Mabibi na mabwana heshima kwenu na moja kwa moja kwenye mada.
Kiswahili lugha ya mama zetu iliyo shehenishwa na semi mbalimbali, ama kwa hakika ni kitamu kweli kweli.
Hujafa hujaumbika, utavuna ulichopanda, usitukane wakunga, usiwatukane mamba, nk nk ni baadhi ya semi hizo ambazo kwa hakika zinamhusu sana leo, nguli au jembe letu bwana jiwe, kama anavyopenda kujiita yeye mwenyewe.
Mkuu wetu huyu kwa kweli katenda mengi katika kipindi chake. Kwa hulka za kibinadamu katenda yote yaliyo mema na yaliyo fyongo. Yeye kama binadamu yapo mema mengi kufanya na pia yaliyo fyongo kwani yeye siyo malaika wala si Yesu Kristo (cc. Kange).
Yote hayo binadamu sisi tuliyashudia kwa namna mbalimbali. Mwenyezi Mungu naye akiyashudia kwa namna yake.
Katika kipindi chake kuna walioshuhudia madege yakinunuliwa, ma flyover, madaraja kama ya busisi yakijengwa. Madaraja ya salenda na barabara za kuizunguka Dodoma yakijengwa kupendezesha majiji. Ma SGR, viwanja vya ndege kama vya Chatto, Msalato, viwanda nk vikijengwa.
Mengine yakiwa hata kupendezesha majiji tu! Fursa iliyo je? Ama kweli staajabu ya Firauni.
Yapo maeneo yali sahaulika hapa hapa nchini na kuwa kama si sehemu ya nchi hii:
Ziara ya Kagera, Magufuli usiende pekee tu Wasaidizi wako wanakokupangia kwenda
Hali ya mbaya mno ya barabara Nyakanazi Rusumo vipaumbele vyetu ni nini?
Barabara ya Rusahunga Rusumo mtaji kwa wagombea
Kupo kwingine nako, wengine hata majoto ya mawe waliyaonja kama wafanyavyo mijusi. Kuna waliokumbwa na matetemeko, waliookotwa kwenye viroba, waliopotea, walionusurika mithili ya ngamia kupita kwenye tundu la sindano kama kina mh. Lissu, kuna waliotekwa, nk nk.
Kwa hakika kila mtu au watu wa sehemu fulani wana yao ya kumwelezea nguli huyu kwa namna zao za kipekee. Hii ikiwa ni mithili ya wale vipofu saba waliopata fursa adimu ya kumpapasa tembo na kumwelezea ki vyao vyao.
Kipofu aliyepapasa mkia akidhani tembo ni kama ufagio wa chelewa chelewa, aliyepapasa pembe akidhani tembo ni kama mchi wa kutwangia, aliyepapasa sikio akidhani tembo ni kama blanketi tu nk nk.
Waswahili wanasema chema chajiuza na *kile kingine* chajitembeza. Wengine wakisema "mwana wacha kupiga mayowe waache waone wenyewe" au "penye ukweli uongo hujitenga."
Barabara ipi alijenga mzee Kikwette, ipi Mkapa (rip), ipi jiwe zote tunazijua kama naye anavyozijua. Hii ni siri iliyo wazi. Kila mtu na ashinde mechi zake na si busara kusafiria nyota za wengine kama zako pasipo na kuweka yote wazi. Ndiyo ustaarabu wa kisomi huo.
Itoshe kusema ng'ombe hanenepi siku ya mnada!
Kwa aliyoyafanya mzee baba, yote kabisa "maji ga nyanja" tunayajua vyema na kwa hakika, ni sawia kusema "huko atavuna alichopanda." Ikizingatiwa historia huwa haiandikwi upya.
"Tusimlaumi dobi kaniki ni rangi yake." Huu ni ukweli mchungu.
Alipopanda bangi atavuna bangi kama alivyoipanda yeye mwenyewe kwa mikono yake. Pia atavuna maharage kote alikopanda maharage yeye mwenyewe. Kwenye haya hayupo wa kumlaumu wala wa kumsifu bali mhusika ni yeye mwenyewe na nafasi ya kufanya vinginevyo alikuwa nayo kama yote.
Katika misahafu kwa kiswahili inasema "mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe." Mwisho wa kunukuu.
Labda kama analo jipya la kutufanyia au kutupeleka mzee baba, basi ilikuwa vyema tukakutana kwenye midahalo ili kwa hayo tusiyoyajua sote tukaswalishana.
Yaliyopita si ndwele kila siku kama watanzania wenye subira kukubaliana kuganga yajayo ni jadi yetu wala si muhani.
Ninawasilisha.
Kiswahili lugha ya mama zetu iliyo shehenishwa na semi mbalimbali, ama kwa hakika ni kitamu kweli kweli.
Hujafa hujaumbika, utavuna ulichopanda, usitukane wakunga, usiwatukane mamba, nk nk ni baadhi ya semi hizo ambazo kwa hakika zinamhusu sana leo, nguli au jembe letu bwana jiwe, kama anavyopenda kujiita yeye mwenyewe.
Mkuu wetu huyu kwa kweli katenda mengi katika kipindi chake. Kwa hulka za kibinadamu katenda yote yaliyo mema na yaliyo fyongo. Yeye kama binadamu yapo mema mengi kufanya na pia yaliyo fyongo kwani yeye siyo malaika wala si Yesu Kristo (cc. Kange).
Yote hayo binadamu sisi tuliyashudia kwa namna mbalimbali. Mwenyezi Mungu naye akiyashudia kwa namna yake.
Katika kipindi chake kuna walioshuhudia madege yakinunuliwa, ma flyover, madaraja kama ya busisi yakijengwa. Madaraja ya salenda na barabara za kuizunguka Dodoma yakijengwa kupendezesha majiji. Ma SGR, viwanja vya ndege kama vya Chatto, Msalato, viwanda nk vikijengwa.
Mengine yakiwa hata kupendezesha majiji tu! Fursa iliyo je? Ama kweli staajabu ya Firauni.
Yapo maeneo yali sahaulika hapa hapa nchini na kuwa kama si sehemu ya nchi hii:
Ziara ya Kagera, Magufuli usiende pekee tu Wasaidizi wako wanakokupangia kwenda
Hali ya mbaya mno ya barabara Nyakanazi Rusumo vipaumbele vyetu ni nini?
Barabara ya Rusahunga Rusumo mtaji kwa wagombea
Kupo kwingine nako, wengine hata majoto ya mawe waliyaonja kama wafanyavyo mijusi. Kuna waliokumbwa na matetemeko, waliookotwa kwenye viroba, waliopotea, walionusurika mithili ya ngamia kupita kwenye tundu la sindano kama kina mh. Lissu, kuna waliotekwa, nk nk.
Kwa hakika kila mtu au watu wa sehemu fulani wana yao ya kumwelezea nguli huyu kwa namna zao za kipekee. Hii ikiwa ni mithili ya wale vipofu saba waliopata fursa adimu ya kumpapasa tembo na kumwelezea ki vyao vyao.
Kipofu aliyepapasa mkia akidhani tembo ni kama ufagio wa chelewa chelewa, aliyepapasa pembe akidhani tembo ni kama mchi wa kutwangia, aliyepapasa sikio akidhani tembo ni kama blanketi tu nk nk.
Waswahili wanasema chema chajiuza na *kile kingine* chajitembeza. Wengine wakisema "mwana wacha kupiga mayowe waache waone wenyewe" au "penye ukweli uongo hujitenga."
Barabara ipi alijenga mzee Kikwette, ipi Mkapa (rip), ipi jiwe zote tunazijua kama naye anavyozijua. Hii ni siri iliyo wazi. Kila mtu na ashinde mechi zake na si busara kusafiria nyota za wengine kama zako pasipo na kuweka yote wazi. Ndiyo ustaarabu wa kisomi huo.
Itoshe kusema ng'ombe hanenepi siku ya mnada!
Kwa aliyoyafanya mzee baba, yote kabisa "maji ga nyanja" tunayajua vyema na kwa hakika, ni sawia kusema "huko atavuna alichopanda." Ikizingatiwa historia huwa haiandikwi upya.
"Tusimlaumi dobi kaniki ni rangi yake." Huu ni ukweli mchungu.
Alipopanda bangi atavuna bangi kama alivyoipanda yeye mwenyewe kwa mikono yake. Pia atavuna maharage kote alikopanda maharage yeye mwenyewe. Kwenye haya hayupo wa kumlaumu wala wa kumsifu bali mhusika ni yeye mwenyewe na nafasi ya kufanya vinginevyo alikuwa nayo kama yote.
Katika misahafu kwa kiswahili inasema "mwanamke mpumbavu huivunja ndoa yake kwa mikono yake mwenyewe." Mwisho wa kunukuu.
Labda kama analo jipya la kutufanyia au kutupeleka mzee baba, basi ilikuwa vyema tukakutana kwenye midahalo ili kwa hayo tusiyoyajua sote tukaswalishana.
Yaliyopita si ndwele kila siku kama watanzania wenye subira kukubaliana kuganga yajayo ni jadi yetu wala si muhani.
Ninawasilisha.