abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
Mbunge wa Kyela (CCM), Dk.Harrison Mwakyembe, amekirushia kombora Chama cha Mapinduzi kwamba kama kitaendelea na mivutano ya ndani, kuna uwezekano mkubwa wa kubwagwaa katika chaguzi zijazo na vyama vya upinzani.
Alisema hayo jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara na mamia ya wananchi wa mji wa Kyela uliofanyika katika viwanja vya John Mwakangale wakati wa ziara yake ya siku tatu baada ya kutokuwepo jimboni mwake kwa zaidi ya miezi saba kutokana na kuugua na kulazwa nchini India."Chochoko ndani ya CCM haziishi, kuna watu utafikili wamechanjiwa kwa ajili ya chokochoko, Katibu sitanii tupo kwenye ushindani mkubwa wa kisiasa, vyama vya upinzani siyo vya kuchezewa tena vina nguvu kubwa, na CCM tukiendelea na hizi ngumi za ndani tutabwagwa," alisema Dk. Mwakyembe huku akishangiliwa na wananchi.
Dk.Mwakyembe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, alisema baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge aliingia na hamasa kubwa na kuwa mtu wa pili kitaifa kuanzisha vikundi vya ushirika Vicoba ambavyo viliibuka kwa kasi na kuwa na mtaji Sh. bilioni tatu benki.
Alisema baada ya mafanikio hao kupatikana siasa ikaingia na kuanza kupiga fitina hali iliyopelekea mfadhili aliyekuwa ameahidi kutoa Sh. milioni 100 kusitisha mpango huo baada ya kuandikiwa barua na baadhi ya viongozi ndani ya chama kwamba yeye (mfadhili) anaendesha upinzani ndani ya CCM.
Aliongeza kuwa baadaye ilibainika kuwa waliokuwa wakipiga vita Vicoba walikuwa ni mafisadi ambao wameiba fedha za chama na serikali hivyo wanataka wao ndio watawale kwa jeuri ya pesa zao na kutotaka wananchi wapate msaada kutoka kwa watu wengine.
Dk. Mwakyembe aliweka msimamo kuwa atakapoamua kupumzika ubunge atakayembadili atakuwa mtu mwenye viwango na kasi ile ile, mwenye sifa ya ubunge kwa kutokuwa muoga ambaye akifika bungeni atakuwa hajikombi kwa kubeba mabegi ya mawaziri kwani huo ndio mwanzo wa kudharauliwa.
"Ndugu zangu usipokuwa na msimamo kwenye siasa za kitaifa, watakudharau, mara unasema unajua wazee eeeeh twendeni tukapate supu watakuambia sawa," alisema na kuongeza:
"Hapana tunataka mbunge makini anayemwambia waziri chukua begi lako tukutane jioni tuongelee masuala ya maendeleo ya Kyela, nao watakuheshimu kuwa huyu jamaa ana kamsimamo."
Dk. Mwakyembe alisema miradi yote aliyoiahidi wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2010 atahakikisha inatekelezwa ikiwemo ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kyela kwenda Matema.
CHANZO: NIPASHE
Alisema hayo jana wakati akizungumza kwenye mkutano wa hadhara na mamia ya wananchi wa mji wa Kyela uliofanyika katika viwanja vya John Mwakangale wakati wa ziara yake ya siku tatu baada ya kutokuwepo jimboni mwake kwa zaidi ya miezi saba kutokana na kuugua na kulazwa nchini India."Chochoko ndani ya CCM haziishi, kuna watu utafikili wamechanjiwa kwa ajili ya chokochoko, Katibu sitanii tupo kwenye ushindani mkubwa wa kisiasa, vyama vya upinzani siyo vya kuchezewa tena vina nguvu kubwa, na CCM tukiendelea na hizi ngumi za ndani tutabwagwa," alisema Dk. Mwakyembe huku akishangiliwa na wananchi.
Dk.Mwakyembe ambaye pia ni Naibu Waziri wa Ujenzi, alisema baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge aliingia na hamasa kubwa na kuwa mtu wa pili kitaifa kuanzisha vikundi vya ushirika Vicoba ambavyo viliibuka kwa kasi na kuwa na mtaji Sh. bilioni tatu benki.
Alisema baada ya mafanikio hao kupatikana siasa ikaingia na kuanza kupiga fitina hali iliyopelekea mfadhili aliyekuwa ameahidi kutoa Sh. milioni 100 kusitisha mpango huo baada ya kuandikiwa barua na baadhi ya viongozi ndani ya chama kwamba yeye (mfadhili) anaendesha upinzani ndani ya CCM.
Aliongeza kuwa baadaye ilibainika kuwa waliokuwa wakipiga vita Vicoba walikuwa ni mafisadi ambao wameiba fedha za chama na serikali hivyo wanataka wao ndio watawale kwa jeuri ya pesa zao na kutotaka wananchi wapate msaada kutoka kwa watu wengine.
Dk. Mwakyembe aliweka msimamo kuwa atakapoamua kupumzika ubunge atakayembadili atakuwa mtu mwenye viwango na kasi ile ile, mwenye sifa ya ubunge kwa kutokuwa muoga ambaye akifika bungeni atakuwa hajikombi kwa kubeba mabegi ya mawaziri kwani huo ndio mwanzo wa kudharauliwa.
"Ndugu zangu usipokuwa na msimamo kwenye siasa za kitaifa, watakudharau, mara unasema unajua wazee eeeeh twendeni tukapate supu watakuambia sawa," alisema na kuongeza:
"Hapana tunataka mbunge makini anayemwambia waziri chukua begi lako tukutane jioni tuongelee masuala ya maendeleo ya Kyela, nao watakuheshimu kuwa huyu jamaa ana kamsimamo."
Dk. Mwakyembe alisema miradi yote aliyoiahidi wakati wa Uchaguzi Mkuu wa 2010 atahakikisha inatekelezwa ikiwemo ujenzi wa barabara ya lami kutoka Kyela kwenda Matema.
CHANZO: NIPASHE