Nimeshagundua mapinduzi ya kimaendeleo yatakwamishwa na udini.Ni lazima kuwe na respect between hizi dini mbili hapo bongo.
However swali linakuja; ni kivipi respect hiyo itapatikana?je inaweza kupatikana bila vurugu?
Ni uweli usiopingika kuwa hii issue haiwezi kuwa ignored if we are to move forward...Nitaelezea kwa ufupi ni kwanini...
Inaonekana kuna wakati kila mtu itabidi atangaze dini yake kabla ya kusema chochote in respect to campaingning for elections.
Ile issue ya kupokezana uongozi wa nchi kwa vigezo vya kidini ni wazi inaelekea ukingoni.
Kwasababu kama wananchi hawaletwi tena pamoja kwa kutumia issue za kitaifa ie ufisadi,umasikini nk,then sidhani kama muungano wa wananchi wenye kuzingatia udini utaleta manufaa zaidi ya kuzichapa wenyewe kwa wenyewe.
Nilipotembelea bongo 2007,niligundua Tanzania imebadilika sana,imebadilika kwa misingi ya kidini,yani siasa na dini havitenganiki tena,ukimzungumzia mwanasiasa ambaye ni mkristo mbele ya musilam,basi ni kumtia kichefuchefu musilam huyo,sikuamini.
Na tokea hapo niliamini kuwa ni lazima kuna siku tutazichapa,itatokea kwasababu kama kelele za udini za waislamu zinatokea wakati rais ni muislam,then sijui itakuwa vipi kama rais ni mkristo ama anayegombea ni muslam.
Tunapouliza maswali mbona haya malalamiko hayakuwepo when rais alikuwa mkristo hatupati majibu sahihi.
Shida ya maextremist being from Moslems or Christians,most of the time si kwamba wanataka usawa,bali dini moja iwe juu ya nyingine!No living side by side with peace and harmony and with mutual respect...Kuna wenye kuamini kuwa ni lazima dini moja itawale in every aspect of our lives,na ukiwa dini ya tofauti ni uadui mkubwa sana tu, na maneno mengi ya dhihaka dhidi ya wasio wana dini wao,na ndio maana kuna wenye kuamini udini in everything,na ndani ya watu wenye kufikiri namna hii kwasababu wanahisi all the time kuwa kila uamuzi unazingatia udini,basi watakuwa wenye kulalalmika tu,na ukiwapa nafasi,wao wataendeleza udini kwasababu ndicho wanachokiamini,yani kiongozi asipokuwa wa dini yao,basi wanaamini kuwa maslahi so yako hatarini.However kama wakimpata kiongozi mwenye dini yao ie JK,watataka kuprotect maslahi ya dini yao ambayo wanadhani yako hatarini,kwa hiyo utaweza kuona kuwa kupokezana uongozi kwa misingi ya udini ni kikwazo kikubwa cha maendeleo yetu....Kiongozi atayetuondoa kwenye umasikini huu ni yule ambaye atakuwa hafungwi na maslahi ya kidini.Tatizo ni kwamba kuna wanaoamini kuwa kiongozi wa kutuletea maendeleo ni lazima atokee kwenye dini yao..Na kwa misingi hiyo basi,the only way tutapa kiongozi mwenye kujali issue za wananchi wote kiujumla,ni pale atakapokubalika na wananchi walio wengi kuwa atayatatua matatizo tuliyonayo kama jamii ya watanzania na si kama jamii ya dini hii ama ile.
Yale yaliyokuwa yakifanyika kwa nia nzuri kutoka kwa viongozi wenye busara ie Mwalimu Nyerere kwa kuwashirikisha wananchi wa dini tofauti kwenye uongozi wa nchi ili kuleta umoja wa kitaifa yanaweza kupotea kama umoja huo wa kitaifa ukitafsiriwa vibaya na vibaraka wa kidini wenye nia za kuwatetea viongozi wa kisiasa bila kujali madhara yake kwa jamii.
Kwa mfano wananchi wengi sasa wanunganishwa na vita dhidi ya ufisadi,umasikini,ujinga,njaa na maradhi..Hata hivyo kwa kustaajabia ya Musa ni kwamba viongozi wa dini especially huyu Mufti Simba,anaelekea kuamini kuwa shida hizi si za kitaifa,maybe ni shida za wakristo peke yake,sasa nashangazwa shida za waislam ni zipi?Je hatuwezi kupigania maendeleo ya nchi moja yenye wakristo,waislam,Hindu,wapagani nk?
Unapoona kuna viongozi wenye kushabikia yale yanayotutenganisha,ujue huyo ni wa kuogopwa kuliko kifo chenyewe.
Je hatuwezi kupata maendeleo ya kitaifa bila kuuana kwanza?Tafakari.