Dk Slaa asema Mufti hakufanya utafiti

Dk Slaa asema Mufti hakufanya utafiti

Ww upo nchini kweli ? ww ni mtanzania kweli ? unafuatilia mambo ya Tanzania yanavyoendelea ? kampeni za uchaguzi mkuu ulizifuatilia nyendo zake kwa karibu ?, majibu unayo mwenyewe !


Are you real Genune Brain or EMPTY BRAIN...? I think you are empty brain.
 
Siku zote Nyani haoni kundule....... Lakini all in all Chadema lazima wabadili mtazamo na kuwa wa Kitaifa.
 
GeniusBrain kwa hiyo vyama vimegawanyika kwa mfumo wa dini na hivyo kutokana na mwelekeo wako wa mawazo CCM ni chama cha WAISLAM??brother haya mambo ya kudhania na kufikirika ebu tuyaache hayana faida!!!!
 
Siku zote Nyani haoni kundule....... Lakini all in all Chadema lazima wabadili mtazamo na kuwa wa Kitaifa.

naona mtazamo wa sasa ni sahihi sana,ant-fisadi 100%.
Zitto alileta ujinga akidhania ataogopwa kwa sababu ya dini YAKE.amepewa ukweli tena kama kuondoka aondeke zake asilete ufisadi akitegemea kifua cha dini mjinga yule.
Get out zitto, get lost isemwe cdm ni wakristo tu haina shida hata kidogo kuliko kukuvumilia ukihujumu harakati.
 
Kweli unachosema, kwa nature ya wakristo, kwanza hawana muda wa kujibizana na ni easy taker. kwa sababu tunaujua udhaifu wao, then INAHITAJIKA AKILI kudeal nao, nadhani mtoa hoja amesimamia hapo. Failure to do that mwisho wa siku chama ndio kina loose! na our ultimate goal siyo KUONGEA NI KUIONDOA CCM madarakani. Ni ushauri mzuri na hatutaki CDM ipotee hivi hivi. Siasa ni mchezo mchafu na usitarajie CCM kusifia CDM!!!

Bila kubadili mtazamo basi Chadema Kush nehi
 
Viongozi wa kiislaamu nafikiri hawajui ni nini hasa wanataka, maana ukiyaangalia madai yao kwa undani utaona kuna mambo makuu mawili. Moja ni kuwa Tanzania inaongozwa na mfumo wa Kikristo toka nchi ilipopata uhuru. Suala lao la pili ni kuwa Chadema ni chama cha kikatoliki.

Ukiyaangalia madai haya mawili unashindwa kuelewa ni wapi yanapokutana. Maana kama mfumo kristo upo nchini toka uhuru, je nani wa kulaumwa?? Chadema au CCM??? kama Serikali ya CCM imetoa Bil 90 kwa makanisa je kwa nini wasiandae maandamano dhidi ya CCM??? Kwa nini wailaumu Chedema??? Haya wanasema Chadema ni ya kikatoliki, je CCM ni ya Kiislamu?? NCCR je?? UDP, TLP nazo ni vipi???. Kikubwa nachokiona mimi hapa ni viongozi wa kiislamu kutumiwa na CCm kuwapunguza nguvu Chadema, hakuna cha madai ya mfumo kristo au la. Ninachowaomba viongozi wa Chadema ni kutokata tamaa, bali ongezeni juhudi za kupiga vita ufisadi na muonyeshe kuwa mpo kwa ajili ya watu wote wa TZ.
 
naona mtazamo wa sasa ni sahihi sana,ant-fisadi 100%.
Zitto alileta ujinga akidhania ataogopwa kwa sababu ya dini YAKE.amepewa ukweli tena kama kuondoka aondeke zake asilete ufisadi akitegemea kifua cha dini mjinga yule.
Get out zitto, get lost isemwe cdm ni wakristo tu haina shida hata kidogo kuliko kukuvumilia ukihujumu harakati.

Mtazamo uliopo hapa sio ule tu wa Ukristolization bali na Ukanda na Ukabila. Lazima muwe na mtazamo wa kitaifa nchi nzima.

We ujui kwanini Zitto alikataliwa kugombea uenyekiti na Mbowe?
 
Hivi karibuni Sheikh Mkuu alitoa kauli ya kuwataka waislam wasishiriki maandamano yanayoandaliwa na Chadema. Baada ya siku moja Katibu mkuu wa Chadema Dr. Slaa akajibu kwa kusema Sheikh Mkuu hakufanya utafiti. Kauli ya Slaa ni sahihi lakini haikustahili kutolewa na kiongozi kama yeye katika kipindi hiki ambacho kuna tension kubwa ya udini na mikakati ya makusudi ikifanyika kukihusisha chama hicho na mambo hayo. Slaa kwa kufanya hivyo anataka kukiingiza Chadema na yeye binafsi kwenye mtego wa malumbano ya kidini kitu ambacho kitawanufaisha wapinzani wao CCM. Naishauri Chadema kuwa waangalifu sana na mitego ya aina hiyo na ikiwezekana baadhi ya majibu au matamko yawe yanatolewa na viongozi wa chini kama wenyeviti wa mikoa au viongozi wa jumuia za chama kama BAVICHA ili iwe rahisi kukihami chama endapo kutakuwa na utata kutokana na kauli iliyotolewa. Chadema isione aibu kujifunza kutoka CCM kwa kutoa matamko kupitia jumuia zao kama UVCCM viongozi wa juu wanapotakiwa kuthibitisha husema 'hayo ni maoni yao' hata kama ndio msimamo wa chama. Naomba kuwasilisha.

Acha uwoga mzee, hawa jamaa hawawezi kutufanya tubadili system zetu ili kukizi mapandikizo yao. Dr aliokaa kimya kuhusu kuibiwa kura kila mtu alikuwa analia hapa. Hawa waislamu wakitaka wote kwenda CCM waache waende. tukiwaogopa hawa watachupapa viboko sasa hivi waulize Sudan Kusini
 
Welcome to the world! that is politics now

Mkiendelea hivi CDM will not be just a normal political party , it ( she ) will be a Unique and Fabulous Political Party; the land of democracy and equality...where every member's dream will be fullfilled accordingly.

Big up!

Huna lolote ulilobaki nalo mzee zaidi ya kujishebedua tu
 
Viongozi wa kiislaamu nafikiri hawajui ni nini hasa wanataka, maana ukiyaangalia madai yao kwa undani utaona kuna mambo makuu mawili. Moja ni kuwa Tanzania inaongozwa na mfumo wa Kikristo toka nchi ilipopata uhuru. Suala lao la pili ni kuwa Chadema ni chama cha kikatoliki.

Ukiyaangalia madai haya mawili unashindwa kuelewa ni wapi yanapokutana. Maana kama mfumo kristo upo nchini toka uhuru, je nani wa kulaumwa?? Chadema au CCM??? kama Serikali ya CCM imetoa Bil 90 kwa makanisa je kwa nini wasiandae maandamano dhidi ya CCM??? Kwa nini wailaumu Chedema??? Haya wanasema Chadema ni ya kikatoliki, je CCM ni ya Kiislamu?? NCCR je?? UDP, TLP nazo ni vipi???. Kikubwa nachokiona mimi hapa ni viongozi wa kiislamu kutumiwa na CCm kuwapunguza nguvu Chadema, hakuna cha madai ya mfumo kristo au la. Ninachowaomba viongozi wa Chadema ni kutokata tamaa, bali ongezeni juhudi za kupiga vita ufisadi na muonyeshe kuwa mpo kwa ajili ya watu wote wa TZ.

Acha kujichanganya kama ujachanganyikiwa nakushauri kabla hali yako kuwa mbaya basi wahi kwa Babu ukapate Kikombe.

Hivi ni nani mwenye akili asiyejuwa kuwa Chadema ina Sura ya Kikanda, Kikabila, Kidugu na Kidini? kama hujui hilo basi umelogwa. Ndio maana utaki kuona *******
 
Nadhani imefika wakati kukaa na viongozi wa dini ya kiislam kuwasikiliza kwanini chadema imekuwa kero kwao? kwanini kila kukicha Chadema imekuwa ikisemwa vibaya na viongozi wa dini hiyo. inawezekana hamusikii kwa kuwa hayatolewi ktk vyombo vya habari visivyo vya dini. lkn kila kukicha tuhuma za waumini wa kiislam inashika kasi, kila pembe ya tz .
hii kama taachwa iendelee na kutokaa nao meza kuangalia sorce au kutumia vyombo vyao vya habari kuwasiliana nao itaathiri kwa kiasi kikubwa mustkabali wa chadema kisiasa. Inawezekana wanatumiwa kisiasa na wapinzani wa chadema, lkn ni wazi chadema kama chama kinachotaka kujaribu kujikosha ktk jamii ya kitanzania hakuna budi kutafuta njia mbadala ya kuondoa dhana hii. njia pekee ni kukaa na viongozi hao, kuwasikiliza malalamiko yao na pengine kaungalia nini source: au kutumia redio zao kuwaeleza uzuri wa chadema kwao na kuwaondoshea wasiwasi watz hao

Hakuna kitu bora zaidi ya mazungumzo na kila kona duniani leo pale pande mbili wanapokaa na kutatua tatizo lao kwa nia njema basi matokeo huwa mazuri!
Mfano Kenya ilipoingia ktk mgogoro mkubwa wa Kikabila na Kisiasa viongozi waliamua kukaa chini na kuzungumza iwe ni kwa nia njema ama ni kwa kulazimishwa na jumuia ya kimataifa lakini walikaa pamoja na kumaliza mgogoro ule!
Zanzibar walipokuwa na mgogoro wa Kisiasa ingawaje miaka ya nyuma walishakaa mara nyingi kuzungumza bila mafanikio lakini walipoamua kuutatua kwa nia njema tumeona mafanikio leo Wa ZAnzibar wote wamekuwa ndugu tena na kueka nyuma tofauti za Kisiasa! mifano iko mingi!

Hapa kwetu TZ tatizo kubwa lipo ni la UDINI ingawaje Dini zingine zinakanusha kuwa hakuna udini! Waislamu wamethibitisha kwa maandishi, kongomano, vitabu, Radio, Mikutano ya hadhara, Mihadhara na hata kumkabidhi nyaraka za siri kuhusu Udini aliyekuwa Rais wa Awamu ya Kwanza, Mkapa, Mwinyi na hata KIKWETE! lakini mpaka sasa hakuna hatua zilizochukuliwa!

Kinyume chake tumeona Serikali ya Awamu ya Kwanza kuchukua hatua za Makusudi kabisa kuwasaidia makabila ya Wabarbaig wapate elimu ili wanufaike na matunda ya Uhuru!

Waislamu ambao wanalalamika na kuthibitisha hakuna anaewasikiza na tumeshuhudia mara kadhaa Serikali ikiwajibu kwa Kuwakamata Viongozi wao na hata kutumia Polisi kutawanya Maandamano yao na hata kuwaua! rejea kitabu cha Profesa H.NJOZI Pictures - Mwembechai Killings and The Political Future of Tanzania

Chadema kama wanania nzuri na Taifa hili na nia yao ni WA TZ wote wafaidike na matunda ya Uhuru bila kujali dini, rangi, kabila au ukanda hawana budi kuthibitisha hilo kwa vitendo na wala mazungumzo na Waislamu hayatazaa Matunda ikiwa nia ya CHADEMA sio nzuri!
nasema hivyo kwa sababu historia huwa inajirudia kwani Wakati TANGANYIKA inapata uhuru Wasomi wengi walikuwa Wakristo na Waislamu hawakwenda shule ambazo nyingi zilikuwa za Wakoloni ambao walikuwa MISSIONS!

Viongozi wa Kiislamu waliliona hilo na kumkabili Julius Nyerere ili Uhuru ukipatikana Waislamu nao wawezeshwe ili kupata fursa sawa! Nyerere alikubali hilo ktk meza ya Mazungumzo lakini alipokuwa Ikulu alifanya kinyume na makubaliano kwa kauli yake mwenyewe alisema haya:
"I have established in TANU a department of political education and I have put a Lutheran Minister in charge. He was not a great politician, but I selected him because of his balance, his gentleness and his strong solid faith..."

Gonga hapa kupata maelezo yote kuhusu Asili ya UDINI TZ!!! ISLAM AND POLITICS IN TANZANIA

Mimi si msemaji wa Waislamu ila nadhani hawako Tayari kudanganywa kama Watoto wadogo! bila shaka wako tayari kuzungumza na chama chochote cha kisiasa lakini kwa masharti yafuatayo wengine wanaweza kuongeza:

1) Wanataka haki na usawa ktk nyanja zote za Maendeleo ya Kisiasa, Kijamii nk.!
2) Waislamu hawataki upendeleo bali usawa!
3) Waislamu wanataka Katiba mpya itakayowashirikisha moja kwa moja!

Kama CHADEMA wako tayari kukaa meza moja na viongozi wa Waislamu basi ni hatua moja kubwa kwani Waislamu ni sehemu ya Wapiga kura waliowengi kama walivyo Wakristo lakini ushauri wangu kwa Waislamu ni kuwa ikiwa CDM watakubali kukaa meza moja na Waislamu basi kuwe na mkataba maalum ambao ni matakwa ya Waislamu na ikiwa CDM watafanikiwa kuongoza TZ basi mkataba huo ni lazima utekelezwe!

Hata huko Amerika kawaida Vyama vya Kisiasa huzungumza na makundi tofauti tofauti kama vile Wayahudi na kura zao huamua nani awe Rais!
"Tanzania haina DINI" kauli hii imepitwa na wakati na sasa umefika wakati wa kuweka kila kitu ktk meza ya mazungumzo vinginevyo.......
 
Nadhani imefika wakati kukaa na viongozi wa dini ya kiislam kuwasikiliza kwanini chadema imekuwa kero kwao? kwanini kila kukicha Chadema imekuwa ikisemwa vibaya na viongozi wa dini hiyo. inawezekana hamusikii kwa kuwa hayatolewi ktk vyombo vya habari visivyo vya dini. lkn kila kukicha tuhuma za waumini wa kiislam inashika kasi, kila pembe ya tz .
hii kama taachwa iendelee na kutokaa nao meza kuangalia sorce au kutumia vyombo vyao vya habari kuwasiliana nao itaathiri kwa kiasi kikubwa mustkabali wa chadema kisiasa. Inawezekana wanatumiwa kisiasa na wapinzani wa chadema, lkn ni wazi chadema kama chama kinachotaka kujaribu kujikosha ktk jamii ya kitanzania hakuna budi kutafuta njia mbadala ya kuondoa dhana hii. njia pekee ni kukaa na viongozi hao, kuwasikiliza malalamiko yao na pengine kaungalia nini source: au kutumia redio zao kuwaeleza uzuri wa chadema kwao na kuwaondoshea wasiwasi watz hao

Is very simple. Ni kuwasikiliza na kukili yote hadharani kuwa ni kweli ni chama kinachopata support kubwa ya kanisa lakini sasa tunajirekebisha ili kiwe cha wananchi wote bila kuzingatia hayo na kuwa tunataka usawa na kuahidi kutekereza yote wayatakayo mfano Mahakama ya kadhi, OIC, mgawanyiko wa madaraka kama vile ilivyo nigeria, etc
 
Bila kubadili mtazamo basi Chadema Kush nehi

Wewe wasema! ila Sio mimi wala walio wengi tu, najiandaa kufungua office ya Chadema wilayani kwangu na nitaigharamia mimi mwenyewe, Upo hapo ndugu.
 
Huu ndio ujinga ninao upinga kila siku. Hapo kwenye red unataka watu waamini kama Slaa ana PH D ya kawaida! Ya kwake ni ya magumashi aliyoipata akiwa na certificate tu.A chane ujinga! Kwa JCD hawezi kuwa mchambuzi kama unavyotaka! Labda kunywesha watu divai anajua cannon zake

+++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
EDUCATION
International Eye H. Centre Certificate in Eye Health 1993-1993

TransWorld Tutorial College, London Certificate in Management 1985-1985

St. Thomas Aquinas University Advanced Diploma in Rural Development 1980-1981

St. Urban University, Rome PhD (JCD) Law 1977-1981 [Doctor of Canon Law (Latin: Juris Canonici Doctor or JCD)]

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

Kwa kukusaidia tu kama unataka kumjuwa Dr Slaa CV yake ni hii hapa, hebu tuwekee na CV ya mufti simba hapa tuone.
View attachment 25823
 
Is very simple. Ni kuwasikiliza na kukili yote hadharani kuwa ni kweli ni chama kinachopata support kubwa ya kanisa lakini sasa tunajirekebisha ili kiwe cha wananchi wote bila kuzingatia hayo na kuwa tunataka usawa na kuahidi kutekereza yote wayatakayo mfano Mahakama ya kadhi, OIC, mgawanyiko wa madaraka kama vile ilivyo nigeria, etc

Hapana, masharti haya ni magumu ila cha muhimu hapa ni maridhiano (COMPROMISE)!! kila upande uangalie maslahi ya nchi kwanza! CHADEMA waje ktk mazungumzo kama chama cha Kisiasa na upande wa Waislamu waingie kama Waislamu na kama kama vyama vya Siasa vitaona kuwaridhisha Waislamu au Dini nyingine ni vigumu basi ni vyema Katiba mpya iruhusu vyama vya Kidini ili walinde maslahi ya Waumini wao ktk Bunge!!!!
 
Ww upo nchini kweli ? ww ni mtanzania kweli ? unafuatilia mambo ya Tanzania yanavyoendelea ? kampeni za uchaguzi mkuu ulizifuatilia nyendo zake kwa karibu ?, majibu unayo mwenyewe !

Acha Udini!. nani kakwambia kwamba wakristo hapa nchini wote wako chini ya Pengo, kwa taarifa yako kuna RC, Lutherani, Anglican, Moravian, Sabato, Walokole nk, sasa unaposema Pengo ndio kamtuma Dr wa Kweli Slaa unamaanisha nini?, sasa kwa Taaarifa yenu nyie mnaoeneza Udini kwa niaba ya CCM na Mafisadi Mnapoteza Muda wenu, Sie Wana wa Tanganyika Wakristo kwa Waislamu wenye upeo mkubwa wa Kufikiri na Kuchambua hali halisi ya siasa za nchi hii, Tumesha mkubali Dr Phd Slaa na Chama ndio Chadema, sasa kwa kuwa nyie mpo kazini endeleeni na ufinyu wenu wa mawazo?,

“NAWAHAKIKISHIA NYIE NI FUNGU LA KUKOSA” endeleeni na mchezo wenu mchafu, na Dr Phd Slaa tunamshauri endelee kujibu Hoja ZOZOTE pale atakapoona ni kwa manufaa ya Chama, na kwa manufaa ya jamii yetu sote Wakristu , Waislamu, Wahindu, Wapagani nk.
Mapambano ndio yameanza.
Nawashauri wapenda Maendeleo ya kweli kwa Nchi hii, pelekeni watoto shule bora na sio bora shule ili waelimike na tuwafundishe mageuzi kuanzia nyumbani.
 
Umenena mkuu,nami uwa mara nyingi napenda viongozi wa cdm wawe makini katika kujibu,si kila kitu lazima wakijabu mfano malumbano yanayoendelea sasa ya kuichafua chadema naomba wao wasijibu huo ujinga kwani ni mkakati wa kuonyesha kuwa hawana jipya,wao wajikite kuonyesha ukweli kwa wananchi uozo wa serikali tu,vyama vingine vinahitaji umaarufu tu kwa kujibizana na cdm wakati huo huo kujipendekeza ccm.
Did you find this post helpful? |
icon1.png
Re: Chadema: kwa hili mlitaka kukosea



quote_icon.png
Originally Posted by Quinine
Hivi karibuni Sheikh Mkuu alitoa kauli ya kuwataka waislam wasishiriki maandamano yanayoandaliwa na Chadema. Baada ya siku moja Katibu mkuu wa Chadema Dr. Slaa akajibu kwa kusema Sheikh Mkuu hakufanya utafiti. Kauli ya Slaa ni sahihi lakini haikustahili kutolewa na kiongozi kama yeye katika kipindi hiki ambacho kuna tension kubwa ya udini na mikakati ya makusudi ikifanyika kukihusisha chama hicho na mambo hayo. Slaa kwa kufanya hivyo anataka kukiingiza Chadema na yeye binafsi kwenye mtego wa malumbano ya kidini kitu ambacho kitawanufaisha wapinzani wao CCM. Naishauri Chadema kuwa waangalifu sana na mitego ya aina hiyo na ikiwezekana baadhi ya majibu au matamko yawe yanatolewa na viongozi wa chini kama wenyeviti wa mikoa au viongozi wa jumuia za chama kama BAVICHA ili iwe rahisi kukihami chama endapo kutakuwa na utata kutokana na kauli iliyotolewa. Chadema isione aibu kujifunza kutoka CCM kwa kutoa matamko kupitia jumuia zao kama UVCCM viongozi wa juu wanapotakiwa kuthibitisha husema 'hayo ni maoni yao' hata kama ndio msimamo wa chama. Naomba kuwasilisha.



Umenena mkuu,nami uwa mara nyingi napenda viongozi wa cdm wawe makini katika kujibu,si kila kitu lazima wakijabu mfano malumbano yanayoendelea sasa ya kuichafua chadema naomba wao wasijibu huo ujinga kwani ni mkakati wa kuonyesha kuwa hawana jipya,wao wajikite kuonyesha ukweli kwa wananchi uozo wa serikali tu,vyama vingine vinahitaji umaarufu tu kwa kujibizana na cdm wakati huo huo kujipendekeza ccm.
Wakuu mmesema kweli, kwa watu wenye busara si lazima kujibu kila kitu. Weka mkakati kuimalisha chama, malumbano waachie waganga njaa. Wakuu mkitulia na kufanya kweli hata maadui watawapenda tuu, cos in politics no permanent enemy!!!!!!! Aluta Continua CDM!!!!!!!!!


 
hapo umepotoka cdm haiongozi na wakatoliki wala kauli za wakatoliki. hiyo ni chuki tu dhidi yao. kwani wakatoliki ndio wanaochukia ufisadi peke yao? vp kuhusu ccm na cuf? mimi sikuelewi una ushabiki wa kidini. ukweli ni kwamba waislam wamezidi kutoa kauli dhidi ya cdm lkn msingi unaanzia serikalini na cuf yenyewe kuna kitu hapa.
 
Back
Top Bottom