hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne. katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango. milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.
Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.
Bangusule hakusema hawa wabunge ni vilaza. Alichosema ni kuwa Mwalimu akifufuka atawaita watu wa Same ( yeye mwenyewe akiwemo) kuwa vilaza wa Kilimanjaro. Kuuita uongozi wa wabunge waliopo mbovu ni haki yake kama mpiga kura. Mimi sioni alipotukana.
Re: Dr.Mathayo na Ana Kilango: Same "Wachina" wa Tanzania mpaka "VILAZA" wa Kilimanja
Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga, tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.
Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane! Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.
1. Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule.
2. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga,
3. tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji.
4. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu.
5. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.
6. Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane!
7. Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga.
8. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.
1. hali ya maendeleo katika wilaya ya Same imedorora tangu Dr.Mathayo na Anna Kilango wachaguliwe kuwa wabunge wa same magharibi na same mashariki.
2. hali ya ELIMU ni mbaya sana. wilaya ya same imeshika mkia katika matokeo ya mtihani wa darasa la saba na ule wa kidato cha nne.
3. katika suala la KILIMO ule mradi maarufu wa kilimo cha umwagiliaji Ndungu una hali mbaya sana. kuna maradhi ya mpunga yameingia na wakulima hawana msaada wowote toka kwa mbunge wao Anna Kilango.
4. milimani upande wa Dr.Mathayo ukataji MITI na uharibifu wa MISITU ambayo ni vyanzo vya maji umezidi kuongeza. BARABARA ya mkomazi-bendera-ndungu-gonja-kisiwani-same bado ni kero kubwa kwa wananchi.
5. Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere aliwahi kuisifu wilaya yetu na kutuita "Wachina" wa Tanzania.
6. nina hakika akifufuka leo na kushuhudia uongozi mbovu wa Dr.Mathayo na Anna Kilango, akaona na matokeo ya mitihani ya watoto wetu atageuza kauli yake na kutuita "VILAZA" WA KILIMANJARO.
Quote; Zero
Kitu kimoja ambacho nimejifunza hapa JF ni kwamba kuna makundi mawili makuu ya waandishi. Kuna wachangiaji wa mada (positively) na washabiki wa mada. Kundi la kwanza, yaani wachangiaji wa mada wanaelewa umuhimu wa kuelimishana na wanaamini kabisa maoni na mchango wao unaleta impact fulani katika jamii. Kundi la pili, yaani kundi la washabiki, wanaamini kabisa kwamba hiki ni kijiwe cha wahuni tu waliokosa kazi na wanakuja kupoteza muda wao. Kundi hili linaweza kuamua kumshabulia mtoa mada negatively tu, hata kama wao wenyewe hawana ushahidi wa kutosha.
Nimesema haya baada ya kupitia posts zote zilizochangia hii thread. Kuna waliomponda Bangusule bila wao kutoa ushahidi wowote. Kuna waliomponda na kutoa ushahidi wao (kama alivyofanya FMES). Na kuna wale pia walioshabikia tu positively bila kuwa na vigezo. Labda ningependa kusema tu kwamba, kama huna ushahidi na yale unayotaka kuchangia, ni bora tu ukatoa maoni ambayo hayataathiri mtiririko wa mada. Bangusule katoa ushahidi wa matokeo ya kidato cha nne kama kielelezo kwamba wilaya ya Same inafanya vibaya katika masomo. Hili bado mnalipinga? Website ya matokeo ipo na mnaweza kwenda kuangalia. FMES katoa hoja kuhusu uchimbwaji wa visima. Hili hatuna ushahidi nalo, lakini FMES anaweza kuweka ushahidi wake.
1. Mimi ninachoona hapa ni ushabiki mkubwa unaofanywa na FMES bila kujibu tuhuma halisi zilizotolewa na Bangusule.
2. Bangusule ametoa tuhuma kadhaa kubwa. Moja ni kuhusu wilaya ya Same kufanya vibaya kielimu, pili ni suala la ugonjwa uliokumba zao la mpunga,
3. tatu ni ubovu wa barabara, na nne ni ufyekaji wa misitu ambao umesababisha kuharibiwa kwa vyanzo vya maji.
4. FMES anakuja na hoja kwamba mbunge Anne Kilango amechimba visima 30 na kutoa msaada wa baisikeli 20 kwa walemavu.
5. Huu ni upotoshaji mkubwa wa mada na hakuna jibu liliotolewa kuhusu tuhuma alizotoa Bangusule.
6. Mkuu FMES, tuambie katika tuhuma nne alizotoa Bangusule, mbunge wako Anne Kilango amefanya nini katika kuzitatua? Visima vya maji siamini kama vinatumika kumwagilia mpunga. That is insane!
7. Taumbie visima vyako 30 vinahusiana vipi na ugonjwa uliokumba zao la mpunga.
8. Tuambie visima vinahusiana vipi na wanafunzi kufanya vibaya katika mitihani yao. Tuambie visima vinahusiana vipi na ufyekwaji wa misitu na uharibifu wa vyanzo vya maji.
By Guardian and PST Reporters, IPP Media
Fri, Aug 05, 2005
A number of senior cabinet ministers in the outgoing President Benjamin Mkapas government and party stalwarts face the prospect early exit as Chama Cha Mapinduzis preferential polling entered its final stages yesterday.
Some of the early results showed that Minister for Energy and Minerals Daniel Yona was one of the early casualties having been trounced resoundingly by nominated MP and wife of CCM national vice-chairman, Anne Kilango-Malecela, who polled 286 votes against Yonas 60.
Primary School Renovation and Support
All primary schools in this part of rural Tanzania were built by the local community with little or no money available for the completion of the buildings or for any maintenance. Consequently primary schools frequently have breeze block walls with holes left for the windows and doors, an earth floor and a corrugated iron roof.
Renovation work typically includes:
laying concrete floors
replacing and repairing corrugated iron roofs
putting in ceilings, windows and doors
repairing cracks, plastering and whitewashing walls
making tables, benches and blackboards
The result is that the schools become bright, comfortable places where learning is stimulated. There are medical benefits too, as jiggas - little fleas that live in earth floors - are no longer able to enter the children's skin and debilitate them.
The charity has now renovated the following primary schools: Mauo, Mshiri, Ashira, Samanga, Palangeny, Lyasomboro, Mbahe, Matala, Kochakindo and Kilaremo. Help with building has also been given to Lyakirimu, Nganyeni, Masia Marangu, Masia Mamba, Mbahe, Marimeni, Mseroe, Maande, Kotela and Nkweseko schools.
"People's participation is the focal point in PAMOJA's development practices."
PAMOJA facilitates the collaboration between local government, civil society and the private sector. The organisation does this by transforming mindsets and attitudes, based on the right of equal access to resources. It promotes the practice of Joint Action and participatory local governance often using international experiences in this area.
EDUCATIONAL ACTIVITIES
Many different activities have been funded and initiated by PAMOJA in the education sector. The establishment of the District Education Board in Same District was a first in Tanzania and has won much praise throughout the Region and country. PAMOJA's approach of Joint Action is an especially useful tool in realising the building of classrooms and has achieved remarkable success. The School Milk Project complemented the earlier dairy support project, while the support of the Mkombozi street children project links with the knowledge acquired in the District Education Boards.
The quality of education in Kilimanjaro Region has been greatly affected by the decline of coffee production due to low prices on the world market. Many parents can no longer afford school fees and children have been leaving school early in order to perform economic activities to sustain the family.
Habari za Kitaifa Habari zaidi! Slaa, Zitto, Anna Kilango wawika
Stella Nyemenohi
Daily News; Wednesday,March 19, 2008 @00:03
WABUNGE maarufu Dk. Wilbrod Slaa, Zitto Kabwe na Anne Kilango-Malecela, ni miongoni mwa waliowika jana baada ya kuchaguliwa kuwa wenyeviti wa kamati mbalimbali za Bunge.
Kamati hizo za Bunge zilifanya uchaguzi huo kwa mujibu wa kanuni, kwamba kamati hizo huundwa upya inapomalizika nusu ya mikutano ya Bunge. Mikutano 20 hufanyika katika kipindi chote cha Bunge. Katika kipindi kilichopita, zilikuwapo kamati 14 tofauti na sasa ziko 17.
Wakati Dk. Slaa ambaye ni Mbunge wa Karatu (Chadema), akipita bila kupingwa kuongoza Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa, Zitto ambaye pia ni Mbunge wa Chadema kutoka Kigoma Kaskazini, alishinda uenyekiti wa kamati mpya ya Hesabu za Mashirika ya Umma.
Anne Kilango-Malecela ambaye kwa siku za karibuni jina lake limekuwa masikioni mwa wananchi wengi baada ya mchango wake katika sakata la kampuni ya umeme ya Richmond, sasa ataongoza moja ya kamati yenye nguvu bungeni, Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge.
Mbunge huyo alimshinda Mbunge wa Bahi (CCM), William Kusila, kwa kupata kura nane dhidi ya tatu za mpinzani wake huyo. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana baada ya kuchaguliwa, Dk. Slaa alisema kuchaguliwa kwa wapinzani kuongoza kamati, hakumaanishi kuwaziba midomo.
Jamaa anaona Same tu ndio wamefeli aulize Lindi,Mtwara mbona wanafeli miaka yote na hakuna anayeshtuka
Wasomi Nchini Wachambua Sababu za Kushuka Kwa elimu Ya Darasa La Saba.
Na Kizitto Noya
WASOMI wamechambua matokeo ya mtihani wa darasa la saba nchini na kueleza kuwa masomo ya ziada (tuition) na uwezo mdogo wa walimu katika masomo ya hisabati na kiingereza, vimechangia kushusha kiwango cha kufaulu wanafunzi. Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti jana, wahadhili wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, idara za Hisabati na Kiingereza walisema kushuka kwa kiwango cha kufaulu wanafunzi katika masomo hayo pia kumechangiwa na ukosefu wa motisha na maslahi kwa walimu.
Mhadhiri wa somo la hisabati chuoni hapo, Rashid Mohamed alisema ingawa hesabu ni tatizo la kidunia, walimu wake nchini hawana motisha hivyo hupoteza mori wa kazi ya kufundisha. "Somo la hesabu (hisabati) halina motisha kuanzia kwa mwalimu hadi mwanafunzi mwenyewe na serikali hailikumbuki kwa namna yoyote ile na matokeo yake wanafunzi wanalikimbia," alisema Mohamed. Alisema serikali inapaswa kutambua kuwa somo la hisabati ni msingi wa masomo mengine yote na ikaanza kuliwekea bajeti maalum kwa ajili ya kuwapa motisha walimu na wanafunzi wanaofanya vizuri darasani mabadiliko makubwa yatatokea.
Alibainisha kwa hali ilivyo sasa wanafunzi wameshindwa kufanya vizuri katika somo la hisabati kwa kuwa hawana mori ya kulipenda kwani halina matumizi ya moja kwa moja katika maisha ya kila siku. "Somo hili linahitaji moyo wa dhati wa mwalimu na mwanafunzi kuanzia ngazi ya shule ya awali hadi chuo kikuu na moyo huo utajengeka endapo kuna mazingira mazuri ya kazi na maslahi kwa walimu," alisema. Mahadhiri mwingine ambaye hakutaka kutajwa jina lake gazetini aliulaumu mfumo mzima wa elimu nchini kuwa umechangia kushuka kwa kiwango cha kufaulu wa wanafunzi katika masomo ya Hisabati na Kiingereza.
Alisema Wizara ya Elimu imeshindwa kuwaandaa walimu na kuwatengenezea mazingira mazuri ya kazi kwa kuwaboreshea maslahi, matokeo yake walimu wanafanya kazi katika mazingira magumu na kushindwa kuwajengea wanafunzi wao mori wa kulipenda somo hilo. "Tatizo haliko chini, linaanzia juu serikalini. Kama mwalimu hujui hesabu zinamsaidiaje maishani utawezaje kumfanya mwanafunzi azipende?" alihoji. Alisema kutokana na hali hiyo wataalam wa hisabati wanapungua kadiri siku zinavyosonga wengi wakilazimika kukimbia kazi ya ualimu kutokana na kazi hiyo kutokuwa na maslahi mazuri.
"Hali itabadilika baada ya serikali kuanza kuwajali walimu na kuwathamini kwa maslahi mazuri vinginevyo somo la hesabu litaendelea kuwa tatizo la kitaifa," alisema Mhadhiri mwingine wa Hisabati na Kompyuta, Shaban Nyimvua alitaja masomo ya ziada maarufu kama tuisheni kuwa moja ya sababu zinazowafanya wanafunzi wa mijini kushindwa zaidi katika somo la hisabati kuliko wanafunzi wa vijijini. Alisema tuisheni ni hatari kwa wanafunzi kwani walimu wengi wanafundisha kama biashara kwa lengo la kuongeza kipato na katika kukabiliana na ushindani wa kibiashara, hiyo walimu wanafundisha mbinu za kujibu maswali ya mtihani badala ya misingi ya somo.
"Tuisheni imechangia kwani wanafunzi wanakaririshwa mambo badala ya kufundishwa. Serikali inapaswa kupiga marufuku tuisheni na kuboresha maslahi ya mwalimu ili kumfanya akidhi mahitaji yake kwa mshahara kusudi afundishe vizuri," alisema Nyimvua. Alisema vitendo vya walimu kuuza pipi madarasani na kujipangia muda wa kufundisha masomo ya tuisheni vinatokana na ukosefu wa maslahi ya kutosha kukidhi mahitaji yao. "Siri ya wanafunzi wa vijijini kufanya vizuri zaidi katika hesabu kuliko wanafunzi wa mijini ni tuisheni. Tuisheni inawaharibu watoto kwani wanakaririshwa mambo badala ya kufundishwa misingi yake," alibainisha.
Nyimvua aliishauri serikali kuboresha maslahi kwa walimu ili kuwavuta wenye uwezo kufanya kazi katika shule za msingi na kuinua taaluma badala ya kuwasahau na kuwafanya walimu wenye uwezo kukimbia kufanya kazi katika shule hizo. Profesa mmoja wa somo la kiingereza chuoni hapo ambaye hakutaka kutaja jina lake gazetini alisema kuwa tofauti na zamani ambapo ualimu ulikuwa wito, taaluma hiyo sasa ni ajira inayotafutwa kwa udi na uvumba na watu wasiokuwa na uwezo kuifanya. Alisema matokeo mabaya ya somo la Kiingereza yametokana na mfumo mbovu wa upatikanaji wa walimu wa kulifundisha ambapo kila mwalimu sasa anafundisha somo hilo bila utalaam nalo.
"Inawezekanaje mtu asiyejua kiingereza akamfundishe mwenzake?" alihoji Profesa huyo na kuongeza "Watoto hawafundishwi Kiingereza ila wanadokezwa na kufaulu hivyo kwao ni ndoto". Profesa huyo alitaja mambo yanayomfanya mwanafunzi afanye vizuri katika mitahani kuwa ni umakini wake katika kujifunza, uwezo wa mwalimu anayemfundisha, upatikanaji wa vitendea kazi na mazingira ya kujifunza. Naye Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima nchini, Lambetha Mahai alisema ongezeko la masomo ya kufanyia mtihani mwaka uliopita ni moja ya sababu za wanafunzi hao kufanya vibaya katika mtihani uliopita. Alisema ni jambo la kawaida kwa mwanafunzi kufanya vibaya katika mtihani wake hasa baada ya kubadilishiwa mtaala na kueleza kuwa anatumaini kuwa hali hiyo itaboreka baada ya wanafunzi hao kuzoea.
"Zamani wanafunzi walizoea kufanya mitihani mitatu lakini kwa mara ya kwanza mwaka huu wamefanya mitihani mitano, sasa inategemea mwanafunzi ameelekeza nguvu wapi," alisema Mahai. Juzi Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta alitangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba yaliyoonyesha kuwa kiwango cha ufaulu mwaka huu kimeshuka kwa asilimia 16.3 ikilinganishwa na mwaka jana. Waziri Sitta alisema kufaulu katika masomo ya hisabati na kingereza si mzuri ikilinganishwa na masomo mengine kwani kiswahili watahiniwa walifaulu kwa asilimia 80.23, sayansi 66.66, maarifa kwa asilimia 56.39, kingereza kwa asilimia 31.31 na hisabati kwa asilimia 17.42.
Alisema kati ya wanafunzi 301 wenye ulemavu waliofanya mtihani huo mwaka huu, wanafunzi 212 wakiwemo wasichana 103 na wavulana 109 wamefaulu mtihani huo. Katika matokeo hayo, mikoa ambayo imeshika nafasi 10 za mwanzo kwa kuwa na idadi kubwa ya wanafunzi waliofaulu ni Kagera asilimia 73, Dar es Salaam (71), Iringa (70), Manyara (66), Tanga (64), Mbeya (63), Arusha (61), Pwani (58), Morogoro (56), Tabora (56) na Mwanza (52). Mikoa ambayo imetoa wanafunzi wachache waliofaulu ni Shinyanga (34), Dodoma (41), Mtwara (41), Kigoma (42), Ruvuma (44), Lindi (47), Mara (48), Kilimanjaro (48).
Hata hivyo, mikoa ambayo imefaulisha wanafunzi wengi ni Dar es Salaam (40,323), Mwanza (36,681), Iringa (29,858), Mbeya (29,723), Tanga (25,795), Kagera (24,172), Morogoro (21,442). na ambayo wanmefaulu wachache zaidi ni Lindi (8000), Mtwara (9,775) na Kigoma (13,473). Wanafunzi waliofanya mtihani mwaka huu walikuwa 773,550 sawa na asilimia 97.41 waliokuwa wameandikishwa na kwamba kati yao watahiniwa 419,198 sawa na asilimia 54.18 wamefaulu.
Alisema asilimia 90.26 ya wanafunzi 419,198 waliofaulu mtihani wa darasa la saba mwaka huu, wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwakani katika shule za sekondari za serikali. Naye Andrew Msechu,anaripoti kuwa watalaam wa masuala ya elimu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wameelezea matokeo ya mtihani wa Darasa la saba kama changamoto ya kuweza kuangalia nini cha kufanya baada ya kuonekana kushuka kwa kiwango cha kufaulu mwaka huu.
Maoni hayo yanafuatia matokeo ya darasa la saba yaliyotangazwa juzi na Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi akielezea kushuka kwa kiwango cha kufaulu kutoka asilimia 70 mwaka 2006 hadi asilimia 54 mwaka huu, pia wanafunzi kutofanya vizuri katika masomo ya hisabati na kiingereza. Wakizungumza na Mwananchi, mtaalamu wa masuala ya utafiti kuhusu elimu, Profesa Issa Omari na Mkuu wa Idara ya ufundishaji na Mitaala Profesa Peter Chonjo walisema kushuka kwa kiwango cha kufaulu kwa mwaka huu si jambo la kushangaza kutokana na mabadiliko yaliyotokea siku za nyuma.
Walisema ni mapema mno kutarajia matokeo mazuri sana ya MMEM kwa kuwa katika miaka ya hivi karibuni hasa kuanzia mwaka 2003 kumekuwa na mabadiliko yasiyo ya kawaida katika kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba, suala ambalo ndilo linaloshangaza. Ongezeko la ghafla la kiwango cha kufaulu kwa shule za msingi kwa miaka ya hivi karibuni ndiyo suala la kushangaza, kwa mfano kiwango hicho kiliongezeka kwa ghafla mno kwa namna isiyoelezeka kutoka asilimia 27 mwaka 2002 hadi kufikia asilimia 70 mwaka 2006, ongezeko ambalo si la kawaida na halielezeki," alsiema.
Aliainisha kuwa ongezeko hilo la viwango si la kawaida kwa kuwa lilitakiwa kuongezeka taratibu, akitoa mfano wa matokeo ya mwaka 1998 ambao asilimia 21 ya wanafunzi walifaulu. Mwaka 1999 asilimia 19, mwaka 2000 asilimia 22, mwaka 2001 asilimia 29, mwaka 2002 asilimia 27 na kupanda kwa kasi mwaka 2003 hadi kufikia asilimia 40, asilimia 49 mwaka 2004, asilimia 62 mwaka 2005 na asilimia 70 mwaka 2006.
Wataalamu hao kwa pamoja walisema hali hiyo inaonyesha kuwa kuna hali isiyo ya kawaida katika ongezeko hilo la ghafla na kuwataka wadau wanaosimamia masuala ya elimu kufanya utaratibu wa kutafuta chanzo cha tatizo lililopo. Hata hivyo, wakizungumzia suala la kushuka kwa kiwango cha kufaulu kwa wanafunzi katika msomo ya Hisabati na Kiingereza walisema moja ya sababu ni ufundishwaji usiofaa wa wanafunzi kutokana na kuwa na waalimu wasiojua vyema masomo hayo. "Suala hapa ni kuangalia, mitihani inatungwa na watu wale wale, mtaala unaotumika ni ule ule, mtindo unaotakiwa kufundishia ni ule ule, lakini hapa tatizo kubwa linaweza kuwa ni kuwa na walimu wasioweza vyema masomo haya, hasa waalimu hawa walioingizwa kwa mkupuo wa MMEM,
Walisema inaonekana waalimu wengi wanaofundisha masomo hayo hawayajui hivyo ni bora wizara ikiangalia namna ya kuweka utaratibu wa kuwa na waalimu wa diploma (stashahada) kwa ajili ya kufundisha masomo katika shule za Msingi," alisema Profesa Chonjo. Wakati huo huo, Patricia Kimelemeta na Muhibu Said wanaripoti kuwa ongezeko la wanafunzi waliomaliza darasa la saba na kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka huu katika Mkoa wa Dar es Salaam limeongezeka na kufikia asilimia 16 ukilinganisha na mwaka jana.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Afisa Elimu wa Mkoa huu Bernad Makali, jumla ya wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza ni 40,323 kati yao wasichana ni 17,773 na wavulana ni 22,550. Taarifa hiyo ilisema kuwa jumla ya watahiniwa 56,825 waliofanya mtihani huo,wavulana walikuwa 27,951 na wasichana 28,874 ambayo ni sawa na asilimia 97 ya wanafunzi wote waliosajiliwa, ambao walikuwa 58,326. Taarifa hiyo ilisema kuwa wanafunzi 1,501 hawakufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za utoro,ugonjwa,vifo,mimba na wengine kuhamia mikoa mingine. Ilisema kuwa idadi ya wanafunzi ambao walikuwa watoro wa shuleni ni 1,163,waliokuwa wagonjwa 29, waliofariki 25, waliopata mamba 15 na wengine ambao waliamishwa katika mikoa mingine ni 269.
Ilisema kuwa katika uchaguzi jumla ya wanafunzi 68, wakiwemo wavulana 34 na wasichana 34 walichaguliwa kujiunga na shule za watoto wenye ufaulu mzuri (vipaji maalum). Taarifa hiyo ilisema kuwa wanafunzi 74, wakiwemo wavulana 63 na wasichana 11 wamechaguliwa kujiunga na shule za bweni ufundi. Ilisema kuwa, wanafunzi 76, wakiwemo wavulana 42 na wasichana 34 wamechaguliwa kujiunga na shule za bweni kawaida. Taarifa hiyo ilisema kuwa jumla ya wanafunzi 2,200 wakiwemo wavulana 820 na wasichana 1,380 watajiunga nashule za kutwa za Serikali kuu zilizoko katika mkoa wa Dar es Salaam.
Ilisema kuwa wanafunzi 25,274 wakiwemo wavulana 12,846 na wasichana 12,428 wamechaguliwa kujiunga na shule za wananchi 92 ambazo zimesajiliwa kisheria. Taarifa hiyo ilisema kuwa idadi ya wanafunzi 27,692 wa kidato cha kwanza 2008 waliochaguliwa katika awamu ya kwanza ni kubwa ikilinganishwa na kwana 2007, ambapo jumla ya wanafunzi 25,457 walichaguliwa awamu ya kwanza na ya pili, lakini mpaka sasa kuna ongezeko la wanafunzi 2,235 ambalo ni sawa na asilimia 8. Mkoa unatarajia kujenga jumla ya shule za sekondari mpya 22 ambazo zitachukua jumla ya wanafunzi 6,320 katika awamu ya pili ifikapo Aprili 2008.
Source: Mwananchi
Anayelalamika anaonekana ndio mjinga na wanaokaa kimya ndio wanajua hali halisi.
No wonder tuna wabunge vilaza bungeni na ukifika uchaguzi bado wanashinda tu. Halafu tunaanza kupiga kelele kwanini hatuendelei?
The quality of education in Kilimanjaro Region has been greatly affected by the decline of coffee production due to low prices on the world market. Many parents can no longer afford school fees and children have been leaving school early in order to perform economic activities to sustain the family.
Mtanzania
.....umeeleza vizuri sana ni kw anji agani kiongozi anahitajika kwa jamii.....na anategemewa vipi.......
........bangusule kaleta concern....which is ok as a concern citizen....na concern yake.............does apply sehemu nyingi tu nchini.........
.....now.......check hiyo highlight ya kwanza in red...........tell me how do one arrive to such a conclusion.......!!!
....sidhani kama itakuwa ni kumtendea haki Mh Mbunge kumsema Mbunge eti kuna maradhi ya mpunga na yeye hakuwa na msaada wowote kwa wakulima.........how do one substantiate this claim...........kwa ambao tumekulia kule kajunjumele....tunatakiwa tulielewe hili jambo better than anybody........nafikiri unanisoma............
........Mtu unaweza kuwa na hoja nzuri sana........lakini ukishindwa namna ya kui-present.............mtu anaweza kuku-ignore.....ukashangaa........
......bangusule ana valid concerns......lakini zinaelea......na ndio maana akina Ogah.....wame-comment walivyo -comment..........
.......bangusule should now tell us amelifanyia nini au ana mpango wa kulifanyia nini jimbo lake.........
Kuna mtu hapa kazungumzia suala la wabunge kuwa na ToRs na Performance indicators........wow it might be good idea to start with.....however, we should be able to see and say Mh Mbunge did 1, 2, 3..........to the satisfaction of who......this is debatable.......
Originally Posted by Kaizer
Hivi kazi ya wabunge ni KULETA maendeleo?
Kumbe ni nini?
Swali la Kaizer ni la msingi.
Dhana hii ya kumwona Mbunge ndiye anayewajibika kwa maendeleo ya endeo lake ndiyo inayoturudisha nyuma kimaendeleo. Dhani hii inawatutumua Wabunge kujiona ndiyo wenyewe, wanayoyasema lazima yatekelezwe nk. Kibaya zaidi, ndiyo dhana inayolipeleka Taifa kwenye siasa zaidi kuliko utendaji.
Kimsingi, Mbunge ni mwananchi, ni mwakilishi wa wananchi katika maamuzi na kutunga sheria. Mbunge si Serikali, hana bajeti ya miradi ya maendeleo, hapokei kodi. Serikali ndiyo inayopokea kodi, ndiyo yenye bajeti. Ndiyo inayopaswa kutekeleza miradi ya maendeleo. Mbunge ni sawa na diwani katika kata na Halmashauri yake.
Kwa kuwa inadaiwa kuwa kodi zetu, pamoja na mapato mengine ya Serikali hayatoshelezi mahitaji ndipo suala la wananchi kuchangia ili kutekeleza miradi linakuja. Inapotokea suala la kushirikisha wananchi ndipo diwani na Mbunge wanapohitajika sana ili kupitisha maamuzi na kuwashawishi wananchi.
Msimamo wangu:
Mimi naomba hivi; tujenge tabia ya kuimarisha utendaji na watendaji. Tujenge tabia ya kuwafanya watendaji wawe wawajibikaji. Kazi ya diwani na wabunge iwe ni kusimamia Serikali kuu na serikali za Mitaa. Wanaopaswa kuwajibia wawe ni Serikali yaani watendaji.
Hofu yangu:
Tunapojenga mfumo au mtazamo 'Mbunge ndiye mleta maendeleo' tunakuwa tumemwinua sana kiasi cha kujiona yupo juu ya Serikali hali inayoweza kuathiri utekelezaji wa mipango ya maendeleo hasa ile ya muda mrefu. Mbunge atapenda mipango ya muda mfupi ili kuonyesha alichokifanya katika muda mfupi. Atafanya hivyo kwasababu anataka kura za ndiyo.
Hofu yangu ni kujenga Taifa la wanasiasa. Wanasiasa hawajengi nchi, wanaojenga nchi ni watendaji. Tunapokuwa na Taifa lililojaa wanasiasa, kitakachopewa kipaumbele ni michezo ya kisiasa badala ya kutafuta teknolojia na kutekeleza masuala ya maendeleo.
Kwa mfano Mkuu bangusilo anatoa hoja kuwa Mama Anne Malecela (MB) hafai kuwa Mbunge kwa kuwa kidato cha nne wamefeli mitihani. This is redicolous! Hapa Mbunge kama mwananchi, alaumiwe katika jambo ambalo hakulitekeleza.
Hoja ambayo ingeleta msingi, ilitakiwa kuwa, kwa mfano: walimu katika shule hizo hawapo/hawatoshi na katika bajeti kulikuwa na code ya kuajiri walimu, Serikali haikuajiri na Mbunge hajaihoji Serikali. au kulikuwa na tatizo la vitabu shuleni, serikali ilipendekeza vununuliwe lakini madiwani/Mbunge walikataa kupitisha bajeti ya kununua vitabu. nk,
Hoja za namna hii, ndiyo zenye maana yaani zinawajibisha wataalam/watendaji. Mbunge au diwani anawajibika kwa kuto wasimamia watendaji au kukwamisha mipango mizuri ya Serikali.