Hii ndio ile "faida ya dola" aliyoisema Bashiru Ally?

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,620
46,261
Aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CCM, Katibu mkuu kiongozi na sasa mbunge wa kuteuliwa Bashiru Ally aliwahi kunukuliwa akisema watatumia dola sana kubaki madarakani na akaendelea mbele kusema ni uzembe kuondolewa madarakani ukiwa na dola.

Japo kauli hii iliibua mjadala mkali lakini ikitazamwa kwa upana wake ina uhalisia mkubwa sana kwa mifano kadhaa, hembu tazama

Katibu mwenezi wa chama tawala anaweza kupokelewa na kwenda kwenye mkutano wa siasa wa chama chake na watendaji na watumishi wa serikali wa eneo husika, idara mashirika na vitengo mbalimbali na wakawa wanafanya kile kinchoitwa kusikiliza na kutatua kero za wananchi. Hakuna chama cha upinzani chenye fursa hiyo.

Katibu mwenezi wa chama tawala anaweza kuwapigia simu mawaziri na wakuu wa mashirika akiwa katika mkutano ya hadhara ya chama wanachama wa chama wakapata fursa ya kuona wanatatuliwa kero zao na kupewa ahadi za kutosha. Hakuna chama cha upinzani chenye fursa hiyo.

Inawezekana pia chama tawala kikawa hakilizamiki kuomba kibali cha kufanya mikutano au maandamano yake mbalimbali kutoka polisi kama inavyovipasasa vyama vyote vya upinzani kufanya hivyo.

Haya ni baadhi ya mambo tu ambayo huenda ndio Bashiru Ally Kakurwa alikuwa akimaanisha ni faida ya kuwa na dola.
 
Majeshi yote yapo chini ya CCM yanafanya kazi kwa ajili ya CCM sio kwa ajili ya Watanzania.
Hapa ndipo katiba inapohitajika kufanyiwa marekebisho haraka sana... Chama kujitwisha mamlaka mpaka pia jeshi kuwa chini ya chama ni mbaya sana kama Nchi... Jeshi linapaswa kuwa huru na kulinda masilahi ya wananchi na Nchi, lakini lenyewe linaua demokrasia likisaidiana na chama cha madarakani.

Katiba inahitajika sana
 
Yes Tanzania ni nchi yenye chembechembe zilizo salia za mifumo ya nchi za kikomunisti.

Hilo la dola kuwa chini ya chama ndani ya mifumo ya ukomunisti ni sawa jambo la kawaida kabisa kwa sababu hata katiba zao za nchi zinaweka wazi kabisa chama chenye mamlaka ya kuunda serikali ni chama kimoja tu cha kikomunisti pamoja ya kwamba mifumo ya vyama vingi wanayo ila hivyo vyama vingine vina kazi nyingine kabisa isiyo husika na kutwaa dola ili kuongoza nchi.

Ndani ya nchi za kikomunisti zilizo salia mfano China na Vietnam mamlaka ya utawala yana anzia ndani ya chama ndipo yana kuja ndani ya serikali hivyo chama kina nguvu katika kila kitu ndani ya nchi hakuna kingine kilicho na nguvu kuzidi chama.

Mfano Rais wa China au Vietnam hana nguvu ya nchi ila nafasi ya katibu mkuu ndani ya chama ndiyo yenye nguvu kubwa ya kimaamuzi ndani ya chama na serikali ili kuondoa tatizo la hivi ndio maana China ilifanya mabadiliko ya katiba ili katibu ahodhi nafasi zote mbili yaani ukuu wa chama na ukuu wa serikali ili kuondoa mgongano licha ya kwamba nafasi yake ya ukatibu wa chama ndio yenye nguvu.

Kumbuka hawa China na Vietnam wenyewe nafasi kubwa ya chama iliyo baki ni ukatibu mkuu wa chama huku Tanzania nafasi ni mwenyekiti ndio anafuatia makamu, katibu na wengine hao wajumbe wote wa kamati kuu ya chama.

Kutokana na mifumo ya siasa ya namna hii ya kikomunisti chama ndicho chenye nguvu na ndicho kinashika na kuongoza dola tena bora kidogo Tanzania tuna jificha ficha kuwa jeshi halishiriki siasa za nchi .

Hao wachina na Vietnam ndio balaa kabisa jeshi lina kitengo ndani ya chama na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa chama anakuwa mwanachama wa chama cha kikomunisti huku jeshi likiwa chini yake na viongozi wote wa jeshi wakipokea muongozo kutoka kwa chama.
 
Majeshi yote yapo chini ya CCM yanafanya kazi kwa ajili ya CCM sio kwa ajili ya Watanzania.
Hayo ni madhara ya chama kukaa madarakani muda mrefu kwa shuruti Hadi kupoteza mvuto. Chama hicho hufukia kufanya siasa za kulazimisha ili kupata mvuto ambao hauwezi kupatikana tena, huishia kufanya siasa za vitisho, huku vikililazimisha kupendwa bila ridhaa ya umma.
 
Hapa ndipo katiba inapohitajika kufanyiwa marekebisho haraka sana... Chama kujitwisha mamlaka mpaka pia jeshi kuwa chini ya chama ni mbaya sana kama Nchi... Jeshi linapaswa kuwa huru na kulinda masilahi ya wananchi na Nchi, lakini lenyewe linaua demokrasia likisaidiana na chama cha madarakani.

Katiba inahitajika sana
Hizi ndio changamoto watu wanafikiri kuna siku jeshi lolote litakuwa upande wa wananchi na kuwaacha watawala. hili ni jambo gumu sana kwa namna mifumo yetu ya kisiasa na kiutwala ilivyo sukwa jambo la muhimu ni sisi wananchi kuungana na kupigania mabadiliko ya lazima
 
Yes Tanzania ni nchi yenye chembechembe zilizo salia za mifumo ya nchi za kikomunisti.

Hilo la dola kuwa chini ya chama ndani ya mifumo ya ukomunisti ni sawa jambo la kawaida kabisa kwa sababu hata katiba zao za nchi zinaweka wazi kabisa chama chenye mamlaka ya kuunda serikali ni chama kimoja tu cha kikomunisti pamoja ya kwamba mifumo ya vyama vingi wanayo ila hivyo vyama vingine vina kazi nyingine kabisa isiyo husika na kutwaa dola ili kuongoza nchi.

Ndani ya nchi za kikomunisti zilizo salia mfano China na Vietnam mamlaka ya utawala yana anzia ndani ya chama ndipo yana kuja ndani ya serikali hivyo chama kina nguvu katika kila kitu ndani ya nchi hakuna kingine kilicho na nguvu kuzidi chama.

Mfano Rais wa China au Vietnam hana nguvu ya nchi ila nafasi ya katibu mkuu ndani ya chama ndiyo yenye nguvu kubwa ya kimaamuzi ndani ya chama na serikali ili kuondoa tatizo la hivi ndio maana China ilifanya mabadiliko ya katiba ili katibu ahodhi nafasi zote mbili yaani ukuu wa chama na ukuu wa serikali ili kuondoa mgongano licha ya kwamba nafasi yake ya ukatibu wa chama ndio yenye nguvu.

Kumbuka hawa China na Vietnam wenyewe nafasi kubwa ya chama iliyo baki ni ukatibu mkuu wa chama huku Tanzania nafasi ni mwenyekiti ndio anafuatia makamu, katibu na wengine hao wajumbe wote wa kamati kuu ya chama.

Kutokana na mifumo ya siasa ya namna hii ya kikomunisti chama ndicho chenye nguvu na ndicho kinashika na kuongoza dola tena bora kidogo Tanzania tuna jificha ficha kuwa jeshi halishiriki siasa za nchi .

Hao wachina na Vietnam ndio balaa kabisa jeshi lina kitengo ndani ya chama na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa chama anakuwa mwanachama wa chama cha kikomunisti huku jeshi likiwa chini yake na viongozi wote wa jeshi wakipokea muongozo kutoka kwa chama.
Kimsingi ccm sio kama huko china na Vietnam, kwa hapa baada ya ccm kupoteza mvuto, kwa sababu za kihistoria ikabidi ijishikishe kwenye vyombo vya Dola.
 
Hayo ni madhara ya chama kukaa madarakani muda mrefu kwa shuruti Hadi kupoteza mvuto. Chama hicho hufukia kufanya siasa za kulazimisha ili kupata mvuto ambao hauwezi kupatikana tena, huishia kufanya siasa za vitisho, huku vikililazimisha kupendwa bila ridhaa ya umma.
Yes tunahitaji mabadiliko ya lazima ya kiutawala ndani ya nchi yetu pasipo kujali njia gani itatumika kuleta mabadiliko hayo.
 
Aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CCM, Katibu mkuu kiongozi na sasa mbunge wa kuteuliwa Bashiru Ally aliwahi kunukuliwa akisema watatumia dola sana kubaki madarakani na akaendelea mbele kusema ni uzembe kuondolewa madarakani ukiwa na dola.

Japo kauli hii iliibua mjadala mkali lakini ikitazamwa kwa upana wake ina uhalisia mkubwa sana kwa mifano kadhaa, hembu tazama

Katibu mwenezi wa chama tawala anaweza kupokelewa na kwenda kwenye mkutano wa siasa wa chama chake na watendaji na watumishi wa serikali wa eneo husika, idara mashirika na vitengo mbalimbali na wakawa wanafanya kile kinchoitwa kusikiliza na kutatua kero za wananchi. Hakuna chama cha upinzani chenye fursa hiyo.

Katibu mwenezi wa chama tawala anaweza kuwapigia simu mawaziri na wakuu wa mashirika akiwa katika mkutano ya hadhara ya chama wanachama wa chama wakapata fursa ya kuona wanatatuliwa kero zao na kupewa ahadi za kutosha. Hakuna chama cha upinzani chenye fursa hiyo.

Inawezekana pia chama tawala kikawa hakilizamiki kuomba kibali cha kufanya mikutano au maandamano yake mbalimbali kutoka polisi kama inavyovipasasa vyama vyote vya upinzani kufanya hivyo.

Haya ni baadhi ya mambo tu ambayo huenda ndio Bashiru Ally Kakurwa alikuwa akimaanisha ni faida ya kuwa na dola.
Ccm ndiyo 'dola ' yenyewe, huwezi kuwatenganisha kila mmoja humtegemea mwingine kwa uhai wake.

Petro E. Mselewa
 
Kimsingi ccm sio kama huko china na Vietnam, kwa hapa baada ya ccm kupoteza mvuto, kwa sababu za kihistoria ikabidi ijishikishe kwenye vyombo vya Dola.
Ni kweli CCM haifanani na China na Vietnam kwa mambo mengi lakini hivi vyama vitatu vya Tanzania, China na Vietnam vina ukaribu mkubwa sana ambao kwa asilimia chache kuna mifumo wana jaribu kuiga huko inayo wanufaisha CCM.

Nakubaliana nawe CCM ni tofauti na Vietnam na China kwa mambo mengi sana ila kuna machache yenye manufaa kwa CCM yanaigwa
 
Yes Tanzania ni nchi yenye chembechembe zilizo salia za mifumo ya nchi za kikomunisti.

Hilo la dola kuwa chini ya chama ndani ya mifumo ya ukomunisti ni sawa jambo la kawaida kabisa kwa sababu hata katiba zao za nchi zinaweka wazi kabisa chama chenye mamlaka ya kuunda serikali ni chama kimoja tu cha kikomunisti pamoja ya kwamba mifumo ya vyama vingi wanayo ila hivyo vyama vingine vina kazi nyingine kabisa isiyo husika na kutwaa dola ili kuongoza nchi.

Ndani ya nchi za kikomunisti zilizo salia mfano China na Vietnam mamlaka ya utawala yana anzia ndani ya chama ndipo yana kuja ndani ya serikali hivyo chama kina nguvu katika kila kitu ndani ya nchi hakuna kingine kilicho na nguvu kuzidi chama.

Mfano Rais wa China au Vietnam hana nguvu ya nchi ila nafasi ya katibu mkuu ndani ya chama ndiyo yenye nguvu kubwa ya kimaamuzi ndani ya chama na serikali ili kuondoa tatizo la hivi ndio maana China ilifanya mabadiliko ya katiba ili katibu ahodhi nafasi zote mbili yaani ukuu wa chama na ukuu wa serikali ili kuondoa mgongano licha ya kwamba nafasi yake ya ukatibu wa chama ndio yenye nguvu.

Kumbuka hawa China na Vietnam wenyewe nafasi kubwa ya chama iliyo baki ni ukatibu mkuu wa chama huku Tanzania nafasi ni mwenyekiti ndio anafuatia makamu, katibu na wengine hao wajumbe wote wa kamati kuu ya chama.

Kutokana na mifumo ya siasa ya namna hii ya kikomunisti chama ndicho chenye nguvu na ndicho kinashika na kuongoza dola tena bora kidogo Tanzania tuna jificha ficha kuwa jeshi halishiriki siasa za nchi .

Hao wachina na Vietnam ndio balaa kabisa jeshi lina kitengo ndani ya chama na mwenyekiti wa kamati ya ulinzi wa chama anakuwa mwanachama wa chama cha kikomunisti huku jeshi likiwa chini yake na viongozi wote wa jeshi wakipokea muongozo kutoka kwa chama.
Hata katiba ya sasa (1977) inatamka wazi, Tz ni nchi inayofuata siasa ya ujamaa na kujitegemea ila kiuhalisia hata hatupo tena huko.

Tuna katiba ambayo inaruhusu demokrasia ndani ya chama kimoja tu na sio ya vyama vingi, ndio maana dhulma na ukandamizaji wa vyama vingine na vyombo vya dola upo kila siku.

Katiba mpya haiepukiki.

JokaKuu zitto junior
 
Ni kweli CCM haifanani na China na Vietnam kwa mambo mengi lakini hivi vyama vitatu vya Tanzania, China na Vietnam vina ukaribu mkubwa sana ambao kwa asilimia chache kuna mifumo wana jaribu kuiga huko inayo wanufaisha CCM.

Nakubaliana nawe CCM ni tofauti na Vietnam na China kwa mambo mengi sana ila kuna machache yenye manufaa kwa CCM yanaigwa
Ni kweli na yanaigwa kwa kubabiababia kwakuwa wananchi ni waoga. Lakini siku uoga ukiwatoka wananchi hutoana huo uigwaji wa hivyo vyama vya China ama Vietnam.
 
Hata katiba ya sasa (1977) inatamka wazi, Tz ni nchi inayofuata siasa ya ujamaa na kujitegemea ila kiuhalisia hata hatupo tena huko.

Tuna katiba ambayo inaruhusu demokrasia ndani ya chama kimoja tu na sio ya vyama vingi, ndio maana dhulma na ukandamizaji wa vyama vingine na vyombo vya dola upo kila siku.

Katiba mpya haiepukiki.

JokaKuu zitto junior
Upo sahihi kabisa tulihama mfumo wa chama kimoja kinadharia Ila kivitendo hatukuhama kabisa ile pressure ya nje kuhusu hali ya kiuchumi ndio ili tufanya kufanya ulaghai huu huku kiuhalisia hata mabadiliko ya kikatiba kupokea mfumo mpya wa vyama vingi hayakufanyika kabisa.
 
Upo sahihi kabisa tulihama mfumo wa chama kimoja kinadharia Ila kivitendo hatukuhama kabisa ile pressure ya nje kuhusu hali ya kiuchumi ndio ili tufanya kufanya ulaghai huu huku kiuhalisia hata mabadiliko ya kikatiba kupokea mfumo mpya wa vyama vingi hayakufanyika kabisa.
Kimsingi mfumo wa chama kimoja haukuletwa na wananchi, Bali uliletwa na mtu mmoja ambaye ni Nyerere. Na katiba yetu ilitungwa kuendana na utashi wa Nyerere ambaye hakuwa muumini wa kutofautiana mawazo. Hata mfumo wa vyama vingi baada alituingiza yeye yeye kwa kutumia ujanja, na kubakiza katiba hii hii ya mfumo wa chama kimoja.

Kinachofanyika Sasa ni madhara ya utawala wa Nyerere. Ni machafuko tu ama mapinduzi ya kijeshi yataleta mabadiliko.
 
Aisee JWTZ NI CCM
 

Attachments

  • 20231111_155521.jpg
    20231111_155521.jpg
    199.6 KB · Views: 5
Sasa ndugu mbona koz ya politics science rahis sana kuelewa
Hiv chama kilichopo madarakan kinatimiza ahad zake kwa wananch
Ilani ndio mkataba kat ya chama kinachounda serikal na wananch. Iweje anayeeneza ilan akapata hoja ashindwe kuipatia majibu sasa atakua anaeneza nini?
 
Sasa ndugu mbona koz ya politics science rahis sana kuelewa
Hiv chama kilichopo madarakan kinatimiza ahad zake kwa wananch
Ilani ndio mkataba kat ya chama kinachounda serikal na wananch. Iweje anayeeneza ilan akapata hoja ashindwe kuipatia majibu sasa atakua anaeneza nini?
Rudia kusoma uzi uuelewe.
 
Back
Top Bottom