Dkt. Bashiru Ally, Mjamaa aliyeshindwa kutuonesha ujamaa kwenye Uchaguzi

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,505
51,106
Alianza na kauli, kwa kusema chama chenye dola kushindwa kutetea dola yake ni uzembe!. Alishangaa iweje uwe na dola kisha upoteze dola.

Naam!. Kwenye uchaguzi huu tumeona alichomaanisha!. Bila shaka sote tuliona nini maana ya kutumia dola kubaki na dola, Tulishuhudia Kura kwenye vikapu vya akina mama, nyingine kwenye mabegi. Wapo waliozishika hizo kura na kuzipekeka polisi, polisi wakawajibu kwa mkato tu "Hatushughulikii masuala ya uchaguzi".

Maelfu kwa maelfu ya Mawakala wa vyama shindani wakapigwa zengwe, wakazuiwa kuingia, na wale walioningia wakapigwa zengwe wasipate nakala za matokeo.

Kule Zanzibar watu wakaonekana wanaopiga kura kwa lumbesa, mtu mmoja kura lundo.

Falsafa ya Bashiru Ally Kakurwa mtoto wa Kiislamu huyo aliyepitia madrasa!

Lakini huyu ni mwalimu wa chuo kikuu, msomi mkubwa, kafundisha wanafunzi wengi tu nadharia za demokrasia, ushirikishwaji wa wananchi katika maamuzi ya nchi yao wenyewe. Kafundisha sana masuala ya class struggle, ni role model wa maelfu ya wanafunzi wake wa ndani ya darasa na nje ya darasa! Sijui ametuma ujumbe gani kwa watu ambao walikuwa inspired naye kabla ya kuingia kwenye siasa pale wanapoona amekuwa katibu mkuu wa chama ambacho leo kimenufaika kwa mchakato feki na haramu kabisa wa uchaguzi, uliogubikwa na wizi wa kura wa kutisha katika historia ya nchi hii toka uhuru!

Lakini cha kuchekesha zaidi, Sheikh Bashiru Ally Kakurwa eti ni mjamaa, mfuasi wa Nyerere. Eti naye alikuwa mdau mkubwa wa Kigoda cha mwalimu. Eti naye alikuwa akiimba kama kasuku kuhusu uadilifu na sense ya haki ya mwalimu Nyerere.

Haya hatukuhadithiwa, tumeona kwenye TV mihadhara ya kigoda cha Mwalimu, Tumemuona Bashiru Ally Channel ten akielezea falsafa za haki, uadilifu, demokrasia, uhuru, umoja, n. k lakini hatukujua kuwa miaka michache baadaye, Bashiru huyuhuyu atakuwa ni katibu mkuu wa chama kilichonufaika kwa kuhujumu wananchi kuwaweka madarakani watu wawatakao wao wenyewe kupitia sanduku la kura!

Nikiangalia miaka michache ijayo nini itakuwa Legacy ya Bashiru Ally kwenye utumishi wa CCM, Siioni zaidi ya kushiriki kuwanyima wananchi viongozi na wawakilishi wawatakao watokanao na ridhaa zao wenyewe!. Kiufupi naye ni mshiriki asiyeweza kujivua lawama kwa dhulma hii kubwa waliyotendewa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata kama ngazi ya urais wa Muungano mlikuwa mkiitaka kwa udi na uvumba lakini Bashiru, hivi kweli Hussein ni wa kumshinda Maalim Seif kwa zaidi ya 57%?

Bashiru hivi kweli Tulia ni wa kumshinda Sugu Mbeya?

Hivi kweli Zitto ni wa kushindwa na yule Jamaa pale Kigoma? na mifano ya ya namna hii ni mingi nchi nzima!

Msomi na Mjamaa Bashiru hongera sana kwa kushiriki ipasavyo kuithibiti demokrasia vilivyo!, Maana sasa demokrasia ni kama adui yenu mliyefanikiwa kumdhibiti asifurukute!, But ngoja nikwambie kitu kimoja mko myopic sana kwa hizi moves zenu, kwa sababu ili mfanikiwe katika lengo lenu hilo ovu itabidi muwe wanafiki zaidi, walaghai zaidi, waonevu zaidi, madhulumati zaidi, msiheshimu wananchi zaidi.

Mtafanya hivyo mpaka mtakapokutana na kigingi kutoka kule ambako hamkukudhania kabisa, kisha hapo common sense zitawarudia kuwa ni USELESS KUDHANI KIKUNDI KIDOGO KINA AKILI KULIKO UMMA, maana umma utasimama na nguvu yeyote itakayokema yaani itakayoweka kigingi cha kuzuia dhulma zenu, nguvu ya kuzuia uonevu wenu, nguvu ya kuzuia ulaghai wenu!. Nguvu hiyo Ama inaweza iwe ni nguvu yoyote ya ndani ya nchi au ya nje ya nchi au zote mbili kwa pamoja as long as wananchi wataona hii inasimama nao na inawatetea wataiunga mkono kwa maua, nderemo, vifijo, bashasha, kucheza, kusifu, n. k!.

Mwalimu Bashiru, Nikukumbushe tu kuwa mahali popote pale duniani uchaguzi hovyo na corrupt, huzaa serikali hovyo na corrupt na hutengeneza bunge hovyo na corrupt lisiloogopa wananchi bali wale waliowawezesha kuingia bungeni kwa njia corrupt!. Kamwe haiwezekani kupata maendeleo kwa bunge na serikali ya aina hiyo, maana hiyo si serikali na bunge la watu kwa ajili ya watu, bali ni kundi tu la watu wachche tu wenye "special interests" lenye kumiliki silaha na kwa silaha hizo huwatisha wananchi wasinyanyuke na kudai haki yao ya kuwa na viongozi watokanao na ridhaa yao, lakini ukweli ni kuwa serikali ya hivyo na bunge la hivyo havina legitimacy mbele ya watu hao!

Bashiru Umeshiriki dhambi ya kuwadhulumu haki wananchi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, unajisikiaje, "umewaweza" wapinzani au "umeiweza" nchi?. Kwamba umeacha alama ya heshima au alama ya aibu?

Shame on you!
 
Socialism is a philosophy of failure, and it's adherents like Bashiru are nothing but a caboodle of swindlers, common thieves and charlatans.
Eti wanataka Tanzania ifuate mfumo wa China. China wana miaka zaidi ya 5000 ya kujitawala wale, wana experience ya kufa mtu kwenye mambo ya kuendesha nchi yao!, eti CCM wanataka kujilinganisha nao.
 
Eti wanataka Tanzania ifuate mfumo wa China. China wana miaka zaidi ya 5000 ya kujitawala wale, wana experience ya kufa mtu kwenye mambo ya kuendesha nchi yao!, eti CCM wanataka kujilinganisha nao.
Hata kule nchini Uchina, Ujamaa uko tu kwenye mgawanyo wa rasilimali (distribution of wealth) na siyo kwenye uendeshaji wa masoko (control of market forces): Command Economy nao iliwashinda.
 
Hata yule (mzee kijana kwa sura) kipindi kile ziko timamu hajanywa maji ya rangi ya kijani, alisema.
"Uchaguzi ukiwa huru na wa haki ccm ijiandae kukabidhi ikulu"
Aliamini hivyo na ndiyo ilivyo hata leo ,ila njaaa , njaaa njaaa, ni ya kuisikia tu kwa mwenzio.

Sio kila aokotae chakula ni kichaa, wengine ni tumbo humtuma kufanya matendo kama kichaa .
 
Utawala wowote wa kijamaa huwa ni utawala wa mabavu na kukandamiza haki. Kwa hiyo kama Bashiru kafanya hivyo , yuko sahihi kabisa.
 
Hata kule nchini Uchina, Ujamaa uko tu kwenye mgawanyo wa rasilimali (distribution of wealth) na siyo kwenye uendeshaji wa masoko (control of market forces): Command Economy nao iliwashinda.
Labda unaongelea China ya sayari nyingine na sio China ya Xi Jinping, juzi tu billionaire Jack Ma ametaka ku-flot IPO ya kampuni yake Beijing waweka kibano.
 
Mie Binafsi nimemuelewa Vizuri kabisa Mwalim Wangu na amezidi kunithibitishia kuwa Prof Smith alikuwa sahihi juu ya Bongo Zetu sie watu weusi kama msomi mchambuzi wa Siasa za ujamaa na haki ndio amefanya haya mie msomi wa darasa la Saba B kutoka Msimbazi Mseto ni nani mpaka ni pinge ila Yote ya Yote Afrika ni vibaya kuongea wakati wa kula.
 
Mie Binafsi nimemuelewa Vizuri kabisa Mwalim Wangu na amezidi kunithibitishia kuwa Prof Smith alikuwa sahihi juu Bongo Zetu sie watu weusi kama msomi mchambuzi wa Siasa za ujamaa na haki ndio amefanya haya mie msomi wa darasa la Saba B kutoka Msimbazi Mseto ni nani mpaka ni pinge ila Yote ya Yote Afrika ni vibaya kuongea wakati wa kula.
Africa ina wasomi ambao hawana elimu
 
Africa ina wasomi ambao hawana elimu
Upo sahihi kabisa.
IMG_20201105_040501.jpg
 
Tunashindwa nini kufuata mfumo wa China?
Tofauti ya CCP ya China na CCM ni kuwa CCP wana akili kubwa matumbo kidogo wakati CCM wana matumbo makubwa akili kidogo!, wanafikiri kurudi nyuma badala ya kwenda mbele kutatuletea maendeleo!.

Tulikuwa nchi ya chama kimoja kama China kwa miaka 30 je tulifika wapi? zaidi ya kuwa hohehahe wavaa midabwada ambao kunywa chai ya sukari ilionekana ni anasa.

Tumepata mafanikio makubwa zaidi ya kiuchumi kutoka mwaka 1995 mpaka leo chini ya mfumo wa vyama vingi kuliko kuanzia mwaka 1994 hadi 1967 chini ya chama kimoja!
 
Hao "wajamaa" feki wa Tanzania wana ahadi kwenye chama chao eti:

1. Rushwa ni adui wa haki siatoa rushwa wala kupokea rushwa- Wakati wao na rushwa damudamu
Kura za maoni ndani ya chama chao ilikuwa ni rushwa tupu!

2. Nitasema kweli daima, fitina kwangu mwiko
Usanii mtupu, wamewalaghai wananchi kwa kuendesha zoezi la uchaguzi la kila namna ya udanganyifu

Hatuna chama tena pale, bali ni genge la wasanii ambalo bahati mbaya lina command ya vyombo vya dola. Ila dawa yao itapatikana one day maana bahari huwa haikai na uchafu
 
Labda unaongelea China ya sayari nyingine na sio China ya Xi Jinping, juzi tu billionaire Jack Ma ametaka ku-flot IPO ya kampuni yake Beijing waweka kibano.
Mkuu unaelewa vizuri hata maana ya Control of Market Forces, Command Economy and Economic Planning ???
Ungekuwa unafahamu basi usingenitolea huu mfano usio na kichwa wala miguu hapa, maana hata nchi za kibepari huwa zinafanya Blocks to IPO Auctions, Blocks to Mergers and Acquisitions au kulazimisha kampuni kufanya IPO. Hili suala liko kiuchumi na kisheria zaidi na hata sielewi utaliwekaje kunithibitishia kwamba hichi kilichofanyika ndiyo Uchumi wa Kijamaa.

Sababu za mamlaka husika kuzuia IPO-Auction and Listings huwa ni nyingi lakini kubwa na za kisheria huwa ni Usalama (National Security), Ushindani ( Fair Competition and Anti-Trust Laws) na Rushwa kwa makampuni yanayouza hisa. Hili la kupinga IPO ya Ant Group halijaanzia Uchina bali limeanzia Marekani ambako baadhi ya wawakilishi wao kama Marco Rubio alishauri serikali ipinge IPO ya Ant kwasababu ya sheria za Ushindani (Anti Trust Laws): Kwa Marekani IPO ya Ant Group itayaumiza mabenki yao.

Haya sasa sema jingine, ukishindwa endelea kumfanyia Raisi Magufuli Ibada ya sifa na kuabudu.
 
Alianza na kauli, kwa kusema chama chenye dola kushindwa kutetea dola yake ni uzembe!. Alishangaa iweje uwe na dola kisha upoteze dola.

Naam!. Kwenye uchaguzi huu tumeona alichomaanisha!. Bila shaka sote tuliona nini maana ya kutumia dola kubaki na dola, Tulishuhudia Kura kwenye vikapu vya akina mama, nyingine kwenye mabegi. Wapo waliozishika hizo kura na kuzipekeka polisi, polisi wakawajibu kwa mkato tu "Hatushughulikii masuala ya uchaguzi".

Maelfu kwa maelfu ya Mawakala wa vyama shindani wakapigwa zengwe, wakazuiwa kuingia, na wale walioningia wakapigwa zengwe wasipate nakala za matokeo!

Kule Zanzibar watu wakaonekana wanaopiga kura kwa lumbesa, mtu mmoja kura lundo.

Falsafa ya Bashiru Ally Kakurwa mtoto wa Kiislamu huyo aliyepitia madrasa!

Lakini huyu ni mwalimu wa chuo kikuu, msomi mkubwa, kafundisha wanafunzi wengi tu nadharia za demokrasia, ushirikishwaji wa wananchi katika maamuzi ya nchi yao wenyewe. Kafundisha sana masuala ya class struggle, ni role model wa maelfu ya wanafunzi wake wa ndani ya darasa na nje ya darasa! Sijui ametuma ujumbe gani kwa watu ambao walikuwa inspired naye kabla ya kuingia kwenye siasa pale wanapoona amekuwa katibu mkuu wa chama ambacho leo kimenufaika kwa mchakato feki na haramu kabisa wa uchaguzi, uliogubikwa na wizi wa kura wa kutisha katika historia ya nchi hii toka uhuru!

Lakini cha kuchekesha zaidi, Sheikh Bashiru Ally Kakurwa eti ni mjamaa, mfuasi wa Nyerere. Eti naye alikuwa mdau mkubwa wa Kigoda cha mwalimu. Eti naye alikuwa akiimba kama kasuku kuhusu uadilifu na sense ya haki ya mwalimu Nyerere.

Haya hatukuhadithiwa, tumeona kwenye TV mihadhara ya kigoda cha Mwalimu, Tumemuona Bashiru Ally Channel ten akielezea falsafa za haki, uadilifu, demokrasia, uhuru, umoja, n. k Lakini hatukujua kuwa miaka michache baadae, Bashiru huyuhuyu atakuwa ni katibu mkuu wa chama kilichonufaika kwa kuhujumu wananchi kuwaweka madarakani watu wawatakao wao wenyewe kupitia sanduku la kura!

Nikiangalia miaka michache ijayo nini itakuwa Legacy ya Bashiru Ally kwenye utumishi wa CCM, Siioni zaidi ya kushiriki kuwanyima wananchi viongozi na wawakilishi wawatakao watokanao na ridhaa zao wenyewe!. Kiufupi naye ni mshiriki asiyeweza kujivua lawama kwa dhulma hii kubwa waliyotendewa wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hata kama ngazi ya urais wa Muungano mlikuwa mkiitaka kwa udi na uvumba lakini Bashiru, hivi kweli Hussein ni wa kumshinda Maalim Seif kwa zaidi ya 57%?

Bashiru hivi kweli Tulia ni wa kumshinda Sugu Mbeya?

Hivi kweli Zitto ni wa kushindwa na yule Jamaa pale Kigoma? na mifano ya ya namna hii ni mingi nchi nzima!

Msomi na Mjamaa Bashiru hongera sana kwa kushiriki ipasavyo kuithibiti demokrasia vilivyo!, Maana sasa demokrasia ni kama adui yenu mliyefanikiwa kumdhibiti asifurukute!, But ngoja nikwambie kitu kimoja mko myopic sana kwa hizi moves zenu, kwa sababu ili mfanikiwe katika lengo lenu hilo ovu itabidi muwe wanafiki zaidi, walaghai zaidi, waonevu zaidi, madhulumati zaidi, msiheshimu wananchi zaidi.Mtafanya hivyo mpaka mtakapokutana na kigingi kutoka kule ambako hamkukudhania kabisa, kisha hapo common sense zitawarudia kuwa ni USELESS KUDHANI KIKUNDI KIDOGO KINA AKILI KULIKO UMMA, maana umma utasimama na nguvu yeyote itakayokema yaani itakayoweka kigingi cha kuzuia dhulma zenu, nguvu ya kuzuia uonevu wenu, nguvu ya kuzuia ulaghai wenu!. Nguvu hiyo Ama inaweza iwe ni nguvu yoyote ya ndani ya nchi au ya nje ya nchi au zote mbili kwa pamoja as long as wananchi wataona hii inasimama nao na inawatetea wataiunga mkono kwa maua, nderemo, vifijo, bashasha, kucheza, kusifu, n. k!.

Mwalimu Bashiru, Nikukumbushe tu kuwa mahali popote pale duniani uchaguzi hovyo na corrupt, huzaa serikali hovyo na corrupt na hutengeneza bunge hovyo na corrupt lisiloogopa wananchi bali wale waliowawezesha kuingia bungeni kwa njia corrupt!. Kamwe haiwezekani kupata maendeleo kwa bunge na serikali ya aina hiyo, maana hiyo si serikali na bunge la watu kwa ajili ya watu, bali ni kundi tu la watu wachche tu wenye "special interests" lenye kumiliki silaha na kwa silaha hizo huwatisha wananchi wasinyanyuke na kudai haki yao ya kuwa na viongozi watokanao na ridhaa yao, lakini ukweli ni kuwa serikali ya hivyo na bunge la hivyo havina legitimacy mbele ya watu hao!

Bashiru Umeshiriki dhambi ya kuwadhulumu haki wananchi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, unajisikiaje, "umewaweza" wapinzani au "umeiweza" nchi?. Kwamba umeacha alama ya heshima au alama ya aibu?

Shame on you!
Hana ujamaa wowote. Diwani wa Tabata Mama moja hivi alimhonga 10 mln. na jamaa akapokea....
 
Back
Top Bottom