Dk. Possi: Nimejiuzulu

Dk. Possi: Nimejiuzulu

Baada ya Kujiuzulu maana yake nafasi iko wazi, nadhani mkuu alipoona amekosea kupitiliza idadi ikabidi amteue kuwa balozi na kuachia nafasi ya ubunge na unaibu waziri
 
Daaaah kama Rais kwenye mambo sensitive kama haya anakosea .......

Sasa kwenye mambo madogo madogo si ndio kabisa jamaa ana waburuza..........

Kiukweli ni hatari kuwa na Rais asiyefuata katiba................

Mungu tu ndio anajua tunakoenda Kwa Sasa kama nchi.............
Mkuu ulisikiliza clip ya mwakasege?
 
Tuendelee kuwa wachambuzi wakati wakenya na wahindi wanamiminika kuja kuanzisha viwanda. Hayo yote unayoyadai yanapaswa kufanywa na sekta binafsi kwani serikali ilijiondoa kwenye uzalishaji baada ya kuridhia SAP. Usitegemee serikali iwe na kiwanda chake kwa sasa.
Mkuu tatizo watu wengi hawajui mkataba wa SAP......
Laiti watu wakiujua ndio watajua hata aje malaika kuendesha hii nchi bado watu watamlaumu tu huyo malaika anaendesha nchi vibaya.

Mwacheni Ngosha afanye yake akimaliza aende zake.....
Kwa jinsi mkataba wa SAP ulivyo mwacheni tu Ngosha awe ananunua vitu vya mabilioni kupitia mikutano ya hadhara
 
Kuna mijitu wajinga humu, eti katiba imevunjwa Mara inachezewa, wapi katiba imevunjwa au kuchezewa???
Rais sio kwamba alikuwa hajui kateua wanaume 6 alikuwa anajua Sana ingekuwa kosa tu kama angewaapisha prof. Na bulembo ila kabla hajaapisha akatengua nafasi ya Posi na kabla hajaapisha Posi kajiuzulu. Sasa nyie mabush lawyer tuelezeni wapi kavunja au kachezea katiba, mmekurupuka Rais kacheza na technicalities za kikatiba.
 
Je, Dr. Abadallah Possi kwa sasa ana mtazamo upi juu ya 'political gymnastics' kwa Kiswahili "salakasi za kisiasa" msemo ambao ameuasisi yeye mwenyewe?
 
hiyo ndo shida ya ushindi wa mezani angeusotea kama wenzie asingeichezea nchi na kutukana wapiga kura wala kukimbia na rambirambi.
 
We usijidanganye huwezi kuwa na viwanda bila biashara (masoko),viwanda lazima vi integrate kilimo nishati etc huwezi kuzungumzia viwanda huku umejifungia ndani the issue inahitaji dimensions nyingi sana labda unazungumzia viwanda vya matofali
Kujifungia ndani unamaanisha nini?
 
Asema atakuwa na uroho kiasi gani kung'ang'ania ubunge.

Awasilisha barua ya kuachia ngazi kwa mamlaka husika.

Chanzo:Mtanzania

Swali:

Kikatiba, Mbunge wa kuteuliwa na Raisi akijiuzulu au kukoma kuwa mbunge kwasababu yoyote ile inayotambulika Kikatiba,idadi ya wabunge walikokwisha teuliwa na Raisi inapungua au inabaki pale pale?
Na suali jengine lipi linakuja mwanzo Yai au Kuku ?
Kuhusu wabunge hao 10 hata wakifa wote hakuna nafasi nyengine kwa mkuu kuteua.
 
Basi sisi ni watu wazima tumeshaelewa.mkubwa hakosei huambiwa kateleza haya Bw.Possi tunashukuru kwa kumuondolea aibu Mkuu.
 
Kuna mijitu wajinga humu, eti katiba imevunjwa Mara inachezewa, wapi katiba imevunjwa au kuchezewa???
Rais sio kwamba alikuwa hajui kateua wanaume 6 alikuwa anajua Sana ingekuwa kosa tu kama angewaapisha prof. Na bulembo ila kabla hajaapisha akatengua nafasi ya Posi na kabla hajaapisha Posi kajiuzulu. Sasa nyie mabush lawyer tuelezeni wapi kavunja au kachezea katiba, mmekurupuka Rais kacheza na technicalities za kikatiba.

Hivi wale mabolozi ambao walikuwa wapangiwe kazi mbali na hawa walioapishwa juzi tayari wote wamepangiwa vituo vya kazi? Kama hapana vipi tena bado wananchi wanateuliwa kuwa mabalozi? Hivi unaposema 'kucheza na technicalities za kikatiba' una maanisha nini?
 
Bila JF wala wasingeshtuka, Mwakyembe mwenyewe na Mwanasheria mkuu wanategemea JF.

Inawezekanaje makosa kama haya yatokee wakati kuna wataalamu wa sheria wamemzunguka Rais? Hii serikali inatia aibu sana.
 
Asema atakuwa na uroho kiasi gani kung'ang'ania ubunge.

Awasilisha barua ya kuachia ngazi kwa mamlaka husika.

Chanzo:Mtanzania

Swali:

Kikatiba, Mbunge wa kuteuliwa na Raisi akijiuzulu au kukoma kuwa mbunge kwasababu yoyote ile inayotambulika Kikatiba,idadi ya wabunge walikokwisha teuliwa na Raisi inapungua au inabaki pale pale?

Yani inchi hii kama watu nje ya wenye inchi kusema bwana yule kavunja katiba yangeisha kimyakimya,namshauri bwana yule akeshe akikariri katiba aielewe kama alivyoweza kujua urefu wa barabara zote TZ.huyu anaekubali kushauriwa asingeinyea katiba ila kwa namna hii,mhh
 
Asema atakuwa na uroho kiasi gani kung'ang'ania ubunge.

Awasilisha barua ya kuachia ngazi kwa mamlaka husika.

Chanzo:Mtanzania

Swali:

Kikatiba, Mbunge wa kuteuliwa na Raisi akijiuzulu au kukoma kuwa mbunge kwasababu yoyote ile inayotambulika Kikatiba,idadi ya wabunge walikokwisha teuliwa na Raisi inapungua au inabaki pale pale?
Tatizo bila matukio hamna cha kusema, je unajuaje walipanga iwe hivyo? Wanajua ninyi watu wa matukio, hivyo wawatengenezee tukio ili wiki nzima mkimbie nalo na msifanye mambo productive kwenu. Au tuseme ni kweli walikosea, na sasa wamerekebisha, je ni vibaya kurekebisha makosa? Kuna asiyekosea? Msiwe watu wa matukio sana. Jifunzeni kuibua agenda mpya na kuwa na ubunifu japo kidogo.
 
Kila anyeombea urais anataka na ana nafasi ya kuendesha nchi kwa utashi wake popote pale ulimwenguni acheni kudanganyana na videmokrasia vyenu vya darasa la nne!
We kenge kweli mtu aendeshe nchi kwa utashi wake? Labda Gambia hiyo , halafu ngoja nikuulize kile kiapo ambacho unaapa kuilinda na kuitetea katiba huwa unakielewa?
Ni bora wakati wa kuapishwa muwe mnashika chupa za Pombe na siyo vitabu vitakatifu mtakuja kupata laana.
 
Basi sisi ni watu wazima tumeshaelewa.mkubwa hakosei huambiwa kateleza haya Bw.Possi tunashukuru kwa kumuondolea aibu Mkuu.

Hivi PhD huwa inafuata nini kwenye siasa wakati lengo lake kubwa na maalum ni kufundisha na kutafiti tu?
 
Kocha kafanya mabadiliko baada ya kuona kelele na malalamiko ya washabiki.
 
Back
Top Bottom