DulleShaibu
Member
- Jun 5, 2015
- 98
- 14
Wano uhuru wa kufanya hivyo hii ni demokrasia ila waepuke kukashifu wanasiasa wengine huo sio mtaji sahihi wa kisiasa
Mbona kuna mmoja alisemaga KAMWE hawezi hama ccm, kama kuna asiyemtaka ccm ahame yeyeSi alisema ameamua kuachana na siasa?
Tumia Basi Akili Zako Mkuu. Unajidhalilisha Sana Kudhani Magufuli Ataweza Kuibadilisha Tanzania Ambayo Chama Kile Kile Sera Zile Zile, Ambazo Zimeshindwa Kufanya Kitu kwa miaka 50?
Uwezi kusafiri Kwa usafiri wa Kiforokobe. Utegemee utafika Kwa wakati. ccm Imechoka Haifai ipumzike.
Kije Chama Chenye Mtazamo Mbadala, kwa Maendeleo ya Taifa, wale wote Wanaopingana na Mabadiliko basi Watu hao wameridhika na umaskini wa nchi hii chini ya chama cha mapinduzi.
Ni lazima uwe mpumbavu uliyevuka viwango KUMUAMINI Sumaye, niloshangaa sana aliposema CCM walituahidi maisha bora ila mpaka sasa hamna kitu, NILISHANGAA sana na nikawashusha kabisa viwango ukawa hii yote kwa kumuamini huyu muongo na kumuita eti mwana mabadiliko.Nchi hii ina rundo kwa mazuzu, hivi kweli mtu mwenye akili zake anaweza kuamini kuwa Sumaye ni mpenda mabadiliko? Huyu aliyeitwa Zero! Muulizeni ataleta mabadiliko yapi ili na sisi wengine tushawishike. Sumaye ana rekodi ya kuwa Waziri Mkuu aliyekaa madarakani kuliko yeyote, lakini Hana chochote cha kuonyesha kuwa akijifanya. Leo hii eti anaitwa mpenda mabadiliko!
Wapande, hypocrites Mwanaume unatupiwa mabegi na Mwanamke nchi angeongoza vipi? Kama mwanamke ndio final say??
Lowossa fisadi naye ni msaliti.Wote wana sifa moja inayofanana, USALITI!
Kwahiyo lowasa na sumaye walikuwa wanasubiri kupigwa chini ccm halafu ndio ghafla wapende madiliko!, hamna lolote ni uroho wa madaraka tu si lowasa wala sumaye mwenye uwezo wa kuleta mabadiliko zaidi ya kuendeleza wizi waliouanzia ccm
Lengo lao ni kuhakikisha kwa uvumba na ubani watanzania hawapati mabadiliko wanayotaka na pia kuhakikisha ccm haiondoki madarakani.
Hili litakuwa ni pigo kubwa kwa wapinzani.
Hongera sana CCM kwa kuwapata wasasiasa hawa mahiri na wabinafsi.
Mimi hapa ni chadema ya Dr. Slaa, hivyo siukubali mfumo wa ccm, najua hilo, ila mtu anapokuwa waziri mkuu (wote wawili ni jumla ya miaka 13), walikuwa na nafasi kubwa sana ya kuleta mabadiliko, mikataba michafu chafu ya awamu ya tatu ilipitia kwa Sumaye, mingine kwa Lowassa, kama ni hayo mambo, wangegoma kuisaini kisha kung'atuka, ila waliisaini na wakakaa kimya, leo nao wanalalamika hasa Sumaye kuwa maisha bora hayapo, wakati ni upofu wake wa kusaini mikataba mibovu ndo unanyonya wananchi, HAWA WAWILI WASITHUBUTU KABISA, hasa huyo mouthpiece Sumaye kuongea suala la mfumo. Kama ukikubaliana nao mimi pia nitaona hauko sawa!Nakushangaa sana jogoo dume kama unashindwa hata kujua kuwa mfumo wa chama cha ccm ndio ulioongoa na unaoongoza nchi na sio mtu. Umewahi kujiuliza kama ccm walikuwa wanajua kuwa lowasa ni mmiliki richmond kwanini hawakusema waje kusema leo? Guys you have to be serious kidogo aisee. Msitufanye watoto
Naona dozi inakuingia sawia...!Wanaichukia ccm baada ya kukatwa? wee jamaa jinga sana.