Dk Slaa asema Mufti hakufanya utafiti

Dk Slaa asema Mufti hakufanya utafiti

Hilo halitawezekana na viongozi wa kiislamu hawatakubali kwani CDM wao wenyewe waliisha jipambanua wako upande gani wa kidini. Sasa itaonekana kama wanawaletea mzaha mzaha hivi. Na hili liweke utaniambia siku sijazo, wajaribu tu utaona mkuu


Wewe na waliokutuma tunajua nia zenu, sasa kawaambie kuwa hamtaweza kufanikiwa kamwe.
 
Sioni ambacho Chadema wanatakiwa kujifunza toka CCM, Chadema hawawezi kuwa na wasemaji wengi wa Chama na alichoongea Dr Slaa ni sawa na wala hakina ubaya, so Chadema msiige mabo ya CCM ambapo sasa hakuna msemaji wa Chama kila mtu anaropoka tu.
 
Hivi karibuni Sheikh Mkuu alitoa kauli ya kuwataka waislam wasishiriki maandamano yanayoandaliwa na Chadema. Baada ya siku moja Katibu mkuu wa Chadema Dr. Slaa akajibu kwa kusema Sheikh Mkuu hakufanya utafiti. Kauli ya Slaa ni sahihi lakini haikustahili kutolewa na kiongozi kama yeye katika kipindi hiki ambacho kuna tension kubwa ya udini na mikakati ya makusudi ikifanyika kukihusisha chama hicho na mambo hayo. Slaa kwa kufanya hivyo anataka kukiingiza Chadema na yeye binafsi kwenye mtego wa malumbano ya kidini kitu ambacho kitawanufaisha wapinzani wao CCM. Naishauri Chadema kuwa waangalifu sana na mitego ya aina hiyo na ikiwezekana baadhi ya majibu au matamko yawe yanatolewa na viongozi wa chini kama wenyeviti wa mikoa au viongozi wa jumuia za chama kama BAVICHA ili iwe rahisi kukihami chama endapo kutakuwa na utata kutokana na kauli iliyotolewa. Chadema isione aibu kujifunza kutoka CCM kwa kutoa matamko kupitia jumuia zao kama UVCCM viongozi wa juu wanapotakiwa kuthibitisha husema 'hayo ni maoni yao' hata kama ndio msimamo wa chama. Naomba kuwasilisha.


Mkuu naheshimu mawazo yako, lakini mtu yeyote anaesimamia ukweli hawezi kuhofia kusema ukweli eti kisa awaridhishe akina Mufti, mimi nakupinga kwa 500% Dr Slaa ni PHD holder na anajuwa nini maana ya sekretarieti, ndio maana akasema mufti akufanya utafiti, kama angefanya utafiti angejuwa CHADEMA inasimamia nini, lakini mimi binafsi nashindwa kumlaumu mufti kwa sababu mufti elimu yake ni darasa la saba kwa hiyo hawezi kuwa na upeo mkubwa wa kuelewa mambo ya administration ya nchi.
 
CCM wanacheza mchezo wa kitoto kweli. Yaani hakuna haja ya CDM kuwajibu waislamu kwa uoga. CCM itajimaliza yenyewe.
 
Najua mtatukana na kutumia maneno mazito ya kila aina. But let me say it again.

"Hakuna chama kitakacho ungozwa na Sheikh, Padri, Mchungaji, Askofu kitachukua madaraka ya nchi hii", Be carefully guys.
 
Mimi sifikirii kukaa pamoja na waislam itasaidia bali ni vizuri mkabadili mtazamo wenu kabisa kutoka kwenye UKANDA, UKABILA na UDINI na kukifanya Chama chenu kiwe cha KITAIFA zaidi.
 
Ww ndio sasa una mapepo, kwani ni ukweli uko wazi kuwa kampeni za uchaguzi mkuu CHADEMA walitumia sana makanisa kufanya kampeni, sasa kama ww huishi Tanzania huwezi kujua, na nina wasiwasi huo. Mambo ya wakatoliki Sumbawanga unayajua ww ?


humo makanisani uliingia ukasikia wakifanya kampeni? unajua chanzo cha sumbawanga au unadandia treni kwa mbele?
 
CDM ina wafuasi na mashabiki wengi sana waislamu, mbao kauli zisizo na maana za viongozi wao wa dini hazitawaondolea imani yao kwa CDM. So, CDM iwajibu hao viongozi, tena kwa kauli kali zaidi ya hizo.
 
dogo punguza pumba hayo mawazo aliyo toa mh ni ya msingi na viongozi kama viongozi wanatakiwa kuyafata....waislam bado ni kundi muhimu sana ktk ustawi wa cdm,kauli ya kudai waachwe kama walivyo ni ya kitoto sana na haina mashiko hata kidogo.mi naamini kabisa mtandao huu ni wa watu walio makini sana na wanapenda maendeleo ya nchi hii kwa watu msio na upeo naomba muwe makini ktk ku post pumba zenu....mnaweza ligawa taifa ili.

By dizle

from udom




unapoandika from udom unamaana gani? Kunawalakini hapa
 
Mkuu naheshimu mawazo yako, lakini mtu yeyote anaesimamia ukweli hawezi kuhofia kusema ukweli eti kisa awaridhishe akina Mufti, mimi nakupinga kwa 500% Dr Slaa ni PHD holder na anajuwa nini maana ya sekretarieti, ndio maana akasema mufti akufanya utafiti, kama angefanya utafiti angejuwa CHADEMA inasimamia nini, lakini mimi binafsi nashindwa kumlaumu mufti kwa sababu mufti elimu yake ni darasa la saba kwa hiyo hawezi kuwa na upeo mkubwa wa kuelewa mambo ya administration ya nchi.
Tuko pamoja mkuu hata mimi sipingi kauli ya Slaa yuko sahihi kabisa ninachoona kinaweza kuleta madhara ni timing ya kauli.
 
CDM ina wafuasi na mashabiki wengi sana waislamu, mbao kauli zisizo na maana za viongozi wao wa dini hazitawaondolea imani yao kwa CDM. So, CDM iwajibu hao viongozi, tena kwa kauli kali zaidi ya hizo.
Mkuu huoni kuendelea kuwajibu ni kuingia kwenye mtego wa CCM na vibaraka wake?
 
sa umeongea ukwel gn? kusema slaa ka2mwa na pengo ni ukwel? hata moyo wako unajua ulichoandika co kweli!

Ww upo nchini kweli ? ww ni mtanzania kweli ? unafuatilia mambo ya Tanzania yanavyoendelea ? kampeni za uchaguzi mkuu ulizifuatilia nyendo zake kwa karibu ?, majibu unayo mwenyewe !
 
siku zote usiogope kuongea UKWELI,hata kama watu 1000 wakipinga utaendelea kuwa ukweli.Dr.Slaa hajakosea.
 
Inashangaza sana jinsi usemi wa 'jambo usilolijua ni kama usiku wa giza'
Matamshi mengine kamaya huyu mwanzilishi wa hii topic ni wazi kuwa hajui ubaya kuendeleza udini, na kuwaza kwa mitazamo ya kidini.
Hapa tanzania lazima mtu atakaechauliwa atakuwa wa dini moja au nyingine.
Kwa hiyo nadhani ni bora tujifunze kufikiri juu muonekano wa nje wa dini ya mtu.
Hatukatai kikwete ni muislamu 'safi',
hatukatai slaa ni mkrisu 'safi', ila vigezo hivi kamwe visiwe kigezo cha kumhukumu mtu.
Humu kwny blog, tunawatu amabo ni wakritu/waismau wengi ambao tunawatazama hawa viongozi wa vyama, na hasa rais tuliemchagua kwa muonekano wake kwa raia wote, si kwa dini yake.
inauma sana pale unapodiminish utendaji wa mtu simply kwa kuwa ni wa dini fulani, au unapofunika maovu yake simply kwa kuwa ni wa dini yako, utakuwa huitendei haki imani yako, na wewe sio muumini wa ukweli.

Bahati mbaya, wengi tumenuaika kwa namna moja au nyingine, na uongozi mbovu, kuanza kuitazama HAKI machoni tunaogopa.
Ni haki tuogope, lakini ni bora tujitoe kuipigania haki hii, japo tutatolewa sadaka, kwa Tanzania bora, italeta maisha bora kwa watoto wetu.
tutakuwa mashujaa wa kipindi chetu.
Ni bora tupiate haki, ili amani ya ukweli ipatikane,
haki bila uwazi haitapatikana,
uwazi kwenye kazi za uongozi,
ni viongozi wachache wanaoonekana kuwa wamejitoa kwa ajili ya kupigania haki ya mtanzania, tuwasaidie hao tusiwanyanyase kwa ajili ya dini zao au za wazazi wao.
alternative ni mbaya zaidi.
 
Hv ni vigezo gani waislamu wanatumia kumchagua mufti wao? Je ni elimu ya masuala ya kurwani au busara? au kuna vigezo vingine vya siri?
 
Dr w slaa na cdm wako makini.. Hamna walichokosea hapo, hata kama wananchi wengi wana uelewa kidogo na siasa za majitaka zinazoendeshwa na ccm bado cdm wanatakiwa wasimamie ukweli bila kujali nani atawaelewaje,, that iz true politics sio siasa za kuhonga wapuuzi wachache waongee kinyume kwa maslahi ya wachache which i call stupid and cheap politics za kina YM!
 
Kwa kipindi kirefu sana nilikuwa napinga dhana ya kuwa BAKWATA ni idara tanzu ya TISS, lakini kwa mambo yanayoendelea sasa sina shaka tena na dhana hiyo, ni kweli BAKWATA ni kiengo cha UWT. Lakini pia ni ukweli usiofichika kuwa Waislamu wengi tu wenye upeo wa kufikri wanakerwa na jinsi CCM inavyotumia Uisalamu na Waislamu kufikia malengo yao ya kisiasa, na kwa mtindo huu naliona kaburi la CCM linavyokuja kwa kasi.Ule utabiri wa kuwa CCM itamfia KIKWETE mikononi unaanza kutimia, aliasisi sera ya udini kuibeba CCM lakini ni sera hiyo hiyo itakayoimaliza CCM, kwani waislamu siyo mbumbumbu kama mafisadi wanvyowachukulia.
 
Back
Top Bottom