Dk Slaa asema Mufti hakufanya utafiti

Dk Slaa asema Mufti hakufanya utafiti

Mi siwashangai,coz i know them ni vibaraka.So hawataongea la kupingana nao lazima wajipendekeze kwao ili wapate mabaki ya mkate.Hawana huruma na waumini wao njaa zimewaganda kama ruba,maisha magumu no one cares.
 
Kikwete anawaharibu hata wazee wa watu jamani... duh, kishamuharibu shekhe wa watu.
 
Kama kuna mtanzania yeyote anayedhani kuna mtanzania yeyote yule ambaye amewahi kuwa religion extremist (yaani alikuwa kiongozi wa dini, call it Sheikh, Mchungaji, Askofu au Padri) atawahi kuongoza nchi hii nadhani atakuwa amepotoka mno na hiyo ni ndoto ya mchana....

Watanzania hapendi extremist yeyote... yanayongolewa kuhusu wanasiasa ambao wamekuwa viongozi wa dini kwenye maisha yao sio kwamba wana makosa yoyote bali it is simply the fact that hakuna uwezekano kwa kiongozi aliwahi kuwa wa dini kuongoza nchi hii... mjadala mwema!
 
Kama kuna mtanzania yeyote anayedhani kuna mtanzania yeyote yule ambaye amewahi kuwa religion extremist (yaani alikuwa kiongozi wa dini, call it Sheikh, Mchungaji, Askofu au Padri) atawahi kuongoza nchi hii nadhani atakuwa amepotoka mno na hiyo ni ndoto ya mchana....

Watanzania hapendi extremist yeyote... yanayongolewa kuhusu wanasiasa ambao wamekuwa viongozi wa dini kwenye maisha yao sio kwamba wana makosa yoyote bali it is simply the fact that hakuna uwezekano kwa kiongozi aliwahi kuwa wa dini kuongoza nchi hii... mjadala mwema!

Yaani bora tuongozwe na Kingwendu!!
Umepotoka na wewe, pia hujafikiria vizuri, sijajua ni bahati nbaya au ndivyo ulivyo!?
 
Nadhani Sheikh Mkuu ameteleza kwenye kauli yake au amefanya makusudi huku akijua anamtumikia nani. Kauli ambayo imekuwa ikitolewa na watawala kwa miaka nenda rudi hasa wananchi wanapodai maslahi yao imekuwa ni neno "Uvunjifu wa Amani". Nathubutu kusema neno hili limetumiwa vibaya na watawala wetu kuingiza hofu kwa watu wenye mioyo minyonge ili waendelee kuwakandamiza.

Tunamheshimu sana Sheikh Mkuu na nafasi yake...ila tungependa pia kumuonya asije akaacha majukumu yake ya msingi na kununuliwa na watawala kwa sababu zozote. Ningetegemea Sheikh Mkuu akipigia kelele uadilifu, haki kwa watu wote bila ya kujali chama au mahali walipo. Kinyume chake Sheikh anatumia kauli zilezile za watawala kwa kisingizio cha amani.

Tanzania haitaweza kuwa na amani ya kweli iwapo haki hazitendeki...polisi, uhamiaji, magereza, afya, mahakama, TRA, NHC, kila mahali zinapopaswa kutolewa huduma za kijamii na serikali au taasisi zake nk hakuna haki...kumejaa rushwa, upendeleo na uonevu. Amani itatoka wapi? Tangu lini mwenye njaa akawa na amani? Au hamuoni siku hizi ajali ikitokea tu kama una gari yako wanakomba site mirror mpaka tyre iliyofungwa. Amani iko wapi hapo? nadhani ili amani ya kweli iwepo ni lazima kwanza tutengeneze mazingira ya haki kwa raia ikiwa ni pamoja na ajira na viongozi kutekeleza kauli zao kwa vitendo, mambo ambayo kwa mtazamo wangu naona watawala wameshindwa na sasa wameamua kutumia viongozi wa dini kututishia kwa kisingizio kilekile cha zamani.

Nawashihi viongozi wa dini wasijiingize kwenye michezo michafu ya watawala vinginevyo heshima zao kwenye jamii zitayeyuka kama ilivyo kwa watwala wetu.
 
Mpevu, binafsi nimekupata. Lakini kauli hii kama ni ya kuasa ingefanya kwa Watanzania wote bila kutaja neno Waislamu. Kwanini: itajenga hisia kuwa kwa sasa wanaoandamana ni Wakristo na siyo Waislamu, hivyo baadhi ya Waislamu wanaweza kujitokeza kuleta vurugu katika maandamano hayo kwa kusema kuwa Wakristo wanataka kuiangusha serikali inayoongozwa na Muislamu. Huu ni upande mmoja.
Upande mwingine ni kwamba Waislamu pia wanaweza wakapuuzia agizo la Mufti na hapo Mufti anaweza akawagawa Waislamu katika makundi ya kuhasimiana yenyewe kwa wenyewe!! Na kama Waislamu wakiendelea kuwepo kwenye maandamano Mufti atachukua hatua gani?
Ni vizuri watu wakajua kuwa maandamano yanayotokea yakiongozwa na Chadema, Je yanasema serikali iliyopo madarakani hatuitaki au inasema mapungufu ya serikali ili kuiamsha serikali ifanye kazi yake ya kuhudumia wananchi.
Lakini ya Mufti sishangai maana aliyeanza kulalamika ni JK mwenyewe wakati akiwa kama Rais na Mwanasiasa Mwenyekiti wa Chama Kinachotawala cha CCM ilitakiwa ajibu hoja zilizokuwa zinashadadiwa na Chadema kuwa kama ni uongo aseme kama serikali wamefanya nini na kama hawajafanya nini mipango yao na tutarajie nini wakati gani. Wananchi tungeweza kuelewa na kuipa serikali muda lakini kwa serikali kulalama kwa wananchi, sasa wananchi walalame kwa nani?
Hayo matatizo yaliyopo yafanyiwe kazi na hilo ndilo suluhisho la manung'uniko ya wananchi. Wakumbuke tu kuwa Misri ilipiga marufuku maandamano kwa miaka 30 iliyopita na hata juzi wananchi wake walipoandamana mpaka Mubaraka akaachia ngazi bado sheria hiyo ilikuwapo na kwa sasa imefutwa.
Jamani viongozi wafunguwe masikio na macho wawasikilize na kuwatazama wananchi na wasitumie uwezo na vyeo vyao vibaya. Usipowasikiliza wananchi, masomo utayajifunza Mwanza kwa Masha na Diallo. Waliona wao walifika lakini walisahau kuwekeza kwa wananchi wapiga kura!!!
Nanu,
Hii imetulia. You are a real senior Expert member. Nakuongezea thanks ingine.
 
huenda ukawa na lengo zuri sana la kufikisha ujumbe lakini maneno uliyotumia hayapendezi, hayajengi zaidi ya kujaza chuki baina ya mtu na mtu, yule sheikh ni kiongozi wa watu na unaposema hana akili ya kufanya hivyo ina maana hata waliyeridhia yeye kuongoza hawana akili. Kauli hizi zichungwe kwa sababu ndo huwa mwanzo wa chuki ambazo baadae huzaa machafuko katika nchi. Yaliyotokea rwanda yalisababishwa kwa kiwango kikubwa na kauli zenye chuki ambapo hamna mtu mwenye akili aliye tayari kuzipokea na kukubaliana nazo. Unapaswa kuwa na kauli za busara hasa linapokuja suala linalogusa imani ya mtu kama hili.
Nimekusikia kaka. Nimekurupuka. Kumradhi!
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Wakuu kauli ya Sheikh Mkuu Simba inaweza kuwashangaza wasiofuatilia siasa za BAKWATA na CCM.

BAKWATA kama taasisi ya waislam Tanzania imeshindwa kutekeleza majukumu yake ya msingi,si ajabu waislam wengi Tanzania wanaiona kama ndiyo chanzo cha kudidimia kwa Uislam Tanzania katika sekta za kiuchumi,kijamii,elimu na Afya.Ofisi za makao makuu BAKWATA Kinondoni ni kielelezo halisi jinsi ilivyoshindwa kusimamia mambo yake yenyewe,kuna kipindi hata mkutano wa kumchagua Mufti ulishindwa kufanyika kisa uswahili na ubabaishaji ulipitiliza.

BAKWATA imeshidwa hata kumlipa mshahara Sheikh Mkuu hali iliyoilazimu serekali kujitolea kinyume cha katiba kumlipia mshahara Sheikh Simba jambo hamblo ni aibu kubwa kwa Waislamu wote Tanzania.Baada ya viongozi kubaini utamu wa kulipwa mshahara na marupurupu kibao wakaleta hoja ya mahakama ya Kadhii ili kutanua uwigo wa viongozi wengi kulipwa mishahara na serekali.

Sheikh Mkuu lazima aseme upupu wowote ili mrija wake usikatwe.
 
Nafikiri kwa jinsi tunavyokwenda naona kabisa sio rahisi kama tunavyofikiria kutenganisha dini na siasa. Huu uchaguzi uliopita hizi fikra za kidini zilipata nafasi zaidi labda kuliko chaguzi nyingine.

Wakati mavugu vugu yanaendelea natumaini hadi mwaka 2015 tutajua nini maana ya kutenganisha dini na siasa.
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Wakuu kauli ya Sheikh Mkuu Simba inaweza kuwashangaza wasiofuatilia siasa za BAKWATA na CCM.

BAKWATA kama taasisi ya waislam Tanzania imeshindwa kutekeleza majukumu yake ya msingi,si ajabu waislam wengi Tanzania wanaiona kama ndiyo chanzo cha kudidimia kwa Uislam Tanzania katika sekta za kiuchumi,kijamii,elimu na Afya.Ofisi za makao makuu BAKWATA Kinondoni ni kielelezo halisi jinsi ilivyoshindwa kusimamia mambo yake yenyewe,kuna kipindi hata mkutano wa kumchagua Mufti ulishindwa kufanyika kisa uswahili na ubabaishaji ulipitiliza.

BAKWATA imeshidwa hata kumlipa mshahara Sheikh Mkuu hali iliyoilazimu serekali kujitolea kinyume cha katiba kumlipia mshahara Sheikh Simba jambo hamblo ni aibu kubwa kwa Waislamu wote Tanzania.Baada ya viongozi kubaini utamu wa kulipwa mshahara na marupurupu kibao wakaleta hoja ya mahakama ya Kadhii ili kutanua uwigo wa viongozi wengi kulipwa mishahara na serekali.

Sheikh Mkuu lazima aseme upupu wowote ili mrija wake usikatwe.

mkuu ngongo heshima sana

kimya chako kina kishindo..... nimekusoma sana
 
Heshima kwenu wanajamvi,

[
Sheikh Mkuu lazima aseme upupu wowote ili mrija wake usikatwe.

Ndiyo lakini huo mrija kwa thamani ya watanzania wote! Maana tayari nimeona kwenye thread nyingine, ushabiki mkubwa kwa kauli yake. Wapo waumini wake wanamwamini sana tena hawataki hata kuulizwa maswali kuhusiana na imani yao hio. Hawa wakichokonolewa kidogo tu au kwa makusudi ama bila kukusuidiwa wanaweza wakaleta takfrani kubwa. Hawa wanaweza wakachukua silaha kuanza vita.

Nd Magobe ameuliza maswali ya msingi. Na ninakubaliana naye kwa kauli yake kwamba viongozi wa dini wana majukumu makubwa ya kuwalea waumini wao.

Ninalazimika kumwona Mufti Simba kama mtu hatari katika taifa, maana ameshatangaza upande wa pili ni wabaya! Ameshachokoza na kama wakikosa subira, fujo ni dhahiri. Lakini pia, tayari naona shida kuu kwani kina Mufti Simba hawataruhusu maandamano ya CDM yafanyike kwa amani maana itapunguza nguvu ya hoja yao. Kwa ajili hii wanaweza wakapandikiza watu wao ndani ya maandamano ili wafanye vurugu.

Mungu tuepushe na hili! Ibariki Tanzania na watu wake!
 
Heshima kwenu wanajamvi,

Wakuu kauli ya Sheikh Mkuu Simba inaweza kuwashangaza wasiofuatilia siasa za BAKWATA na CCM.

BAKWATA kama taasisi ya waislam Tanzania imeshindwa kutekeleza majukumu yake ya msingi,si ajabu waislam wengi Tanzania wanaiona kama ndiyo chanzo cha kudidimia kwa Uislam Tanzania katika sekta za kiuchumi,kijamii,elimu na Afya.Ofisi za makao makuu BAKWATA Kinondoni ni kielelezo halisi jinsi ilivyoshindwa kusimamia mambo yake yenyewe,kuna kipindi hata mkutano wa kumchagua Mufti ulishindwa kufanyika kisa uswahili na ubabaishaji ulipitiliza.

BAKWATA imeshidwa hata kumlipa mshahara Sheikh Mkuu hali iliyoilazimu serekali kujitolea kinyume cha katiba kumlipia mshahara Sheikh Simba jambo hamblo ni aibu kubwa kwa Waislamu wote Tanzania.Baada ya viongozi kubaini utamu wa kulipwa mshahara na marupurupu kibao wakaleta hoja ya mahakama ya Kadhii ili kutanua uwigo wa viongozi wengi kulipwa mishahara na serekali.

Sheikh Mkuu lazima aseme upupu wowote ili mrija wake usikatwe.

Inasikitisha sana.....
 
we Slaa mpuuzi sana acha kudharau dini za wenzako, Pengo alipotoa maoni yake kuhusu maandamano alifanya utafiti lini? yani nyie mnaposifiwa hakuna comment yoyote ila mkikoselewa tuu,ndo mnakuja na matamko ya kipuuzi! hiyo siasa badilikeni na acheni ulimbukeni coz mnatubero sana

Maneno kama haya ni mafanikio ya watu wa system kuwagawa wa-TZ. walijua fika kwamba ukimtumia Sheikh Simba, utakuwa umeondoa kundi fulani. Sasa unaona itahwa hataki kusikia chochote juu ya Simba. Limekuwa la kidini badala ya siasa!

Nionavyo mimi ni kuwaasa viongozi wa kidini wasiwe watu wa bei ndogo kiasi hicho. Wao ni watu wa heshima na bei kubwa sana kiasi kwamba hawatakiwi kuzungumza lolote ambalo wanaambiwa.

CCM tunaijua. Wakizozwa wao kama CCM hulipeleka serikalini. Kakobe alipomsifu Mrema akina Nchimbi wakageuka kuwa wasoma mashairi ya UVCCM na kutukana kwamba alikuwa dj. Miaka imeenda Kikwete kasifiwa chaguo la Mungu, wanakenua meno kudaka sifa hiyo. Kila wakati sifa ni zao, wengine NO!

JF tujenge heshime zetu. Sifa kwa Simba au Pengo hainipi faraja yoyote ktk maisha yangu. Wanafanya hayo ili wapewe manufaa binafsi na siyo manufaa kwa Waislamu au wakristu wote.
 
Hivi Yale makontena ya kura kuna utafiti ulifanyika? Mh Slaa pamoja na kuwa sina mlengo wowote lakini nashauri si kila hoja ukurupuke kujibu maana viongozi Wa dini yenu wakikusifia unakaa kimyaaa wala huuulizi utafiti huwa sipendi kuchangia masuala ya dini lakini hapa imebidi I am not happy with Padri Dr Slaa Statement yenye kamfumo ka dharau kwa mbaaaali
 
Kama kuna mtanzania yeyote anayedhani kuna mtanzania yeyote yule ambaye amewahi kuwa religion extremist (yaani alikuwa kiongozi wa dini, call it Sheikh, Mchungaji, Askofu au Padri) atawahi kuongoza nchi hii nadhani atakuwa amepotoka mno na hiyo ni ndoto ya mchana....

Watanzania hapendi extremist yeyote... yanayongolewa kuhusu wanasiasa ambao wamekuwa viongozi wa dini kwenye maisha yao sio kwamba wana makosa yoyote bali it is simply the fact that hakuna uwezekano kwa kiongozi aliwahi kuwa wa dini kuongoza nchi hii... mjadala mwema!

Unaposema kuongoza nchi nahisi una maana kuwa Rais.

Nimewahi kusikia eti Mchaga hawezi kuwa Rais, Msukuma hawezi kuwa Rais, Muhaya hawezi kuwa Rais, Mnyakyusa naye hawezi kuwa Rais. Sababu inayotolewa eti ni makabila makubwa yataleta shida za ukabila. Haya yamesikika sana bila kuandikwa. Nawe sasa umeongeza hayo ya kwako. Hicho ni kiapo gani? Tumeshaondoa makabila makubwa yote, sasa unaondoa viongozi wa kidini wote, baadaye sijui ni nani ataondoka lakini mwisho wa yote unadhani hawa wote watabaki kuwa ni wapiga kura tu!

Ni misingi gani ya kisiasa unayodhani ipo ambayo haitaruhusu hao watu wasishike U-Rais. Nani alijua kwamba Roman na Greek empires itaja anguka? Huko CCM nani alijua kwamba watashuka chini kiasi cha kuwa na katibu mkuu waliye naye sasa hivi? Nani alijua watafikia kutojua hata sera yao ni nini na kuanza kusema ni amani na utulivu. Muulize Wasira kama alitegemea kuwa waziri tena baada ya kuwa mchuuzi wa samaki mitaani.

Tafadhari, angalia muenendo wa nchi ulivyo 'paraganyika' ndo uamini chochote chaweza kutokea. Nahisi kwamba hata mwingereza anaweza rudi kututawala.
 
Hivi Yale makontena ya kura kuna utafiti ulifanyika? Mh Slaa pamoja na kuwa sina mlengo wowote lakini nashauri si kila hoja ukurupuke kujibu maana viongozi Wa dini yenu wakikusifia unakaa kimyaaa wala huuulizi utafiti huwa sipendi kuchangia masuala ya dini lakini hapa imebidi I am not happy with Padri Dr Slaa Statement yenye kamfumo ka dharau kwa mbaaaali
Mbona yale makontena baadhi ya vifurushi vyake vilikamatwa Musoma? Serikali ya CCM ikanyamaza.
 
Back
Top Bottom