Dk. Ulimboka: Ninayejua ukweli ni mimi...

Kama akili yake inafanya kazi sawia,angenyamaza na kuendelea na shughuli zake na kumuachia mungu yote maovu aliyofanyiwa na aliyoyafanya tena anatakiwa amshukuru sana mungu kwa matendo yote aliyomtendea na akumbuke kabisa mungu ana makusudi fulani na yeye ama aishi ili aone matokeo ya yale aliyokuwa akiyatetea au ajutie matokeo ya yale aliyokuwa akiyapigania,....
Umemaliza mkuu HOMOSAPIEN !! Ulimboka fuata maneno ya busara haya. MUNGU anakupenda sana..
 
Swala la kuogopa mtu au kufa halipo kikubwa ambacho tunatakiwa watu wote tujue ni kwamba huu ni muda wa mabadiliko na kiongozi wa kweli ni yule ambae anatokana na misukosuko[crisis] na hii ni kwa maeneo yote.

Hivyo tuache unafiki bali watu wanaoonesha nia hiyo tunatakiwa kuwaunga mkono asilimia mia, to be a good leader it is a proces not instantly kama wanavyofanya CCM, tanzanians we should wake up,

Hivyo kwa Dr. Ulimboka tutapata jibu kama ni kweli alistahili kuwa kiongozi wa madaktari au alivaa viatu visivyo mtosha alafu akataka kupanda ngazi!!
 
Wewe Great thinker, Mwanahalisi aliandika habari za uchunguzi wake binafsi kama gazeti,na mpaka sasa
zaidi ya kulifungia gazeti hakuna aliyekanusha habari hizi watanzania tukamwelewa,na kama hazikuwa na
ukweli wafanyakzi wa tigo kwa nini walifukuzwa kazi?Think Twice"

Uchunguzi wa nini kuhusu nini? Dr Ulimboka ndio muhusika na ndio aliyetekwa na kufanyiwa unyama na yeye mwenyewe ndio anakuambia ukweli wa yeye kutekwa anaujua mwenyewe huo uchunguzi wa Mwanahalisi ni wakwenu nyie...Watanzania wasubiri kauli yake kama huo uchunguzi wa Mwanahalisi ungekuwa wa kweli Dr Ulimboka si angesema Mwanahalisi wameishasema ukweli kutoka na uchunguzi wao, kulikuwa na haja gani tena kusema ukweli anaujua yeye.
 
Nawasiwasi kama ulimboka ataongea ukwel uliomkuta serikali itamtuliza vzur yy na familia yake malezi na ada za watoto ,jumba hko beach,migari ya kufa mtu ehh ndo aongee nn ,,??ngoja muone atakayoongea mtabaki na mshangaoo chezea serikali,, na mihelaaa lets wait n c
 
Kumbe hakuna anayejua chochote kuhusu Dr Ulimboka kutekwa anayejua ni yeye peke yake...kumbe Gazeti la Mwanahalisi linastahili kufungiwa kwa uchochezi, Kubenea acha kukurupuka Dr Ulimboka anawakana sasa...

R.I.P MWANAHALISI.

Mwanahalisi lilikuwa ni gazeti la habari za kiuchunguzi. Kuamini au kutoamini wanayoyaandika ni hiari ya msomaji na asije tokea msomaji akamuaminisha mwenzake kwamba wanachoandika mwanahalisi ni uongo au si uongo. Watch your thinking bro!!!!!.

RIP maana yake hatautarajii kwamba litarudi tena lakini i hope ndicho watawala walichosema kwamba wanalifungia kwa muda usiojulikana.

Kwa kweli kuna kitu nakikosa juu ya gazeti hili. Si kwa sababu nalipenda sana, la hasha ila kwa kuwa limenifanya nipanue wigo wa fikra zangu juu ya mambo yanayotendeka nchini kwangu.
 
Unataka aongee kufurahisha umma pamoja na wewe ili iweje,matatizo ni yake yeye na familia yake, akifa wewe utakuwa umepata faida gani au kupungukiwa kipi katika uhai wako na kama wewe hauogopi kufa kwanini ukiumwa unaenda hospitali kutibiwa, mwacheni Dk. wa watu agange yake mwenyewe asifurahishe umma kwa gharama za uhai wake,yangekukuta wewe ungechukua hatua gani?

Yaani unaambiwa pale kuna chatu anameza watu usichungulie we unaenda kuchungulia nani akusaidie usimezwe na chatu,mimi namshauri apige kimya kabisa tena aachane na malumbano yasiyokuwa na tija, kwani hata alichokuwa akikitetea hakijatekelezwa.

Tena asikimbilie kufanya kazi nje ya nchi kama hao waliomponza komaa hapa hapa TZ tena sasa kivyakovyako mkubwa maisha yako yana thamani zaidi kwako kuliko yoyote humu duniani.
 
Wewe Ritz ndo hujaelewa kauli ya Dr. Ulimboka. Mimi naona alikuwa na maana watu wasiwahoji ndugu zake kama njia mbadala ya kupata habari

Kwa upande mwingine sina shaka na uchunguzi wa Kubenea. Alivyofanya Kubenea ndo hasa ilitakiwa ifanyike. Kwenda kwenye makampuni ya huduma za simu na kupata nakala ya mwenendo wa simu zilizoingia na kutoka simu ya Dr. Ulimboka siku ya tukio na siku chache kabla

@ Ritz unaielezeaje ile ya Ramadhani Ighondu(afisa kutoka Ikulu) kuwasiliana na mwenyekiti wa Mabwepande?

Naona mnataka kulazimisha mnatafsiri kauli ya Dr Ulimboka kwa kutumia mapenzi yenu binafsi hayo mambo ya Mwanahalisi ni ya kwenu, Dr Ulimboka kaishasema ukweli wa tukio lake analijua mwenyewe.
 
Hakuna wa kuogopwa zaidi ya Mungu,nidhamu ya uoga na kumsujudia mwanadamu mwenzako ni mbaya na dhambi mbele ya Mungu,walishashindwa kumuangamiza mara ya kwanza sasa ni zamu yao kupata pigo takatifu ambalo familia zao hawataka kuja kusahau

Naomba sana watu muache ushabiki. Dr. Ulimboka nashauri kwa kupona kwako na mateso yale Mungu anataka umtumikie. Hivyo geuka acha kisasi muachie Mungu atawapatiliza kwa maovu yao jikabidhi kwa Bwana rasmi na ushike amri zake na mafundisho yake hayo mengine waache watanzania siku zote wamejaa unafiki ukiumia wanakugeuka. Kumbuka watu watafanya mradi huo kwa hiyo waache waseme kaa kimya. Na nakuomba hao polisi wasikuite kwa lolote sabb mambo wameamua kupeleka mahakamani kwa nini waanze kurudisha polisi! Huo ni mtazamo wangu lakini vema waone wanasheria watakusaidia ZAIDI. Na ukumbuke Kutoa shukurani kwa Mungu na ukawe dhabihu safi ktk maisha yako yaliyobaki sasa. Na hakikia Ukiamini na kushika Amri za Mungu Utauona UTUKUFU wa MUNGU. KAA KIMYA WAMBEYA ACHANA NAO.
 
Ritz kwa muktadha wa bandiko hili na tukifuata maneno ya mhusika mkuu mwenyewe, Ulimboka, ni kwamba nje yake hakuna anayejua mlolongo wa utekaji wake. Lakini vipi kuhusu watekaje wake?
 
Kitu kilichotokea Dr.Ullimboka maadui zake sasa hivi wako kwenye mazungumzo nae ndio maana analeta siasa hataki kueleza kilichomtokea usishangae asieleze kabisa au akaeleza story tofauti na ile ya mwanahalisi.Manake maadui zake wanaweza kumweleza bwana samehe yale yalikuwa ni matatizo ya kiufundi wakampa shavu akatulia zake kimya.Ndio maana ameanza kuleta porojo.
Manake hili neno:Dk. Ulimboka: Ninayejua ukweli ni mimi... limepigwa kiufundi sio ajabu ameambiwa aliseme ili kunarrow ushaidi.

yah...i think so.
 
Kumbe hakuna anayejua chochote kuhusu Dr Ulimboka kutekwa anayejua ni yeye peke yake...kumbe Gazeti la Mwanahalisi linastahili kufungiwa kwa uchochezi, Kubenea acha kukurupuka Dr Ulimboka anawakana sasa...

R.I.P MWANAHALISI.
KAMA SIYO BANI NI NGEKWABIA KAWAUZIE MASABURI YAKO WALE WOTE WANOKUTUMA:shetani:


 
Nina imani DR. ni mtu mzima. Yeye ndo anayejua tamu na chungu. Afanye maamuzi ya busara. Akijua kabisa hayaidhuru familia yake wala yeye mwenyewe.
Mie namshauri awe kimya tu..nenda zako tukuyu kale ndizi DR.
 
Naona mnataka kulazimisha mnatafsiri kauli ya Dr Ulimboka kwa kutumia mapenzi yenu binafsi hayo mambo ya Mwanahalisi ni ya kwenu, Dr Ulimboka kaishasema ukweli wa tukio lake analijua mwenyewe.

If Dr. Ulimboka decides to reveal the truth today I believe without a shadow of a doubt people will take to the streets to demand dismisal/resignations of the culprits including the president cuz he lied to the nation when he said there was no reason for the government to be involved in the kidnapping of Dr. Ulimboka

On the other hand in the event that he is given hush money so the truth is kept secret, we all know the truth already! The fact that we all speak with one voice here despite our political affiliation is an indicator of people's determination to redeem the country. Hopefully one day these cold-blooded killers will face justice
 
Sasa hii habari si ni Gazeti la jana la Tanzania Daima!! Yaani sasa hivi JF tunaanza kuleteana magazeti ya jana? Am out of thread.
 
ndugu SKYPE ukishaujua ukweli wewe utafanya nini au kutaka kumwangamiza. Mangapi umeyajua ya kweli kwa jamii na mtu mmoja mmoja yakapatiwa ufumbuzi. Hivyo naomba utafakari kwanza si kuongea tu tubadilike watanzania kwani ushabiki ni gharama sana.
 
Dr Ulimboka ataongea muda ukifika.

Ingawa hii picha ya kihindi inachelewa kuanza, lakini muda wake ukifika picha ya kihindi itaanza tusiwe na haraka.

Tuendelee kumuombea Doctor afya yake iwe nzuri, na atakapoongea aseme ukweli mtupuuuu.
Mwanahalisi nao waliujuwa ukweli 90%, ndiyo maana wakafungiwa, habari walizotoa zilikuwa na details za kutoshaaa, walifanya kazi nzuri sanaaaa, ambayo serikali haikutegemea kutoka kwa wandishi wetu wa Tanzania na pia hawakuogopa kutoa details.
Binafsi nawaamini sana Mwanahalisi kwa hili jambo la Dr Ulimboka.

Doctor Ulimboka tulizana, upone vizuri halafu utakuja siku moja kutuhabarisha, ila ni lazima uwe muangalifu sana, maana serikali this time wakikupata watakuuwa hawatafanya kosa tena kama walilolifanya, watakuchoma moto au watakupiga risasi huo ni ushauri wangu kwa Doctor Ulimboka.

Kwa bahati mbaya sana serikali za kiafrika ni za kishenziiiiiiiiiiiiii sanaaaa, siyo hapa Tanzania, ni Afrika nzima mambo na michezo ni hii hii tuuu, serikali za kiafrika hazitaki kukosolewa wala kuelekezwa.

Nawatakia siku njema
 
Movie inaelekea mwisho kwa hiyo kauli kwamba ukweli anaujua yeye dr....mbaya tu ni kwamba inaishia tofauti na matarajio ya wengi,.....miafrika ndivyo tulivyo......Nyani Ngabu.
 
Back
Top Bottom