Dk. Hamis Kigwangalla aikana kampuni ya Qnet

Dk. Hamis Kigwangalla aikana kampuni ya Qnet

Nchi hii haiishi Vituko,

Baada ya Kampuni ya Qnet kuanza kukalalamikiwa na Wananchi kwamba inawatapeli hela zao, Waziri wa Utalii Kigwangalla ameibuka na kusema
Ukweli ni kuwa, siwajui wao binafsi ‘at personal’ level na wala biashara yao, umiliki wake na muundo wake siujui zaidi ya kuelewa kwa juu juu kuwa ni ‘network marketing’.

Waziri Kigwangalla akiwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dk. Adelhem Meru Mshauri wa bodi ya QNET David Sharma, meneja mkuu wa QNET-Tanzania Benjamin Mariki wakisoma gazeti lenye bidhaa za kampuni hiyo mara baada ya Ufunguzi wa ofisi ya shirika hilo nchini Tanzaniza..

Screenshot from 2018-02-16 09-50-38.png

Waziri wa Maliasili na Utalii, Hamis Kigwangalla kupitia ukurasa wake wa Instagram amekana kuwafahamu wamiliki waendeshaji wa biashara ya QNET

> Soma nukuu niliyoiweka hapa chini!


''Nimeona nitoe ufafanuzi kwenye hili jambo. Maana kila mjadala juu ya hii kampuni ya QNet unapoibuka, jina langu linakuja, na mara nyingine picha yangu inawekwa.

Ukweli ni kwamba, nilialikwa kwenye shughuli ya uzinduzi wake kama mgeni wa heshima; mgeni rasmi alikuwa ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji wa wakati huo, Dr. Adelhelm Meru.

Niliamini kwa heshima ya kuzinduliwa rasmi na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji, ambao ndiyo wenye dhamana ya usajili wa biashara zote nchini, ni lazima ni watu halali na bado ninaamini kama kuna shida mamlaka husika zitachunguza na kuchukua hatua stahiki na kama hakuna shida basi ni vema mamlaka husika zikatoa mwongozo utakaowaondoa hofu wananchi wenzetu wenye ‘interest’ ya kushiriki kwenye biashara hii.

Baada ya kufika eneo la tukio, kiitifaki ikaonekana nami lazima nishiriki zoezi, nikashindwa kukataa. Nadhani inafahamika kwamba nimekuwa mstari wa mbele kuunga mkono kwa vitendo jitihada nyingi mbalimbali za wajasiriamali vijana ambao wameamua kutoka [HASHTAG]#NjeYaBox[/HASHTAG].

Hata hawa nilishindwa kuwakatalia. Ukweli ni kuwa, siwajui wao binafsi ‘at personal’ level na wala biashara yao, umiliki wake na muundo wake siujui zaidi ya kuelewa kwa juu juu kuwa ni ‘network marketing’.

Ifahamike hapa kuwa sina maslahi yoyote yale kwenye biashara hii na wala sikushiriki uzinduzi wake kwa malengo ya kutoa ushawishi ili watu wajiunge, na natoa rai kwamba wanaotaka kujiunga ama kuacha kujiunga wasitumie picha za ushiriki wangu siku ya uzinduzi, kwa namna yoyote ile, kujenga uhalali wa aina yoyote ile, bali watumie vipimo vyao vingine kufanya uamuzi na siyo picha zangu.

Sintohusika na matokeo yoyote yale, chanya ama hasi, ya ushiriki wa mtu yeyote yule ama taasisi yoyote ile, kwenye shughuli za kampuni hii.

Naomba pia izingatiwe kwamba, jina langu ama picha yangu haijaruhusiwa kutumika kama bango la matangazo ya biashara ya mtu au taasisi yoyote ile, na hivyo kufanya hivyo ni kosa kisheria na ikibainika nitachukua hatua kali za kisheria''

#HK
=====

Screenshot from 2018-02-16 10-19-53.png

Hapa ni Waziri wa Utalii Kigwangalla wakati akiwa Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo, Jinsia, Wazee na Watoto, (wa pili kushoto), akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo la Qnet uliofanyika Dar es Salaam, wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Bodi ya Qnet, David Sharma, Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dk. Adelhelm Meru na Wakala wa Qnet Tanzania, Benjamini Mariki.

JamiiForums kuliletwa thread ya Malalamiko nikawa nashangaa kwanini hawachukuliwi hatua? Nini kinafanya wasishughulikiwe kama wengine? Qnet Company "biashara mtandao" ni utapeli unaoenea kwa kasi Tanzania. Serikali mko wapi?

=====
My Take:
Hapo mimi ndo nashangaa, anakataa vipi wakati yeye ndo alizindua Ofisi? Alikuwa hajapewa maelezo wanajihusisha na nini?

Bora angekaa kimya sababu wakati anazindua alifanya hivyo hadharani.

Haikwepeki kwamba ana maelezo ya kutosha kuhusu hii Kampuni.
 
Hahahha kumbe kweli bhana, Jamaa ni bingwa wa kujamba na kuwasha feni fastaaaaaa.....atakuja kukana kuwafungia geti wafanyakazi pale Wizara ya Afya. Heri yake yule ndugu yake yeye ana wapambe wanaokuja kila siku kusema "hamkumuelewa vizuri, hakumaanisha kuwa watu wazaliane, au hakukataza michango mashuleni...."
 
Bizaa gani au bizaa ni kuingiza na kusajili watu wapya. Kwamba ulete vichwa utakula mabonas kibao
 
Mpwa wangu figganigga ungeweka na statement aliyotoa ya kukana/kuikana Qnet ingenoga sana, story inge-balance vinginveyo akiona hii ianaweza kuikana pia
 
Anakataaje wakati picha na video za uzinduzi zipo mitandaoni na anaonekana waziwazi akishiriki?

Mkuu hebu tuwekee maelezo yake hapa tuyapime!
 
Hiyo Kampuni wana ka ' branch ' kao kamoja hivi kapo Sinza jirani na Hostels za UDSM ukienda hapo hata kama ni Saa Saba ( 7 ) mchana utasalimiwa kwa kuambiwa ' Good Morning ' na baada ya hapo utaanza ' Kuhubiriwa ' Kitapeli na Wanawake tofauti tofauti ambao huzungumza haraka haraka utadhani wamebanwa na Haja Kubwa na wanataka kuwahi Kujisaidia.
 
Afuu kafunga Comment kwenye hiyo.post kule insta maana anajua kafanyaa upuuzi wa kiwango cha Lamiiii....!! Jamaa bataa sanaa...
 
Husije shangaa kwa mtu kama Kigwangala kumkana hata baba yake mazizi,kwa ushahidi huu unakana vipi kuwa uifahamu kampuni ya QNET? Msomi wa kiwango chake,mbunge na waziri wa serikali anawezaje kuzindua/kushiriki kuzindua kampuni/bidhaa hasiyo ijua?
 
Hiyo Kampuni wana ka ' branch ' kao kamoja hivi kapo Sinza jirani na Hostels za UDSM ukienda hapo hata kama ni Saa Saba ( 7 ) mchana utasalimiwa kwa kuambiwa ' Good Morning ' na baada ya hapo utaanza ' Kuhubiriwa ' Kitapeli na Wanawake tofauti tofauti ambao huzungumza haraka haraka utadhani wamebanwa na Haja Kubwa na wanataka kuwahi Kujisaidia.
We GENTA mtani umeanza eeh...by the way vipi matokeo ya jana kule Shy? (off the book).
 
Simpendi Kigwa. Sijui kwa nini? Labda kauli zake.
 
Kigwangalla ameongea kisiasa lakini ameeleweka... Kwa mtu anayeelewa maana ya kuangukiwa na 'jumba bovu' hatashangaa kinachomkuta HK... Pole zake..
 
Hahaha halafu wakikupeleka pale golini kwao makumbusho wanakuonyesha na daily news fent fod ma nigga kigwa akiwa amezungukwa na lundo matapel, wanakwambia wao ni legit thats why muheshimiwa alifika kwenye uzinduz wao ila kwa sis wenye negative energies sensers tunatambuaga negative energies from kilometer away nikajua tu apa kuna ujizi unaendelea

Aisee mimi siku nimepelekwa pale nikauliza legitimacy ya hiyo kampuni walinitolea clip ya video inaoonesha siku inazinduliwa TZ na kuniuliza kama namjua HK nikasema namfahamu wakaniuliza cheo chake nikawaambia, then wakasema unadhani Naibu waziri anaweza kuzindua mambo ya kitapeli?. Nikavuta picha ya HK na drama zake nikasema kwa ushawishi wa HK hamjanipata, nikasema nitarudi hadi wa leo hawajaniona. Yaani wanakutajia watu waliocha kazi TRA, NSSF, BOT nk. Zile kazi ni utumwa ukishajiingiza maana utaanza kutafuta wa kuingiza huko mpaka ukome. Binafsi napenda utajiri lakini si wa mateso ya hawa walaghai.
 
We GENTA mtani umeanza eeh...by the way vipi matokeo ya jana kule Shy? (off the book).

Shinyanga Simba SC tumetoka sare ya magoli mawili kwa mawili na Mwadui FC na bado tunaongoza Ligi kwa tofauti ya alama tano na wale ' Wendawazimu ' wanaotufuatia ambao Kwao matokeo ya jana yalikuwa ni ' Sherehe ' Kwao kana kwamba vile wameshakuwa na alama sawa na Mnyama Mnyamani ( Simba SC ) wakati ukweli ni kwamba watajitahidi kuifukuzia Simba SC ila kuipita Simba SC wasahau.
 
Aisee mimi siku nimepelekwa pale nikauliza legitimacy ya hiyo kampuni walinitolea clip ya video inaoonesha siku inazinduliwa TZ na kuniuliza kama namjua HK nikasema namfahamu wakaniuliza cheo chake nikawaambia, then wakasema unadhani Naibu waziri anaweza kuzindua mambo ya kitapeli?. Nikavuta picha ya HK na drama zake nikasema kwa ushawishi wa HK hamjanipata, nikasema nitarudi hadi wa leo hawajaniona. Yaani wanakutajia watu waliocha kazi TRA, NSSF, BOT nk. Zile kazi ni utumwa ukishajiingiza maana utaanza kutafuta wa kuingiza huko mpaka ukome. Binafsi napenda utajiri lakini si wa mateso ya hawa walaghai.
Hahaha kuna mchizi ananiambia yeye ni injinia wa bandari ameamua kuacha kaz maana qnet inalipa balaa alaf nikimchek mchizi amechoka kidizain kuliko mimi mwingine alikua muhandis barric ameacha mwingine tbl yaan utapeli flan ivi wakitoto
 
Kwanza wakikuita kwenye ofisi zao hawakwambii unaenda kufanya nn utasikia "njoo rafiki kuna opportunity nzuri" ukienda unaweza juta poteza mda wako.
Kuna rafiki wa mchumba wangu alimualika pale Sinza, aliponieleza nikamkubalia.
Picha linaanza alipofika kituoni akampigia simu then akajamchukua, chakushangaza baada ya kuingia kwenye ofisi zao tu shosti yake akamgeukia akamwambia "good morning madam" alishangaa sana inakuaje jioni hii shosti ananiambia good morning? tangulini ananiita madam?

Baada ya semina ya siku tatu"udwanzi wa kiwango cha lami" akaja nieleza yote pamoja na kiingilio, kwakua hesabu hazijanipiga chenga tukaanza kunyumbulishaa.

Alitakiwa kutoa kiingilio cha 4m then atafute watu wawili watakao jiunga kupitia yeye, na kila mmoja atoe 4m, ukijumlisha wote watatu itakuwa 12m then yeye ndio anaanza pokea mgao ambao hauzidi laki 4.

Pia anatakiwa awasimamia hao wawili nao waingize watu wawili wawili yani wapatikane wapya 4 na kila mmoja atoe 4m jumla 16m, ili yeye mgao wake uendelee kupanda kufikia around 1.2m na asipofanya hivyo basi hautapanda. Jumla mpenzi wangu na tawi lake lote atatakia kufikisha 12+16= 28m ili mgao wake ufikia around 1.2m

Nikamwambia siwezi kuruhusu uzwazwa wa kiwangu hiko.
 
Hiyo Kampuni wana ka ' branch ' kao kamoja hivi kapo Sinza jirani na Hostels za UDSM ukienda hapo hata kama ni Saa Saba ( 7 ) mchana utasalimiwa kwa kuambiwa ' Good Morning ' na baada ya hapo utaanza ' Kuhubiriwa ' Kitapeli na Wanawake tofauti tofauti ambao huzungumza haraka haraka utadhani wamebanwa na Haja Kubwa na wanataka kuwahi Kujisaidia.
hahahaha goodmorning saa 7 uwii u made my day
 
Kwa kwel nimemsikitikia sana kigwangala. Kwel waziri tena anayejiita DR. unaburuzwa kuzindua kitu usichokijua kweli??
 
Back
Top Bottom