Kwanza wakikuita kwenye ofisi zao hawakwambii unaenda kufanya nn utasikia "njoo rafiki kuna opportunity nzuri" ukienda unaweza juta poteza mda wako.
Kuna rafiki wa mchumba wangu alimualika pale Sinza, aliponieleza nikamkubalia.
Picha linaanza alipofika kituoni akampigia simu then akajamchukua, chakushangaza baada ya kuingia kwenye ofisi zao tu shosti yake akamgeukia akamwambia "good morning madam" alishangaa sana inakuaje jioni hii shosti ananiambia good morning? tangulini ananiita madam?
Baada ya semina ya siku tatu"udwanzi wa kiwango cha lami" akaja nieleza yote pamoja na kiingilio, kwakua hesabu hazijanipiga chenga tukaanza kunyumbulishaa.
Alitakiwa kutoa kiingilio cha 4m then atafute watu wawili watakao jiunga kupitia yeye, na kila mmoja atoe 4m, ukijumlisha wote watatu itakuwa 12m then yeye ndio anaanza pokea mgao ambao hauzidi laki 4.
Pia anatakiwa awasimamia hao wawili nao waingize watu wawili wawili yani wapatikane wapya 4 na kila mmoja atoe 4m jumla 16m, ili yeye mgao wake uendelee kupanda kufikia around 1.2m na asipofanya hivyo basi hautapanda. Jumla mpenzi wangu na tawi lake lote atatakia kufikisha 12+16= 28m ili mgao wake ufikia around 1.2m
Nikamwambia siwezi kuruhusu uzwazwa wa kiwangu hiko.