Dk. Possi: Nimejiuzulu

Dk. Possi: Nimejiuzulu

Angalau umenisaidi kukionesha kile ambacho labd mimi ningekisema ningeonekana nina nongwa. Katiba ni ya wananchi si ya chama chochote cha siasa katika nchi yenye wanasiasa waungwana, wazalendo wanaoipenda nchi yao. Katika nchi ambayo wanasiasa wanajali matumbo yao, katiba ni ya kikundi ili waweze aidha kushiriki kula au iwawezeshe kuingia na kukaa madarakani.

Watanzania bado hawajaelimika na bado haijawa jamii yenye kuwajibika. Kuelimika ninakokuzungumzia mimi ni kuwa responsible, kufahamu kuwa mwananchi ndio mwenye nchi, mwenye haki ya kuhoji na kuuwajibisha uongozi. Jamii yenye kufahamu kuwa uchaguzi ni kasehemu kamoja tu ka demokrasia, afahamu kuwa demokrasia ina segmeny nyingine nyingi tu. Hatuna mtanzania anayesimamia uwazi, anayesimamia usikivu, uwajibikaji wa serikali na viongozi. Jamii ambayo haina check and balance institution katika kusimamia mambo muhimu ikidai katiba ni bure kwani bado haitaweza hata kuisimamia hiyo katiba yenyewe.

Jambo muhimu kwa sasa wacha ainyooshe nchi, wacha watu watie akili na adabu, wakitia akili na adabu watayatafuta hayo niliyoyasema hapo juu na hapo tutapata katiba ya maana.

Sipendi kujadili majina ya wanasiasa hasa hawa wanasiasa 'wachumia tumbo' wa nchi hii. Wakati katiba ikidaiwa miaka ya 1990 Lowasa alikuwepo. Lakini kwa vile kwake katiba sio ya wananchi ni ya kikundi akabaki na kikundi chake ili waendelee kutawala. Mchakato wa katiba ulipokuja alikuwepo lakini hakusema kama huo mchakato si sahihi. Kwa nini? Jibu ndio hilo hilo kwake katiba si ya wananchi bali ya kikundi cha watu. Akateuliwa kuwa mbunge katika Bunge la katiba, akakubali uteuzi na akaingia bungeni. Katika kupiga kura sina hakika kama alipiga au la lakini chama chake kilisimamia msimamo wake na kikashinda. Maisha yakaendelea, akaendelea na chama chake na akachukua fomu akiomba nafasi yakugomea urais kupitia chama chake na ofcouse baadae uenyekiti wa chama. Labda alikuwa na dhamira yakurudisha katiba ya wananchi si eti eeenh? Labda. Kilichotokea ni historia!

Swali kwa wanasiasa wengine wa upinzani! Je wao hawakujua kuwa ule mchakato si sahihi? Walilisema hilo kabla? Walipoitwa kuubariki ule mchakato wao walifanyaje? Walikimbilia zile posho au walikataa tangu mwanzo? Nani aitishe mchakato tofauti na huo? CCM? Ili iweje? Waondoke madarakani? Jamani tujitahidi kufikiri jamani!

Mimi nimekuwepo nao hao wapinzani na CCM inawajua uzuri ndio maana hawawasumbui, wanajua na kufahamu udhaifu wao, wanawapa chambo kinono, waroho wanakifuata baadae hao wanavuliwa. Mara nyingi hushtuka wakati wameshapotea na tabia hii haikuanza leo. Katika mazingira haya ya wananchi wanaofichwa ukweli na pande zote za watawala na wapinzani, katika mazingira haya ya kutotaka kuwajibika kwa mwanasiasa yeyote wa tawala wala wa upinzani, kwa kweli tumuache jamaa anyooshe nchi, watu waone umuhmu wa kuambiana ukweli pasipo kuoneana haya, umuhimu wa kuwajibika na tuache kuifanya nchi kijiwe cha Mafioso. Eti ubaya unajadiliana na wema? Wapiga dili duniani kote hawajawahi kuwa marafiki wa kweli wa wananchi, wanajipaka tu poda ya urafiki wa kinafiki. Ukiamua kufumbua macho na ukatazama kwa umakini utaona.

Mkuu mbona hatuelewani nimesema ijibu kwa mtazamo wa mwananchi wa kawaida kma mmi unawaingiza wanasiasa wa nini??? Hivi mbowe akiwa fisadi au lowasa akiwa fisadi ndio katiba mpya tusidai ama??

Hao kina mbowe walishatoka bunge kwa kuona mchakato umevurugwa ingawa walikuwa na hope kuwa labda utaenda vzuri kwa hyo kazi yao waliifanya 100% wakamaliza kishujaa sana na wananchi hawawezi kuwalaumu sasa awamu mpya imekuja na tuliomba mchakato urudiwe sasa iweje ajibu vile kna kwamba rasimu ya warioba haikuwa na miiko ya kuwabana hao watumishi wa umma unaodai wamepinda?? Wwe unataka anyooshe nchi kwanza mpaka akili zitukae sawa haya mbona zilitukaa sawa ndio tukadai katiba mpya enzo za kikwete sema mchakato ukavurugwa sasa ina maana watanzania bado tu HAWAJAELIMIKA kma unavyodai wwe??

Kma wananchi hawajelimika iweje walitoa maoni TMK na yakazaa rasimu bora zaidi i guess yenye matumaini kuwahi kutumika hapa tanzania???

Sawa lowasa hakupigania katiba kumbuka hta slaa alikuwa ccm likewise mbowe na huko nako am sure walisupport katiba iliopo....ilamindset ukibadilisha na ukaamua kuleta mabadiliko ni kosa?

Kibaki alitetea sana katiba ya enzi za kina moi iendlee coz alikuwa makam wake na aliwapinga sana kina odinga waliotaka katiba mpya ila si baadae alijiunga upinzani?? Na akajiunga na kina odinga na mwisho wa siku akaleta katiba mpya kuke kenya sasa lowasa na kibaki tofauti yao ni nini?? Lowasa angeshinda unafkiri angekataa rasimu ya warioba wakati ndio hoja ya kwanza ya UKAWA??

Cha kushangaza unajua kabisa kuwa ccm hawataki katiba mpya kwa kuwa watatoka madarakani sasa iweje unawatetea kwanni sasa unatumia nguvu nyingi sana kutaka tusiidai katiba more so reference yako ni WANASIASA

Kwanni usitoe solution for instance labda asasi za kiraia au wanazuoni kutoa elimu ya uraia na umuhim wa katiba kwa wananchi wasio na elimu kuliko wwe unakatisha tamaa tu eti WATANZANIA HAWAJASOMA sasa kwanni usitoe ushauri jinsi ya kuwaelimisha??

Hao zanzibra waliopata katiba mpya 2010 wameelimika sana kuliko huku bara?? Katiba hii ya sasa wakati inaletwa wati walikuwa wamelimika kuliko sasa???
Nakusubiri unipe majibu kuelemiika gani huk kunakofanya tusipate katiba mpya ambao wazanzibar wanayo io elimu
(Naomba usiingize wanasiasa njoo kiSOCIAL zaidi political factors achana nazo maana utaisia kwenye kujadili lowasa na sijui ufisadi wa mbowe)
 
Mkuu mbona hatuelewani nimesema ijibu kwa mtazamo wa mwananchi wa kawaida kma mmi unawaingiza wanasiasa wa nini??? Hivi mbowe akiwa fisadi au lowasa akiwa fisadi ndio katiba mpya tusidai ama??

Hao kina mbowe walishatoka bunge kwa kuona mchakato umevurugwa ingawa walikuwa na hope kuwa labda utaenda vzuri kwa hyo kazi yao waliifanya 100% wakamaliza kishujaa sana na wananchi hawawezi kuwalaumu sasa awamu mpya imekuja na tuliomba mchakato urudiwe sasa iweje ajibu vile kna kwamba rasimu ya warioba haikuwa na miiko ya kuwabana hao watumishi wa umma unaodai wamepinda?? Wwe unataka anyooshe nchi kwanza mpaka akili zitukae sawa haya mbona zilitukaa sawa ndio tukadai katiba mpya enzo za kikwete sema mchakato ukavurugwa sasa ina maana watanzania bado tu HAWAJAELIMIKA kma unavyodai wwe??

Kma wananchi hawajelimika iweje walitoa maoni TMK na yakazaa rasimu bora zaidi i guess yenye matumaini kuwahi kutumika hapa tanzania???

Sawa lowasa hakupigania katiba kumbuka hta slaa alikuwa ccm likewise mbowe na huko nako am sure walisupport katiba iliopo....ilamindset ukibadilisha na ukaamua kuleta mabadiliko ni kosa?

Kibaki alitetea sana katiba ya enzi za kina moi iendlee coz alikuwa makam wake na aliwapinga sana kina odinga waliotaka katiba mpya ila si baadae alijiunga upinzani?? Na akajiunga na kina odinga na mwisho wa siku akaleta katiba mpya kuke kenya sasa lowasa na kibaki tofauti yao ni nini?? Lowasa angeshinda unafkiri angekataa rasimu ya warioba wakati ndio hoja ya kwanza ya UKAWA??

Cha kushangaza unajua kabisa kuwa ccm hawataki katiba mpya kwa kuwa watatoka madarakani sasa iweje unawatetea kwanni sasa unatumia nguvu nyingi sana kutaka tusiidai katiba more so reference yako ni WANASIASA

Kwanni usitoe solution for instance labda asasi za kiraia au wanazuoni kutoa elimu ya uraia na umuhim wa katiba kwa wananchi wasio na elimu kuliko wwe unakatisha tamaa tu eti WATANZANIA HAWAJASOMA sasa kwanni usitoe ushauri jinsi ya kuwaelimisha??

Hao zanzibra waliopata katiba mpya 2010 wameelimika sana kuliko huku bara?? Katiba hii ya sasa wakati inaletwa wati walikuwa wamelimika kuliko sasa???
Nakusubiri unipe majibu kuelemiika gani huk kunakofanya tusipate katiba mpya ambao wazanzibar wanayo io elimu
(Naomba usiingize wanasiasa njoo kiSOCIAL zaidi political factors achana nazo maana utaisia kwenye kujadili lowasa na sijui ufisadi wa mbowe)

Sijui kwa nini unadhani kutoa maoni ni kuelimika. Halafu katika mijadala epuka kumuingizia mwenzako maneno ambayo hajayasema ili ujenge hoja kwa maneno yako mwenyewe. Sijasema watanzania hawakusoma. Bahati mbaya sana misimiati ya kiswahili ina mipaka. Kuelimika hapa ninapokuzungumzia hapa ni informed and responsible citizenry, sina msamiati mzuri wa kiswahili zaidi ya walioelimika.

Mimi nawazungumzia wanasiasa kwa sababu ndio hasa wasimamiaji wa mchakato wa katiba na hata kabla serikali haijaunda NCCR kulikuwepo wanasiasa wanaotaka mabadiliko ya katiba, wananchi peke yao siwaoni mahali popote wakidai katiba. Kama wewe unawaona nijulishe tafadhali.

Ukianza kuangalia harakati za kudai katiba kwa akina Mbowe ni wazi utawaona ni mashujaa na hicho ndicho kitu wanachokitaka. Mifano yako yakina Kibaki haibadilishi ukweli akina Kibaki ni wale wale wanaogombania katiba kama kikundi wala si katiba ya wananchi. Kama Kenya ndio mfano wako wa mafanikio basi yakupasa utafakari upya. Bila kujali nani atakuwa wapi au yuko wapi, Kenya inaongozwa na kundi moja tu la marafiki au la familia moja, ukichunguza utaona. Kuwa raia wa nje hakuwafanyi wao kuwa bora.

Una hiari ya kumuona huyu au yule ni mwanasiasa mwema kwako, inategemea na uzoefu wako na taarifa ulizo nazo zilizokufanya ujenge imani. Labda nikupe rai kuwa hata kama unawaamini hao wana siasa jaribu basi kuhoji mambo madogo madogo. Inakuwaje unakaa ndani ya chama miaka 39 pasipo kuona makosa yoyote wakati hali ya nchi iko mbaya hivi? Wewe uliwezaje kuwa tajiri na ukwasi huku nchi ikiendelea kuwa masikini? Angalau kutoka katika kuhoji huko tunaweza kupata mbinu za medani za ujasiriamali tukaziiga. Mengine unaweza ukayafikiri na kuyahoji mwenyewe.

Kwagu tatizo si katiba. Kwangu ni uwezo wa usimamiaji. Muda muafaka wa kudai katiba ulikuwa ule wa miaka ya 1990, CCM ilikuwa katika presha kubwa na kilichodaiwa kilitolewa kwa sababu hali ilikuwa mbaya na misaada ilihitajika. Walipoweza tu kutoroka kipindi kile wakawapofusha watu macho.

Unaweza ukadhani kuwa katiba ile iitwayo ya wananchi ilikuwa ya wananchi kweli. maoni mengi yaliyopingwa na CCM yalitokana na busara za waandishi wa katiba ile na mahitaji ya muda kwa kadri walivyoona inafaa. Utunzi wa katiba ile ya wananchi haukuwa tofauti na uamuzi wa kuingia katika mfumo wa vyama vingi. Wengi wamekataa lakini mahitaji ya muda yalitulazimu. Wananchi wa watanzania hawakujua mahitaji ya muda, vyama vingi tuliamuriwa!

Waandsishi wa katiba ya wananchi walichambua mawazo ya wananchi na kufanya tafsiri. Rasimu ile ilikuwa ya kisomi zaidi yenye kuendana na muda lakini isiyokidhi mahitaji ya kisiasa ya wagombea ndani ya CCM na isiyikidhi mahitaji ya kiitikadi ya CCM mojawapo likiwa idadi ya serikali katika muungano. Rasimu isiyokidhi mahitaji ya CCM ipitishwe na CCM? Hapo ndipo napata tabu kufahamu hawa wanasiasa wa upinzani wana fikiri vipi na akili zao zikoje. Hivi kama wangegoma toka mwanzo kabisa ule mchakato ungeendelea naa tungepoteza kiasi kile cha fedha?

Namna nzuri ya kufanya Bunge la katiba ipo na hata akina Mbowe wanafahamu, Issa Shivji ameandika sana kuhusu namna hiyo, lakini linapokuja suala la posho wenzetu wanasahau. Wanakimbilia posho na starehe za Dodoma. Wakigundua wamepigwa wanarudi kwa wananchi kutafuta huruma.

Labda kama huijui historia ya Zanzibar, Zanibar kisiasa wameelimika zamani zamani sana, sio leo. Kama kuna matukio makubwa ya kisiasa yaliyowahi kutokea katika Tanzania basi Zanzibar ina matukio makubwa na mengi yenye kuchukua na kuamsha vinyweleo katika ngozi ya kimataifa kuliko bara. Wazanzibar wameelimika hasa kisiasa, hata kama utakwenda leo au kesho, iwe unguja au pemba hilo utaliona wazi. Wanazifahamu haki zao na wako radhi kuzitetea na kuzipigania. Wanajishugulisha kila uchao kufahamu nchi yao inaongozwa vipi. Mwanasheria wa Zanzibar hasubiri eti ipite miaka 39 ndipo aseme hapa kuna dhuluma, Mzee wa chama Moyo hafichi kusema kuwa Karume alishindwa kura akamuomba akaongee na Maalim Seif ili machafuko yasitokee. Ukifahamu yaliyomkuta Jumbe utafahamukuwa Zanzibar imepata mwamko zamani. Abdulhaman Babu uwezo wake wa kujenga urafiki binafsi na China ndio uliwaleta wachina mpaka leo Tanzania, vifo cha Kassim Hanga na Mdungi Ussi vinaashiria Zanzibar ni anga nyigine kabisa kisiasa, hatuwafikii hata ukucha.

Zaidi ya hapo unaweza kufungua kwenye google ukasoma 100 days that made Zanzibar, document ya CIA iliyofikia muda wa kutolewa public ili uifahamu vizuri Zanzibar na ufahamu bara tuko nyuma kiasi gani.

Kwa uelewa wetu huu na mwamko wetu huu, kwa wanasiasa wetu hawa tuliowaamini, hatuna haja ya katiba, tumuache tu Mzee wa Kaya atunyooshe! Ukweli atatunyoosha wote, wa tawala na wasio tawala. Pamoja na yote, angalau huyu anaifikiria nchi, hata kama atakuwa anafanya vibaya basi anafanya vibaya kwa nia njema.
 
Wanawake wengi hawawezi kazi, hivi utampa tu mtu nafasi ya ubunge sbb ni mwanamke..? Hizi sheria za kijinga tumepokea kwa wazungu wakati hao hao wazungu hawana huo usawa wa kijinsia.. pelekeni ujinga wenu huko, mnakariri tu mambo ya wazungu, hivi umeangalia usawa wa kijinsia U.S, UK, Europe in general, Canada, Australia, Russia, China, au mnakurupuka tu kumpigia kelele Mh. Rais..

Kama ni mm ningeweka Wanaume min. 70%, alafu wanawake maximum 30% kwa kila sekta ya serikali nzima.. acheni uzungu wa kukariri hapa, hao wazungu wenyewe hawana hiyo 50/50.. hakuna hata nchi moja..
 
Kwa nini Dr. Posssi anasema kuwa yeye hana uroho wa madaraka? Anajua fika kuwa bila kufanya alichokifanya angemuweka Mtukufu kwenye mzozo wa kikatiba? Nani asiyejua? Basi kwa nini asijiuzulu kwanza then uteuzi uchukue nafasi yake?

Sisi si wajinga kabisa tena tusitaniane ohooooo. Kumbukeni ilikuwa kabla ya hawa wapya kuapishwa ililazimu kabisa Dr. Possi ajiuzulu ili kusiwe na mzozo sasa eti kwa nini ning'ang'anie madaraka!!!! Duuu nchi kweli iko episode 5.
 
Mkuu Congo arguments zako hazina mashiko. Hayo unayoyaita "makosa" si ya kikatiba sana sana ni ya kimaadili zaidi na kufanya mambo kinyume na utaratibu tu. Tukubaliane kuwa Mambo yakifanywa kinyume na katiba,hiyo ni issue very serious na inahitaji mjadala mpana ili kurekebisha hali hiyo kwa maslahi mapana ya nchi. Kuna Wakati Mwalimu Nyerere alimteua Chediel Mgonja kuwa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara huku akiwa amehukumiwa na Mahakama Kuu kuwa asishiriki kwenye uongozi kwa muda wa miaka mitano (5). Nakumbuka Joseph S. Warioba akiwa mwanasheria mkuu wa Serikali alimfuata Mwalimu na kumweleza "Mwalimu umekiuka Katiba"! na Mwalimu Nyerere akakubali yaishe akatengua uteuzi huo. Hivyo hisia za kukiukwa kwa katiba ya nchi ni kitu cha kukitilia maanani sana ndiyo maana Viongozi wanaaswa kila siku kufanya mambo kwa busara kwa kuzingatia Katiba ya Nchi, vinginevyo nchi itakuwa, "Banana Republic".
Naona haya majibu yako yana mashiko. Nashukuru kwa kunijibu.
 
Back
Top Bottom