ni baada ya wafanya biashara kuikimbia.
Mamlaka ya Bandari nchini TPA imesema inakabiliwa na upungufu wa mizigo ambapo sasa kwa siku inahudumia magari 1500 tu tofauti na uwezo wake wa kuhudumia magari 3500 kwa siku yatokayo nje ya nchi na kuwa kutokana na hali hiyo hawawezi kupeleka magari kuhifadhiwa bandari kavu kwani hata yenyewe haina mzigo wa kutosha.

Mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo Deusdedit Kakoko amesema hayo baada ya kumalizika kikao kilichoitwa cha ndani kati yake na baadhi ya wahariri wa vyombo vya habari nchini kilicholenga kujua hali halisi ya bandari ilivyo na mipango yake ya kuiboresha.

Aidha mkurugenzi mkuu huyo wa mamlaka ya Bandari amesema kulikuwepo na udanganyifu katika utoaji wa mizigo bandarini kwa baadhi ya mawakala wa forodha ambao mzigo wa kupeleka nje ya nchi ulikuwa ukiuzwa hapa nchini kitu ambacho kimekanushwa vikali na chama cha mawakala wa forodha.


Awali katibu wa jukwaa la wahariri Neville Meena amesema walifika bandarini hapo na kufanya kikao cha ndani na uongozi wa bandari hiyo baada ya kuwepo alichokiita mtikisiko katika utoaji wa huduma katika mamlaka ya bandari nchini.

Chanzo itv
 
Back
Top Bottom