Dk. Slaa aajiriwa supermarket

Dk. Slaa aajiriwa supermarket

Watu wengi wanapiga kelele tu, lakini hawajui hata COSTCO ni mdudu gani. Hivi kweli kwa wanaoifahamu COSTCO wanaweza ilinganisha na NAKUMAT, Imalaseko na viduka vya kibongo kweli? Unaposema COSTCO unazungumzia the largest American membership-only warehouse club. It is the second largest retailer in the world after Walmart. Yaani kama ingekuwa ijengwe pale Mlimani City, inakusanya kale kajengo kote na eneo lote linakuwa na duka moja - hapa nazungumzia mpaka vile vibanda/nyumba zilizopangishwa. Si kwamba wanauza bidhaa za nyumbani tu, huu ni udhalilisha kama si upotoshaji usio na maana, wanauza mpaka mafuta ya magari - Petrol Filling Stations, matairi ya magari na vifaa mbalimbali vikiwemo vya ujenzi, huduma za upimaji wa macho na miwani pia huduma za masikio - audiology dept. Kuna wafanyibiashara wengi yakiwemo mahoteli yanajiendesha kwa kutegemea bidhaa zinazouzwa COSTCO. Kifupi wanakwenda COSTCO kufunga mzigo wa kuuza kwenye maduka na mahoteli yao.

Kuhusu mishahara, wanalipa vizuri kuliko supermarkets zozote unazozijua humu duniani. Hii ni policy yao uliza mfanyakazi yeyote aliye kwenye Retail or Wholesale industry atakwambia juu ya COSTCO iwe ni USA, CANADA, UK na hata Japan. Kwa hiyo kwa Dr Slaa kufanya kazi huko, si kwamba ka-lost, hapana ni maamuzi yake kuamua kuishi kwa namna hiyo. Nina uhakika kwa ngazi aliyopo Sales Advisor, atakuwa analipwa hela nzuri kwa fortnightly - kila wiki mbili kuliko hata Full-time lecturer wa Tanzania. Na kwa usawa huu wa Magufuli, wabongo wengi tunaisoma namba. Pia pamoja na mapungufu yake ya kisiasa, nina uhakika huko aliko atakuwa anakula good times kuliko wabongo wengi na viongozi wa kisiasa waliobaki Bongo. Job security nzuri, social services za uhakika, hakuna mizingwe ya mshahara, na bado usafiri na mazagi zagi mengine ya kumwaga. Mwacheni Mzee wa watu amalizie siku zake kwa amani huko aliko!

View attachment 628021
COSTCO Gasoline station

View attachment 628018

View attachment 628019

Kwa sifa ulizozianisha kuhusu hiyo supermarket, na kwa mshahara wanaomlipa mzee wetu, kwa kweli wanamnyonya. Hao wamiliki ni wanyonyaji kuliko maelezo, yaani supermarket ya pili kwa ukubwa huko ulikotaja halafu wamlipe mshahara sawa na milioni 11 za Kitanzania? Dah...heri mzee sasa afikirie kurudi nyumbani.
 
Kwa sifa ulizozianisha kuhusu hiyo supermarket, na kwa mshahara wanaomlipa mzee wetu, kwa kweli wanamnyonya. Hao wamiliki ni wanyonyaji kuliko maelezo, yaani supermarket ya pili kwa ukubwa huko ulikotaja halafu wamlipe mshahara sawa na milioni 11 za Kitanzania? Dah...heri mzee sasa afikirie kurudi nyumbani.

Alipokuwa katibu mkuu wa CHADEMA alikuwa analipwa kiasi gani?
 
Duh, kama amelazimika kufanya kazi Supermarket basi Mbowe anatisha.
 
As far as I know, Dr. was paid around 8 Million (Tshs)....not so sure.


Kama hivi ndivyo, basi he is better off at COSTCO in Canada kuliko CHADEMA. Ni kazi ambayo haina stress kwa sana kulinganisha na Ukatibu Mkuu, pia hela yake ina uhakika sio ubabaishaji wa kibongo. On top of that kama akiendelea nao kwa ninavyoifahamu COSTCO CANADA uwezekano wa kupanda ngazi ni mkubwa sana hasa ukionesha kuwa uko competent katika utekelezaji wa majukumu yako. Na kadri unavyopanda ndivyo na mshiko unavyoongezeka!
 
Kama Sikosei Atakuwa Analipwa 9milion Mpaka 11milion Na Ukiunganisha Nahyo Kazi Nygne Anazofanya Atakuwa Anapokea More Than 2omilion Kitu Ambacho Kwa Chadema Hapati,cdm Walikuwa Wanamlipa 6milion Na Stress Juu Plus Matusi,ni Bora Mara Alfukumi Kuwa Canada Kuliko Kuishi Na Wanasiasa Na Wanaharakati Uchwara
 
Kama Sikosei Atakuwa Analipwa 9milion Mpaka 11milion Na Ukiunganisha Nahyo Kazi Nygne Anazofanya Atakuwa Anapokea More Than 2omilion Kitu Ambacho Kwa Chadema Hapati,cdm Walikuwa Wanamlipa 6milion Na Stress Juu Plus Matusi,ni Bora Mara Alfukumi Kuwa Canada Kuliko Kuishi Na Wanasiasa Na Wanaharakati Uchwara


Ha ha ha ha ha ha ha..lakini wajua milioni 20 kwa nchi za Ulaya ni hela ya kawaida sana!
 
Najua uzi na hilo gazeti viliandikwa kama chokonozi flan hivi. Ili watu wamhurumie waseme arudi tu nyumbani. CDM, jiandaeni, ufipa kuna siku mtakuta kufuli jingine juu ya hilo lenu na kuwa Katibu mkuu karudi kazini baada ya likizo bila malipo. Je, mlishafanya kikao cha kumuondoa chamani?
Siku mtakapoitisha kikao, hadi atoke mjumbe kule Ngara na Tukuyu mwakaleli kuja Darisalama kwenye kikao, tiyari atakuwa kishaingia na backup kubwa ya dola kumlinda akiwa ofisini.
Poleni CDM majeruhi tiyari,
 
Tz alikuwa anakula mihogo nadhani kwa jinsi vyuma vilivyokaza kwa wadhamani wake wa hapa nchini, basi huko alikuwa anakula makombo.
Lakini hongera yake, walau mkono uende kinywani. Kazi kazi.

Dah nimecheka
 
Watanzania watu wa ajabu saana,kweli leo hii kuna mtu anadiriki kumkashifu Dr Slaa ama kweli bongo,dr slaa ndio kawaamusha watanzania,kajenga upinzani kwa nguvu zake zote,kaona mambo hayaendi sawa kaamua kufanya maisha mengine nalo ni kosa?kaamua kuachana na siasa,hata kama ni wewe Slaa ndio kazunguka nchi nzima kusema lowasa fisadi,leo hii tena ndio yuko mgombea wa chadema,hata mimi sikupenda kabisa,hapo sisi chadema tukubali tulikosea.
 
Kwa vyovyote vile Dr.Slaa huenda atakuwa ameshinikizwa na mkewe kufanya hiyo kazi. Yule mkewe sio wa mchezo mchezo aisee, sijui kamlisha nini yule mzee?

Na unaweza kushangaa mkewe ametulia zake ndani bila kazi huku akitafuna mkwanja wa jasho la Dr.Slaa bila huruma.


Mshumbusi Mungu anakuona aisee!

Nimecheka kwa sauti..
 
Asiyefanya kazi na asile chakula!
 
Wekeni picha ya ka babu tukaone kanavyomenyeka na kubeba vyombo!!
 
Waswahili tuna msemo wetu wa..'kazi ni kazi, ilimradi mkono uende kinywani'; yaani haitakiwi mtu kuchagua kazi, kikubwa kazi husika iwe halali na iwe inakulipa.

Kama kichwa habari kinavyosema kuwa, Dk. Wilbroad Slaa aliyewahi kuwa katibu mkuu wa CHADEMA amepewa ajira ya afisa mauzo wa supermarket huko Canada, je, hii tuite kupanda na kuangakuka kisiasa kwa Dk. Slaa?

Itakumbukwa pia, Dk. Slaa aliwahi kuwa Rais wa bodi ya hospitali ya CCBRT, ya jijini Dar Es Salaam.


=======

ALIYEKUWA Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa, ameajiriwa katika duka kubwa la bidhaa za majumbani (Supermarket) la Costco lililopo Oakville, Toronto nchini Canada, imebainika.

Dk. Slaa, kwa sasa anaishi nchini Canada alikokwenda kwa masomo, tangu alipotangaza kuachana na siasa Septemba 1, mwaka 2105.

Kwa muda wa wiki kadhaa, ziliibuka taarifa katika mitandao ya kijamii kuwa mbunge huyo wa zamani wa Karatu, amemaliza masomo yake na sasa anafanya kazi katika moja ya maduka makubwa ya bidhaa mbalimbali nchini humo – Supermarket.

Supermarket ya Costco anayofanya kazi Dk. Slaa akihudumu kama Mshauri wa Mauzo (Sales Advisor), akilipwa Dola za Marekani 10 (zaidi ya Sh 20,000) kwa saa, ina hadhi kama Nakumat, Shopers, Imalaseko, Game na maduka mengine makubwa nchini.

Akizungumza na MTANZANIA jana kwa simu katika mahojiano maalumu, Dk. Slaa alisema kuwa kwa sasa anaishi kwa kazi ya mikono yake kwani ili aweze kuishi anahitaji kufanya kazi zaidi ya mbili hadi nne kwa siku.

“Niko, ninafuatilia matukio Mutukula (ziara ya Rais Dk. John Magufuli jana). Siku zote nimesema ninaishi kwa jasho na kazi ya mikono yangu. Canada ili uishi vizuri, unahitaji kazi zaidi ya mbili au tatu mpaka nne. Hayo nimeweka wazi, sijui jambo jipya kama mtu alikuwa hafuatilii.

“Mimi ninafanya kazi PWD/CDS/COSTCO kama Sales Advisor, baada ya kumaliza masomo yangu hasa Interpersonal Communication. Costco ninakofanya kazi ina members (wanachama) 10,000. Kwa siku wanaofika Warehouse ni kati ya 5,000 hadi 7,000,” alisema Dk. Slaa.

Mbali na hilo, alisema kuwa pia anafanya kazi nyingine ikiwa ni pamoja na ushauri (Consultancy).

Alisema kila mara amekuwa akiwataka Watanzania na vijana wafanye kazi kwani fedha haziji kwa kukesha kwenye mtandao wala propaganda.

“Canada ni kazi, Profesa wa Chuo Kikuu anafanya kazi ya Uber. Sijui kama Uber inafahamika Tanzania, ni dereva Taxi kwa kutumia gari lake binafsi. Ofisa wa Serikali usiku anaosha vyombo hotelini.

“Ndiyo maana familia ina magari mawili au zaidi, TV, nyumba ya kisasa, chakula cha kisasa. Wanatekeleza sera ya ‘Hapa Kazi Tu’ kwa matendo. Nadhani nimekupa taarifa za kutosha ikiwa ni pamoja na kujibu propaganda kuwa nilihongwa mabilioni.

“Niwahakikishie tena, wakati wa kusoma nilikuwa na scholarship, tangu nianze kazi ninaishi kwa jasho la mikono yangu. Mke wangu yeye ameingia Chuo Kikuu cha York baada ya Diploma yake na bado anapata scholarship.

“Ndiyo maana tuna uwezo wa kuwa na magari mawili aina ya Jeep na Dodge, ukifanya kazi utaishi vizuri. Hii ni pamoja na kugharamiwa bima ya afya (Health Insurance), watoto kusomeshwa na Serikali ya Canada,” alisema Dk. Slaa.

Mei mwaka huu, Dk. Slaa, alisema hana mpango wa kurudi nchini kwa sasa na kwamba taarifa zinazosambazwa kwenye mitandao ya kijamii hazina ukweli wowote.

Akizungumza na gazeti hili kwa simu wakati huo, alisema pamoja na kumaliza masomo yake, anatafakari uamuzi wa kurudi nchini ama la.

Hata hivyo, Dk. Slaa ambaye alipata kuwa Mbunge wa Karatu kwa vipindi vitatu mfululizo, hakuweza kuainisha mazingira yaliyomfanya aondoke nchini na kwenda kuishi ughaibuni.

Septemba, 2015 wakati wa Uchaguzi Mkuu, Dk. Slaa alijiweka kando na siasa, kwa kile alichokieleza kutofautiana na viongozi wenzake ndani ya chama chake juu ya masharti ya kumpokea aliyekuwa mgombea urais wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa.

“Sina tabia ya kuyumbishwaa, sina chuki na mtu yeyote, sipendi siasa za udanganyifu na propaganda. Nimeachana na siasa tangu Julai 28, 2015, baada ya kuona misingi ya chama nilichoshiriki kukijenga imepotoshwa,” alisema Dk. Slaa siku alipotangaza kuachana na siasa.

Alisema sharti la kwanza ambalo alitaka Chadema izingatie, ni kiongozi huyo wa zamani ndani ya Serikali ya CCM, kujisafisha dhidi ya tuhuma ya kashfa ya sakata la Kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond aliyohusishwa nayo akiwa Waziri Mkuu.

Chanzo: Mtanzania
Unajiuliza mtu mkubwa kama Dr.Slaa anawezaje kuwa mpumbavu kiasi hicho asijue laghai za kisiasa...JK huyo huyo aliyempoteza alitufundisha kuwa akili za kuambiwa changanya na zako...
 
Safi sana
Kukaa ndani bila shughuli sio nzuri.

Hongera Bosi wa zamani wa chama kilicho mahututi.. sasa hivi wapenda pesa tu. Yote ulipigania kwishney..
Kuna uzi jingalao kaanzisha unahusu ujenzi wa chato airport. Kamuungr mkono.
 
Halafu utashangaa akiwa humu JF anawakejeli wasomi wanaolalamika kukosa ajira hapa Tanzania kwa kuwaambia watumie usomi wao kujiajiri wakati yeye mwenyewe ameajiriwa.
Hao ndiyo wanasiasa. Wakiwa majukwaani. Ohh vijana mjiajiri, tumia usomi wako ujiajiri. Aisee
 
Watu wengi wanapiga kelele tu, lakini hawajui hata COSTCO ni mdudu gani. Hivi kweli kwa wanaoifahamu COSTCO wanaweza ilinganisha na NAKUMAT, Imalaseko na viduka vya kibongo kweli? Unaposema COSTCO unazungumzia the largest American membership-only warehouse club. It is the second largest retailer in the world after Walmart. Yaani kama ingekuwa ijengwe pale Mlimani City, inakusanya kale kajengo kote na eneo lote linakuwa na duka moja - hapa nazungumzia mpaka vile vibanda/nyumba zilizopangishwa. Si kwamba wanauza bidhaa za nyumbani tu, huu ni udhalilisha kama si upotoshaji usio na maana, wanauza mpaka mafuta ya magari - Petrol Filling Stations, matairi ya magari na vifaa mbalimbali vikiwemo vya ujenzi, huduma za upimaji wa macho na miwani pia huduma za masikio - audiology dept. Kuna wafanyibiashara wengi yakiwemo mahoteli yanajiendesha kwa kutegemea bidhaa zinazouzwa COSTCO. Kifupi wanakwenda COSTCO kufunga mzigo wa kuuza kwenye maduka na mahoteli yao.

Kuhusu mishahara, wanalipa vizuri kuliko supermarkets zozote unazozijua humu duniani. Hii ni policy yao uliza mfanyakazi yeyote aliye kwenye Retail or Wholesale industry atakwambia juu ya COSTCO iwe ni USA, CANADA, UK na hata Japan. Kwa hiyo kwa Dr Slaa kufanya kazi huko, si kwamba ka-lost, hapana ni maamuzi yake kuamua kuishi kwa namna hiyo. Nina uhakika kwa ngazi aliyopo Sales Advisor, atakuwa analipwa hela nzuri kwa fortnightly - kila wiki mbili kuliko hata Full-time lecturer wa Tanzania. Na kwa usawa huu wa Magufuli, wabongo wengi tunaisoma namba. Pia pamoja na mapungufu yake ya kisiasa, nina uhakika huko aliko atakuwa anakula good times kuliko wabongo wengi na viongozi wa kisiasa waliobaki Bongo. Job security nzuri, social services za uhakika, hakuna mizingwe ya mshahara, na bado usafiri na mazagi zagi mengine ya kumwaga. Mwacheni Mzee wa watu amalizie siku zake kwa amani huko aliko!

View attachment 628021
COSTCO Gasoline station

View attachment 628018

View attachment 628019
Mkuu hata ukiandika vipi kuna ambao nia yao ni moja tu -kumdhalilisha Dr. Walisema amehongwa mabilioni hapa sasa kama ingekuwa kweli angekuwa na maisha tofauti. Amesema alikua anasoma na scholarship sasa amemaliza ili abaki lazima awe na kazi. Ameondoka amewachia siasa zenu lakini shida tupu-aseme asiseme maneno. Labda wanataka arudi halafu afanye kama yule professor ndo watamuelewa. Hata kama sikubaliani naye kwa mambo mengine lakini ni mfano wa mtu anaesimamia principles zake.
 
Back
Top Bottom