Dk. Mwakyembe aitahadharisha CCM

Dk. Mwakyembe aitahadharisha CCM

Mpuuzi kweli huyu, yeye mwenyewe ni part ya malumbano na kusingizia watu, leo anatoa onyo
 
Sintamwelewa Mwakyembe mpaka atakapotimiza ahadi yake alipokuwa APOLO India kuwa akirejea nyumbani angeweka hadharani sababu za kuumwa kwake !!!!!!!!!
 
Huyu naye mnafiki mwingine mtu wa kutafta umaarufu na public sympath, yeye na mwenzake Sitta hawana jipya kazi kuropoka.

Hebu fikiria Mwakyembe na kauli zake tata; Mara kuna mambo hakuyasema kwenye report ya richmond. Kwanini mpaka leo hajayasema? Kama si unafiki ni nini? Mara kalishwa sumu lakini hataki weka mambo wazi mwisho wa siku kaibuka tuaachie vyombo vya usalama vifanye kazi yake tusijadili afya yake wakati mwanzo alisema hana imani na polisi.

Huyu mropokaji tu anatafta umashuhuri mimi alishanichosha japo mwanzo nilikuwa namkubali.

Magamba wanavutana acha wazikane

Huyu jamaa nilikuwa na mkubali sana ila badaee nikagundua ni mnafiki kama magamba wenzake
 
Maneno hayo yatanoga pale utakapoachana na magamba we ni mkweli sana ila umebanwa please njoo sehemu sahihi si nyingine ila ni CHADEMA.
 
Kuna wadau wa mtandao huu wanadai unamilikiwa na CHADEMA kumbe wanashindwa kuelewa kuwa watanzania wa leo sio wa mwaka 47 - Karumekenge aliwahi kupost akidai huu ni mtandao wa uchochezi akatoa mifano ya Rwanda na Burundi akasahau kuwa wale walichapana hatimaye wakaheshimiana ndo maana leo wako juu kiuchumi kuliko sisi, kule hakuna ufisadi, wizi, kulishana sumu, kudhurumiwa wala kubambikiwa kesi. huwezi kutishia watu kwa vita wakati unaiba madini, mnagawana majumba, viwanda, EPA, ajira ni kwa watoto wa vigogo.Sasa Mwakyembe na Sitta wao wanataka utawala ndo maana walimtosa Mpendazoe, kama kweli wana uchungu na nchi hii ni kweli wajitoe CCM.
 
mm nazani labda huyu DK hajapona vizuri,sasa hajaribu tiba za maji marefu labda watamsaidia maana haeleweki
 
Mwakyembe na Kiwira wapi na wapi, inaonyesha ni jinsi gani mamluki mlivyojazana humu kuchafua watu, subirini kushikishwa kuta na hao wafadhili wenu.

Wewe umeshikishwa sana ukutu unadhani na wengine wanashikishwa? Naona umeadhirika kwa kuvaa pampers wewe
 
Mwakyembe amenena kazungumzia hatma ya chama kwa makundi yaliyopo kwa sasa haiwezi kuipa chama afya ni mawazo mazuri tuyaheshimu kwa wale wenye mapenzi na chama hiki.:rockon:
 
maswali ninayojiuliza.....
1. Mwakyembe
anapambana na nani na katika lipi?
2. Je adui ni nani na
malengo ya vita yake /yao ni nini?
3. Kwanini imekuwa vita isiyotaja adui? Kwanini asitaje watu anaopambana
nao kama CHADEMA
walivyofanya katika "list of shame?" Je hii ni vita hewa
kwa ajiri ya kuhitaji
huruma ya wananchi au
kuna agenda nyingine
tusiyoijua?
4. Lowasa naye kasema
yupo tayari kwa
mapambano, hawa wote
wako ndani ya CCM...je
inawezekana wapo kundi
moja katika upambanaji
wao?
 
huyu naye amezidi sasa si anyamaze aendelee kujiuguza?? au ndo kuutaka uraisi ki style kupitia public sympathy, kama kweli ni mpambanaji na haogopi kufa aweke wazi kila kitu (Kama kweli vipo), sio kutupigia kelele kila siku na kutuumiza macho yetu kumtazama kwenye tv akiongea *****..
 
Hivi huyu jamaa udokta wake upo bado kichwani kweli? Hivi anaweza kurudi darasani akanoa bongo za wanasheria watarajiwa kama alivyokuwa akifanya kabla ya kuingia kwenye siasa? Am just thinking aloud.
 
makembe iko nafiki ndani yake.Pengine nawesa kuwa M.N.Y.A.N.G'.A.U mwingine in different form from Gambas.Okaoge mpaka ukurutu wake wa kujitakia uishe ndio aongee na mimi nimsikilie nimuelewe
 
Hivi huyu jamaa udokta wake upo bado kichwani kweli? Hivi anaweza kurudi darasani akanoa bongo za wanasheria watarajiwa kama alivyokuwa akifanya kabla ya kuingia kwenye siasa? Am just thinking aloud.

Sidhani kama anaweza, kwani bongo yake kwa sasa inawaza utawala na si uzalendo. Kama ye ni msafi kweli na aachane na ccm kwani CCM si mama yake (kama mwl JKN alivyosema) atoke huko na ajiunge na wenye nia yadhati ya kuijenga nchi.
 
Dk. Mwakyembe alisema miradi yote aliyoiahidi wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2010 atahakikisha inatekelezwa ikiwemo ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kyela kwenda Matema.

hizi pesa za ujenzi wa barabara hazitoki mfukoni kwake ila anajivunia ushawishi wake ndani ya serikali ya ccm katika kuhamisha utajiri wa taifa na kuupeleka jimboni kwake.................sina uhakika kama hicho ndicho kipaumbele cha taifa kuijenga hiyo barabara.............au lengo ni kumhakikishia mbunge ugali uchaguzi ujao..................la muhimu kwa mwakyembe akazane na matibabu na kujipatia mapumziko sioni kama jina lake litakuwepo kwenye ballot box comes 2015.............most likely whatever is troubling him will ultimately consume him be4 the D-Day...............

attachment.php
 
Viva mwakyembe viva! Walaaniwe wote wanaokunenea mabaya.
 
Mimi binafsi namuheshimu sana Mwakyembe, tatizo langu linakuja pale anapojisahau kwamba yupo kwenye CABINET-maswala mengine siya kuongea adhalani, unadhalilisha Baraza la Mawaziri na chama chako kwenye kadamunasi-wewe time yoyote unaweza kwenda kwa JK bila kipingamizi; kama una nia nzuri kwa nini usitenge muda wa kuonana na Jakaya in confidence ukumueleza duku duku lako, mbona namuonaga ni mtu msikivu sana. Msikilize atakujibu nini au ana maoni yepi au kama atatoa mapendekezo kwamba hili swala lifikishwe kwenya Baraza la Mawaziri au NEC hili lipatiwe ufumbuzi bila ya kukimbilia kwenye publicity STUNT.

Binafsi nimesikitishwa na kauri zako sijuhi ulikuwa unataka kutuma ujumbe gani kwa wananchi, lakini si Kikwete huyu huyu aliyekuteua kwenye nafasi ya Unaibu wa Waziri againist all ODDS - kama kweli angekuwa anavisikiliza vikundi vyenye nia ya kukigawa chama au kufitinisha watu-ebu tuwe wakweli kama angekuwa hana msimamo ungeteuliwa kweli kuwa naibu WAZIRI?

Kuhusu mambo ya VICOBA, mimi binafsi ni mmoja wa watu ambao hatukuwa comfortable na zoezi hilo; it never sank in my system to be frank - kweli walikuwa wana wasaidia wakina mama-lakini uki-play back kilichokuwa kinafanyika wakati wa kutoa misaada hiyo mtu mwenye akili za ku-analyse mambo unakuwa a bit concerned, maanake ilikuwa inageuzwa kama jukwaa la siasa especially kuzungumzia mambo ya ufisadi - kila raia nchi hii anachukia ufisadi, lakini watuhumiwa si wanashughulikiwa? Kulikuwa na faida gani ya kurudi rudia mambo hayo kila saa hasa hasa unapotoa misaada. Mbona mtu kama BAKHRESA anatoaga misaada chungu nzima kimya kimya, sijawahi kuona anaitisha wahandishi wa habari kutagazia dunia kwamba katoa hiki mara kile - tuwe wagarifu jamani, watu wenye long term plan wana njia nyingi za kufakinikisha malengo yao.

Mwisho niseme, ni kweli kuna baadhi ya watu/viongozi ni wazushi na wafitini au kuaribia sifa wenzao hasa wakiwaona ni tishio kwao; lakini mimi nina imani JK anaweza ku-deal na watu wa sampuli kama hiyo fasta, si mifano hipo-kama angekuwa ana-entertain vitu kama hivyo asingemteua Mwakyembe kwenye nafasi ya Unahibu wa Uwaziri. Niliyosema humu ni kwa nia ya kujenga si kwa nia mbaya, Nakutakia afya njema Mh.Mwakyembe (MB). ASANTENI.

Kwenye hiyo tahadhari mi sijaona wapi kamtaja JK. anawaambia wana CCM wenzake kuwa kuna marumbano ndani ya chama chao hapo kuna ubaya gani. unasema akaongelee kwenye baraza la mawaziri kwani kila alichoongea hapo ni cha level ya juu hivyo?. mwache atoe dukuduku lake maana kwenye mikutano ya ndani mnamziba mdomo!
 
Kumsikiliza Mwakyembe na Sitta ni mara mia umsikilize Lusinde. Maana hawa wawili ni wasomi na wataalam waliobobea ila wanafiki wa kutupwa. Lusinde yeye anajulikana ni mropokaji na kutukana tu. Ah Mwakyembe na Sitta wananiboa sana
 
Back
Top Bottom